Saturday, July 5, 2025

DESPERATE WOMAN

 

DESPERATE WOMAN.🥹

       Mita chache kutoka pale tuliposimama Barabara kuu pembeni Kuna kichaka kilichoota nyasi zilizokauka. Tulikua tunapigisha moshi wa Dawa 🚭pamoja na kustawisha mioyo kwa Visungura na Double kiki 🍾tulimuona Demu 🚶‍♀️flani matata akija location yetu. Kwa appearance yake 
alionekana kavalia gauni 👗Moja refu lenye kitambaa laini na chepesi lililoendana na umbo lake umbo la Kuku wa kizungu 🐓 (Modo).

       Mkono wake wa mashoto alishikilia Kikoba👜 kidogo chenye rangi nyeusi, Cheni ya Dhahabu Og iling'ara shingoni kwake, vitobo pua na hereni masikioni.

 Chini miguuni alitinga kiatu 👠Cha mchuchumio ulioambatana na vikuuku miguuni. Aliendelea kujivuta kwa mwendo wa Nyau (Cat 😺 walk) kainamisha kichwa chini, 😞huzuni flani ilifunika na kugubika sura yake nzuri, muda wote alitizama aridhi, lakini Who cares!! Ni nani anajali?🤷 Kama Mie Nyanda na kaka yangu Kabundi tuko bize kusaka mali za wizi, unyang'anyi, pick pocket na magendo.

       Yule mdada mwenye Figure ya kizungu aliendelea kuja usawa wetu, Mwendo wa Nyau haukumtoka kwenye Malundi yake.🐆🐾 Uzuri mkononi aliishikilia simu ya Iphone 19📱🧐😋

        "Oyah! Kabundi zamia huko mpakani." Nilizima kipisi changu Cha Dawa nikaamuru Kaka Kabundi afichame kwenye kichaka kidogo kilichokuwepo pale tulipozamia, alitii na mie nilifuatia, tulijipanga kumfanyia 'ambush' yule mrembo.

     "Kitu hicho mwanangu mali ya Dhahabu."Kabundi alininong'oneza sikioni.👂


     "Ulaji" 😜Nilimsapoti kaka yangu. Yule Dame alijikatisha na kutuachia mgongo.Kitu pasina kuchelewa tulinyata mfano wa Chui 🦁🐆amvamiaye Umbwa koko🐕 aliyelala. Hatua ya kwanza ilikua ni kuikwatua ile l phone 19 🤳kutoka mkononi mwake. Holla! Kama upepo vile hatukupata tabu kuinyakua ile simu, tendo lile lilikua kama vile kumsukumiza mlevi adondokee kisimani. I phone 19📱 tuliiweka kibindoni.


        Alitutazama kwa jicho la upole👁️‍🗨️ na madaha, hakusema neno, hakupiga kelele🧟 za kutuitia watu nyomi. Kawaida tumepigiwa sana kelele za 'Mwizi! Mwizi ! Mwizi' pindi tufanyapo uarifu kama ule. Hatukufika mbali mbio za sakafuni uishia ukingoni tuligeuka kumtazama yule Dada. 'Duh!' Mbona hapigi kelele 🔊🫨 za kutuitia mwizi! Mimi na kakangu tulitazamana kwa mshangao, Dame aliendelea 'kumuvu on' kwa mwendo wa Nyau kama vile yupo kwenye Jukwa la maonesh ya mavazi ya Louis Vuliton.


    'Twende tena' Uporaji ulitunogea. Tukamkimbilia. Kitendo pasina kuzembea tulizinyofoa cheni zake za Dhahabu shingoni, zilikua ni Mali ya mamilioni maana ni Og, kutoka Uingereza🇬🇧 au Arabuni 🇦🇪sio kama zile feki za Manzese na Kariakoo.🇹🇿

     "Naomba mchukue pia Pesa zangu zilizo ndani ya mkoba." 💰Aliongea wakati huo sie tuloanza kumkimbia tulijiona kama tumeupiga mwingi.🤪😜😝


 "Twende tuchukue." Nilimwambia Kabundi. Tulimvua ile saa ya Dhahabu mkononi,⌚ tukauchukua mkoba wake ambao ndani kulikua na Madolari 💵💵💵💰. Aliendelea kutembea usoni akiwa mnyonge mnyong'evu na dhaifu.


       "Whuuuza! Wizi wa Leo ni Noooma" Kaka alifurahia.🤪

      "Woooooh!"🤪🤪Tulijipagaza baada ya kuiona simu 📱 Babu kubwa tena ya bei Kali, cheni za Dhahabu na Madolari bunda💸 ya kutuheshimisha mjini kwa hakika Pombe🍺 ingetukoma, vyuku🐓 vingetukoma, vyura👩‍❤️‍💋‍👩 vingenesanesa juu ya viuno vyetu, mende wangekufa miguu juu, kwetu ilikua zari.

