Monday, July 28, 2025

OBIMO CHETA




 OBIMO CHETA


MY LOVE REMEMBER 💕

Tulipoishia

Nisamehe Derila.”Singa alilia akipita pita ndani ya kiijiji chao, kijiji cha Maasai Land,wanajamii wakiendelea na shughuli zao za kijamii, wanawake walionekana wakijenga nyumba, wengine waskikamua maziwa, vijana wadogo wakirejesha mifugo nyumbani kutoka malishoni, wakati wazee wakiketi vikundini wakijadiliana.

           

             ***************

Sehemu ya Sita


        “Ondoka tu, ondoka kama unavyotaka Mwanaharamu wewe.”Babaye Singa aliongea, ni mwenye hasira, anachukia kwa sababu ya umasikini, anamchukia mwanaye, anamuona msaliti.


        “Nenda huko huko unakokuita mjini umeshindwa kuniletea mifugo nyumbani unaniletea majonzi na masikitiko.” Baba aliongea kwa haasira.


        “Nitarudi na utajiri safari hii Baba yangu, wala hautalala njaa tena, hautalalamika wala hautanisema kwa ubaya.”Singa akiwa tayari anaondoka kuelekea Arusha mjini.


        “Nenda zako mwanaharamu wewe, hufai kitu, wewe ni zigo ndani ya nyumba hii, wenzio wanawaletea faida wazazi wao, wewe unaleta hasara kutoka mjini.” Baba alipiga kelele, Singa hakuwa mtu wa furaha tangu aingie kijijini amekuwa ni mtu wa huzuni, maneno na masimango. Leo hii amebeba kibuyu cha maziwa pamoja na mapande ya nyama ambayo mamaye amemuandalia, anaondoka na kupanda basi la kijiji, basi kuukuuu, japo lina mwendo wa kufika pale Arusha mjini.

~~~~~~~~~~

Singa alikuwa akipeleleza huku na kule akimtafuta mpenzi wake wa zamani Derila apate kumpigia magoti amwombe msamaha, Jua linachomoza, Jua linazama, Singa hajapata kumwona yule amtafutaye, mvua nayo inamsulubu, inamnyima raha na furaha ya kumwona yule amtakaye, siku ya tatu leo anapeleleza peleleza kati kati ya jiji, juu ya pahali anapoishi Derila huyu mwana mama mwenye sauti iliyowateka Watanzania, Wakenya na Waganda, Warwanda na Waburundi, hapati kujua pahali walipo.


        Lakini ghafla Singa analiona tangazo, tangazo limebandikwa ukutani nalo linasema:


        “Mwanamama mwenye sauti tamu ya kuvutia wengi atakuwepo akitumbuiza Makumira tarehe 25/4/2024..” Waoooh! Singa alirukaruka na kukiondoa kile kibandiko/tangazo, akaibusu ile picha ya mwanamama aliyerembwa akarembeka, Derila ndio jina lake.

                                ***********************************

        “Rejea tena, rejea mpenzi,

         Rejea, rejea, rejea,

          Nayakataa mapenzi yote,

          Nawakataa wapenzi wote,

           Kwako wewe narejea.


           Nipokee, nipokee, nipekee,

           Nipokee mpenzi wangu,

           Bado ningali ninakupenda.”


Ilikuwa nio sauti tamu ya mwanamama Derila, maelfu ya wale wote waliohudhuria tamasha lile waliburudika, walimpongeza na kumsifu Derila. Walimpigia makofi na kufurahi pamoja naye. Moe-Joe alijivunia kumtoa huyu mrembo ilikuwa ni neema kwake, anapata pesa nyingi zinazotoka kwenye mgongo wa Derila, Derila pia hana shaka, mialiko na matamasha ni mengi, anavuna alichostahili kuvuna, Uche ni mwenye furaha na uzuri wa muziki anaoimba Derila, umefanya apatane na wazazi wake Baba na Mama yake wale waliomfukuza na kumtupilia mbali leo hii wamemsifu na kumwongelea kwa marefu na mapana.

                    ++++++++++++++

        Derila akiwa jukwaani anaimba wimbo wake asloupa jina la “Rejetena.” Mara ile alimwona mwanaume kijana amevalia mavazi ya utamaduni wa Kimaasai, ana sime kiunoni, amesuka rasta za Kimaasai, ana shanga nyingi na vito vingi vya Kimaasai miguuni, mikononi na shingoni mwake. Derila alimtambua, sio mgeni machoni kwake, anamjua vizuri sana mtu huyo anayepita katikati ya kundi la watu ili apate kufika pale alipo Derila, Moyo wa Derila ulikuwa ukienda kasi mara ile yule mtu alivyokuwa akija, ni mweusi wa rangi, meno yake ni meupe peee, ana urefu na wembamba wa mwili.


