Friday, October 25, 2024

SINGO MAMA MPAMBANAJI.

 


    DONT TRY TO MESS WITH SINGLE MAMA.

Miaka miwili iliyopita mie Belinda nilitengana na James Mume wangu wa ndoa niliomba talaka kinguvu maana hakuwa tayari kutengana na mimi. Sababu kuu ya kutengana na James mwanaume awezaye kuniridhisha kitandani (Nilimpendea sana kwenye tendo.) alikua ni mlevi na mvivu, mlevi yaani mlevi nyoko akiaanza kunywa pombe asubuhi na kumaliza atamalizia jioni, ukimuona huwezi kumtambua kama ni yeye maana ujigaragaza topeni sio kwa aibu na fedhea ile.


     Alikua ni mvivu hataki kufanya kazi yoyote ile, mwanaume kutwa kuchwa alijifungia chumbani akikiroma 'ngrooo ngrooo ngruuu' ๐Ÿ˜ด๐Ÿ˜ชkwake usingizi ulikuwa kama chakula na aliupenda sana usingizi kuliko Binti zake wawili wadogo Jena na Mariamu. Mwanaume alifanya kazi ya kulala tu, pesa ya chakula hakumbuki ni lini mwisho aliitoa zaidi ya kuitoa mie mwanamke. Haya Sasa ninaitoa kutoka wapi!? Shuhuli na vibarua vidogo vidogo nilivyojishuhulisha.


    Ila ni jambo la kumshukuru Labuka maana baada ya James kufukuzwa kwangu akapunguza sana ile tabia yake ya kunywa pombe akapunguza ulevi nyoko akajikita kazini angarau apate pesa ya kula, ubaya wake hakuleta pesa za matumizi ya watoto nyumbani. Basi mwanamke nikapata akili ya kujbidisha Mimi mwenyewe kufanya vibarua vidogo vidogo vilivyonipa vijisenti vya kuwanunulia watoto mahitaji yao ya kila siku.


     Mara Leo niitwe kulima au kupalilia shamba, mara niitwe kupika au kusafisha vyombo maharusini na kwenye shuhuli mbalimbali, siku zingine nilipigwa Simu na mabosi wakubwa nikasafishe Ofisi, nyumba  au kuwafulia nguo lukuki. Belinda mie nilikua kiguu na njia ilimradi nipate tonge la ugali na jinsi watoto wanavyosumbua, du! Kuwa Singo Mama yataka moyo.

    "Mama Leo twaweza kwenda Kigamboni Beach."Jesu! Huko Kigamboni Beach kwani mtu anaingia Bure!? Mwendo wa pesa, tulienda angarau Beach za Bure.

   "Mama Leo pika Pizza na Baga." Toba! Watoto Hawa wanalilia vinono na vitamu. Lakini singo mama mie nilijitahidi kufanya watakacho.

**********

        Basi mie Singo Mama nilikua najiandaa kutoka nyumbani kwangu, October ya tarehe kumi nilipigwa Simu na kibosile fulani huko Gogolamboto kwenye birthday ya mwanaye. Mie nikapike na kupakua mahanjumanti, manono na manonozi. Tajiri aliniahidi  kitita cha shilingi laki Moja kama malipo ya shuhuli nzima ya kupika na kupakua.

        "Belinda Jirani wa mie." Sauti ya mwanamama  iliniita niligeuka na kuacha kutembea mtaa wetu wa Segerea

    "Abee dada" Nilimwitikia MAISHA, Maisha ni Jirani wangu mgeni na mpya katika mtaa wetu amehamia hapo yapata miezi SITA iliyopita na tushamzoea. MAisha kama watu wengi wanavyomwita MASHA P. DIDY (nicheke mie๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿ‘Œ) nisijue hilo jina wenyewe wamelizoa wapi? Anapenda starehe kila siku, kila wiki, na kila mwisho wa mwezi. Kwenye nyumba aliyohamia utasikia mapigiti ya Muziki mnene wenye sauti ya juu. Huyo Masha anafanya sherehe za kula na kunywa  kila mara ndani ya mtaa wetu wa Segerea

    "Nakuona una haraka Dear Kuna jambo naomba tuongee" Mh! Niliguna nikasimama nimsikilize au anataka kunialika kwenye hizo party za kula kunywa na kumwaga pesa.

    "Sina haraka Dear Nashukuru kama Kuna jambo nono unahitaji kuniambia." Nilijishebedua hamu na shauku ya kujua.

    "Dear, Nyumba yangu ipo chafuu chafukoge haitamaniki. Jana tumethrew part la nguvu, watu wamekula, kunywa na kufanya vurugu"Aliongea huyu Jirani ambaye nimesikia tetesi zake watu wengi wananiambia: 'Shuhuli yake ni kuomba omba misaada kwenye mashirika ya Dunia akisingizia ati anaipeleka hiyo misaada kwenye vituo vya watoto Yatima na wale wanaoishi kwenye mazingira magumu.' Teh teh teh๐Ÿค“๐Ÿ˜น nacheka kama mazuri. Sijui hao wanaokula, kunywa na kufanya vurugu ndio Yatima na watoto wanaoishia kwenye mazingira magumu? Mh! I don't know,

       "Ndio Dear hapa umefika lazima nikusikilize" nilisimama kumsikiliza.

       "Naomba Leo uachane na shuhuli yoyote uliyonayo ninahitaji mtu wa kunifanyia usafi nyumbani kwangu nipo tayari kukupa shilingi laki tano mara baada ya kazi kukamilika' Kabla sijakubali au  kulikataa Lile donge nono Masha alichomoa funguo za nyumba yake anayoangushia Party kila wiki.

    "Oh! Dear kwanini tusifanye kesho maana Leo nina shuhuli ambayo sipaswi kuikosa." Niliongea lakini moyoni nikizitamani zile laki tano mashallah!

   "Jirani, nyumba yangu itaoza na kuharibika ukitegemea siku mbili zijazo ninategemea kuwapokea wageni kutoka Ulaya Kuna mambo fulani ya Documentary nahitajika kujaza na kuita Saini yangu"MASHA P. DIDY alinibembeleza.

   "Ok Haina tabu nipo tayari kukusaidia.Vipi kuhusu malipo, ingekuwa vizuri uniachie Advance"

   "Usijali wewe fanya usafi Kwa siku mbili tu Kisha suala la malipo nitakupatia  ukimaliza kuwajibika. Uzuri ni kwamba ndani ya siku hizi mbili sintakuwepo nyumbani basi fanya kuitawala nyumba yangu iwe kama yako." Aliniambia nikapokea funguo ya nyumba yake na kuahirisha Safari yangu yenye faida kiduchu nikakimbilia ile yenye donge nono.

*******

         Mmh! Mazingira niliyokutana nayo ndani ya nyumba ya Masha P DIDY  Mama ya starehe mbona niliyaogopa Tena ninaogopa hata kusimulia kila sehemu ya ile nyumba ilikua chafu tena chafu zaidi ya chafu. Sebule nzuri ilibadirika na kuwa pambo la mabakuri machafu.  Mabirauli machafu, makopo  na chupa zilizotumika usiku wa Jan.  Vyakula vilimwagwa kila Kona ya ile nyumba kuanzia kwenye Masofa, kutani  jikoni huwezi kuamini hata ndani ya choo kulitisha Kwa matapiko na vinyesi vya hao watu waliokuwa wakafanya starehe ambazo hata sikuzijua zaidi ya furaha ya kula pesa za Mashirika, Makampuni na Wadhamini,

     Pombe pamoja na mabaki ya chupa za pombe zilinitibua. Nilijiuliza naanzia wapi kufanya usafi? Tisa kumi sikufahamu zaidi ya ya kufagia sebule iliyoharibiwa Kwa chupa zenye kilevi, nilipomaliza kuishuhulikia ile sebule nikaanza kukusnya vyombo na mabaki ya vyakula kisha nikaanza kuvikosha vyombo vingi sana, yamkini watu Mia walifanya Party ndani ya lile lijumba likubwa. Sikuchoka tu bado nilifahamu Kuna kukosha masofa, vitanda, mashuka n mablanket mazito.  Kazi ile nzito ilinichukua zaidi ya siku mbili kuimaliza

      ilikua ni kazi nzito kidogo nilipoa baada ya kubeba manyaji na vyakula ambayo havikuharibika nikawapelekea wanangu. Baada ya siku mbili za kazi mwenye mali alirejea kimya kma MAJI mtungini, hakunitafuta wala hakutuma mtu aje aniite sembuse anifate. Kwa ustaarabu wa kudai CHANGU nikamwendea Ili kumkumbusha kuwa ahadi ni deni na deni lazima lilipwe.
    
      "Nini?" Unanidai shilingi laki tano Kwa kazi Gani haswa?" Eh! Masha huyu vipi!?" Maswali Gani Tena haya au ametumia dawa za kulevya zilizompu,mbaza?

       "MAISHA au umelisahahu donge nono uliloniahidi kunipa baada ya shuhuli hii nzito inayochosha na kuumiza mikono, mgongo na mwili wangu? Kumbuka ndani ya siku mbili hizi mie nimekosa usingizi" Nilimkumbusha

    "Belinda  wewe ni mtu mzima Tena mwenye akili na kumbukumbu, nilipokuja kwako nilikuja kuomba unisaidie kufanya ile shuhuli 'FREE' bila malipo. Sasa ilo donge nono la shilingi laki tano umelitoa wapi?" Makubwa! Masha huyu huyu aliyenibembeleza nimfanyie usafi Leo hii anakuja kuniambia aliniomba nimfanyie ile kazi free huo muda wa kumifanyia kazi free nitautoa wapi mie Singo mama ninaye waangaikia wanangu waupate ugali na tembele?
   
       "MAISHA naomba usijitoe akili na ufahamu yaani ile kazi nzito ya  kuchomwa na chupa zilizovunjika, kuzoa matapiko na makombo ya walaji, kusafisha vinyesi  vilivyotapakaa hadi jikoni utafikiri wanyao hivyo vinyesi ni Kuku na nguruwe. Nimekuoshea Masofa yote, Mablanketi, Mashuka, Vitanda yaani hadi kuisugua Dari ya nyumba yako Leo hii unakuja na Motion  inayoitwa FREE ." Nililalamika,`

       MWANAMKE UNAPASWA KUWA NA HURUMA JUU YA MWANAMKE MWENZIO ANAYEJITOA KUKUSAIDIA. NImeumia sana Masha, kichwa changu kilichoka kujitwika maji ya kisimani, hadi Leo hii bado ninaumwa kichwa na mgongo alafu wewe unakuja na Mada inayoitwa Free,"Huruma hizo siziwezi. Niliongea

     "Bwana we fanya mambo yako, embu nipishe nipite na uniachie niende." Masha aliingia ndani ya Gari yake Kisha akaikoki na kuondoka kwa Kasi huku nyuma akiacha sauti kubwa ya kiicheko chake . Teh teh teh ๐Ÿ˜น๐Ÿ˜น๐Ÿ˜น. Nilifura Kwa hasira. nikaona hizi sasa hii ni dharau na dhuruma. Singo mama mie sipaswi kucheka na Binti ambaye anapaswa kuniita Dada. Je, alipanga dhuruma hizi tangu awali? Je, ndio mchezo wake mchezo wa dhuruma? Ndivyo anavyowafanyia hao Wadhamini wenye Mashirika na Makampuni anayoomba misaada ya kuwasaidia  watoto yatima na wale wanoishi katika mazingira magumu? Kwa hiyo hayo mazingira magumu ndo' yale ya kurusha part  za  kunywa na kula kisha kuchafua nyumba? Hapana, kama ni kumharibia issue zake sipo tayari lakini ngoja Sasa ngoja tuone nitakavyomfanyia kitu kibaya. Atanikoma na kunikumbuka, atakumbuka neno Moja la kizungu "DONT MESS WITH SINGO MAMA"

    "Yes!" Nilitabasamu. 