      Macho yangu yakatua kule anakoelekea yule Mwanadada, taa 💡🔦 ya ubongo 🧠🤯wangu iliwaka ghafla, nilihisi Kuna hatari💥 anaelekea kuitafuta. 'Mbona kama anataka kuvuka Barabara wakati Magari🚘🚗🚕 ya mwendokasi yanakimbizana. Nikamwacha Kaka Kabundi anaifurahia ile pochi yenye mapesa, nikakimbilia yule mrembo kwa kasi ya ajabu.🚀 Pale Zebra cross🦓🚸 alikua anavuka🛣️ wakati Magari hayajasimama kuruhusu watembeao kwa miguu kupita.

         Nikafanya kuwai, nikaushika mkono wake kwa nguvu zangu zote kiumeni nikamsukumia kifuani kwangu, Gari lilikuja kwa kasi ya mshare🏹 tukadondokea upande wa nje ya Barabara, ilibaki kidogo litugonge na kututupilia mbali.

       "Kwanini unataka kujiua!?"⁉️ Nilimuuliza nikiwa nimemkumbata kiunoni mwake baada ya kudamka kutoka pale sakafuni.

     "Niache tafadhali," Alinijibu akijaribu kujitoa mikononi mwangu.

      "Nikuache ili ujiue" ⚰️Nilimfokea. Kaka Kabundi alitufuata pale tulipokua tunabishana.

      "Vyovyote vile, kama mnataka mali🌟🚕💒 zangu zingine twendeni nyumbani niwape, sioni faida ya kuishi, sioni faida ya hizo mali." Lugha yake ilinipa wasiwasi 

      "Mambo moto!"🔥 Kaka aliongea kwa furaha.

      "Tupeleke please!" Kaka alitabasamu hadi majino yake Therathini  mdomoni 🦷yalichomoza, tamaa iliwaka.🎆🔥 Dame akageuza kuelekea  nyumbani 🏠 kwake, tulifuata, Safari iliiva wakati Kaka akifurahia twaweza pata mali nyingi mie moyoni nilikua nawaza kuhusu yule Dame aliyejikokota akitembea kwa huzuni.😭

Tulifika nyumbani kwake, Horofa 🏘️ya pili kati ya tatu alizomiliki. Bila woga bila wasiwasi Wahuni tuliingia ndani ya Sakafuni la sebule ile nzuri ya kuvutia kama imepakwa Dhahabu, Almasi na Lulu. Majumba ulipendeza: Kuna sofa za bei gharama, kuna makabati yenye vyombo vya China, America na Jerumani. Kuna Tv screen Moja kubwa ukutani, Zuria chini lina mvuto yaani Zuria Og. Sifa zitajaa Viroba, tukomee hapo. Kabundi alitabasamu mara Moja akakimbilia kabati la vyombo vya China macho pima akilishangaa.👀

     "Tumetajirika Nyanda." 🌟🌟Furaha yake haikumiridhika. Niliisikia vibaya kwanini tumuibie Mwanamke akiwa anatukodolea macho. 'Sio poa.' 👎 Nikamchukua yule Dame nikampeleka Restroom (Toilet.)🚻 Nikamfungia mlango kwa nje Kisha nikamfuata Kaka Kabundi aliyekua akifurahia Kila kitu chenye thamani ndani ya ile nyumba utadhani ni Mali zake halali.☺️💩

     "Kabundi nikabidhi Simu ya huyu Dame"☎️ Nilimwambia Kaka.

      "Nini!? Nikupe simu iliuongee na nani? Mbona umeanza kubadilika ghafla mdogo wangu, ucheshi uliokua nao siku zote umetoweka."🙂‍↕️Kabundi alianza kuhisi mabadiliko yangu ghafla.

     "Nipe nahitaji kumpigia mtu muhimu, yamkini mume wake. Je, huoni Dame huyu anaonekana ana stress." Niliongea.

     "Nyanda una matatizo wewe, yaani tumpigie mumewe alafu kitukute kisanga.🧨🎇🔥🥵 Tupo hapa kubeba Mali sio kupigia Simu watu." Sikujali kauli zake.

      "We nipe tu." 👿 Nilimkasirikia. Aliitoa na kunikabidhi ile Simu akiwa na wasiwasi mkubwa juu ya usalama wake na wangu."

Niliwasha ile Simu, nikaingia missed call📞 Kisha nikasechi nambari ambayo nilihisi yule Dame anawasiliana nayo sana, sikukosea niliiona Moja imeandikwa 'Habibu wangu." Nambari hiyo alioneka ameitumia sana kuwasiliana. Nikafikiria huyu atakua ndio mumewe basi nianze na yeye.