        Derila alitamani kuacha kuimba Ili apate kumkimbilia, uvumilivu ulimshinda mara ile alipomwona Singa akija kwa kasi juu ya ule ukumbi, akafurahi sana Derila, furaha iliyoendana na mapigo ya moyo wake, Walinzi waliojiweka tayari kumlinda Derila hawakutaka Singa amsogelee Derila, walidhani anaweza kumletea fujo na kumdhuru, hivyo wakamwamuru kinguvu arejee pale alipotoka.


        Derila kuona Singa wake anasumbuliwa, hakufanya ajizi, aliacha kuimba na kumkimbilia yule ampendaye. Oooh! Akamrukia na kumkumbatia, wawili wale walishikana kinguvu, wakitizamana na kulia kama wendawazimu, umati wela watu uliohudhuria burudani ile uliwatizama kwa hisia nyingi sna.

        “Nisamehe My Love.” Singa alilia na kuomba radhi.

        “Nilikwisha kusamehe siku nyingi mpenzi wangu, bado nakupenda.”Derila alilia, watu walizidi kushangaa.

        “Nimekukosea mpenzi.”

        “Wala usijari Singa wangu, yaliyopita wacha yapite, sie tuendelee na safari yetu ya kutafuta maisha.”Derila alimbusu Singa kwenye mashavu yake, Derila kwa ule wingi wa Furaha alishindwa kuendelea kuimba, akaondoka pamoja na mpenzi wake wa zamani Singa, watu walifurahi na kuwapigia makofi wale wawili waliopendana, Singa na Derila, wakapanda gari moja nzuri ya fahari ambayo Derila alinunuliwa kama zawadi kutoka kwa produce wake Moe-Joe.

        Walihitaji kwenda kwenye nyumba anayoimiliki Derila, amejenga Derila, amejenga maeneo ya Majengo na uzuri wa siku ile Derila alipigiwa simu akiambiwa kwamba Uche mwanaye mpendwa amerejea kutoka kwa Bibi na Babu yake huko Usa River. Derila alifurahi, alifurahi furaha ya kutaka mpenzi wake wa zamani amuone mtoto jinsi wanavyorandana, wanafanana sana, hakuna mfano.


        Simulizi hii ya kusisimua inaishia hapa, inaishia pale tulipomwona Derila alivyokuwa na moyo wa msamaha, ajabu mapenzi yake ana machozi ya karibu, ana msamaha na huruma, ana moyo wenye upendo mkuu, alikubali shida zote, tabu na mateso, alikubali kuitwa ombaomba, alipojikita kwenye muziki, akajibidisha, akatoboa na kubomoa, akawa juu, hata pale mafanikio yake yalipozidi kuongezeka Singa akajitokeza na kumpatia msamaha, furaha yao ikaongezeka, raha yao ikarudi tena, tayari wamesameheana, Derila anampenda sana Singa, na uzuri wa Derila hachoki kumpatia pesa mingi huyo mpenzi wake wa moyo wake aitwaye Singa, anampenda sana, pesa anazompatia Singa huzitumia vizuri, Singa huwapelekea Baba na Mama yake waliochekwa kwa umasikini, tizama sasa wamefurahia utajiri unaokuja wasijueni wapi unapotokea.


MWISHO


MWENZENU N'SHAPENDWA




MIPASHO YA MAMSAPU 


MWENZENU N'SHAPENDWA 


Tulipoishia


        Sasa shoga zangu ikawa siku moja mie nipo barazani nachambua chambua mboga ya harage kwetu twaiita Nguniani , nikitwanga twanga kipome au kwa kifupi karaga za kuchanganya kwenye Nguniani, nikatembelewa na ugeni nyumbani. kanijia huyu mwanamke anitishaye surani, mmh! kwa mwonekano wake si ningelimwita chizi mwenda wazimu, lakini aka! yatanikuta mie, nizibe mdomo wangu, sio kila neno kuropoka.



SEHEMU YA SABA

            Mgeni huyo kakonda na kudhoofika, kaja na manywele tipwatipwa, yamekosa dawa ya nywele, yana rangi ya udongo na kipilipili si ni heri na mie Mama la kitanga ninayezisuka nywele zangu zisipoteze uzuri wake. Si ni heri na mie Mama la kitanga ninaye nenepa na sasa nina kibedi tumboni,🤰 basi mwaya huyu mgeni asiyetamanika kanivalia nguo kuukuu na kandambili zilizokwisha na kuchanika kisiginoni, mavazi yake machakavu kama tambala la dekio, kabeba kirago chake kichwani kufika tu naye kakitua hicho kiragoche pembeni ya mlango wa nyumba yetu mie na wangu wa rohoni💕  pompo.


               “Mgeni karibu,” nilimkaribisha nikijua fika kuwa huyu ni mhitaji ana shidaze, anahitaji msaada kusaidiwa.


                 “Asante mke mwenzangu,” 


                “Mmmh!” Mie kuguna. Kanishitua kwa kaurize amabazo nalishindwa kumwelewa, mie nikatamka,


               “Mbona sikuelewi mgeni kwa lako tamko?”


