Sunday, October 6, 2024

BABY PROTECTOR

Niite Pydex

Mimi ni Baba wa Giza 

Lakini sio BABA mbaya

Pale mtu anapohtaji huruma na msaada

Nipo tayari kuitoa roho na nafasi YANGU

Kusaidia

 

BASI Bwana katika pita pita YANGU

Jioni Moja

Yapata saa kumi na mbili

Si nikamuona

Jibaba mmoja kashika kisu kikali kuwili

Kifuani kwake kamgandamiza mtoto ambaye alikua akilia

Kilio Cha kulitaka Jibaba limuachie

Kilio Cha kutaka arejee mikononi mwa MAMAYE

Ambaye alisimama pembeni amejaa huzuni na kumlilia mtoto wake.



"Kama hauna millioni mbili nakwambia huyu mtoto sikupi" Jibaba 

Lilimpigia kelele yule mama mwenye uchungu wa mwana

" Sina pesa hizo, tafadhali nirudishie mwanangu" Mama alilia

" Wewe Mume wako si anauza madini, unashindwa vipi kwenda kumuibia unipe Mimi"
Jibaba lilimshawishi mwanamama akaibe.

" Siwezi kuiba, kuiba ni zambi na ni kosa. Ukitegemea Mimi na mwanangu HATUNA kosa ni wapita NJIA tu"

"Alah! Unanijibu jeuri, Sasa namchinja huyu mtoto"

"Hapana, hapana... Muhurumue mwanangu"

Mwanamama alilia. 

Niliyasikiliza maongezi yao

Nikagundua kumbe Jibaba ni Jambazi

Limemteka mtoto makusudi Ili lilipwe

BASI roho YANGU ikaniambia "fanya kitu.. do something"



Nikaivua kofia YANGU

Kofia inayoficha MAOVU

Kofiabinayotenda maovu

Nikalitazama JIbaba

Lile lenye ndevu za Osama
Nilichokifanya Najua Mimi

Maana Mimi ni SHETANI wa USIKU

Baba wa giza
Likadondosha kisu chini

Likamuacha mtoto

Mtoto akakimbilia Kwa mama yake

Mimi bado nilikua nafanya kitu

Nadani ya kofia yangu

Jambazi likadondoka chini

Limeshikiliankifua

MOYO unaliumaa

Likatapika damu

Na kutapatapa
Likapiga mayowe

Kifua, kifua, kifua
Oooh! Kifua kinanibana
Maweee! Nisaidie

Sikujali bado tu nikaendelea kufanya Ushetani wangu


Nilipohakikisha limezima

Limezima taaπŸ•―️πŸ’‘, taa ya MOYO wake

Nikajipongeza Kwa kuutoa MOYO wake

MOYO niliounyofoa kishetani SHETANI

Dawa yake ilikua ndogo

Tena ndogo sana

Asijitokeze Tena Jibaba mwenye tabia kama zake

Nitammaliza Mimi

Oooh!
Chezea Shetani wa USIKU
Chezea roho nyeusi.


No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...