     'Driiip.....driiiip....driiiii' 📳Simu iliita. Muda si mrefu yule aliyeitwa 'Habibu wangu' akaipokea. Kabla sijajitambulisha na kuongea neno Habibu alianza kufoka, bahati nzuri niliweka loud 🔊 speaker kaka Kabundi aliyasikia maongezi yale.


      "SAMOA, UNAMATATIZO GANI WEWE MWANAMKE MPUMBAVU? 👿 NIMEKWAMBIA SIKUTAKI, SIKUPENDI, WALA SINA HAJA NAWE. MWANAMKE MNUKA KWAPA WEWE, MIE N'SHA MPATA💘 BIBI WA KITANGA ANANIPA HUBA💕 NA VITAMU VYENYE MAFUTA NA SUKARI YA TENDE NA ARUA. KUANZIA LEO STOP 🚫KUNIPIGIA SIMU. NAWEZA KUKUUA AU KUKUFANYIA KITU KIBAYA MAISHANI MWAKO, KENGE WEWE .MXIIIUUU🥴😠😵‍💫." Habibu alikata simu mimi na Kaka tulitazamana kwa mshangao uliojaa viulizo tele. ‼️‼️

      Tukiwa tungali twashangaa Ghafla mlango wa Sebuleni ulifunguka. Tulitetemeka kidogo tukijihoji wapi tufichame, aibu yaweza kutuzika ndani ya nyumba ya watu tusowajua. Lakini tulikuja kupoozeka tulipomwona mtoto👼 mwenye kadirio la miaka mitatu alkiingia pale sebuleni. Mtoto hakuonesha darili za kutuogopa alitusalimia kwa adabu na heshima Kisha akatuuliza sie ni wakina nani?

      "Sisi..... Mmmmh ......mmmh!"😎😶‍🌫️ Tulijing'ata ulimi tusijue tumweleze Nini mvulana yule  mwenye  tabia nzuri.

      "Sisi ni marafiki 💑🤞wa Mama yako" Kabundi alimjibu yule mtoto.

     "Mama yupo wapi!? ⁉️Au yupo chumbani kumeza dawa zake." 💊💉 Alitushitua zaidi tusijue Mama yake anameza dawa gani na kwanini anameza dawa!?"  Mimi na Kaka tukatazamana.👁️👁️‍🗨️

    "Hapana Dear ☺️....... Rafiki tunaweza kwenda Jikoni tuandae chai na mayai mchemsho?" 🍵🥚 Kaka alihitaji kufanya jambo la ziada.

    "Ndio tunaweza." ☑️Mtoto yule mwerevu alielekea Jikoni kuandaa chai na mayai pamoja na kaka Kabundi. Chale zilianza kunicheza 'Yamkini huyu Dame atakua yupo hatarini,⚠️ embu ngoja nimfate huko aliko chooni.  Nikaelekea Maliwato nikaufungua mlango wa chooni 🚽na kujitoma ndani.

 'Makubwa!' ⁉️😥

Nilimkuta yule Dame ameketi chini ya sakafu yenye marumaru pale chooni, chozi 😢 lambubujika, ameshikilia kikopo cha rangi nyeupe ndani Kuna Dawa 💊💊tayari kakifungua na kuujaza mkono wake kwa Dawa lukuki, bado kidogo kumeza. Nilimkimbilia na kumpokonya vile vidonge vingi mkononi mwake Kisha nilimkemea.😡😧

    "Unataka kujiua? Kwanini unataka kujiua?"😡

     "Niache Bwana, niache nimeumizwa sana, nimechoka kuishi Bora kujiua. 😿 aliongea akilia kwa uchungu.

     "Hapana Daring 💕kujiua sio suluhu ya matatizo yanayokuandama." Niliongea kwa upole.

     "Suluhu ni nini baada ya kuumizwa na mwanaume niliyempenda hatimaye kunibwaga!?" Nikamwambia 'Calm down baby' nitakusaidia. Kisha nikaendelea kunena.🗣️

      "Kumbuka Bado unae mtoto mdogo anayehitaji mapenzi 👩‍❤️‍💋‍👨ya Baba na Mama Sasa wewe hujui ni nani  atakayeonesha upendo kwa mwanao, ikiwa Baba yake mwenyewe haeleweki,  nani atamuelewa mwanao? Aliinua macho yake kisha akanitazama kwa uchungu mkuu, akaanza kulia kilio cha Kwi Kwi Kwi uwiiii! 😿😭Hisia za uchungu zilimpanda.