    "Si funguo za nyumba yake kaniachia! Ah! No kazisahahu. Nilipata akili ya kuzaliwa. 

     "Haya  tuone Sasa si yeye SINGO Dada, tapeli mpenda starehe na Mimi ni ni SINGO mama mpambanaji na mpenda haki. Nilitamani kufanya sherehe hata kabla sijatimiza biashara yangu.

    Nikafanya hima kwenda Sokoni kununua Viroba karibia kumi na Tano Kisha nikakodisha Gutta baada ya kupata vitu hivi muhimu kwangu nikakimbilia Dampo la Tabatha huko nikaanza kuchimba na kuchimbua kila aina ya taka taka, uchafu na ujinga.

 Maganda ya ndizi zilizooza, maparachichi yaliyooza, maembe yaliyooza. Pedi zenye vinyesi vya watoto. Mifuko iliyooza na ile yenye vyakula vilivyooza tena Uzuri hata zile chupa na sahani zilizovunjika nilizoziondoa nyumbani kwake bado zilikuwepo Jalalani. Sikusahau vinyesi vya wanyama pusi na umbwa ng'ombe na nguruwe. Usiniulize nilivitoa wapi maana SINGO mama mpambanaji ninalijua vizuri Jiji na vijiji.

 Kwisha kukamilisha zoezi la zoa zoa nilihakikisha ninapita NJIA ambayo hakuna mtu angeliniona. Napita vinjia na vichochoro vya kuelekea nyumbani Kwa MAISHA. Nilipofika nyumbani Kwa MAISHA nilianza kazi ya kurenew kile kilichopotea. Teh teh teh๐Ÿคฃ๐ŸคฃUfunguo nilikua nao basi nikajifungia ndani Mimi na Viroba vyangu na magunia mazito yenye uchafu, kilichofuatia sidhani kama kuna haja ya kusimulia.

        Nilipakaza vinyesi vya wanyama kila chombo kilicho kabatini mwake, nilipakaza vinyesi vya wanyama Jiko lake lote. Kuta za Jiko na Kuta za choo chake cha ndani nilipakaza matunda yaliyooza na kutoa wadudu Nilipakaza mashuka yake yote meupe pee. Nilipakaza kwenye masofa, mapazia vitambaa hata juu ya Dari. Sikuchoka bado tu nilisambaza yale mabakuri na shahani chafu juu ya meza yake. Pedi za watoto, chupa na takataka kibao nilisambaza sakafuni kwake. Nyumba yake ilitisha mfano wa HALF HELL nusu Jahanamu. Kwisha kumalizia ile shuhuli nikaufunga mlango mkuu wa kuingilia SEBULENI, Ufunguo nikaupachika chini ya kapeti dogo la kuingilia ndani likiwa limeandikwa Wellcome Guest.

Ingawaje mtimani niliumia kumfanyia Jirani yangu UBAYA UBWELA lakini  nilipaswa  kujipongeza sababu yeye binafsi amenidharau. Mie huyo nikarejea nyumbani kwangu kukoga na kuwapikia wanangu vinono nilivyobeba kutoka Kwa Tapeli wangu MASHA P DIDY. Vilikua vinono kweli, Kuku wawili wakuba, debe moja la mpunga, lita tano za mafuta bila kuhesabia unga na spices mbalimbali za mboga

**********

 'Ngo ngo ngo' Wanangu walishituka na mie pia nilishituka
   
      "Belinda tafadhali naomba Ufungue mlango" Sauti ya MAISHA iiliunguruma Kwa hasira NILIENDA KUUFUNGUA MLANGO WANGU.

      "Gonga Kwa ustaarabu tafadhali. Hii ni nyumba yangu Wala sio choo"Nilimkaripia MAISHA ambaye alitibuka akafura Kwa hasira hasara, hasira za mbogo alojeruhiwa.

   " Ndio Nini ulichonifanyia Belinda?" Aliniuliza

     "Kwamba nimekufanyie Nini?"Nilirudisha swali.

     "Ina maana huelewi jinsi gani umenichafulia nyumba yangu na kuniharibia"Alinipigia kelele.

     "Una uhakika kwamba ni Mimi ndiye niliyekuchafulia nyumba yako?"Nilimtupia swali.

   "Kwanini nisiwe na uhakika ikiwa wewe ndiye uliyenifanyia usafi na wewe ndiye ulierejesha uchafu ndani" Aliongea mate na povu likimtoka mdomoni. Mie sikutetereka nilimjibu na kumuuliza kadri alivyoniuliza,

     "Tafadhali naomba uondoke nyumbani kwangu mambo ya hisi na hisia za kufikirika siziamini wala sizikaribishi nyumbani kwangu"  Nilimtaka asepe.

     "Belinda I will call Police, nitaita police"

    "Ita Bibi ita hata Sasa chukua simu yangu ita" Nilimpa simu yangu.

    "Ita Tena waambie Belinda amenihujumu.  Wakikuuliza aliingiaje nyumbani kwako utajua jinsi ya kuwajibu maana mie hata Ufunguo wa Nyumba yako sina tena siujui "Niliongea maneno yaliyomfanya MAISHA aondoke Kwa hasira.

    Teh teh teh ๐Ÿคฃ ๐Ÿคฃ ๐Ÿคฃ ๐Ÿ˜˜ Sikuogopa wala sikutishika. Unadhani hao  POLISI waliitwa? Waitwe wapi? MAISHA alipata funzo. Siku  ile nililala salama salimini  mie na wanangu. Nina Imani hawezi tena kuja kuniita nimfanyie kazi Free ya bure bin utapeli.

************

DONT MESS WITH SINGO MAMA WEWE ๐Ÿ”ซ

..................

TCHAO

DNA TEST

 


TEST YA DNA

ILIVYOMPONZA BIBI MAMA MKWE

       "Mama anaendeleaje?Anasemaje pia? Naomba msalimie mwambie nimampenda sana" Hii ilikua ni kauri yangu ya kila siku niliyomwambia mchumba wangu Jese. Wakati huo tupo University collage.

      "Mama hajambo, anakupenda sana na pia anatamani siku moja akuome na akufurahie"Jese aliongea Kwa furaha Lugha tamu masikioni. Nilikua ni mwingi wa tabasamu Nilifurahia pia nilijiona kama Nina bahati ya kupata  mchumba mzuri kama Jese. Basi mie nikasubiri sana siku njema ya kuonana na Mama yake Jese. Na ikawa kweli Jese akanikutanisha na mama yake aliyenipenda ghafla akanipokea Kwa mikono miwili na kunikaribisha chakula Cha usiku yaani Dinner na mara nyingine aliniomba nimsindikize Supermarket kununua bidhaa.

       Uchumba wangu mie na Jese hatimaye ulikuja kuzaa harusi kubwa ya furaha ambayo baadaye harusi hiyo ikafanya ndoa ambayo ilikuja kuleta matokeo Lukasi wanangu wa kwanza alizaliwa. Ilikua ni furaha tele kwetu kumkaribisha Lukasi mbarikiwa wetu lakini ajabu ya furaha yetu Bibi mama Mkwe yaani Mamaye Jese hakufurahia ujio wa yule mtoto.

      "Nina wasi wasi sana na ujio wa mtoto uliyemleta nyumbani."Bibi mama Mkwe  aliongea Akimaanisha ana wasi wasi na ujio wa Mwanangu Lukasi.

      "Wasi wasi Gani Mama?"Nilimuuliza Bibi mama mkwe ambaye Kwa kumsoma usoni alieonekana kutokuwa na furaha

     "Mia ina maana kusoma hauwezi hata picha kutazama hautazami?"Sikuelewa swali lake lakini Kwa upole na Kwa busara Nilimjibu.

    "Sijakuelewa mama tafadhali naomba ufafanue."

      "Mia, Tazama kucha za Lukasi kucha za Lukasi hazifanani na kucha za Babaye Jese. Macho ya Lukasi Yana rangi ya Paka wakati Babaye ana macho rangi nyeusi Nywele za Lukasi ni nywele zenye Ualibinio yaani za Kaki wakati Babaye nywele zake ni nyeusi. Sasa  unataka kuniaminisha Nini hapo?" Bibi mama Mkwe alitoa ya moyoni.

       "Mama nawe" Nilicheka kidogo "Hayo ni majaliwa  watoto wote ni Mali ya Mungu." Niliongea bila kujua kama nnamkasirisha.

      "Tafadhali Mia naomba tuongee kama watu wazima, kila nikizitazama picha za mwanangu Jese na picha za mjukuu naona kama wawili Hawa hawaendani.Lukasi hajabeba appearance ya Jese Je unataka kuniambia Nini hapo?" Aliniuliza.

    "Kha! Mama ya kale hayanuki na yalopita sindwele tuyangoje yajayo."Nilizidi kumfumba Bibi mama Mkwe. Moyoni nilijisemea 'Bibi anatania hili nalo ltapita'
Lakini kumbe nilijidanganya ikawa kila ikiwa Leo Bibi mama Mkwe lazima  amkague mwanangu na kuanza kumkosoa Kwa nguvu ya ile Topic yake ya 'Lukasi hajafanana na Jese.' Uvumilivu ulianza kunipiku nikaingia wasiwasi juu ya kelele za Bibi mama Mkwe.
.........

     "Au ulichepuka Kwa bahati mbaya Mia?Nina wasi wasi na mtoto huyu unayesema ni mtoto wa Jese mwanangu. Sura ya mtoto, meno na hata tabia yake sio vya Jese." Alimkosoa mwanangu mwenye umri wa MIAKA Miatano

      "Mama tafadhali Topic ya kumjadili mwanangu naomba sana ife.'Jese Mume wangu alinitetea, tukiwa mezani twapata Dinner.

    "Mia ndiye anayemjua Baba wa huyu mtoto na huyu mtoto ni wangu fullu stop!" Jese alimkemea Bibi mama Mkwe.

     "Jese usimkemee Bibi Mama Mkwe."Nilimuonya Jese ambaye alikua akila chakula kilichokataa kupita kooni.