                “Utanielewa tu, kwanini usinielewe, wakati mie nimefuata mali yangu.” yule bibie mnuka domo, vundo kwapani, na ukurutu mwilini kanijibu kwa nyodo za mwanamke


                 “Bibi, unashida gani nikusaidieni?” Niliongea kwa ukali kidogo, nikatamka tena,


                  “Nisikuelewe Kiswahili unijibucho!” Nikamwambia, nikimshangaa yule bibi mwenye sura mkomavu ambaye hata salamu hajanigea.


                  “Mbona ninaeleweka, au unataka kunielewa kwa manati” Alinijibu, kisha kaendelea kuongea.


                  “Kwanza kabisa Pompo nampata?” Alinishitua kulitaja jina la roho wangu.


                  “Wamjua?” Niliharakia kumuuliza


                  “Vema sana, tangu zama za kale za mawe, kabla weye kumjua.” Alinijibu, bahati mbaya moyo wangu Pompo hakuwepo nyumbani, nalikuwa mpweke mbele ya huyu mgeni mwenye komwe kitisho, anitishaye kwa manenoye.


               “Wamjuaje, eeh!⁉️ Mwanamke?”Nilihoji tena,


              “Bibie nielewe mie nasema wewe kwangu ni mke mwenza, labda Pompo hajakueleza kuhusu mkewe wa kwanza Maua ndo’ mie hajapatikana mwingine zaidiye.” Yule Bibi mwenye sura mkomavu aliongea.


‘kumbe huyu ndo’ bibie Maua, Yule msaliti aliyelewa maneno ya mashoga na mashangingi wa Jiji’ Nalijisemea mie na moyo wangu.


              “kwa hiyo umefuata nini kwenye nyumba ya yule aliye kwisha kupendwa?” Nalimuuliza Maua.


              “Mashallah! Nimemfuata yule nimpendaye, tena nasema hivi bibie usiyempenda kaja, Kaja na gia zake, hapa siondoki hapa namwaga mafuriko.” Yule bibi mwenye sura mkomavu, alijaribu kunitisha. Aki! kweli anasura mkomavu nasema Shoga hata akipaka Rosheni itamkataa. Mmh! Kababuka kawa majivu majivu, podali imemkataa. Teeh teehteeh!🤣🫢 Ai! nicheke mie.


                “Teeh teeh teeh,” 😂Mie nikacheka kwa uzuri zaidi, kwa cheko la kimapozi na kebehi, nikimrembulia jicho langu, jicho kungu babu we!, nikimpasha ajue fika kuwa mie n’shapendwa.


               “Nadhani umeruka njia bibie, umeruka ukuta, upofu umekutafuna,” Nikaendelea kumchamba.👌


              “Labda niseme ushachelewa, ndege ishakuacha na hata ikirudi tena bibie lazima ikukatae maana weye jasusi mtu mbaya uso na mapenzi hufai kuigwa,” Maua alinisikiliza, domo kunuka hiyo ni ishara ya njaa kumkamata.


             “Pompo kanieleza kisa chako chote,baada ya kisa mkasa uliyataka weye na roho yako, ulichagua kudanga na kutanga tanga na njia sasa yamekushinda eeh, ya kwetu utayaweza” Nili mnanga ka vile n’shamzoea kitambo.


            “Bibi uso yajua yatakusumbua, hivi weye walijua penzi la mie na Pompo lilivyokuwa?” Maua kaniuliza.


          “Halikuwa, bali kwa umbea, kwa magubu na masimango ya shogazo ndo’ ukamfanyia yaya huyu muuza kahawa, leo umesikia ati katajirika na weye ushaona heri umrejee?” nikamsuta yule bibi mwenye sura mkomavu, nikamchamba tena.


            “Si ulisusa wenzio twala, bibi hapa umefika kula huli utishia kunawa, tena uniondokie haraka kabla Ibilisi wangu hajapanda” Nikamfokea Yule bibi aliyekuwa akinitizama kwa matamanio ya kunipoka roho wangu.


            “Wanijua mie weye?” Maua kapandisha shetani, hasira zishamjaa.


                “Nikujue kwa faida gani? Mbovu weye, mbovu uso na akili za kupenda, miaka mitisa yote hiyo ulo mtelekeza kampata ampendaye tena enenda ukawasimulie na hao shogazo walo kupotosha na kukuacha ‘dillema’, njia panda, kawaambie ulomkata kampata alomkubali” Naliongea kumthibiti shwetaini wake.


             “Sema nini hunijui miye mtoto wa kizaramo, umbwa weye nitakufanyizia kitu mbaya, kwa taarifayo Pompo atarejea mikononi mwangu.”


