Thursday, September 19, 2024

Love aniversary

 KARAMU YA MAPENZI



Leo tumeadhimu, tuiweke na karamu


Sherehe yetu ni tamu, wawili tuliodumu,

Pasipo na uhasimu, ni miaka themanini,

 

Penzi hili vumilivu, penzi hili tulivu,

Mwanga wake angavu,laonekana bado bivu,

Penzi hili subirivu, halina doa wala kovu,

 


Ni miaka themanini, miaka tuliyodumu,

Wale wenye uhasimu, penzi kwao ni hadimu

Kushiriki kama timu, kuyatatua magumu.

 

Penzi lenye uhakimu, ulinzi na usalama,

Pendo mekuwa mwalimu, ni mzazi bora mama,

Mahaba yenye timamu bure hayana gharama,




 

Leo ninaitwa bibi, mwenzangu aitwa babu,

Wajukuu  mashababi, wazuri wenye adabu,

Twawaombea maombi, wawe wema matabibu.

 

Tumeipanda milima, tumeyaruka mabonde,

Japokuwa tulikwama,tukasonga mbele twende,

Kwa zake mola huruma, twala arua na tende.



 

Leo twaweka karamu,kunyweni tena kuleni,

Leo twaweka karamu,furaha tena chezeni,

Karamu yenye mapenzi upendo pia mahaba.

 

Karamu yenye mapenzi, upendo pia mahaba,

Watoto wetu wapenzi, zipokeeni nasaba,

na Baraka zenye enzi, muishi katika 'haba

 



 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...