    "Uzee ni dawa mwanangu Jese, ishi kwingi uyaone mengi. Nakwambia ipo siku utakuja kuniambia juu ya ukweli wa huyu mtoto unayedai ni mwanako."Bibi Mama Mkwe alipalia makaa.

   "Ukweli Gani? Kitanda hakizai haramu Mama.Mimi ndiye ninaye lala na Mia na Mia analala na Mimi. Mia ananijua na Mimi ninamjua vizuri, hajawai kunisaliti sembuse kutamani kulala nje"Jese alinitetea Bibi mama Mkwe alikasirika akaacha kula chakula cha usiku ule akafanya kueleka chumbani kwake akajibwaga kitandani akiwa ni mwingi wa hasira. Mie na Jese Mume wangu tulimshangaa.


   ###

Siku ziliendelea kusogea Wala hazikukoma Bibi Mama mkwe aliendelea kupiga kelele juu ya mwonekano wa Mwanangu Lukasi Tena safari hii akaanza kufanya vitimbi na Mikasa ya hapa na pale. Nilipomwita Mezani akuje tujumuike pamoja chakulani lakini Mmh ! Bibi mpMama mkwe alinishangaza sio Kwa mgomo ule. hAKUTAKA KULA CHAKULA NILICHOPIKA ZAIDI YA YEYE KUINGIA JIKONI NA KUJIPIKIA. ZAMANI NILIKUWA NA KAWAIDA YA KUMFULIA NGUO LAKINI TANGU AMESHIKILIA TOPIC YAKE  NA HISIA MBAYA JUU YA MWANANGU ALIGOMA MGOMO MZITO TENA HAKUTAKA NISHIKE NGUO ZAKE BAYA ZAIDI HAKUTAKA KUONGEA AU MIMI KUMUONGELESHA, KILA WAKATI ALINUNA.

     "MAMA NAOMBA UKUJE SEBULENI TUANGALIE TAMTHILIA" NILIMWITA.

    "NENDA MITAANI KAWAITE NA KUWAKUSANYA MAALIBINO MUANGALIE HIZO TAMTHILIA ZA KUCHEPUKA." Alinijibu Jeuri. Nilifadhaika nikawa ni mtu wa mawazo na kilio. Nikakonda na kudhoofika lakini Uzuri Mume wangu Jese hakunitupa mbali alinifariji pia alimuya mamaye juu ya kauli zake zinazoumiza na kuchoma MOYO."

    "Nilikuwa nakuona kama Binti mmoja safi sana  zamani lakini kumbe Malaya mchepuko. Umemzalia mwanangu damu haramu Kisha umeamua kumpumbaza na kumuaminisha kuwa huyo mtoto aso riziki ni wake Jese" Jesu! kauri za Bibi Mama mkwe zilifanya niague kilio kikuu kilio cha Mwendawazimu. Niliiona Dunia chungu Tena nilijuta na kutamani kuondoka pale nyumbani, lakini ningelienda wapi mie Mia mama Lukasi?

   Bibi Mama Mkwe akaendeleza Libeneke akilalamika ati mtoto Lukasi kamwe hafanani na Babaye Jese Safari hii akaja na Topic mpya Lazima Lukasi afanyiwe Partenity Test Yaani DNA ili ijulikane kama mtoto Lukasi ni wa ile familia au la! Nilimsaliti mume wangu.

       Wee! Nilikubali !?? Teh teh teh ๐Ÿ˜„๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚ Niligoma na kukataa katakata nikamwonya Bibi mama Mkwe Kwa kumwambia kama yeye haniamini basi Mume wangu Jese ndiye wa kuniamini maana yeye ndiye aliyenioa na nyumbani kwetu sikutoroka nije kulazimisha kuishi na yule kikongwe.

    Akatilia mkazo na usumbufu wake ukapamba moto hatimaye Jese akanibadilikia akageukia upande wa Bibi Mama Mkwe akamsikiliza mamaye, akazisikiliza kelele za Bibi mama Mkwe.

    "Ina maana na wewe hauniamini Jese? Hauamini kama Lukasi ni mtoto wa damu yako?" Nilimuuliza Jese.

   "Sio kwamba sikuamini Mia Nina kuamini sana Tena sana lakini makelele ya mama ndiyo yanayotunyima Raha ya usingizi wetu. Kwanini tusikubali kuichukua DNA test tumridhishe aridhike?"Jese aliongea.

    "Tumridhishe mama yako kwani mama yako ndiye aliyekuzalia mtoto?" Niliuliza nikiwa na hasira shingoni

    |"Mama yako alikuzaa wewe na wewe umemleta Lukasi hakuna different this is your blood kid, niamini tafadhali," Nikiambembeleza machozi yakinitoka.

   "Kubali Mia" MUME WANGU ALINIBEMBELEZA PIA, MOYONI NILIWAZA kwanini Bibi mama Mkwe ananifanyia hivi? Je, haoni kama anataka kuibomoa ndoa yetu? Je, haoni kama anaweka nyufa juu ya penzi la Mimi na mwanaye Jese? Kwanini anaingilia MAPENZI yasiyomuhusu? Je, anafikiria Mimi ni sawa sawa na Wanawake wapumbavu wanaoishia KUCHEPUKA na kuharibu ndoa zao."Nililia, nikakonda na kudhoofu.


####

     Jese alimwita Dakta wa familia, Dakta Ayubu. Dakta Ayubu akamchukua Jese pamoja na Lukasi  kwenda  Hospitali kuchukua Sampuli za damu  pamoja na nywele zilizofanyiwa vipimo. Huku nyuma mie Mia nilikua katikati ya Depression, kukonda na mawazo kunisumbua. Kichwa kilikua na wazo Moja tu Kuomba talaka, sikupendezwa kuona Bibi Mama Mkwe anaingilia ndoa yangu. Sikupendezwa kuona Jese anafuata wazo ambalo sikuona umuhimu wake, Lakini Jese angelifanyaje? Alipaswa kuheshimu mawazo ya Mama yake.

      "Hallow Mia!"Mchana wa siku ile Jese Alinipiga simu.

        "Hallow! My Husband" Nilimwitikia.

        "Majibu ya DNA test tayari yamekwishatoka

        'Eh! Nakusikiliza" nilimwambia.

       "Lukasi ni mwanangu na ni damu yangu kabisa,"Jese aliongea.

        'Bila shaka umefurahia."Nilimwambia.

         "Itisha kikao, tupo njiani kuja huko Mimi, mwanangu Lukasi pamoja na Dakta Ayubu.  Mwambie Mama qkae mkao wa kula kuyapokea matokeo"Jese aliongea.
           "Sawa" Nilimjibu. Kisha nikamwita Bibi Mama mkwe mwanamama anayeninunia na kunichukia, nikamweleza awe tayari  kikaoni KUYAPOKEA majibu ya DNA test. Walengwa walifika kikaoni wakaketi SEBULENI, Mie Mia niliyekonda na kudhoofu Kwa kelele na gubu la Bibi Mama mkwe, Jese Mume wangu, Bibi Mama Mkwe, Lukasi mwanangu pamoja na Dakta Ayubu  Dakta wa familia. Kisha Dakta akasimama kueleza matokeo ya DNA test.

        "Vipimo vya DNA TEST VINAONESHA KUWA LUKASI NI MTOTO WA JESE yaani Original copy." Dakta aliongea.

           "Damu ni ya Jese macho, pua, mikono, nywele na miguu ni ya Jese."Ayubu aliongea.

     "What!? I cant believe it."Bibi Mama Mkwe alitokwa macho pima.

          "Ndo hivyo Bibi hata tukijaribu kwenda Hospitali mia Bora za Dunia bado tu Lukasi atabaki kuwa damu ya Jese" Dakta alieleza

         "Lakini mbona mtoto hafanani na Jese?Nywele za kialibino, pua, macho, mdomo, kucha na hata tabiaau matendo ya Lukasi ni tofauti na Jese mwanangu?" Bibi  Mama Mkwe aliuliza.

        "Swali lako zuri sana Bibi, Kuna matokeo ya pili baada ya kufanya uchunguzi wa DNA test. Tumeangalia Vinasaba  yaani Heredity na Jeni upande wa mama mzazi wa Lukasi yaani Mia na upande wako Bibi Mama mkwe matokeo yetu yakaja kuonesha kuwa LUKASI ana Jeni nyingi kutoka upande wako wewe Bibi mama Mkwe" Dakta aliendelea kudadavua.

      "Mjukuu wako Lukasi amechukua vitu vingi kutoka upande wako, mjukuu wako Lukasi  amechukua vitu vingi kutoka kwa Babu aliyemza baba yako wewe Bibi mama Mkwe, nywele hizi za kialibino nywele ambazo hakuna mtu katika familia hii anazo ni nywele ambazo Babu yako wewe Bibi mama Mkwe alikua anazo. Sura kucha, midomo, pua na hata matendo anayoyatenda Lukasi yalitendwa na Babu yako wewe Bibi Mama mkwe. Yamkini  hujapata kumuona au kuijua Historia ya Babu aliyemza baba yako "Dakta Ayubu alihitimisha. Bibi mama Mkwe alitazama chini Kwa Aibu.

          "Mama "Jese alimwita Bibi Mama mkwe.

           "Tafadhali naomba uingie chumbani kwako, ubebe kila kilago au kikolokolo na kikolombwezo chako Kisha  uondoke nyumbani kwangu"Jese alimwambia mama yake.

         "Jese my son!" Bibi Mama Mkwe alitoa macho kama Jusi lililobanwa mlangoni.

        "Unanifukuza niende wapi mwanangu?Nirudi kijijini kulima? Kumbuka Mimi ni Mama yako." Bibi mama Mkwe aliteta.

      "Tafadhali mama ninakupa dakika Tano tu uingie chumbani ubebe kila kilicho chako uondoke" Jese aliongea Kwa hasira mie Kimya Wala sikumtetea Bibi mama mkwe.

      "Nisamehe Mia, Nisamehe Jese."Alitia huruma
      "UMEMVUNJA MOYO MKE WANGU UMEMUACHIA DEPRESHENI, STRESS NA MAWAZO LUKUKI YAMEMNYIMA HAMU YA KULA AU KUNYWA. JE, ULITAKA AFE? Tafadhali beba kila kilicho chako Kisha uondoke"Jese hakutania Bibi Mama mkwe akatoka chozi Kwa Aibu na fedhea aliyoipata. Akaelekea chumbani kwake akabeba vilago vyake akatoka ndani ya nyumba. Kwani nilimsindikiza? We koma!๐Ÿ‘‰ ๐Ÿคฃ๐Ÿ‘ŒWacha aondoke na nyumba  yetu ianze kutabasamu sio Kwa gubu na mnuno ule.

>>>>

        "Nisamehe Mia, nisamehe mke wangu nilifanya vile kumridhisha mama yangu''Jese aliniomba msamaha.

