Tuesday, September 17, 2024

BLESS ME WITH YOUR LOVE ๐Ÿ’–๐Ÿ‘ผ

 



 NIFUNIKE KWA MAPENZI.


Nifunike kwa mapenzi, kama tando la buibui,

Unizike kwenye zizi, nitulize moyo tuli,

nikuone kwenye njozi, haya mapenzi  sukari,

usinijaze huzuni, unipe furaha kweli .

 



Nifunikie udongo, mapenzi yaote mizizi,

Pembeni kwenye ukingo, maji yenye utelezi,

Udongo uzae mihongo, idumu katika mapenzi,

Usinijaze huzuni, nipe furaha kweli.



 

Nikingie mwamvuli, mvua sinighiribu,

Kwe' masika na vuli, penzi lako la ajabu

Gharika ikiwasili, iniepushe adhabu

Dhoruba kwenye  bahari, puta puta ni aibu.

 


Nizike kwa mapenzi, nitulie moyo tuli,

Penzi 'silo na majo'zi,twe' nalo twende mbali,

Sitopatwa na simanzi, nitapata raha kweli,

Huzuniko na majonzi, kwangu havitawasili.



 

Nikuone kwenye njozi, haya mapenzi  sukari,

Nyimbo pamoja  tondozi, ziniongeze .jeuri,

Mengi sana majambozi, yasiyotaka tunguri,

Nitakupa mwanagenzi, omba sana usijali.

 

Nisikutie huzuni, nipe furaha kweli kweli

Nikupende abadani, wewe kwangu ni wakili,

Penzi hilo la kijani, lina vito vya johari

Unizike kwa mapenzi, niridhikie mapenzi.



 

No comments:

Post a Comment

ZEE LA ZAMANI

  SEHEMU YA KWANZA. HOTELINI Ndani ya Hoteli Paradiso katikati ya Jiji la Mzizima (Dar es salaam) ZEE LAZAMANI akiwa na Mwanagenzi wake JAN...