Uturi wa Zanzibari,
Hayo marashi asili,
Basi mapenzi pulizia.
Basi mapenzi pulizia,
kama maua kuvutia,
heri nazo kukujia.
Ewe mpenzi Tanzania
Kama ua wavutia,
Heri nazo kukujia.
Tena mpenzi we pendendeza,
Waone wenye kengeza,
Jinsi unavyokatiza.
Jifukizie uturi
Unukizie hu, mwili
Tena uende sanjari.
Tena uende sanjari,
Na mavazi ya Hariri,
Yenye rangi za Johari.
Yenye rangi ya Johari,
Hazichuji kama bahari
Machoni zina fahari.
Manukato ya Commoro
Mazuri yaso kasoro,
Uyapake unyoro.
Ndege watakuimbia,
Nyimbo zinazosifia,
Uzuri wako majaliwa.
Tuvuke twende ngazija,
Mapenzi kule yamejaa,
Tukaimbe kwa lahaja.
Mpenzi twende anjuani,
Mapenzi kule ni thamani,
Thamani ndani moyoni.
Penzi lako lanukia,
Wengi wannatamania,
Kamwe hawakupatia.
Basi mpenzi nukia,
Nisichoke kuangalia,
Nazo sifa kusifia.
Basi mpenzi nukia
Uvae taji dunia
Taji lake Malikia.
Taji lake Malkia,
Sasa utaabudiwa,
Mema nayo taambiwa.
Nyimbo tamu kukwimbia,
Harufu njema wasikia.
Kwako wakimbilia.


No comments:
Post a Comment