Monday, October 14, 2024

Donda la wivu... Sehemu ya sita

 


SURA YA SITA

TUZO.

            Shughuli nzito ya kutambikia  lile zoezi ilianza, shughuri nzito ya kuomba Mizimu ilianza, ilikua ni shughuli nzito kweli kweli,  yalikua ni maombi makuu, ngoma za jadi zilichezwa, watambikaji wakala nyama ya hilo tambiko wakanywa pia vileo vilivyo andaliwa kwenye lile tambiko, tena wakaimba na kucheza.

                              “Mwenye makosa aonekane,

                                Mmwenye makosa ahadhibiwe,

                                Adhabu! Adhabu! Adhabu!

                                Adhabu itolewe!                    

                                Liwepo funzo katika jamii,

                                Watendao haki wahesabiwe

                                Watendao haki waheshimiwe,

                                Hiyo tuzo! Hiyo tuzo! Hiyo tuzo!

                                Tuzo wapewe.

 

Watambaji waalimba nyimbo zao, wakiiomba Miungu itende haki, pale haki inapotakiwa kutendwa pamoja na kuiomba Miungu itoe adhabu pale  uvunjifu wa haki ulipoonekana kushika nafasi yake, maombi yaliendelea kuombwa. Mizimu iliombwa itende haki ili apate kuonekana ni nani aliye na makosa ama ni nani asiye na makosa? Ni upande gani ulio stahiri kupewa adhabu ama ni upande gani ulistahiri kutunukiwa tuzo ya  heshima?  Kwa sababu ya  ukweli na uwepo wa haki isiyo na kasoro.

                 Wazee wa mila walikua na kibarua cha kupiga manyanga, walipiga manyanga, walipiga manyanga, walipiga manyanga, walipiga manyanga weee! Walipiga manyanga kama wendawazimu masaa nenda masaa rudi waliendelea kupiga manyanga wala wasichoke kupiga manyanga, kelele za mayoe pamoja na nyimbo, makofi vifijo na nderemo  kwa pamoja vilisikika mbele ya hadhira kubwa  iliyo hudhuria.

                  Mwisho ngoma ilifikia tamati, Mizimu pamoja na roho wengine waovu wakajibu  sala za  wazee wa mila.

Matokeo ya maombi yao yalionekana mbele ya hadhira, kila mwenye macho mawili aliyaona matokeo ya lile tambiko, masikini mzee Jamali yaliyo mkuta yasiwe ya kuadithiana  yaliyomkuta ni mazito ya dunia, yaliyomkuta yanatisha na kuogopesha.

                    Kumbe ni yeye binafsi aliyekutwa na hatia kumbe ni yeye ndiye mkosaji, kumbe ni yeye binafsi ndiye….. loh! Waswahili walisema umdhaniaye kuwa ndiye kumbe sie. Waswahili walisema  hisia hazijengi, wengine walisema fikiria kabla ya kutenda, heri nusu shari kuliko shari kamili. Looh! Masikini mzee Jamali  alibadirika na kuwa na umbo la mnyama wa kufugwa.

                     Kila aliyepata kumuona mzee Jamali akiwa katik a umbo lile alisikitika na kuogopa pia. Tizama haraka haraka imemnyima baraka, tizama kuficha ficha kwake mambo  kumemfanya  apungukiwe heshima mbele ya jamii iliyomzunguka, aibu ya karne aibu kuu. Mzee Jamali alikimbilia nyumbani kwake, alikimbia kama vile Ng’ombe akimbiavyo akajificha ndani ya nyumba yake, huko akalia machozi, akalia kilio cha kwi! Kwi! Kwi!

Itaendelea

No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...