Monday, June 22, 2026

 love is all


Given and found,🌹


It's all around,πŸ₯°

It's hard to tell about,😍

Easy to show,🀩

One sure thing when you feel it
You know it.😘

Love is always aroundπŸ’—

Like the sound of the beat,❤️‍πŸ”₯❤️‍πŸ”₯

Of your heart,♥️

Like sun in the sky.πŸ’ž


Hugs and caringπŸ’›

The laughter and tears that fall,πŸ’œ

The mundane and the magical,🀎

Love is all, all is love.πŸ’š


There is me you have always known🧑

The me that's a stranger still❤️

The you that feels like homeπŸŽ‰

And the you whatever willπŸ’

But still here we lieπŸ’‹πŸ’‘

Tender and trusting and true,

With every thing that we have been through.🎁
 

Love can make you feel so glad,🎊

Love is comfort when you feel bad.🎈

When you hold me like this πŸŽ‡πŸŽ†

So many memories fill my eyes

The first time we kissed,

The time we nearly said goodbye 

But still here we are 

Tested and tried and still true

And stronger than we ever knew.

Working and sharing love,

Love is all l have to give,

Love is all as long as l shall live,

So take it all and l will always be there,

When you call my name

I know, l know that Love is all.



Most people find that love is kind

When you feel it and know it,

Tell it and show it,

Whisper it

Shout it,

Feel good about it,

Given and found

It's all around

And around love

The cares word,

 the healing touch

The getting and the giving of
All is love,

You can't use it up,

Love is always around
You can't grab it, or take it

When you give it you make it,

Love does not stay the same.

It changes as people changes

Grows as people grow

You can come and go,

Say good bye or hellow

Hold or let go Love,

Love is part of your life till you die,

But love can make you angry,

Troubled and sad


Some people don't believe it,

Have to doubt it,

Try to keep it

From their mind.

All the glory, all the pain

All the passion 

That turn to ashes

Only to rise again.



follow me face book link

https://www.facebook.com/beli.A.4/

Friday, March 13, 2026

Good love

 Mapenzi Mema.





πŸ’–πŸ’–


Natuijenge dunia, yenye mapenzi mema,

Dunia yenye ujamaa, mapenzi tuyape heshima.

 

Upendo uwe neema, msamaha pia rehema,

Pasina tumia gharama, tupendane daima.

 

pasina tumia gharama, tupendane daima,

Tuishi kwa kujituma, tuzipokee karama.

 

Mapenzi yetu yatavuma, tayabariki karima,

Matunda tutayachuma, furaha italindima,

 

Mioyo iwe bima, tuuzike uhasama,

Daima tukijinyima, mapenzi yawe salama,

Daima tukijinyima, mapenzi yawe salama,

Tunyime vile vya gharama, mapenzi yatalindima.

 

Mapenzi yajenge hema, shamba yapate kulima,

Yaipande mbegu njema, yavune Dhahabu njema,

 

Mapenzi yajenge boma, lidumu likadumika,

Liwe mfano  wa Jua, giza litafunika,

 

Liwe mfano wa Jua, giza litafunika,

Mwanga utajikunjua, mabaya tutayazika,

 

Mwanga utajikunjua,  mabaya tutayazika,

Mema tutayajua, mapenzi taimarika.

 

I thought 'bout love πŸ’ž

 

                                                                                  

 

NILIYAWAZA MAPENZI





Mapenzi niliyawaza, machoni kuniangaza,

Mapenzi sijaona kiza, moyoni meng’anganiza,

Mapenzi menikimbiza, menishika menimeza,

Mapenzi yenye huruma, nimeyawaza siku zote.

 

Mapenzi niliyawaza, kwangu meyadunduliza,

Hakika yameshangaza, mema yameniongeza,

Mapenzi menitongoza, kwake yananiburuza,

Mapenzi menisogeza, raha yake naiwaza.

 

Mapenzi menitongoza, kwake yananiburuza,

Raha inaniunguza, joto la kwangu kupoza,

Nami ninayokoleza, kamwe sintayapoteza,

Kiapo changu apiza, mapenzi yanibembeleza.


chorus

Mapenzi sio utumwa, kama mnayodhania,

Mapenzi si kusukumwa, upigwe ukaumia,

Mapenzi ni ukulima, tunda nalitamania,

Mapenzi yenye heshima, hayo najimiminia.


 

Mengi menisaidia, mengi yamenivumia,

Mengi nimeyasikia, mengi yatanipatia,

Mengine meniwekea, hakiba isipotea,

Ndugu nitawagawia, kamwe sintawuzia.


Mapenzi meniusia, upendo kukazania,

Hilo nalitimizia, milele naliangalia,

Mvua inaamiminia, maua yalotulia,

Milele nitayawaza, milele tayatangaza.



