USIKU WA MAPENZI
Nimpweke natetereka, baridi natetemeka,
Moyo unashituka, mwili waweseka,
Gonjwa limenishika, dawa ninaisaka,
Mapenzi nahangaika, usiku wa mapenzi.
Mapenzi nahangaika, usiku wa mapenzi
Tazama napepesuka, mapenzi ninayasaka,
Mikono imekunjuka, mwili walalamika.
Walalamika mapenzi, dawa ya kuponyeka.
Walalamika mapenzi, usiku wa mapenzi,
Tazama napepesuka, mapenzi ninayasaka,
Mikono imekunjuka,mwili walalamika,
Walalamika mapenzi, dawa ya kuponyeka.
Unipe hayo mapenzi, ambayo ninayasaka,
Kwa wingi maandalizi, ndivyo ninavyotaka
yajaponitoa chozi, mapenzi tafarijika,
asante midomoni, hiyo itanitoka.
Asante midomoni, hiyo itanitoika
Tamwaga shukjurani, za wingi wa Baraka,
Tuwepo wote ndotoni,watulinde malaika.
Maua bustanini, moyoni tuje kunjuka.
Maua bustani, moyoni tuje kunjuka,
Tubebane migongoni, tupate kupumzika,
Tutiane machoni, siwe kuja toroka,
Tupendane abadani, tupone tukaponeka.
No comments:
Post a Comment