Friday, October 4, 2024

Ndoto ya kutisha... Sehemu ya tatu.

 3


Ndoto ya kutisha

SEHEMU YA TATU.



 Psevejicho-kudopto           pyave                                                                                              

Psevejicho- kudopto            pyave

(Tu wajinga tumekosa)         (sisi)

 

Pitukubashite-piziro               petee

Pitukubashite-piziro                petee

(tunaomba tusamehe)            (wote)

 

Pjigijigi –patuko                        pisele

Pjigijigi –patuko                        pisele

( Ewe wetu mtukufu)               (Mungu)

 

Fahamu ziliponirudi, nilihisi maumivu makali mno usoni kwangu, yaani maumivu yasiyoelezeka kwa jicho moja nililobaki nalo, nililitambuausiku ulishaingia na nikaliona kundi la wanawake wangunjwasi likiimba, ni wakina mama wa makamo wamenizungukuka wakiwa kama walivyozaliwa. Miili yao inatisha, nilitumia mwanga hafifu wa mbalamwezi kuwaangalia lakini nilikuja kugundua kuwa walikuwa na michubuko na makovu ya aina mbali mbali kwenye robo tatu ya miili yao kama ilivyoikuwa kwangu pia.

                 Walipogundua nimezinduka waliacha kuimba wakawa wanaomboleza kwa chini chini mwishowe nikanyamaza kabisa kisha wanawake wawili wakajongea katikati ya duara nilipolazwa. Mmoja akakaa upande wangu wa kuume mwingine upande wa kushoto pale chini nilipolala. Kisha mbibi mmoja akatusogelea akatumwagia vitu vilivyo katika hali ya unga unga ambavyo viliniuma sana vilipoingia kwenye vidonda haswa kidonda cha jicho. Alipomaliza kutumwagia akawaamuru wale wanawak e wasimame, halafu akawapa visu vidogo kila mmoja kisha akawaambi kwa kinjwasi kuwa ili tambiko la kumzuia Joka kuwauwa wao litimie ni lazima wao kwa mikono yao waniue mimi.


                      Nilijikuta maumivu yamekata, nikaanza kuomba kimoyo moyo, nikiwa kati kati ya sala mwanamke mmoja aliyararua mavazi yangu nami nikawa kama wao, kisha kwa gadhabu akanikata viungo vyangu vya siri, nilipata maumivu ambayo nilijihoji kwanini asingeniua kabisa, halafu kwa kwa kile kisu kinachovuja damu damu yangu alinichana shavuni. “aaahgh!” nililalamika yule mwanamke alimalizia kwa kunidunga kisu kwenye kiganja changu cha mkono w a kushoto.


                Nilihagaika pale chini nisipate msaada zaidi ya makofi ya shangwe yaliyowatoka wakina mama walionizunguka huku nikishuhudia mmoja akizitafuna sehemu zangu nyeti, wengine wakimchochea yule mwanamke mwingine animalize. Maumivu yalitawala mwili wangu kuanzia kwenye ncha ya unywele hadi unyayoni. Huyu mwanamke wa pili alikuwa na sura ya kikatili zaidi na alipoonesha kuniinamia anishughulikie wote walishangilia, aliponisogelea zaidi wote walinyamaza wakisubiria kwa hamu kuona kifuatacho.


             Nilishukuru mungu kwa muda wote niliokuwa aridhini nikamshukuru na babu yangu mzee Kidasi kwa kunilea vema na kunifundisha kuwinda ambapo leo Swala amenifikisha hapa, hapa nilipo. Nikawakumbuka wanakijiji wenzangu na marafiki zangu waliopo Mg’etta ambao bila shaka watakuwa wananitafuta kwani sio kawaida yangu kuwinda mpaka usik ofu. Masikini mzee kidasi wangu, nilishangaa jicho langu nasubiri kifuatacho.


              Ghafla nikasikia kelele za shangwe nisijue linaloendelea, nilipojaribu kufungua jicho niliuona mguu wangu ukiwa umetengana nami kiha nikakiona kisu kinanijia moyoni, ila alipofikisha kifuani alikilaza kisu baada 

ya kunichoma. Niliganda kwa muda. Wote walishangilia kisha kile kibibi kikasema pingingoswera pswira pshaka shenme mingizi( tumuacheni halpo afe taratibu, kesho tuifate nyama yetu.) wote waliafiki wakatawanyika.


                               #########################################


      “Uwwwwuuuuuuuuuu!!” Ni sauti za umbwa mwitu nilizo zisikiaa baada ya kuzinduka kabla sijazimia kwa kitambo. “ Uwuuuuu!!” sauti ziliendelea huku upepo wa baridi ukivuma taratibu uhuuuu! Uhuuuu! Taratibu pia nikaanza kuhisi maumivu ambayo nilkikuwa siyasikii kutokana na kupitiliza kwake. Nikajifanyia tathimini fupi ya mwili wangu nikagundua sina jicho, sina mguu sina sehemu za siri, sina vidole saba vya mikononi sina nywele, sina meno ya mbele sina sikio la kulia hakuna hata kiungo kimoja kilichopo mahali pale ina maanisha vyote walikula hadi nywele.


               Nikaendelea kujitathimini, nikatambua mwili wangu ni vidonda vitupu, ukiacha sehemu ambazo nimekatwa viungo, shavuni mimechanwa, makalioni nimetobolewa mikononi nimechorwa reli kwa visu mguu mmoja nao uliobaki umetobolewa tobolewa vya kutosha pia kwenye paji la uso nina michaniko ya kila aina. Nililia sana nililia kwa uchungu nililia kwa sauti. Ni kama kilio change kilisikika punde mtu akatokea ni Mgunjwasi, mwanamke aliyeshika kisuu mkononi. Kwa hasira nilimlaani nikamtukana yeyena jamii yake ili animalize vizuri, kwani hali niliyokuwa nayo ni heri umauti.na kuwa chekundu kutokan na wingi wa damu nyingi iliyonitoka. Sijui kama niulimuona vizuri au la! Kwani uoni wangu haswa kwa jicho moja ulizidi kuwa mtihani, sekunde hata sekunde ila nilimuona yule mwanamke wa pili mwenye sura ya kikatili ambaye alipopewa nafasi ya kuniua alikilaza kisu kifuani kwangu badala ya kunichoma aniue huku wenzake wakiwa hawana habari kutokana na giza. Akiwa amenikanyaga kifuani alinipiga mateke mawili kichwani, ndipo nilipozimia.


            Ingawa nilikuwa natamka maneno kama mtoto anaye jifunza kuonge lakini adhima yangu ilifanikiwa, yule mwanamama alipandwa na hasira akanijia na kunirukia kwa miguu yake kifuani, zikanitoka damu nyingi sana kifuani hadi kufikia sasa kile kipande cha aridhi niliyolala kiligeuka

No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...