Saturday, October 5, 2024

MANZI ALIYENIOGOPESHA


 Naitwa Dominick

Mimi ni Artist yaan mwanasanaa, 

Mchoraji mkubwa.. East Africa

Ni maarufu Kwa kuchora picha za Marais na maceleb.. Watu maarufu


Napata madili💸💰🤑 mengi KUPITIA sanaa na kipAJI CHANGU

PESA NJE NJE

NAAMKa na pesa nalala na pesa

Weuwee😅💕 naipenda kaz YANGU.

BASI bwana siku Moja nikatembelewa

Na MANZI FURANI

ANAFIGA YA KUKU

KUKU WA KIZUNGU

Mrefu mwembamba, .....slim body😂

Sifa zisijae gunia


"HI BRO!" MANZI KANISALIMIA"

"HI" NIKAMJIBU YULE MANZI MWENYE SUNLIGHT NA BARAKOA MDOMONI

"NAWEZA PATA PICHA"

"PESA YAKO TU MADAME." NILIMJIBU





Ukinichora poa nitakuachia laki tatu" YULE dame kajinadi

" Duh MANZI ana mpunga huyu, lazima nimchoree good" Nikajisemea mtimani

"Ok karibu, keti." Akavuta kiti kilichokuwa Kona, akaketi

Sket yake ndefuu ya damu ya MZEE, viatu vyake vyeusi vinang'ara, blouse yake nyeusi ilimpendeza



"Nakuchora pamoja na BARAKOA?" Kuuliza sio ujinga, nilihitaji kujua.

"No, nahitaji picha perfect. Kamili. Ngoja niondoe BARAKOA.

Akaondoa miwani yake na BARAKOA. 



Jesu!! " Nilitoa macho pima, kama mjusi aliyebanwa mlangoni

MANZI huyu" nilishangaa.

Mmh, kazi ninayo Leo" 




"Waeza endelea nichora" Aliongea. Mie Mshangao!!!

"Huyu mtu au Jini?" Nilijiuliza

"Sijapata ona" woga na kutetemeka kukanivaa

Mkojo kidogo uniaibishe. We acha tu


Mwanaume ngangari nikaingia kazini
Mwendo wa kumchora Kuku wa kizungu
Mwendo wa kufutA NA kurudia
Mwendo wa kutetemeka na kutia jasho
Mwendo wa kuwaza na kujisemea sijui nitoke balu!
Nimepatikana Leo!

Mwanaume nikamaliza kumchora yule dame

Ningali nateremeka nikamkabidhi picha yake ajitazame


Sijui ataipeNDA!! MMH! 

DAME AKAIPOKEA ILE PHOTO DRAWING


Akaitazama
Wakati huo Keisha vaa tayari Yale mawani yake ya Sunlight
Na BARAKOA juu

Akaitazama Tena
Na Tena
Mmh!




Uwii! Akapiga mluzi

Kisha akatikisa kichwa

Alafu akaninyoshea dole👍👌 ishara ya kwamba Mali ipo perfect

Weuweee😂💕 na pesa akatoa, laki tatu na nusu.

Dah!


 


Asante, akatamka

Kisha MANZI akasepa

Mimi chini puu! Kama nimepata Stroke.

Ndu ndu ndu ndu, mapigo ya MOYO

Kazi zetu hizi zina changamoto

Kubwa Sana na nzito


Mtu Hana mdomo lakini anaongea

Hana pua lakini anapumua

Hana macho lakini anaiangalia photo 


Naogopa kusahau Ili tukio maishani mwangu.

No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...