          “Una wazimu nini weye? Au ushalewa na kupagawa, atinikujue mtoto wa kizaramo, enyooo! Weye ndo’utanijua miye mtoto wa kitanga, kamwe Pompo hawezi kuwa tayari kuyarudia matapiko alokwisha kuyatapika, teh teeh teeh (nikacheka kimadoido), bibi umeruka mkojo na kuyakanyaga mavi, teeh teeh teeh (nikamcheka kwa dharau, na kejeli nikiubetua mdomo wangu kumfyonya.) Ushaingia choo cha kiume sasa subiri wanaume wakuchangamkie, punga weye, bwabwa ulokosa soko.” Nikamkejeli nisitake anitie machoni,


              ‘Piiiiiiii piiiii piiii’ Ilikua ni sauti ya Tax ya roho wangu Pompo Keisha kuja , yupo mlangoni anapiga honi apate kufunguliwa, Jose mlinzi wangu, mtoto wa miaka kumi na mitano kamfungulia Pompo Pompo kaingia na kuipaki gari yake pale alipozoea kuipaki kwisha kufanya hivyo akaja pale naliposimama na huyu bibi mwenye sura mkomavu.


                Maua kumwona Pompo akalitupa begile kuukuu chini, akamkimbilia Pompo, kwisha kumfikia akamparamia mwilini, Pompo Kamshangaa mwanamke huyu, akamtoa haraka haraka na kumtupa chini kama zigo la taka taka, alikwisha kumtambua kuwa yule ni Maua kaja kumchefua.


             “Nisamehe Pompo, nisamehe mume wangu,” Maua alilia Machozi ya uchungu, mie nikamsogelea Pompo nikatua ubavuni kwake tukimshangaa yule mwendawazimu.


           “Nikusamehe kwa lipi baya au lipi zuri Maua? weye si ulichagua njia zako na sasa uzirudie hizo njia ulizojiendea.”


            “Pompo ni Ibilisi ndiye aliyenipitia,tafadhari rudisha moyo wako kwangu.” Maua aliongea Mie kimya nayasikiliza maongezi ya hawa wawili waliopotezana miaka na miaka.


            “Nawe enenda ukampitie huyo Ibilisi aliyekupitia. Sikia Maua n’shampata wangu wa mapenzi, yeye ni huba langu, moyo wangu, roho na nafsi yangu. Yeye ni mahaba na mapenzi yangu, huyu hapa ubavuni kwangu, ninampenda sana nisitarajie kumuumiza na kumuacha.” Pompo akanikumbata na kunipiga mabusu niliyoyapokea kwa dhaati yakamchoma yule msaliti yakamuuma na kumtia kijicho.


          “Najuta Pompo,najuta kwanini niliwasikiliza mashoga zangu, sikujua kuwa wale ni wanafki, wabaya wenye nia mbaya kwangu.” Machozi yalimtoka Maua angali pale chini ni mwenye huzuni.


            “ Sasa ushajua kuwa wale shogazo ni wanafki wabaya wenye nia mbaya kwako?” Pompo alimuuliza Maua.


             “ vemaa kama utawafuata, hao hao uliowasikiliza sana kuliko mie niliekupenda. Maji ushayamwaga ushindwe kuyazoa, tena ondoka hapa nyumbani kwangu, usiniletee mizigo nisiyoweza kuibeba.”Pompo alimjibu Maua, wakati huo huo akimnyanyua pale sakafuni apate kumwondoa aende zake huko alikotoka


            “ Usinitese Pompo, usinitese uliyekuwa wangu, nipe tena nafasi moyoni mwqako nirejee.”


             “Huna akili mwanamke, siwezi kupenda wawili, siwezi kuyarejea matapshi niliyoyatapika, tafadhali nifute na pia nisahau moyoni mwako, wewe ndiye uliyenitesa, umetanga tanga sana na sasa umeona heri urejee baada ya kupata dhiki za dunia.” Pompo alifanya kumsukuma Yule mpuuzi.


            “Ondoka ondoka nyumbani kwangu.” Pompo aliongea kwa sauti kuu.


              “Usinifukuze Pompo dunia imenifunda, sina mbele sina nyuma, sina pa kulaza kichwa change sina chakula change,” maua aliongea . Pompo hakujali kuhusu matatizo ya Maua akamwita mlizi Jose mlinzi wa lango kuu la kuingilia nyumba ile, akamwambia amwondoe Yule msaliti, Jose akafanya kama alivyo agizwa.


           “Please Pompo please nipokee tena.” Maua aliongea.


            “ Rejea kwa hao waliokupokea hapo awali, watakupokea tena.” Pompo alimjibu Maua.


              “Nimekataliwa, nimekataliwa na ndugu ,jamaa na marafiki, NITAKWENDA WAPI MIE Pompo? Nina kutegemea wewe pekee. “ Maua alilia kwa sauti kuu.


              “Na mimi ninakukataa nisikutake tena, ulipenda sana starehe hukunipenda mie sasa wanidai nini kingine? Sina unidaiacho, nimeridhika na huyu niliyemwomba Mola anipatie.” Pompo aliongea akanikumbata kwa mapenzi yote.