 


 Hukutendea haki mapenzi




πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”

πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”πŸ’”

 πŸ’–πŸ’”πŸ’–πŸ’”πŸ’’πŸ’₯😭😭





Hukutendea haki mapenzi,

Mara uliponifukuza,

Ulisema nimekuudhi,

Moyo wako nimechukiza,


Mara ulinipigiza,

Thamnani ya langu chozi,

Lote umelikanyaga.

 

Hukutendea haaki mapenzi

Mara uliponitukana

Maneno yenye puuzi,

Mdomoni uliyapayuka


Siku nimekufania,

Chumbani ukibarizi,

Mwengine ukifurahia

 

Mwengine ukifurahia,

Zawadi njema mapenzi,

Mimi unaniuchukia,

Waniona jinamizi,


Mimi wanichukia,

Waniona kama mbuzi

Penzi ulininyimia.

 

Hukutendea haki mapenzi,

uliponifukuza,

Njiani nalimwaga chozi,

Dunia imeshanifunza,


Penzi lataka  heshima,

Sio kwa mafarakano,

Ungelitumia hekima,

Sio kwa matukano

 

 Chorus

Pesa zimekupa jeuri,

Zimekujengea kiburi,

Wanifanyia ukatiri,

Penzi lako kwangu ajari,

Tukae chini tujadili,

Mapenzi uombe msamaha

Kwanini ukunifikiri,

Moyoni ukanipuuza,

Hukutendea haki mapenzi,

Hukutendea haki.

 


 SARAFINA πŸ’–







Katika mji wa Soweto, Afrika ya kusini,


Binti mwenye mvuto, japo kuwa mutu duni,


Mapenzi yake vito, Dhahabu ing’aayo gizani,


Ninani huyo mrembo, Sarafina mwenye mapenzi.



 
Mandela angalipo jela, Amefungwa na makaburu,


Mapenzi mema yenye sera, za kuwapatia uhuru,


Afrika iwe moja dola, isiwe mwoga wa kunguru,


 Kwa mtutu na amani, freedom freedom free


 
Sarafina mwenye mapenzi, wima akajasimama,


Kuwakusanya wanagenzi, chehe kuzitema,


Tuupinge ubaguzi,tukiepuke kiama,


Mauaji yenye majonzi,uonevu na hujuma,


Tuupinge ukandamizi, katika aridhi mama.


 
Free Mandela….. free Mandela, Free Mandela free at last,


Vita! Vita! Vita Afrika, Damu zikamwagika,


Na Mali zikaharibika, mateso yakaamka,


Vitisho vikatumika, hofu pamoja shaka,


Njaa isiyo na huruma, Afrika ikateseka.


 
Lakini twafurahi, JUHUDI MESHINDA kudura,


Afrika yaona fahari, kuachiwa kwa Mandela,


Uhuru sasa tayari, kongole nyingi hongera,


Sarafina mwenye mapenzi, ametuchangia mapenzi.


 
Sarafina mwenye mapenzi,mapenzi amechangia,


umekoma ubaguzi, uhuru kwa wote pia,


hakuna ukandamizi,Afrika yashangiria,


uishi maisha mema, Sarafina mwenye Mapenzi.




 MAPENZI YA ZAMANI



mapenzi huko zamani, sio haya ya sasa,

Bibi kumpenda babu,  heshima kumtunzia,

Hakutokuwa sababu, ya babu kumwaibia,

Bibi kwa majabu, babu katulia,


Mapenzi huko zamani, sio haya ya sasa.

Mapenzi huko zamani, yalikuwa na heshima,

Nguo  fupi na vimini, hakuna hizo zamani,

Ukitaka kuamini, waone wakiwa ndani,


Mapenzi huko zamani, sio haya ya sasa.

Vijana hawa wa sasa, hesima kwao jalaa,

Wakisha pata mapesa, hula mpaka kusaza,

Ukitaka kuwahasa, wanajitia waelewa,


Mapenzi huko zamani, sio haya ya sasa,,

Mke kutoka na huyu, mume kutoka na yule,

Kama tunda za ubuyu, utupwa hapa na pale,

Wanakua kama kuku, ukikosa mtama tele,


Mapenzi huko zamani, sio haya ya sasa.

Michepuko sio  dili, shikeni hiyo kauli

Kwanza mvae akili, kutenda na kufikiri

Kama nyie majeuli ,wenzenu wamekithili,

Mapenzi huko zamani sio haya ya sasa

 

 


πŸ’‹πŸ’•πŸ’–


Uturi wa Zanzibari,

Hayo marashi asili,

Basi mapenzi pulizia.


 

Basi mapenzi pulizia,

kama maua kuvutia,

heri nazo kukujia.

Ewe mpenzi Tanzania

Kama ua wavutia,

Heri nazo kukujia.


 

Tena  mpenzi we pendendeza,

Waone wenye kengeza,

Jinsi unavyokatiza.

