UTURI WA ZANZIBARI
Yapendeza mahandhari, ya ndege na vipepeo,
Yanayonukia uturi, uturi wa Zanzibari,
Upepo ukiwa shwari mapenzi yawe Johari
Upepo ukiwa shwari mapenzi yawe Johari
Mapenzi ni kama kito, cha johari maishani,
Yana mwili wenye joto, na burudisha moyoni,
Penzi lenye manukato uturi wake maanani.
Moyo una burudiko kwa uturi wako mama,
Ningalipo na sisimuko kwa yako mandhari mema
Nataka niwe kwako, niishi katika usalama,
Uturi wa hali pevu, uturi wa Zanzibari,
Ningali bado mwenye nguvu, nikae kwako mwanamwari
Unipe maarufu, nakupenda Zanzibar.
Ewe binti Sultani, Uzuri wangu mbinguni,
Unipe matumaini, niwe nawe maishani,
Na makuli unilishe ni nenepe ni bukheri
Niliyasaka sana, mandhari yenye mapezi,
Lakini sikuyaona, mazuri yalo azizi,
Yaliyo na uungwana, kama yako eh! mapenzi
No comments:
Post a Comment