            “Pompo…Pompo… Pompo… please.” Maua alikwisha kutolewa nje ya lango kuu la kuingilia nyumba ile. Ni mwingi wa huzuni na kilio, anaijutia roho yake, anayajutia maamuzi yake, maamuzi aliyokwisha kuyachukua hapo awali yana muumiza, haki majuto ni mjukuu na sasa leo anajuta.

Itaendelea

               ###################

I MISS YOU CHUGA

 CHOMBEZO






: I MISS YOU CHUGA

Follow :

SEHEMU YA KWANZA



ILALA, DAR -ES -SALAAM


ILIKUWA YAPATA SAA KUMI NA MOJA alfajiri⏱️ nilikuwa nimelala na Mume wangu Jerome milalo yetu siku zote ni milalo ya kaka na Dada, sababu simpendi Jerome na kutokana na sababu kuwa simpendi Jerome nimekuwa mvivu wa kumpa unyumba. Namnyima mapenzi ninampatia pale tu nikijisikia wala sio yeye akijisikia sababu ya kumnyima mahaba Jerome ninaijua mie mwenyewe, ninamchukia sababu mapenzi hayawezi, ni goigoi mapenzini, kimoja tu tayari keisha choka, kimoja tu ndio baaasi,😂 hawezi na wala kamwe hatorudia hadi kesho majaliwa.

 Ndio maana simtaki Jerome, haniridhishi wala hanipi raha za kutosha, ananiachia maumivu ya kukosa penzi nono, ananiacha nikiweweseka kitandani, bado dudu washa washa lamwitaji mwanaume. Any way nilidamka pale kitandani nikaeleka mezani sehemu ilipo simu ☎️yangu aina ya Samsung Touch screen, nikacheki nani mpigaji👁️


 Uwii! 🤔Moyo uliniidunda ndu! Ndu! ndu! Roho ikaniambia “Umwoni mumeo, labda hajalala, usipokee simu, nenda chooni kaipokee uongee na mchepuko wako, maana Jerome akisikia juu ya maongezi yenu atakuuwa 🔪 Mwanaume yule.”


 Basi mie SONIA nikaichukua simu yangu nikaeleka chooni ili nimsikilize OBI mchepuko wangu huyu ndiye anipaye raha za ulimwengu. Obi ni kijana mmoja mrefu kiasi, mwembamba sana, mzuri wa sura, mambo anayaweza sababu ile kitu yake pale kwenye UNO, ni kitu mkono wa mtoto mchanga inanipagawisha kweli, inanipa raha, inanisugua vizuri, inaniondolea stress na pia inanipunguzia miwasho ya kwenye kitumbua changu.Haki jamani Obi ameniteka.

 Lakini kuna kitu kimoja ninakichukia kuhusu Obi, Obi amenigeuza mie BANK ATM. 🏧Obi ananichuna vilivyo, ananilia pesa mingi hanipi penzi bila kumpa pesa, ananinyima nisipompa pesa na mie Sonia ninahitaji kitumbua changu kiliwe chote niwe regerege tepetepe, ujiuji mrenda. 🥲


 Kwake Obi mie siwezi wala sijiwezi, Uzuri wa Obi mambo ananipa tofauti na Jerome Mume mwenye Kibamia mambo hayawezi, vyakula bora hali, mazoezi hataki kufanya, yupo yupo tu kama goigoi punda mzigo.🐎

 Basi mie Sonia nikatoka mle chumbani, kwa tahadhari, nisije nikamwamsha JEROME, niende kumsikiliza Obi anashida gani alasiri yote hii kama ni pesa leo lazima nigome kumpa, na tena kwa lazima namwambia nimechoka kumpampa pesa, hanipi ile dudu mkono wa mtoto mchanga bila pesa, ah! Nimechoka jamani ananiudhi mwanaume huyu wa Dar yaani ananiuzia dudu? Ndivyo walivyo wanaume wa Dar.


 “Hallow!” Nikiwa chooni choo cha uswahili huku kwetu SHARIFU SHAMBA niliipokea ile simu, nikiongea sauti ya chini, majirani wasisikie, wala mume wangu Jerome asije akashitukia. Asije akagundua kuwa mkewe nina Mchepuko.

 “Hallow! Naongea na Sonia?” Mungu! Nilishituka Kidogo, sauti ya mpigaji ni ngeni masikioni mwangu japo simu ya mpigaji ni Obi Mchepuko wangu kama nambari zake zinavyojisoma juu ya Screen. Nilijiuliza Nimjibu au nisimjibu? Hapana, mtu hakatai wito, nikamjibu.


 “Yeah, mie ni Sonia wewe nani mwenzangu.”