 

Jifukizie uturi

Unukizie hu, mwili

Tena uende sanjari.


 

Tena uende sanjari,

Na mavazi ya Hariri,

 Yenye rangi za Johari.


 

Yenye rangi ya Johari,

Hazichuji kama bahari

Machoni zina fahari.


 

Manukato ya Commoro

Mazuri yaso kasoro,

Uyapake unyoro.


 

Ndege watakuimbia,

Nyimbo zinazosifia,

Uzuri wako majaliwa.


 

Tuvuke twende ngazija,

Mapenzi kule yamejaa,

Tukaimbe kwa lahaja.

 


Mpenzi twende anjuani,

Mapenzi kule ni thamani,

Thamani ndani moyoni.


 

Penzi lako lanukia,

Wengi wannatamania,

Kamwe hawakupatia.

 


Basi mpenzi nukia,

Nisichoke kuangalia,

Nazo sifa kusifia.

 


Basi mpenzi nukia

Uvae taji dunia

Taji lake Malikia.

 


Taji lake Malkia,

Sasa utaabudiwa,

Mema nayo taambiwa.

 

Nyimbo tamu kukwimbia,

Harufu njema wasikia.

Kwako wakimbilia.

 



Two birds on the tree πŸŽ„

 NDEGE WAWILI MTINI.



Kuna ndege wawili, wapo juu ya miti,
Wana rangi  bahari, pendo limejizatiti,
Wana mbawa  johari, macho madini ya bati,
Ndani kwenye viota, wametulia tuli.


 
Tuli tuli tuli tuli, maji mtungini.
Sauti zao kasuku, na wivu wao chiriku,
Wakatoka tuku tukuy, macho wameona vitu,
Chakula alacho kuku, hindi mtama mafuku.


 
Njaa haina huruma shibe mwana unikome,
Ndege wakajiparama, kuukimbia ukame,
Tumbo lipate neema, shika jembe ukalime,
Raha ukijipa mwenyewe, jipimie uridhike.


 
Raha ukijipa mwenyewe, jipimie uridhike,
Meno yakasuguliwe, tumbo jaa lkipasuke,
Watanga tanga aguliwe,. Huo mshike mshike,
Dunia mti mkavu, kiumbe siegemee.


 
Hatai! Hatari! Hata! Ooh! Msalie mtume,
Matumbo yakata kata , ni wapi wajiegemee,
Tam ufuta kashata, eh! Mola wahurumie,
Walikuwa zumbukuku, limbyukeni wa chakula.


 
Jamani dezo yaua, vilivyo bure mtego,
Ndege hawakujua, kasuku yao mipango,
Sumu meibugua, megeuka mipingo,
Wapenzi sha tokomea,kuonana majaliwa.
 
 
 


NELIA

 NELIA




Furaha hya mapenzi, awepo umpendaye,

akupae usingizi, presha yako itulie,

huyo ndiye mtetezi,shida zote zilile,

nawe uwe mkimbizi, matatizo atatue.


 

Nelia aliolewa, na Mume mwenye mapenzi,

Kazi akatafutiwa fundi wa kushona mavazi,

Na watoto wakajaliwa, na wakike na wakiume,

Maisha yakawa murua,wakiwa kwao Zimbabwe.


 

Furaha ya mapenzi, Nelia ilimsafisha,

Furaha ya Mapenzi, Nelia ilimtakatisha,

Mume aliye ujuzi, kwa yeye akajikesha,

Mapenzi yalivyo matamu, utamu usio kwisha.


 

Wealisema wahenga mapenzi upepo,

Walinena hekima, mapenzi maua,

Walisema busara, mapenzi sabuni,

Ndipo yakatimia, mapenzi kizungumkuti.


 

Ajari yenye simanzi, Nedlia akawa mpweke,

Mumewe ametwaliwa, kamuacha pekee nyake,

Urithi alojivunia, shemejiye akampoka,

Watoto alowalilia, Nelia anasikitika.


 

Shemejiye akampoka, mashamba ya kilimo,

Biashara iliyoboreka, mifugo itupayo nyama,

Nyumba aloisimika,watoto ni wake mama.

Hakiba aliyoiweka, mali walizochuma

Shemeji akamtaka Nelia awe mke mwema.


 

Nelia hana raha, ameachwa mjane,

dhuruma pia mzaha, matusi atukanwe,

uonevu katika haki, moyo ukamtuma,

kuizika hiyo chuki, yenye wingi wa hujuma.


 

Mahakama akafika, kesi ikanguruma,

Haki ikatendeka, mama kapewa chema,

Mali alizopokwa, Nelia akarejeshwa,

Sheria ndio


msumeno, makali makali kuwili.


 love is all Given and found,🌹 It's all around,πŸ₯° It's hard to tell about,😍 Easy to show,🀩 One sure thing when you feel it You kn...