Sunday, October 6, 2024

Acting went wrong

niite Jordan
Mm ni  POLISI
Mtu mzuri Kwa raia
Mlinzi na mlinda Mali na raia



 

Some time sisi walinzi tunaitwa Dog watch
πŸ•‍🦺 Yaani walinzi
BASI siku Moja
Nilikua Restaurant Moja inaitwa Mac Donald Rest
Nilikua nikipiga kahawa na mabums MDOMONI 🍩
Mung'unywa mung'unywa nilitafuna
Bila wasi wasi
Maana kawaida YANGU kila ifikapo mida ya jioni 
Lazima nipige kahawa na madonats


Bai bwana nikiendelea kumung'unya mung'unywa
Nilishituliwa na masauti ya kilio
Kilio Cha Binti mtu mzima
Upande wa kulia kwangu
Karibu na mlango wa Mc Donald Rest
Nikajisemea mtimani potezea

Lakini bado nilisikia masauti ya kulia
Kama vile mtu alikua ameanguka chini puu!

Mmh! Hapana sio kawaida
Nikageuka kushoto

Mtume!
Raia mwema ametekwa!
Kombe langu la kahawa chini puu
Donati nayo ikanitereza chini puu

Noo! Man life is something precious πŸ’• 

Lazima nifanye kitu
Kuokoa MAISHA ya raia wema

Maana tumewachoka vibaka
WAMEZIDI kuongezeka mitaani
Wanaua
Wanateka
Wanaimba
WanFANYA MAOVU
Wanaweza hata kukupididi... Pidadi
Kamahujielewi hapa mjini

Eey put your stupid knife down"
Lift your fuck hand up"
Nilimshurutisha yule haramia aliyemteka binti

Hakunisikiliza
Usoni alitisha, Hana macho
Meno yake mawili ta juu marefu
Nywele zimesimama kama majani ya ng'ombe
Shingoni amevaa chuma 
Mkono wa mashoto amevaa chuma pia ameshikilia kisu kikali balaa


Hakunisikiliza, alitisha
Mimi Nikajisemea hapana
Ngoja nimlipue kabla hajatenda ubaya
Pyuuuuuu , nikamfyatulia risasi
Bila kupoteza muda

Nyambaaaafu"
Shiti kabisa"
Haifai mijitu hii katika society" 


Risasi Moja tu ilikitoboa kifua Cha yule Jambazi
Akaanguka chini
Tayari amezima
Kadedidi


Nikamsogelea niagalie kama ataleta madhara mengine
Hawezi huyu
Binti aliyevamiwa na yule mwanaharamu
Alikua akitetemeka
Akiogopa
Na kulia sana
Nilimshangaa
Badala ya kunishukuru
Yeye AnaliaπŸ˜…

Hizo ndo za punda shukrani.


Eeeh! Nini?
Nilipigw BUTWAA!!!
Mbona sielewi
Waaandishi???

Mmh!
Wote wananishagaa
Mimi pia nawashangaa
Eeh!

Jesu!!
Waigizaji
Kuna huyu short alievaa miwani
Amebeba ubao umeandikwa
'Cut'

Duh!
Kwaiyo walikua Wana act movie
Au content?
Duh!
Msala,

Nina kesi ya kujibu

Murder case.
Na Jella inanihusu.

No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...