 “Unaongea na Polisi👮‍♂️ hapa kituo cha PANGANI ILALAA BOMA. Je unamfahamu mtu anayeitwa Obi? Maelezo yale yalinishitua kidogo nikajiuliza Obi Mchepuko wangu amefanya nini jamani hadi akamatwe na Polisi?Jamani Mchepuko wangu ana kosa gani? Moyo wangu ulijaa wasiwasi

 “Ndio nina mfahamu, kwani Obi amefanya nini?” nilimjibu na kumuuliza yule mtu aliye jitambulisha kwangu kama Askari polisi,


“Wewe njoo hapa Pangani kituo cha Polisi utapata maelezo zaidi, kwa kifupi mtu wako wa karibu amewekwa ndani ana masaa machache sana kabla hajapelekwa Mahakamani, basi fanya, faster kabla Jahazi halijazama.” 🚣⛵Yule Polisi aliongea, hakutaka kuongea zaidi na mie nikamjibu nikamwambia ninakuja akakata simu.


 Ooosh! 😤nilivuta pumzi ndefu nikaiachia nikiwa bado nimejibanza ndani ya kile choo cha uswahilini, choo chenye mlango wa gunia, moyo mapigo, huzuni ilinijia, nikatia hofu juu ya Obi Mchepuko wangu yule kijana mrefu mwembamba mweusi tii, mwenye dudu tamu, dudu 🍆ndefu nyembamba inayonikosha mie nami nikakosheka, Nampenda Obi kuliko huyu Kibamia wangu Jerome najisikia furaha nikiwa na Obi kuliko huyu Kibamia wangu Jerome. Some time najikuta nikijilaumu kwanini nilikubali kuolewa na Kibamia Jerome? Kwanini nisiolwewe na Obi? Mtu anisuguaye kitumbua changu hadi Napata raha, Jamani bahati hii isinipite.

ITAENDELEA.

Thursday, July 24, 2025

OBIMO CHETA

 


OBIMO CHETA


Sehemu ya tano


Mimba ya Derila ilikuwa kubwa, kubwa tena ya kutaka kujifungua, hakuwa na jinsi, kuombaomba ndio kazi, kazi ya kumpatia Riziki yeye na Frank. Hawana pahali pazuri pa kuishi, popote pale penye nafasi wanalala kwenye maboma, majengo ambayo hayajakamilika kujengwa, Derila haachi kumuwaza Singa, amemmisi sana, ni muda mrefu hajamtia machoni.


        Leo yupo ndani ya Boma, wamelala yeye na Frank, hawana kitu zaidi ya chungu na sufuria wanayotumia kupikia ugali, hawana kitanda wala godoro, wanalalia maboksi, mbu huwachosha, popo huruka ruka, mbwa na paka nyakati za usiku huranda randa kutafuta riziki yao. Leo ameshindwa kwenda mjini kuomba omba, badala yake ametulia ndani ya boma wanalolala, na baada ya mda aliamka kuchambua chambua mboga za majani akazikata kata na kuzibandika kwenye chungu chao kikuukuu. Mboga hiyo (sukuma wiki) ilipoiva iliepuliwa, na baada ya kuepuliwa, Derila alitenga maji ya ugali.Frank atakuja mda si mrefu kula kidogo alichokuta, na baada ya hapo Frank angelirudi tena barabarani kuimba na kuomba omba wapitao njia vijisenti viwili vitatu.


        “Oooh! Oooh! Oooh!” Derilka alianza kuhisi kama tumbo lake linachezacheza naye akapumua kwa kasi, akaendelea kuusonga ugali.


        “Oooh!” Alilalamika Derila, tumbo lake lilikuwa kama vile linanguruma, kitu kinatembea tembea na kumkanyaga kanyaga, ilimbidi aache kupika ule ugali, nguvu zilimuishia, akajilaza juu ya boksi moja walilotumia kulalia, uchungu ulimkamata, alianza kupiga kelele za kuomba msaada.

 Nani aliyejitokeza, hakuna aliyejitokeza, eneo analolala yeye na Frank hakuna watu wengi, ni eneo lililojificha sana, hata wao wamejificha kwa sababu pahali hapo sio pao. Frank alikuwa akikaribia kurejea hapo kwenye Boma lao, alisikia sauti ya mwanamke aliyekuwa akiomba msaada, haraka haraka Frank alielekea kule sauti ya kilio cha Derila iliposikika. Oooh! Alimkuta Derila yupo katika uchungu mkuu, analia peke yake, analia damu zikimtoka na kupita juu ya lile boksi alilolalia Derila.


        Frank alipofika alimkimbilia Derila na kumuuliza;


        “Tatizo nini Derila?”Frank alijaa hofu na mashaka asijue nini afanye kumsaidia Derila.


        “Nisaidie Frank, sina pa kwenda, Hospitali ipo mbali, sijui nifanye nini mie?”Derila alilia kwa uchungu. Frank akaangaza huku na kule akauona ugali unaungulia, haraka haraka akauepua na kuuweka pembeni, kisha akaenda pale alipolala Derila, akamlaza vizuri asijue la kufanya.


        “Sijui Derila, Sijui kuzalisha mie, sijui mambo ya udakta.”Frank aliongea, ni kijana mpole, hata sauti yake imejaa upole mwingi.


        “Nisaidie, hakuna mtu wa kunisaidia, uwiii, uwiii, Yalaah!”Derila alilia kwa uchungu, amelala pale juu ya boksi lililojaa damu.

        ****

        “Ok, mtoe, mtoe basi Derila.”Frank aligeuka Daktari, amekinga mikono yote miwili, anamsubiria huyo malaika atakayekuja.Derila aliendelea kulia kilio cha uchugu. Ndani ya dakika tano zilizofuata, Frank alikiona kichwa cha mtoto kinaanza kuchomoza.


        “Ameanza kutoka, kazana Derila, kichwa chake kimeanza kutoka, je nimvute?” Frank aliongea, hajui kitu, amechanganyikiwa.


        “Hapana Frank, usimvute, atatoka yeye mwenyewe, ukimvuta atapatwa na madhara makubwa.” kisha Derila akaendelea kulia. Frank alikuwa na subira, akamsubiria mtoto, mtoto akatoka tumboni mwa Mamaye, naye akalia kitoto kitoto ‘ng’aaa, ng’aaaa-ng’aaaa.” Hiyo ni ishara ya kwamba mtoto yupo hai, Frank akatabasamu, Derila akachekacheka na kukipakata kitoto chake.

                        **************


MIAKA MITSTU MBELE


        Miaka mitatu imepita sasa, tangu Derila amezaa mtoto mzuri wa kiume aliyempa jinale ‘uche’, mtoto huyu mzuri amefanana kila kitu na Babaye mzazi Singa. Anacheza cheza pembeni ya Mamaye ambaye wakati wote huo ni mwingi wa mawazo, anawaza juu ya mpenzi wake Singa, anamkumbuka sana Singa, hana amani wala hana furaha juu ya penzi liolilopotea na kuzimika mikononi mwake.


        Mara ile Derila anamkumbuka Frank, machozi yanamtoka, masikini loh! Frank yule kijana aliyekuwa ndoto za kuja kuwa Mwanamuziki mkubwa sana ndani ya Afrika ya Mashariki pamoja na Afrika yote kwa ujumla, ajabu mipango ya Mungu.

 Derila analia akikumbuka ile siku anashuhudia Frank akikata roho yake mbele ya macho yake. Ooh! Masikini ya Mungu, ajari ya Gari lililokimbia force force kuingia eneo ambalo wao wameketi kuomba omba kwa waja wake mwenyezi Mungu.


        Derila alipona,  mwanaye Uche alipona pia, ajari ile ilikuwa mbaya ilitafuna uhai wake Frank, masikini Frank alikata roho yake mbele ya Derila, masikini Derila akalia na kuomboleza kifo cha rafiki mwema kama Frank.


        Wakati wote huu, miaka mitatu baada ya kuzaliwa Uche, Derila hakuacha kuwekeza kidogo kidogo alicho nacho, na Mungu yu mwema, haba na haba hujaza kibaba, alipata pesa ya kutimiza mapenzi ya rafiki yake mpendwa Frank, mwanamuziki kwake na daktari kwake, msaada na faraja kwake, Frank aliahidiana na Derila kuingia studio, kufanya kazi ya kuimba, hata kama walitamani kujaribu, waliamini kuwa kujaribu sio kushindwa, mbuyu ulianza kama mchicha.


        Yule omba omba aitwaye Derila aliingia studio, amejiandaa na kujipanga aimbe wimbo wake, wimbo mtamu uliojaa mapenzi.


        “Nimekumiss mpenzi,

         Nimekupenda sana,

Nitakua pamoja na wewe

Wakati sio muda


         Uwe na mimi mpenzi,

         Uwe na mimi Baby,

Nitakua pamoja na wewe,

wakati sio muda.


         Nilikumiss miss kumiss,

         Nilikumiss Baby,

Nitakua pamoja na wewe

Wakati sio muda.


Waooh! Ile sauti yake tamu, tamu ya kumtoa nyoka pangoni ilimvutia sana produzer aliyekuwa akirekodi wimbo wa Derila.


 Producer alihitaji kufanya kazi na yule mwanamama. Produzer Moe- Joe, sio mtu mdogo katika fani hiyo ya Muziki, alikuwepo studio miaka kumi na mitano iliyopita, naye amefanya kazi na wasanii wengi, ndani na nje ya Afrika.


        Mbali na kufanya kazi na wasanii wengi, Moe-Joe amewasaidia wengi ambao hawakuchoka kumrudishia fadhila na shukrani nyingi.


        “Dada, nahitaji kufanya kazi na wewe.” Joe alimwambia yule mrembo ombaomba.


        “Asante sana Produzer, nimefurahi kusikia hivyo.”Derila alitabasamu, yupo pamoja na mwanaye Uche, wametulia tuli ndani ya chumba cha studio ya produze Moe- Joe.


        “Sauti yako inavutia sana, mashairi yako yana ujumbe pia ambao ni rahisi kueleweka, nahisi nikurekodi bure wimbo huu na pia video nitagharamia mimi, kila kitu nitafanya mimi, ilimradi usiniangushe tuweze kuingia mkataba ili tuvune mamilioni ya pesa.” Moe- Joe aliongea, amemfurahisha sana yule mwanamama, mwanamama anayeona bahati ikimtembelea pasina kujua fika kuwa ingelimtembelea mapema namna ile.


        “Unaishi wapi, na pia unaishi na nani?” Produzer Moe- Joe alitaka kujua.


        “Naishi hapa hapa Njiro, nipo mie na mwanangu, japo maisha yangu yamekuwa magumu kutafsiriwa.”


        “Haujaolewa?”


        “Ndio sijaolewa japo tayari nimezaa mtoto.”


        “Ok,. Usijari, nitakusaidia.”


        Moe-Joe alianza kumsaidia Derila, alikwisha kugundua kuwa Derila hana pahali pazuri pa kuishi, hapo ndipo alipojitolea kumpangishia chumba kizuri tofauti na lile Boma lililojaa mbu na viroboto, chakula kizuri Derila na mwanaye walikula, mavazi pia walivaa na afya zao zilianza kurejea. Derila tayari alikwisha tengeneza Video yake ya kwanza akiimba wimbo wake mtamu masikioni mwa wengi. 'Nimekumiss.' Ndio jina la huo wimbo, hakika wengi waliopata kumwona walivutiwa na jinsi alivyokuwa na sauti njema.

                        

*********************


        Singa alipigwa na bumbuwazi pale alipomwona mpenzi wake wa zamani yule aliyempenda kwa mapenzi ya dhati, Derila akiimba kwa hisia na hisia, alimshangaza Singa, alionekana kwenye Televisheni, anasomwa kwenye vitabu na magazeti, anaimba, anaalikwa kwenye matamasha mbali mbali apate kutumbuiza. Ooh! Singa alipigwa na butwaa, macho yakamtoka, akalia ndani ya Getto lake, akalia kwa uchungu, yupo vile vile kama alivyotoka Usa-River miaka minne iliyopita, ameukuta umasikini wa wazazi wake ni mkubwa, tena hautamaniki, amewakuta wazazi wake wanamtupia lawama na kumlaani kwa kitendo cha kuwatoroka na kushindwa kurejea. Singa alijitetea, akajitetea akisema, alinusurika kuuawa na Polisi, ndio maana alikimbilia mjini kuukwepa mkono wa sheria. Utetezi wake haukufaa kitu, bado wazazi wake walimlaani na kumlaumu.


        “Nitafunga safari, nami nitaenda Arusha nikamwombe msamaha Derila.” Singa alijipa tumaini, machozi yakimtoka, ameishikilia picha aliyoipiga pamoja na Derila miaka minne iliyopita.


        “I’am Sorry Derila, please, forgive me.”Singa alilia akijutia tendo la yeye kumtelekeza Derila yule waliyependana mapenzi ya dhati.


        “Nisamehe Derila.” Singa alilia akipita pita ndani ya kiijiji chao, kijiji cha Maasai Land,wanajamii wakiendelea na shuhuli zao za kijamii, wanawake walionekana wakijenga nyumba, wengine wakikamua maziwa, vijana wadogo wakirejesha mifugo nyumbani kutoka malishoni, wakati wazee wakiketi vikundini wakijadiliana.


                        **********************

MWENZENU N'SHAPENDWA

 


MIPASHO YA MAMSAPU 


MWENZENU N'SHAPENDWA 

Sehemu ya sita


      Nikafanya mara kwa mara kumtembelea Pompo nyumbani kwake, kigamboni huko alikopangisha chumba singo, nikimfulia, nikimpikia, nikimpugutia deki, nikimnyoshea nguo na uzuri wa mwanaume yule mie nilipenda jinsi anavyojituma, moyo wake wa kutafuta, moyo wake wa kuleta vitu muhimu nyumbani moyo wa kujali na kukumbuka. Aki! Moyoni nilijisikia kupendwa.


Nikwambieni, nikwambieni shoga zangu, nikwambieni nisikuficheni, Pompo na mie wakati mwingine tulikuwepo kwenye yetu mahaba, Kumbe Pompo ni fundi eeh!😉 Teeh teeh teeh!😂😊 (nacheka mie) Ni fundi seremala, fundi mzuri mambo anayaweza, nisikufiche mwaya, mwenzenu n'shapendwa, Mzee Baba akanikanda kanda kama kando la maandazi, nami nikakandika, akinilainisha kama uji uji wa mrenda kisha akanigeuzageuza kam chapati, ai…. Mwaya nisizidishe chumvi chakula kitadoda.


               Mapenzi yakanoga, Pompo sio mchoyo ana moyo sana ana huruma pia ni muwazi sana, hanifichi kitu, mie ni wake na yeye ni wangu. Kana’mbia mwenyewe anataka kunioa,💍 tena kasemaje, kasema anataka tufunge harusi💒🤵👰, haijalishi hata kama hiyo harusi haitakuwa ya bei gharama ilimradi Pompo kanipenda, posa tayari, kajitambulisha kwetu, keisha nilipia mahari, