Saturday, October 5, 2024

Unconditional love πŸ’•

 


MAISHA YANGU yalikua MAZURI

Kila siku nilikua ni Binti mwenye furaha

Wazazi wangu walinidekeza nami nilideka 



Lakini jambo Moja lililoniuniza MOYO

Ni vile tu majirani na marafiki zangu wakinicheka

Tena walithubutu kunizomea

" Hilo, Hilo... Zaifu hiloo."

"Hilloo baba na mama yako hawana NGOZI... Hiloooo." Maneno haya yaliniuma kila siku


Niliporudi nyumbani kutoka skuli

Sikuwaonesha darili wazaz wangu

Kwamba naumizwa na maneno pamoja na kebehi za majirani

Nilijifungia chumbani

Nilibaki nalia tu😭 chumbani kwangu mie Debora Na Zingo πŸ™ŠπŸ™ˆπŸ¦sokwe wangu

Masikin mieπŸ˜­πŸ˜­πŸ™Š






Baba na Mama walinipenda

Pendo la kupendeka

Pendo lililozidi pendo

Pendo maradufu


Na madekezo yao kwangu yalipaMBA MOTO

Leo navaa gauni jipya na kiatu jipya

Kesho nanunuliwa PIZZAπŸ• midoli na vitu vya kuchezea

Keshokutwa napelekwa ⛱️ πŸ–️ beach kuchezea MAJI 

Lakini bado tu huzuni haikuniisha

Pale majirani na marafiki wakinicheka eti baba na mama YANGU hawana NGOZI







Nooo!

kulia kwangu kuliniumiza zaidi.

Sikuzitaka ZAWADI walizonipa wazaz wangu

Tena nilizibutulia hukooo!

Nikadharau

Sababu ya HASIRA HASARA



BASI USIKU mmoja
Yapata saa saba kamili

Baada ya kulia sana
Na kujishauri hapa niondoke tu
Siwezi kuishi katikati ya mji wenye watu wanaonisema na kunisengenya.



Mie Debo na Sokwe wangu Zingo tukapakia 

Tayari kuondoka

Tena kwenda mbali na nyumbani

Tusirudi Tena

Tusirudi kwenye midomo na kelele zao majirani



Bora kuondoka
Mie na Zingo tukapakia VYETU
TUKAANZA KUSEPA
TUKASHUKA UP STAIRS

LAKINI TUTATOROKAJE WAKATI HATUNA PESA
YA GARI, KULA NA STAREHE ZINGINE





Wazo likaja, 
Tukaibe
Tukaibie baba na mama
WANGALI WAMELALA
YES! Wazo zuri
Mwendo wa kunyata
Cat walk






Tutaiba zote
Hakuna kubakisha
Zooote...

Nikafungua droo 
Zingo Sokwe wangu akabaki mlangoni
Kuni alert iwapo Papa na Ma watashituka,
Nikafungua droo
PESA sikuziona
Ila Kuna bahasha niliiona


Juu ya bahasha paliandikwa DEBORA MWANA MPENZI.
JESU! Jina langu
Au ni urithi?
Au wosia?
Nisiandike mate, wino ungalipo
Nikafungua ile Bahasha

Nilichokikuta ndani ya ile Bahasha sikuamini macho yangu




Mtoto asiye na NGOZI alikua akilia juu ya kitanda
Pembeni watu wawili waliofanana na baba na mama YANGU walikua
Wakilia pia
SIKUELEWA nikabaki kukodoa mijicho.



Lakini kadri nilivyozitazama zile picha

Ndivyo nilivyopata kuelewa

Mtoto asiye na NGOZI alipewa NGOZI ya baba na mama yake

Yaani baba na mama walijuchuna NGOZI zao Ili kumfunika YULE NTOTO ASIYE NA NGOZI

Wale wazaz wawili waliokua wakilia niliwatambua

Ni baba na mama YANGU

Na yule mtoto asiye na NGOZI ni mimi


Kumbe mimi nilizaliwa bila NGOZI

Kumbe baba na mama walijichuna NGOZI na kunifunika Ili NIWE mzuri wa kupendeza

Nikaanza kulia😭😭 Tena Kwa sauti iliyosababisha baba na mama wadamke pale kitandani walipolala.



Nikalia masikini mimi Debo

Nikalia upendo huu wa Wazazi wangu,

Unconditional love, upendo usiopungua

Wamejitoa muhanga Ili Mimi niishi

Wamejiharibu Ili Mimi niishi

Na bado tu NATAKA kuwakimbia

😭😭😭😭


Hapana, Sintakimbia

Wala sintaobdoka

nawapenda wazazi wangu

NATAKA kuishi pamoja nao.


No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...