       "Nilivunjika moyo Jese, nilipoteza Imani na ilibaki kidogo NIOMBE talaka yangu" Nilimwambia ukweli Jese

    "Naomba usiniache Mia niruhusu nitafute Mwanasaikolojia au msuruhishi wa ndoa atuweke sawa kiushauri"Jese aliongea.

       "Wazo lako zuri" nilikubaliana na Jese Mume wangu Kisha nikamsamehe. Nilisamehe maana mawazo ya kutaka kuondoka ndani ya nyumba ile yalinisumbua.




<<<<<<<<<<



 TCHAO

Tuesday, October 22, 2024

FAKE DEATH

 






MWANANGU NA BOYFRIEND WAKE WALIFEKI VIFO LAKINI KILICHOMKUTA MWANANGU MBONA ALIJUTA.

     'Ajali?" Niliuliza Kwa Mshangao mkuu siku ile nilipoletewa taarifa zilizoushitua MOYO wangu.

     "Ajali mbaya sana mama, ajali imetokea Buguruni Malapa Lisa bintiyo na Dani Boyfriend wake wamekufa VIFO visivyotamanisha kuona MACHONI,"Mleta taarifa alifanya MOYO wangu uende mapigo na Kasi ya ajabu.

     "Lisa amekufa, Dani pia? Siamini."Macho yaliniwasha na kunitoa machozi.

      "Mama Lisa ina maana hata taarifa ya habari ndani ta TBC hujaiona sembuse kuisikia. Ninaposema hawatamaniki Nina maanisha hawatamaniki kabisa, Miguu Imekatika, mikono imekatika, viwili wili vimetupwa kule, sura zao hazitambuliki zaidi ya vitambulisho vyao na nguo walizovaa siku ya Leo."Mleta habari alinidodosa habari iliyonifanya nitoke machozi na kulia kilio kikuu

      "Lisa mwanangu Lisa ndoto zako za kwenda University zimemezwa na ajali iliyotoa uhai wako na WA boyfrendi wako Dani "Nililia Kwa uchungu.

       "Pole sana ama Lisa."Mtoa habari alinifariji wakati huo huo marafiki, majirani na watu wengine walimiminika nyumbani  kwangu kuja kunipa pole na KUFANYA matanga. Masikini mie Selina mamaye Lisa nilikuwa katikati ya maumivu kusikia habari hizi za kuumiza MOYO. Kupoteza yule nimpendaye yule niliyemtoa tumboni kwangu. Walahi! Mbona niliumia. Sijui upande wa Dani Boyfriend wa Mwanangu Lisa ninajua na wao pia waliumia.

******
Tulianika matanga, miili ile ambayo tulishindwa kuitambua zaidi ya vitambulisho na mavazi ya Lisa na Boyfriend wake ilizikwa makaburi ya Kisutu, sie tuliewapoteza tuwapendao tulilia usiku na mchana, tukaomboleza juu ya VIFO vya vijana wetu tuliowapenda.

        Siku sio nyingi mara baada ya kuanua matanga nikavamiwa na kampuni iliyojiita KAUSHA DAMU kampuni hii iliniletea madai kwamba Lisa Binti yangu pamoja na Boyfriend wake Dani walikopa mamilioni ya fedha za kampuni Kwa lengo la kwenda kuzitumia waendapo Chuo. Baya zaidi upumbavu wa marehemu Binti yangu Lisa aliwekeza nyumba yangu kama dhamahana.

     Uwii! Mbona nilichanganyikiwa, kichwa kiliwaka mfano wa kifuu Cha nazi. Nilipagawa na kuvurugwa. Siku chache zilizopita nilimpoteza wangu nimpenaye Leo hii naletewa habari nyingine ya kupoteza nyumba yangu. Hapana nitapigana kijike jike. Nilijiambia.

Haraka nikakimbilia mahakamani lakini huko Nako nilidodakea pua, nilibaki rojorojo, dikodiko, mlenda mtupu.Tena Kwa Aibu nzito nilishindwa na nyumba yangu ikapigwa mnada nikiingalia inavyonitoka PASINA kupenda. Nililaani, Nikabwata kwanini Dunia Haina huruma?



###########

MIAKA SITA BAADAE

Serina mie ni Mwalimu yaani mwajiriwa wa Serikali. Basi siku Moja nikapewa barua iliyonitaka niende Arusha  kwenye Semina na mafunzo Fulani ya kunijenga kitaaluma. Siku ya siku Safari yangu ilipamba moto hata Lile tukio la kuuza nyumba yangu MIAKA misita iliyopita nilikwisha aanza kulisahau ingawaje moyoni nilibaki na maumivu ya Lile tukio la kufiwa na Binti yangu.๐Ÿฅฒ๐Ÿ˜ฅ๐Ÿ˜ช

      Nilifika Arusha mjini salama salimini nikalipia HOTELI Moja ya kifahari maana mshiko wa nguvu niliukamata kibindoni. Nikiwa mapokezi kulipia gharama za HOTELI ghafra Kwa mbali  kidogo macho yangu yasiyo na pazia yaliona  vijana wawili mmoja wa kiume na mwingine wa kike wakiwa wanakula Raha za ujanani, wakilishana yakula vinono na vinywaji vya bei gharama.

       Chale Fulani zilinicheza machoni  niliwatazama wale vijana hisia zangu zikaniambia mmoja wa wale vijana ninamfahamu  au nilimwona pahali! Lakini wapi hapo? Sikupata jawabu. Nikajishauri niwache mizigo yangu mapokezi nikawaone wale wawili waliokuwa wakiyashambulia manono na manonozi. Nikawasogelea

          Jesu!  Nilishituka niliogopa pia nilihisi ni jambo la kutisha machoni . Bado niliwatizama wale vijana wawili mwanaume na mwanamke macho hayakunidanganya na MOYO pia haukunidanganya niliwafahamu vizuri wale vijana wawili

         "Lisa" Niliita yule Binti aliyekua akilishwa na mwanaume chakula. Aligeuka na kunitazama. Hofu ilimuingia  Lisa ghafla akadondosha kijiko alichokua anakitumia kula chakula akantazama Kwa woga Dani pia alinitazama Kwa woga.

        "Lisa its you, ni wewe!?" Nilihoji kwa mshangao.

         "Dani naomba tuondoke."Lisa alimwambia Boyfriend wake ambaye bila kupoteza muda alisimama ili waondoke

         "Tafadhali msiondoke nisije nikaita POLISI." Niliwpigia kelele wakasimama wanaangaliana Kwa hofu na kutetemeka.

         "Hapana Mama usiite POLISI tutaeleza." Lisa Binti yangu aliyetangazwa ameaga Dunia MIAKA SITA iliyopita aliongea.

       "Si nyie mliaga Dunia MIAKA SITA iliyopita?" Nilihoji.

        "Nyie ndio mliotangazwa kwenye Radio, Television na mitandao ya kijamii kwamba mmekufa? Leo naota ndoto au?' Nilikua na maswali chungu nzima.

       "Mama tupo tayari kueleza."Lisa aliongea akitetemeka, Dani aliitamani kukimbia mbali na uso wangu lakini angelikimbilia wapi?"

        "Kueleza Nini? Kueleza juu ya ufufuo wenu?"Maswali yalinitoka.

      "Tafadhali keti mama keti chini tukueleze, "Lisa Binti yangu alinitaka niketi kitini lakini nilikataa kuketi akaanza kueleza kisa na Mkasa,

        "Tulifeki VIFO Mama, yote uliyoyaona au kuyasikia kwenye Television na mitandao ya kijamii sio ya KWELI Bali ni feki."Nilimsikiliza.

     "Sababu kubwa ya kufeki juu ya VIFO VYETU ilitokana na  Siri nzito ya mafanikio tuliyoyapata." Niliendelea kumsikiliza.

       "Mafanikio yetu yalitufanya tuisi Dunia na watu wetu wa karibu wangelitusumbua sana kwahiyo tuliogopa usumbufu. "Nilimsikiliaza Binti yangu.

        "Mama tulishinda Bahati nasibu ya Taifa shilingi billioni Moja na nusu kwahiyo hatukutaka watu wajue mafanikio yetu maana tuliona wangelitusumbua,"Binti yangu alipumzika kussimulia.

      "Kwa Sasa sisi ni matajiri wa kutupwa. Tunapata kila kitu muhimu kitupacho raha na starehe za maisha, "Dani alimpokea Lisa kunena.

     "Kwasababu ya pesa, Raha na starehe ndio mfikie hatua ya kufeki VIFO,?"Nilihoji Kwa kisirani. Walishindwa kujibu.

      " Hivi Lisa na Dani mnajua jinsi Gani mlivyotuweka katika wakati magumu? Mnajua jinsi Gani tulivyoumia na kupatwa na mishituko juu ya vifo vyenu feki?" Walishindwa kujibu..   

       "Pesa uondoa utu na ubinadamu. Pesa umpa mtu kiburi na kumuongoza vibaya, nimepoteza nyumba yangu sababu tu ya made ni uliyoyaazima Lisa."Machozi yalinibubujika.

      Silii ati Kwa sababu ya Numba yangu ilizyopigwa mnada na KAUSHA DAMU mlikoazima pesa Kwa Siri na kuiwekeza nyumba yangu kama Dhamana. Nalia Kwa sababu mmetuweka katika majonzi na huzuni alafu Leo tuambiwe waliokufa kwenye ajali ya gari wamefufuka?" Niliongea.

     "Mama utusamehe'Waliniomba msamaha"

     "Kama mnataka msamaha wangu tafadhali Lisa twendeni nyumbani tukaongea na kuyamaliza'Niliwapa mtihani. Lisa alionesha darili za kukubali kurejea nyumbani lakini Dani Alimzuia

      "Lisa UNATAKA kuniacha mpenzi? UNATAKA kuniacha na kumfuata mama yako? Haunipendi Lisa? Dani aliushikiria mkono wa Lisa Binti yangu aliyeonekna kunenepa na kupendeza. Nguo alizovaa zilikua ni nguo za bei gharama. Vidani vyake masikioni na puani vilikua Dhahabu tupu achana na Uzuri wa nywele zake zilizopamba Vito vya lulu na almasi hakika Binti yangu alipendeza."

          "Niruhisu Dani niruhusu nirejee Kwa mama."Lisa alionesha Darili za kunifuata.

"Hapana Lisa, hapana siwezi kukuruhusu. Je, tumepungukiwa Nini? Hatuli vizuri? Hatuvai au kufanya starehe za gharama? hatuizunguki Dunia? Lisa MPENZI tumepungukiwa Nini? Kama pesa tunazo ni pesa za kutulisha MIAKA zaidi ya ishirini bado tu zitabaki nyingi. Tafadhali Lisa, Tafadhali nifuate Mimi ninayekupenda."Dani alimshawishi Lisa nikawaona wanaondoka pale chakulani wakiwa mwameshikana mikono na kukumbatiana viunoni. Niliumia, niliumia sababu damu ni nzito kuliko MAJI. Lisa bado ni Binti yangu ni Binti madogo kuyajua MAISHA. Pesa isiwe sababu ya kunitenganisha na Binti yangu Lisa.