      "Hivi Samoe unajua ni kwanini mimi Nyanda na kaka yangu  Kabundi tunavamia watu mitaani tukiwapora na kuibia Mali zao. Unafikiri twalipenda jambo hili?⁉️ Hapana, tunasababu zetu na sababu zetu zinatuumiza. Nikaanza kumwadithia kwa ufupi Story yetu sie wenye dhiki.💩

       "Mama yetu alipokua hai tuliishi kama Malaika ndani ya Bustani ya Edeni.🏡 Kila hitaji letu nyumbani tulilipata: Kila hitaji letu muhimu na liso muhimu tulilipata : chakula, 🍔🥙manywaji,🍷🍶🥂 malazi,💤🛌 pesa, 🏧💰amani, upendo na furaha. 

Ghafra Mama yetu alipata homa kali, Mola akamchukua mambo yote mazuri tuliyoyapata pale nyumbani yalibadilika na kuwa ovyo.🤬 Baba alianza kuondoka Alfajiri na kurejea usiku wa manane akiwa Bwiii! Kalewa chakali, 🍻hapo haulizi Wala hajui, tumekula Nini!? Tumevaa  ninii? Je, twahudhuria masomo shuleni!? Tumepata ule upendo, amani na furaha⁉️ Hakua  na muda huo Baba yetu. Kwa ufupi Baba yetu alituacha njia panda, hakuna jipya tulilolifurahia mbele zake.

Kwa sababu tuliachwa ilitubidi tuanze kuhaso tungali makinda ya Darasa la tatu na nne. Kuiba ikawa ni kazi yetu, kutekanyara, kupora na kuvamia likua kawaida kwetu. Huwezi kuamini hadi ukubwani tumeikomalia hii shuhuli hatarishi inayotutia wasiwasi juu ya kesho yetu. Kwahiyo Daring mimi nipo tayari kukusaidia.💕

     Nilimfuta chozi na kumpokonya vile vidonge alivyoshika mkononi, Kisha nikavitupa ndani ya sinki la kunawia mikono. Vidonge vile sometime vilikua vinampunguzia strees, masikitiko na mawazo juu ya Habibu mumewe.
    
     "Have peace Samoa." Nilimpooza  nikajitambulisha tena kwake: 'Niite Nyanda' akachangamka kidogo🌞☺️'Mimi Samoa' Samoa alijitambulisha pia, moyoni nilihisi ushindi utapatikana tu hata kwa ncha ya Upanga.🗡️🔪

******:::::::::::::*******

     Basi kuanzia siku ile mimi Kabundi na kaka yangu Nyanda tulianza kumjenga kisaikolojia  Samoa na uzuri wa sie 'Shameless men' tukafanya kuhamia nyumbani kwa Samoa. Tulifanya kila tendo na kila neno la kumrudisha Samoa katika ubora aliokua nao zamani.

     Tiki ikatiki🫰✔️ kwa ubora wa mashauri yetu Samoa alianza kupona kisaikolojia. Mimi nae nikaona hapo Sasa ni nafasi ya kujiongeza. Nikajenga ukaribu  na Samoa akanipokea na kuniweka moyoni mwake, penzi likazaliwa likapendeza na kumea kama Maua  bustanini🌺🌹💐. Samoa akawa ni mtu wa furaha, Raha na amani tele. Hakuwa na muda wa kumuwaza tena Ex- Husband  wake Habibu bali aliniwaza mie Nyanda.


    Uzuri kumbe Samoa alikua anamiliki  Kampuni ndogo,  hilo likaleta 'Blessing' zingine kwetu. Kaka Kabundi akapewa Umeneja wa Kampuni ya Samoa mie nikapewa cheo cha juu  ndani ya Kampuni, 'General Director.' Aki! Maisha yakaanza kutunyokea  from Zero to Hero, Waooo! Leo hatuwapoli tena Raia, hatuwanyag'anyi  au kuwaibia Bali twaendesha Magari ya fahari, utajiri na pesa 💰💰🏧 zimetutembelea hadi zinatuogopa.


     Huu ni mwaka wa tatu tangu mie na sweet Love 😘 wangu Samoa tuingie penzini🔥 miezi miwili ijayo anatarajia kuingia Leba, Mtoto 🤱 tunaye na kutamba tunatamba naye👌💕😹. Nashukuru Mola Samoa alikua anataka amani, upendo, furaha na Raha vyote hivyo sasa amevipata na pia vimerejea baada ya kuvipoteza akiwa Desperate Woman  (Mwanamke Aliyekata tamaa.)



"************
TCHAO 

 💖 LOVE  MUST LEADY

"************
 





No comments:

Post a Comment

OBIMO CHETA

 OBIMO CHETA (MY LOVE REMEMBER). Siku Derila alipokutana na Singa, ilikuwa ni siku nzuri, siku ya kusheherekea sikukuu ya Christmass,🌲🎄⛪...