MPENZI WANGU UGANDA
Amani iwe na wewe, mpenzi wangu Uganda,
MOYO WAKO UKUNJUWE, UNIPOKEE Buganda
Mikononi mwako nituwe, tukae wote Buganda.
Hapa ninaranda randa mapenzi yamenipanda,
Tazama nilivyokonda, sababu ninakupenda,
Kwako mesalenda, kamwe sintaja kutenda.
Uganda urembo wako, ni zaidi ya mapambo,
Mapenzi wanipa sisimko, kwa zako tamu nyimbo,
Ningali ni Burudiko, faraja punde nkitambo.,
Mapenzi utamaduni, nayalilia ya kwako,
Haya mapenzi sabuni, yanasafisha chafuko,
Nitakatishe mwilini, nimwagie manukato.
Nakupenda sana Uganda, nakupenda moyo wote,
Na ahidi kukulinda salama uende popote,
Kama wingu nitakutanda, wengine wasikupate,
Mpenzi wangu Uganda, nakupenda sana Uganda.
Uganda tulia kwangu, mapenzi tuyaboreshe,
Hata wakija wazungu, ya kwetu tusioneshe,
tupike kimoja chungu, nilishe nami nikulishe.
Bernbdera yenye mapenzi,ipeperushe Uganda,
Yenye nguvu yetu mapenzi, wayatamani wanyarwanda,
Dunia uwe kiongozi, Malkia wangu Uganda
No comments:
Post a Comment