        "Lisa Binti yangu MPENZI tafadhali nifuate."Nilimwita Lisa ambaye alikua akitoweka taratibu huku akiwa anaigeuza Shingoye kuniangalia.Hakika MAPENZI yalimtawala Lisa hata afikie HATUNA ya kukataa kunifuata mamaye mzazi. Chozi lilinibubujika

##########

Semina iliisha nikiwa ningali katika dimbwi la mawazo, nilimuwaza Binti yangu Lisa niliwaza alivyoniweka katika Dimbwi zito la wasiwasii, nikaruhusu YAPITE na MAISHA yaaendelee ingekuwa vema niende POLISI kuripoti lakini niliona  hapana Wacha nimpe Lisa nafasi nyingine milango yote ya kuingilia nyumbani kwangu ipo Wazi akiona yafaa atarejea.

     MIAKA mitatu mingine ilikatika bado tu sikuiona sura ya Lisa Binti yangu, sikuenda POLISI kuripoti Nilimpa nafasi, nafasi ya kurejea, na KWELI siku Moja mvua kubwa ilikua ikinyesha nikafanya hima kwenda kumfungulia mgomgaji aliyekua akigonga mlango wangu.
    
       Eeh! Nilishangaa  nilishangaa mara baada ya kuiona sura ya Binti yangu Lisa amesimsma barazani, nguo zake zikiwa zimeloa MAJI, nywele zake nywele zile nzuri zenye afya tele zilikua zimekatika tena zipo ovyo zinanuka. Nguo zake chafuu zimeoza na kuharibika, alidhoofu sana Kwa kifupi alikua kama mwenda wazimu asiyetamanika. Nilimshangaa.

        "Tafadhali mama naomba niruhisu niingie ndani,"Aliomba

        "Ok. ingia'Nilimfungulia mlango na kmruhsu aingie.

 Nikalichukua taulo zito na kumpatia ajifute MAJI yaliyojaa mwilini

        "Utakunywa kahawa au tangawizi? Nilimuuliza

        "Asante Kwa kunijali mama nitakunywa kahawa."Alinijibu nikaingia jikoni kuandaa kahawa ajili ya Binti yangu Lisa. Baada ya dakika chache nilirejea na birika la kahawa na vikombe viwili.

       'Nisamehe mama."Aliongea mara Bada ya kugida fundo zito la kahawa.

      "Pole "Nilimfariji chozi zito lilimtoka

      "Nisamehe Leo nimeamini asiyesikia la mkuu uvunjika miguu, mtoto mleavyo ndivyo akuavyo na mdharau mwiba umchoma."Nilimfuta chozi nikaendelea kumsikiliza.

     "Tuliposhinda bahati nasibu Dani alinidanganya tufeki VIFO Ili jamii isitusumbue maana tulikua na mabillioni ya pesa...... Aah! Jamani Leo hii Dani amenikimbia niponipo tu kama Tajiri aliyefilisika." Aliongea.

     'Tatizo Nini Lisa? Nilimuuliza

      "Bora ningelikusikiliza mama, Bora ningelisikiliza sauti YAKO uliposema nirejee nyumbani pamoja na wewe... Ona mama, ona nimerejea mpweke."Aliongea Kwa hisia

      "Dani amenikimbia pia amekimbia na mapesa yote tuliyoshinda kwenye Bahati nasibu yaani sijui niwapi alipokimbilia?" Aliendelea mkusimulia.

      "Kwasababu tulikuwa na pesa nyingi Dani alinishawishi tuanze kuchezea kamari.Nilikubali Mimi na Dani tukaanza kuchezea kamari kwenye makasino na makumbi makubwa ya Kamari. Kamari ilipomtawala Dani akaanza kuweka dau kubwa kubwa la pesa kumbe ndio HATUA ya yeye kufilisika. Alifeli mara nyingi na alipoona pesa zinakimbilia ukingoni akaend Benki kuzichota pesa zote Kisha akakimbilia pahali nisipofahamu. Dani ameniacha mikono mitupu yaani Sina hata mia mfukoni."Nilimsikiliaza, Lisa mwanangu aiyetoa chozi lenye kamasi.

        "Pole sana marehemu uliyefufuka."Nilimkebehi Binti yangu,

         "Sasa Binti yangu UNATAKA nikusaidiaje maana pesa zilizokupa furaraha na kiburi zimekukimbia?

         "Nisamehe mama ninataka kuishi na wewe Tena." Aliomba uso wake ukiwa tumejaa huruma.

          "Sawa, suala la kuishi na Mimi sio mzigo tunaweza kuishi wote iwapo utalifuata jambo Moja tu.?Nilimwambia     
   
           "Jambo gani hilo mama?'Aliniuliza.

            "Nenda kajisalimishe POLISI pahali salama kwako"

            " POLISI tena mama.?Alishangaa.  

           "Ndio mwanangu POLISI ndio pahali salama ukienda kujisalimisha utakuwa na amani ila usipojisalimisha utaandamwa na wengi na hao wengi watakukata tamaa.'Nilimpa matumaini.

        "Nisaidie mama"Aliogopa

         "Usiogope Binti yangu bado unayonafasi ya kuishi na mmi na Ili uishi na Mimi sharti uwe na amani." Nilimshauri, aliketi Kimya zaidi ya dakika ishirini Kisha akanena.

       "Sawa mama nitaenda lakini si utanisindikiza.

       "Ndio Lisa nitakusindikiza kwanini nisikusindikize? Nashukuru Mungu upo hai, bado ninakupenda Binti yangu,' Niliingia chumbani kwangu nikatoka na nguo mpya safi, nikamtaka Lisa avae tutoke twende POLISI.







######


TCHAO







  

TOXIC DADY



BABA YANGU HAKUMPENDA MCHUMBA WANGU LAKINI SIKUJALI NILILAZIMISHA NDOA.


Nilikutana na mchumba na Mume wangu tarajiwa Jerome katika mgahawa tuliozoe kukutana kila siku. Tulifanya kuagiza kahawa na vitafuno tukaongea maneno mawili matatu.


    ''Mapenzi yetu yamedumu Kwa zaidi ya MIAKA SITA Sasa Shelidani Kuna jambo nahitaji kukuambia.'' Siku ya Leo mpenzi wangu Jerome hakuonesha furaha, sikufahamu kwanini?  Siku zote utanguliza uchangamfu.


       ''Una Nini Jerome mbona Leo nakuona hauko sawa?'' Nilimuuliza


          ''Mbona nipo sawa Sheli,'' Alinijibu Kisha akagugumia kikombe Cha kahawa akatafuna pia vipande vya kashata.


       ''Nipo sawa Sheli. I'm ok'' Aliongea Tena Kisha akasema


       "Ninakupenda niruhisu nikufanyie bonge la sapraizi." Aliongea akiwa  na tabasamu usoni, tabasamu pana.


         "Nipe mkono wako Kisha fumba macho Hadi nikuambie ufumbue." Nilitabasamu Kisha nikatii agizo lake. Aliushika mkono wangu wa mashoto akaupapasa papasa kama vile anaupakaza mafuta laini ya mtoto. Nilihisi Kuna kitu kimegota kwenye dole langu la shahada. Jerome akaniambia


"Fumbua macho  MPENZI"


Waooo! Nilipofumbua macho MOYO wangu uliripuka Kwa shangwe na furaha, nikamrukia Jerome na kumkumbatia.


    "I want to Marry you Sheli." Machozi ya furaha yalianza kunitoka. Muda wote wa MAPENZI yetu Leo hii Jerome wangu amenitamkia ndoa. Wacha we! Kwanini nikatae, ndoa ni TAMU Kwa wale waijuao.


       "Sasa ni wakati wa kuwapa taarifa ndugu, Wazazi na jamaa juu ya harusi yetu." Baada ya kunivisha Pete Jerome alidai ndoa.


      "Tuchukue miezi mitatu tu kukamilisha haya."Jerome aliitamani ndoa.


      "Sawa Daring. I love you"Nilimpiga kiss Shavuni.


"I love you too Sheli."Alinipiga busu lingine shavuni na juu ya komwe langu..


Siku mbili baadaye nilikuwa nimeketi Sitting room nikiwa pamoja na wazazi wangu kuwapa taarifa juu ya nia ya MPENZI wangu Jerome kunitaka ndoa. Nikiwa na  WINGI wa furaha nikapokea baraka tele kutoka Kwa mama YANGU mpenzi.


       "Hongera Binti yangu, hongera MPENZI unaelekea kwenye kundi Bora la maisha" Mama alinibariki.


         "Hivyo ndivyo inavyotakiwa Binti akiisha ingia ukubwani lazima aolewe na adondoke nyumbani Kwa wazazi wake akajitegemee na KUMTEGEMEA Mume au wote wakategemeane." Mama aliongea Tena.


      "Nakutakia baraka Binti yangu uolewe na yule umpendae, umjuaye na yule uliyeridhika naye ambaye yeye pia unajua mtaishi milele pendo la kupendeka. Nilifurahia baraka za Mamangu. Lakini mmh! Wacha nigune Kwa upande wa babangu mambo hayakuwa sawa, niliambulia maneno yaliyonivunja MOYO furaha na matumaini.


      "Uolewe na Jerome  yule kapuku mtoto wa kimasikini atakupeleka wapi wewe mtoto wa Tajiri" Dady aliongea maneno Bitter  yaani machungu,


      "Jerome Hana uwezo  wa kukulisha au kukujengea nyumba ya kuishi zaidi ya kupanga Tena hata mkijaliwa watoto hatoweza kuwasomesha Shule binafsi, Shule za kulipia." Baba alimponda mchumba wangu.


     "Kuna wanaume wengi wanaotoka familia za matajiri wengine ni watoto wa marafiki zangu kwanini usiniruhusu nikutafutie mwanaume Tajiri? Baba alinishangaza kauri yake.


       "Hapana Dady ninampenda Jerome na Jerome ananipenda pia. HAITAWEZEKANA KUTUTENGANISHA," NILIPIGILIA MSUMARI wazo langu.


     "Basi Mimi sintakuruhusu uolewe na Jerome sitaki kusikia habari za mtoto wa Tajiri kuolewa na mtoto  wa masikini." Baba aliongea maneno yaliyoniumiza.


................


     Kwa sababu Dady hakutaka kusikia ninaolewa na mwanaume nimpendaye alichofanya yeye ni kukataa kushiriki mipango ya harusi yetu. Alikataa katakata kubariki Mimi kutolewa na Jerome aliyedai Hana uwezo wa kunilea au kuja kuniboreshea MAISHA. Nilimwambia Dady MAISHA Bora tutayatafuta, tutayatafuta wote wawili yaani mimi na Jerome, lakini wapi! Dady hakuwa tayari kunisikiliza. Mipango yote ya harusi yetu ilifanywa na Mimi mama na Jerome.


 Jerome aligharamia kila kitu muhimu Kwa ajili ya harusi kuanzia malipo ya ukumbi, vyakula, Usafiri, mavazi na mapambo. Alifanya mambo chungu nzima Kwa hakika aliimeza akaunti yake yote ya Bank.


Siku ya harusi ilipofika nilipendeza sana mama pia alipendeza. Muda wa kuingia kanisani ulipowadia mama alinisindikiza nikaingia kanisani nikiwa mwenye furaha  ingawaje Baba alikataa kuhudhuria harusi yangu mie na Jerome.


Lakini jamani nilipoingia kanisani nilipigwa butwaa kuona Jerome wangu hayupo Ndugu zake, wazazi pia hawapo.Niliogopa. Uzuri watu waliohudhuria kanisani waliniambia Jerome alikuwepo pale kanisani muda si mrefu ametoka akiwa anaongea na mtu kwenye simu.


Nikautuliza MOYO Mtima nikaketi mbele ya kanisa nikimsubiria Jerome wangu lakini Mmh!  Jerome hakutokea. Kadri saa zilivyozidi kuyoyoma ndivyo Jerome hakuonekana. Toba!  Nilianza kuaibika.


       "Nini kimempata Jerome?"Nilijiuliza.


        "Simu zake zote zinaita tu lakini hapokei."Nilishangaa.


        "Wana SEMA alikuja Kisha akaondoka ina maana alikuja kuniaibisha?" Nilikosa Jibu, amachozi yalinitoka nikalia masikini. Aibu Gani hii, mwanaume ananiaminisha ndoa alafu siku ya siku anatokomea mitini. Nilimwaga chozi.


>>>>>>>>>>>>>>>

       Lakini kumbe nisiandikie mate wino ukiwepo. Jerome alipowasili kanisani simu yake iliita, alikua ni mama yake ambaye alimtaka Jero haraka sana aelekee Aghakhan Hospital. Mama alimwambia Jerome Shishi mtoto wa marehemu dada yake Jerome yupo hoi taabani amelazwa ICU. Jerome alichanganyikiwa na bila kupoteza muda alitoka Kanisani na kueleka Aghakhan Hospital iliyopo Posta.


     "Mtoto wa marehemu Dada YAKO yupo hoi taabani DAKTARI amesma ana uvimbe unaomsumbua kichwani" Mama Jerome aliongea akiwa na WINGI wa wasiwasi.


     "Dakta amesema zinatakiwa Millioni ishirini Ili mtoto wa Dada YAKO afanyiwe Operesheni" Mama aliongea Kwa uchungu.


    "Kama ujuavyo Jerome sisi ni masikini  HATUNA hata senti Tano ya kuwapa Madaktari wamtibie Shishi mjomba wako. Hili ni pigo kwetu yamkini Mola anatujaribu. Mama yake Jerome alilia.


       "Mama MPENZI wewe na Mimi tunampenda sana Mjomba Shishi, tatizo lake limetoke ghafla kwa bahati mbaya ninatamani sana kusaidia lakini pesa nyingi nimezitumia kwenye maandalizi ya harusi yangu. Nifanyeje mama jamani?"Jerome alihuzunika


      "Sijui mwanangu, sijui tufanye Nini? Je, hauna rafiki mzuri umuazime Pesa baadaye ukifanya kazi kwa bidii utamrudishia"Mama alitoa wazo. Jerome aliinama chini kutafakari baada ya dakika nyingi kupita alimwambia mama yake.


    "Nipe saa chache nijaribu maombi Kwa watu muhimu." Ikawa hivyo basi Jerome hakutokea kwenye harusi yetu.


            #####


      "Hallow Baba mkwe" Jerome alimpigia simu Dady.


      "Hallow nani mwenzangu?"Dady hakuisave nambari ya Jerome aliitupilia mbali, alimuona Jerome kama mtu anayemchechefua.


     "Ni mimi Jerome, mchumba wa Shelidani." Alijitambulisha


     "Unachangamoto Gani kijana? Dady hakutaka hata kutanguliza salamu.


      "Kwanza Shimamoto Baba."Alimsabahi. 


       "Salamu sio chakula nikala na kushiba.... Embu ongea kiutu uzima. Dady alijibu jeuri Kwa mkwewe asiyempenda.


         "Ninashida Baba ninaomba msaada wako nipo chini ya miguu yako." Jerome alishindwa kujieleza.


    "Huna meno, huna ulimi hauwezi kutamka? Ongea kiume."Baba alimkaripia Jerome ambaye alivumilia kauri zinaovunja MOYO.


       "Mtoto wa marehemu dada yangu amelazwa Chumba Cha wagonjwa mahututi yaani ICU Hospitali ya Aghakhan, Posta. Anatakiwa kufanyiwa Operesheni ya haraka, Uvimbe unamsumbua kichwani. Ninaomba msaada wa mkopo shilingi millioni ishirini maana gharama nyingi nimezitumia kwenye maandalizi ya harusi yangu,"


     'Teh teh teh' ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ Baba mkwe alicheka.


      "Harusi YAKO inanihusu Nini Mimi?"Aliuliza Kwa kebehi.


      "UNATAKA msaada wa pesa za Bure.....Aaah kijana hakuna cha bure Duniani. Embu njoo kesho asubuhi haraka sana tupige Dili," Baba alimwambia Jerome. Siku ile ilipita PASINA Jerome wangu kufika Kanisani. Aliniacha NJIA panda mie niliyechekwa na watu walionishangaa kuachwa na yule nimpendaye.


,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,


 Ngrii ngriii ngriii☎️๐Ÿ“ž simu iliita, nilishituka usingizini na kuicheki nikitegemea ni MPENZI wangu Jerome akinipigia lakini kumbe sio Jerome Bali ni Baba. Sikua na Raha Wala furaha Kwa jinsi nilivyolia usiku KUCHA juu ya Jerome liyenishangaza Kwa ahadi feki ya kunioa.


       "Hallow Shelidani naomba saa SITA mchana uje Ofisini kwangu Nina maongezi na wewe." Wakati Baba akiongea ilikua ni saa mbili asubuhi.


      "Sawa baba nitakuja."Moyoni nilijilaumu kwanini sikumsikiliz Dady aliponiambia Jerome sio mtu wa kunioa.


        'Oh my God embu ngoja niende asubuhi hii nikamsikilize Dady" Nilipata wazo la kuondoka asubuhi hata kabla saa SITA tuliyokubaliana haijafika. Nikakurupuka kutoka kitandani na kuingia bafuni kukoga. Saa tatu asubuhi nilikua nimeshafika Ofisini kwa Dady lakini Toba! Kabla sijaingia Ofisini kwenye vioo vya Ofisi ya Dady nilimwona Jerome mchumba wangu aliyenipa Presha kanisani. Uzuri wa madirisha ya Ofisi ile yalinipa mwanya wa kusikiliza kilichokuwa kikiongelewa.


      "Hizo Millioni hamsini nimekupatia Bure sitaki unirudishie kikubwa wewe tia saini huo mkataba kwenye karatasi."Dady aliongea


    "Nadhani tayari ushasoma masharti yaliyopo kwenye mkataba huo. Ni marufuku kuonana au kukutana na Shelidani, kuendeleza MAPENZI au mahusiano na mwanangu Shelidani. Huna uwezo wa kumuona mwanangu Shelidani sababu wewe ni fukara masikini." Kauri za Dady zilinishitua  nikiwa ningali pale dirishani.


     "Utamlisha Nini Binti yangu wewe? Utamvalisha Nini? Kula YAKO na vaa YAKO imejaa mashaka. Sikiliza kijana naomba ukae mbali na Binti yangu Mimi ndiye mwenye uwezo wa kumtafutia Binti yangu mwanaume wa kumuona mwanaume ambaye ataweza kumlea na kumpenda Binti yangu," Dady alitoa mahubiri yake.    


     "Aya Sasa tia Saini hapo Kisha uondoke na hayo maburungutu YAKO,"Jerome alitii, akatia Saini. Sikukubali, yote yaliyoongelewa niliyasika haraka haraka nikauvamia mlango wa Ofisi ya Dady nikaingia nikiwa na hasira, Jerome alishituka aliponiona lakini Dady alitabasamu.


            "Usiisaini hiyo karatasi Jerome, tafadhali," Nilipiga kelele baada ya kuingia Ofisini.


         "Oh! Nitaeleza Shelidani, nitaeleza tafadhali," Jerome aliongea  


        "Ueleze Nini Jerome? Nimesikia kila kitu... Jero Kwa upuuzi wako hupo tayari kuyauza MAPENZI yetu Kwa sababu ya pesa?"


     "Hapana Shelidani nimepata matatizo kidogo ambayo yamekuwa magumu kwangu kuyatatua zaidi ya kuomba pesa Kwa baba YAKO. Mjomba wangu Shishi amelazwa Hospitali zinahitajika pesa nyingi Ili  kumtibia" Aliongea Kwa huzuni.


      "Hata kama Jerome yaani UNATAKA kuniacha sababu ya pesa? Jinsi ninavyokupenda Leo hii niambiwe unaniacha na kunitenga" Machozi yalianza kunibubujika Kisha nikamgeukia Dady nikampa vidonge vyake.


   "Jambo unalolifanya sio ustaarabu Dady unayaua MAPENZI niliyofunga na mtu niliyemuweka moyoni."Niliongea Kwa uchungu


     "Usinipigie kelele Sheli nafanya hivi makusudi kwa faida YAKO. Huwezi kuolewa na mtu hoe hae masikini asiye na mbele Wala nyuma," Dady aliongea.


          "Kama ni masikini au hoe hae Mimi ndiye niliyempenda Dady sio wewe. Umasikini au Utajiri yote ni mipango yake Mola, hatuwezi jua kesho nzuri au mbaya aliyoipanga Mola." Baada ya kusema hayo nilitoka ndani ya Ofisi ya Dady Jerome aliyekua ameshika maburungutu ya pesa pamoja na ule mkataba alinikimbilia.


         "NISAMEHE Sheli sikuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na masharti ya huu mkataba Ili kuokoa MAISHA ya mtoto wa Dada yangu." Aliongea


        "Jerome wewe ni mwenye MOYO uliojaa ubinafsi yaani unakubali kuyauza MAPENZI Kwa sababu ya Pesa. Kwanini usiwasiliane na Mimi unieleze shida hii angarau tujue wapi tungelianzia kutatua. Ubaya wako unakimbilia kuomba ushauri Kwa Dady."Niliongea machozi yakinitiririka.


    "Jana nilipokuwa kanisani nikikungoja sana Sheli, nilipigwa Simu na kuelezwa tatizo la Shihi.. haukuwepo wakati huo Sasa ningelimweleza nani shida hii?


     "Hata kama Jero haukupaswa kwenda Direct kumueleza Dady juu ya tatizo hili, wewe binafsi haumjui jinsi alivyo."


       "NISAMEHE Sheli" MPENZI wangu alitia huruma nikamkimbilia na kumkumbatia wote tukalia machozi.


...........


