Sio kwa sura au mwonekano wake
Bali kwa matendo yake
Realy alikua mtoto
Tena mtoto mwenye utoto
Nilimchukia
Anisukume
Anivute nywele
Anikemee
Bila sababu
Nilimchoka👿
Mimi Agi, Dolla na Linda
Marafiki zangu
Tukipata mlo
Akajipitisha
Aliponiona
Akafanya madoidoi yake
Makusudi tu, akaibonyeza meza
Yetu ya chakula
Chakula Cha bei gharama
Kikamwagika
Nilimchukia
Mtu wa hovyo Trump
Darasani nilikosa furaha
Raha na amani
Sababu ya matendo yake
Anaburuta nywele zangu
Kwa furaha na kejeli
Kama haoni maumivu yangu.
Shit!
Anafanya kunipiga juu kichwani
Nahisi maumivu
Nyota nyota machoni
Nimemvumiliavya kutosha
Sasa lazima nimfunde
Kwa vitendo.
"Kula kofi hilo, mavi ya kuku wewe"
Puuu
Puuu
Puuu
Akatimka
Mwendawazimu yule
Safi sana
Wavulana lazima wawaheshimu wasichana
Wajue sisi pia tuna hisi na hisia na maumivu
Mshenzi yule!
Tuone kama atarudia tena
Nimeshituliwa na habari hizi mtandaoni
Siku ya Leo, siku mbaya.. Bad day!
Habari zinasema
Trump yupo Hospitali
Amepasuliwa juu ya kichwan... Opereshen🙆♀️
Ubongoni
Eti damu imevujia ubongoni
Jesus!!
Mtume!!
Hizi habari au ndoto!
Wamemnyoa nywele na kumshona kichwan
Uwii!
Taarifa zikamininika kutoka Hospitali
Trump Yu hoi, taabani, mahututi
Nilichanganyikiwa
Nikajiona labda mm ni mkosaji
Maana kwa hasira nilimponda kichwani
Habari zikavuma
Trump yule Mkorofi wangu
Hatunaye tena Duniani
UwiiiðŸ˜ðŸ˜
Machozi yakanibubujika
Huzuni ikaniparamia
Akalala pekee
Kwenye giza
Na kupiga kelele
Juu ya kaburi lake
I'm sorry TrumpðŸ˜
I'm sorry TrumpðŸ˜
Please forgive meðŸ˜
Sikudhamiria
Sikujua kama itatokea hivi
Sikujua Mkorofi wangu
Mungu akulaze pazuri pema.
Najiona mkosaji
ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜¢ðŸ™†♀️
No comments:
Post a Comment