          Shishi alifanyiwa Operesheni kuondoka uvimbe kichwani, Operesheni ilienda vizuri akaruhisiwa kutoka Hospitali baada ya majuma kadha hali nzuri ya Shishi ilirejea SHISHI AKAPONA


NILIMSAMEHE jEROME TUKAANZA MIPANGO MIPYA YA HARUSI BAADA YA MIPANGO YOTE KUFANYIKA HARUSI YETU ndogo ilifanyika na kuhudhuria na watu wachache SEMA Dady bado aligoma kuhudhuria harusi yetu.


         Bada ya harusi yetu KUFANYIKA mie na Jerome tulikubaliana kuhama Jiji la Dar es saalam tukahamia Arusha. Niliamua kukata mawasilino na Dady Tena nilifanya uamuzi wa KUACHA kufanya kazi ndani ya kampuni ya Dady, alichokifanya yeye ni kuliondoa jina langu kwenye Documentary za Urithi wa kampuni yake. Sikujali sana mana natambua kati ya upendo na pesa Upendo unanguvu sana.


       Nilibahatika kupata KAZI nyingine Jerome pia alipata kazi nzuri tukajichangachanga na kununua nyumba yetu na baada ya kujichangachanga tena tulikusanya Millioni Hamsini tukamrudishia Dady pesa alizompatia Jerome Kwa matibabu ya Shishi. Dady hakutaka Tena kunisikia sembuse kunijua


           Sikujali. Tuliendelea kumove on, Leo hii tuna watoto watatu na kijacho mwingine yupo njiani kuja. Sie tunapendana pendo lililoshiba pendo lisilojali Mali, pesa Utajiri au Statasi



,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,


 MAPENZI ya KWELI hayabagui hayachagui.




Tchao   

        


Sunday, October 20, 2024

KAZI YA PILI ILINIFANYA NIOMBE TARAKA.


 MUME WANGU ALINILAZIMISHA NITAFUTE KAZI YA PILI LAKINI NILICHOKUJA KUGUNDUA KILINIFANYA NIOMBE TARAKA.


Nilipopokea mshahara wangu wa mwezi October nilijipongeza  na kumshukuru Mola sababu niliona mpango wangu wa kujinunulia gari ๐Ÿš— ulibisha hodi.

    "Nitachukua mshahara wa mwezi October na miezi mingine ilopita nitaichanganya nikajizawadie Prado nyeupe au Rolly Royce." Nilijitania ingawaje uwezo wa kununua Rolly Royce sikua nao mie Mwalimu Husna.

       "Nikiisha keti mbele ya siti ya Dereva nitampungia mkono Mume wangu Jodi, 'Hallow Baby Jodi... By by lm now driving my beautifully Car' " Mbwembwembwe zilinisumbua.
 
    "Lakini mmh! Kumbe nimepuunguki washilingi Million Tano Ili kukamilisha ununuzi wa Gari yangu" Nilikumbuka kuwa Salio halitoshi. Furaha yangu ilianza kuyeyuka taratibu kama barafu Juani.

      "Oh! Mola wangu nihurumie!," Nilihuzunika.

       "Ok. Nitamwambia Mume wangu Jodi aniongezee Millioni tano ililiyobaki" Nilijipa matumaini, wazo langu lilikua faraja kwangu. Huzuni ilinipungua maana nilijua Jodi hawezi kuninyima Salio lililopelea. Jodi anapesa nyingi za kumwaga, kazi yake inalipa maana yeye ni Injinia, Fundi msanifu wa majengo makubwa.
     
       Jioni ilipowasili niliingia Mekoni kuandaa chakula kitamu ambacho Mume wangu hakika angelinisifia. Ninajua kupika na mapishi ninayaweza. Mara baada ya mapishi niliingia bafu kukosha mwili na kujipulizia uturi wa kipemba Ili babu akisikia harufu ya karafuu na tende anipende zaidi. Na nijuavyo mie Wapemba na waunguja mambo tunayaweza.

Aliporejea nyumbani nilimpokea Kwa wingi wa mabusu ๐Ÿฅฐna matabasamu☺️ akaeleka kukosha mwili bafu mie nikaandika meza tule na kulishana mahanjumanti hapo ndipo nikapata  mwanya wa kumueleza Jodi juu ya shida yangu.

     "Muda si mrefu na mie Ua la MOYO wako nitapendeza nikiwa na ndinga langu mwenyewe" Niliongea taratibu nikamega tonge la ugali nikalichovya na mchuzi rojorojo Kisha nikamlisha wangu nimpendae Jodi.

     "Waoo! Hongera Sweet  heart❤️ UNATAKA kuniambia Ndo ndo ndo imekua chururu na kibubu kimetick." Jodi Mume wangu mwenye masharubu yake na na tumbole kubwa kama kabeba mapacha aliniambia.
   
        "Kibubu kimetick Dear ila bado ninashida  Moja ndogo ingawa nzito SEMA ninatumaini KUPITIA wewe wangu wa MAPENZI nitafanikiwa mafanikio mengi kama mchanga wa bahari" Nilimkonyezea JIcho nikarembuka na kudeka.
      
       "Shida Gani Mamie, ongea nikusaidie " Jodi alinipa nafasi ya kueleza dukuduku langu.

     "PESA yakununulia gari niipendayo haijakamilika, hapanilipo Nina kiasi Cha shilingi Millioni hamsini na Tano mfukoni imesalia millioni Tano Ili shuhuli ikamilike, Tafadhali naomba uniwezeshe kiasi cha pesa iliyosalia." Niliwasilisha ombi langu nikasubiri kumsikiliza Nini atasajest.

      "Mmh! Ombi lako kwangu Mlima Daring" Sikuielewa kauri ya Jodi.
      "Una maanisha Nini Daring?" Nilihitaji kujua.

       "Sina pesa hizo Kwa Sasa lakini kama utafuata ushauri wangu lazima utapata hitaji la MOYO wako." Jodi aliongea.

      "Jodi usiniambie hauna pesa nilizoomba kumbuka mshahara wako ni mara nne ya  mshahara wangu." Niliropokwa.
     
   "Mamy usikurupuke, bado sijamaliza kukueleza Nini unapaswa kufanya. Unapaswa kufanya kazi ya pili mbali na kazi yako ya Ualimu"

    "Jodi sintakuelewa unanishauri nifanye kazi ya pili wakati Nina kazi yangu ya kwanza. Aya niambie ni kazi Gani hiyo ya pili." Nilisubiri jibu lake.
     
       "Kama nilivyosema Sina Millioni tano ya kukuongeza ununue gari, tafuta kazi yoyote ile ya pili ikuwezeshe upate pesa." Jordan alinichanganya

      "Kazi Gani Sasa? Nilibadirika furaha yangu ilianza kuchuja.

       "Yoyote ile nzuri" Alisistiza
        
         "Hapana Jodi siwezi, ningali Nina majukumu shuleni kama MWALIMU na Nyumbani kama Mkeo kupika, kufua. Kulisha mifugo, kwenda soko, usafi nakadharika."
     
     "Tafuta kazi nyingine Bana."
 
      "Siwezi Jodi, kama unashindwa kunisaidia hiyo Million Tano basi niruhisu niuze Moja ya magari YAKO Yale SITA Ili na Mimi nifurahie kumiliki gari yangu mwenyewe." Nililitetea wazo langu.

       "Kamwe usithubutu kuigusa gari yangu ukaiuza," Alininyoshea dole. Akadamka pale alipoketi mara baada ya kukosha mikono yake haraka haraka  akaelekea chumbani kulala. Niliogopa kidogo moyoni nilihisi yamkini nimemuudhi Mume wangu, yamkini hajapendezwa ombi langu, nikaacha kula nikanawa mikono na kumfuata chumbani nimbembeleze.

................

       "Ombi la Mumeo lashangaza" Mama yangu Bi. Subira  alishangaa mara baada ya kumweleza maudhi ya mume wangu. Leo nimemtembelea Mama kumuomba ushauri na kumueleza juu ya mabadiliko' ya mume wangu Jodi.

         "Usitake kuniambia kuwa mkwe wangu Jodi hakupi kila kitu nyumbani" Mama alionesha wasi wasi.

      "Kila kitu ninapata Mama lakini hili la kuambiwa NITAFUTE KAZI nyingine Ili nijichange kununua ndinga langu limeniumiza. Jodi ananitwisha zigo zito la majukumu." Nilimwambia mama

       "Kipenda roho ula nyama mbichi Husna" Mama aliendelea kunipa mawaidha.

          "Mke mwema uheshimu na kutii mawazo ya mumewe, tafadhali sikiliza sauti yake labda Kuna MAZURI utayapata kutokana na mawazo yake." Mama alimuunga mkono Jodi.

      "Hapana Mama nahitaji huruma kwa hiyo natakiwa kufanya kazi ya kufundisha watoto Shule na pia kuhangaikia mambo mengine? Ina maana siku Tano niwepo Shule na siku mbili ambazo ni jumamosi na jumapili niwepo kwenye kazi ya pili.

      "Kama unania ya kulipata gari liupedezalo MOYO wako basi fanya lakini kama hauna nia achana na matamanio yako." Mama aliongea. Nilirejea nyumbani kwangu nikiwa mnyonge mnyong'onyevu Sina Raha moyoni zaidi ya HASIRA nilijiuliza kwanini Jodi akatae kunisaidia shilingi millioni Tano tu? Ukitegemea Kwa uwezo alionao angeliweza kunisaidia hata Millioni kumi ya zawadi.

       .............

Wiki mbili zilipita lakini kila nikimbembeleza Jodi kuhusu Salio la Gari alitia msistizo nifanye kazi yoyote ile ya pili itakayoniwezesha kudunduliza dunduliza vijipesa. Ndani ya wiki hizo mbili MOYO wangu uKAANZA kuregea taratibu nikairegeza kamba na msimamo wangu wa kutokufanya kazi ya pili ilihali kazi ya kwanza ninayo. Nikamwambia Jodi nipo tayari kufanya kazi ya pili sababu mwenzangu amekuwa mchoyo hataki kunisaidia pesa ndogo ndoago kama kinyesi Cha lnzi.๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ

Jodi aliposikia kwamba nipo tayari kufanya kazi ya pili alifurahi sana na kunipa baraka zake akasema lazima nitafanikiwa Tena akaongeza madoido yakeq eti akasema mwanamke mpenda maendeleo hamtegemei mumewe Bali hutumia nguvuze kujipigania. Nikamnunia sana hata unyumba nikatamani nisimpe.

    Katikati ya fikra zangu niliwaza ni aina Gani ya kazi itakua fiti Ili nifanikiwe zaidi. 'Je, nifanye shuhuli ya kuuza Duka la mahitaji ya nyumbani?' ' Hapana sikuwa tayari kupoteza akiba yangu kuanzisha biashara ukitegemea damu yangu haipatani na biashara. Je, nifanye kazi za ndani Yaani kazi ya u house geli? Teh teh teh๐Ÿ˜๐Ÿ˜„๐Ÿคฃ nilicheka yaani mie Mwalimu Husna mke wa bosi nikafanye kazi ya kupuguta deki, kukosha vyombo au kulisha umbwa na nyau ๐Ÿ˜….

         Ghafra nikapata wazo nitahudumu Bar, ๐Ÿบ Tena Bar ambayo Mume wangu Jodi upendelea kuketi pamoja na marafiki zake akinywa na kulewa. Nikalifurahia wazo langu sababu huku kwetu Mbezi beach Groceries na Bar zinalipa mno. Haraka nikatoka nyumbani kwangu na kueleka Bar 'KWETU BAR'  Baada ya kufika na kupokelewa na Meneja Nilimweleza shida yangu, kuhudumu Bar. Meneja yule mwenye roho ya kilokole  hakuwa na pingamo alikubali ombi langu akanitaka siku ya kesho yaani Jumamosi niwepo kazini nikihudumia walevi.

      "Kumbuka haupaswi kuja kazini ukiwa umesuka hizo twende kilioni na kuvaa magauni ya twende Kwa Mwamposa." Alinichekesha

  "Vaa kimini Bibi, vaa sketi FUPI yenye mpasuo utakaoonesha Chupi na mapaja yako manono." Aliniambia mie nilipigwa butwaa ๐Ÿ˜ง๐ŸงŸ nikishanga kanuni zile
       
     "Pakaza midomo yako lips ๐Ÿ‘„ rangi nyekundu inayonata nata na kuita wateja, kitopu chako kiwe kinabana na pia kioneshe tundu la kitovu chako kizuri๐Ÿคฃ uhakika uwe umevaa shanga za kutosha kiunoni ilikuvuta wateja sababu wanawake warembo kama wewe ni kivutio Cha walevi. " Alimaliza somo lake, nikamuelewa nakukubaliana na kauri zake nikampa ahadi ya kuwai kazini. Wakati naondoka alinisindikiza Kwa jicho la ngono, matamanio yalimjaa Kisha akatamka.

        "Mteja yeyote yule akikutaka kingono mkubali, nikisikia umemkatalia uwe tayari kumwaga unga." Mtume! Nilishangaa mie Hussna kazi za Bar kumbe zinachagamoto. Hapana, ninalitaka gari  Millioni tano ni pesa Gani!? Nitazipata tu maana Meneja amenihakikishia kila mwisho wa mwezi nitaondoka na shilingi laki tano. Kwa kadirio la miezi michache tu mambo yangu yatakuwa 'Mwaa๐Ÿ˜๐Ÿฅฐ๐Ÿ˜'

    ..............

      "Tayari nshapata kazi Babu we!" Nilimjuza Jodi Rafiki yangu, Mume wangu na Huba langu.
.
        "Woooo! Usiniambie Daring! Hongera sana," Alinipongeza Wala sikutaka kumwambia aina ya kazi niliyotegemea kufanya zaidi ya kumwambia usiku ndio muda mzuri Kwa mie wake wa Huba kuanza kazi.

      "Ushawini Love ๐Ÿ’• " Alinipongeza.

      "Kabisa Daring." Niliongea Kwa tabasamu. Jioni Jodi aliniaga anakwenda 'KWETU BAR' kuinjoy yeye na rafiki zake Moja moto Moja baridi ๐Ÿบ๐Ÿพ๐Ÿป PASINA yeye kujua kuwa huko 'KWETU. BAR  mie pia nitakuwepo kuhudumia walevi.

      "Ungekunywa supu kwanza kabla ya kwenda Ulevini." Nilimtania

       "UNATAKA nitapike eeh! NIWE kichekesho? Au nijinyee huko." Alinichekesha akasepa na Prado yake nyeusi PASINA huruma kunihurumia mie mtembea miguu, mkung'utwa Jua la saa SITA.. Ah! Jamani Constructor wangu๐Ÿ˜ฟ.

     ...............

          "Husna Dear hongera sana Kuwai kufika kazini." Sauti ya mrembo nisiyemfahamu ilinikaribisha mie niliyejimwagia mapodali usoni ilibaki kidogo nifanane na Zombi. Nikamtazama mrembo aliyenipokea. Kabla sijanena neno akanena

     "Niite Preda Meneja amenielekeza KWAKO, ameniambia nikusaidie iwapo walevi watakuletea fujo." Preda msichana mrembo na mzuri aliniambia mie mgeni niliyevaa  kimini, kitopu na skuna zilizosheeni vikuku miguuni.

     "Asante Preda nimefurahi kukujua twaweza kusaidiana"  Mimi na Preda tukaanza kazi ya kuhudumia walevi, tukawapa pombe na Spirit. Macho yangu yalitua pahali nikamuona Jodi akiwa anakunywa na kuelewa pamoja na rafiki zake, sikujali lakini macho hayana pazia na yeye pia aliniona. Hakuyaamini macho yake alinitzama mara mbili mbili kama vile ameona kiumbe kipya. Mie nikaendelea kuhudumia walevi.
 
       Ghafra nilihisi Kuna mtu amenishika mkono.   wangu wa kulia kwa nguvu almanusura nidondoshe Chupa za bia.

      "Husna  unaafanya nini hapa? kwanini umevaa mavazi yasiyo na sitara Kwa Binti wa kiisalamu?" Jodi alijaribu kuishusha sauti yake isipenye kuwafikia walevi wengine.

      "Nipo kazini Babu ninawajibika Tena naomba ondoa mkono wako niendelee kuwajibika."  Nilimjibu Mume wangu Jodi 

     "Husna una akili  wewe? Hivi hizi ndio kazi za kufanya mwanamke mtulivu kama wewe?๐Ÿฅถ๐Ÿ˜ก" Aliongea Kwa hasira.

       "Sasa kumbe!๐Ÿ˜ก Au alitaka nifanye kazi Gani!?  Nikaokote makopo jalalani." Nilimjibu.

     "Niwache Babu we, walevi wengine wanaitaji huduma yangu." Nikajiepusha na mikono ya Jodi Mume wangu aloyesimama amepigwa butwaa. Nikaendelea na shuhuli yangu ya kuhudumia walevi. Moyoni nikijichamba na kujisemea ' Leo kitanuka nikirejea maskani' ' Atanilazimisha niache hii kazi ya kuhudumia walevi' 'Teh teh teh ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿคฉ akitaka niache hii kazi basi awe tayari kuniongezea Millioni tano ya kununulia gari niipendayo. La sivyo tutakuwa tukiongozana kuja Bar.' niliwaza Kisha nikaendelea kuhudumia walevi.

...........

     Baada ya kuhudumia walevi nilirudi kaunta pale nilipomuacha Preda, Preda aliponiona tu akanisogelea na kuniuliza.

     " Shogangu hivi yule Bwana anakutaka!" Aliniuliza akinyosha mkono pahali.

     "Yupi tena Shogangu." Nilimtazama Preda Kisha nikageuza geuza shingo kumuona huyo Bwana anayenitaka.

     "Si yule pale anayekuangalia sana, yule aliyevaa Form six mwenye tumbole kama pipa."Alimaanisha Jodi.

     "Aka!  Kwanini umesema hivyo Preda." Nikajifanya kulinogesha gumzo
 
     "Nilimwona alivyokufata akakushika mkono na Kwa jinsi anavyokutazama nahisi hisia zake zote zipo juu yako."

    Teh teh teh๐Ÿ˜…๐Ÿ˜‚ nilicheka kishambenga.

     "Wamjua Shogangu. " Nikaukoleza ushoga.

"Nisimjue tena yule Bwana mchafu mchafukoge, mchafu na chukizo Kwa wanawaie. Yaani mjaa laana. Kila akimuona Bar maid mpya lazima akamchape huko Guest bubu huwezi kuamini ashatembea na mabar medi  karibia wote hapa 'KWETU BAR'.Preda alinishitua Mtima wangu.

      "Unamjua vizuri Preda?" Nilihisi macho YANGU yanaanza kutetemeka.

     "Nakwambia Jibaba linayaweza matunzo Hilo. Wanaliita Sponsa la Bar. Mimi mwenyewe nishalala nalo Kwa kila mlalo mmoja liliniachia laki tatu." Toba! Preda alikua akimwaga Siri za Mume wangu Jodi PASINA kujua kuwa mwenye Mali naumizwa na habari zile.

      "Baya zaidi." Preda aliendelea kunitonesha donda la wivu.

      "Kulikuwa na Bar maid mmoja jina lake Mwanaisha. Hilo Sponsa lilipomwona bila kuchelewa lilimjaza Mwaisha mimba. Lilipokujagundua Mwanaisha amebeba mimba yake likamruka kimanga likakimbilia mitini likagoma kulea mimba ya Mwanaisha. Mwaisha alipojifungua akalikamata na kulifosi waende wakapime DNA. kitanda hakizai haramu mtoto aliyezaliwa alikua kopyraiti . 

Basi Mwanaisha akaona hapa Dili dilisha akaanza kudai matunzo makubwa  makubwa juu ya mtoto aliyezaliwa.Lile jibaba lilipogoma Mwanaisha akalitishia kwenda kuwaona wansheria au kumpa taarifa mkewe" Preda alinipa ubuyu wa kipemba, ubuyu wenye pilipili kumbe mie mwenzie nawashwa ulimi, natetemeka macho, napata mashaka na kuugua mtimani"

     "Kwahiyo Hilo Jibaba linatoa matunzo Kwa Mtoto wa Mwanaisha?"

       "Sasa kumbe! We haliogopi!!? Linaogopa liapelekwa mbele ya Mwanasheria au mkewe kupewa taarifa Hadi liseme, na taraka juu" 

       "Mmh!" Nikaguna Kwa hasira. Yaani Jodi hataki kunipatia Millioni tano nikajinunulie gari niinjoi na kujisikia kumbe Kuna kimada amezaa nacho, kimada hicho kinammalizia pesa na mshara wake?

 Nikamuacha Preda aliyekua akizipanga panga Chupa tupu za bia pale kaunta nikamwendea Jodi alieonekana Hana amani siku hile

      "Kwahiyo kelele zote zile za kunitaka nifanye kazi ya pili kumbe mwenzangu Ulitaka pesa nitakayolipwa upeleke Kwa kimada wako Mwanaisha kimada uliyezaa nae?" Niliongea Kwa hasira na sauti kubwa karibia walevi wote walioshituka wasikie.

      "Hapana baby๐ŸงŸ hapana. I will explain..... Nitaeleza baby" Jodi akitetemeka sana.

      "Utaeleza Nini Malaya nyoko wewe? Utaeleza Kwa Mwanasheria. Nakwambia Jodi NATAKA taraka yangu." Nilipiga Tena kelele zilizowashangaza wale walevi. Sikutaka kumpa nafasi Jodi hasira zilinikaba kila pande ya shingo yangu nikaondoka pale 'KWETU BAR' nimefura mahasira sitaki tena kulisikia jina la Jodi.


..........TCHAO....

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...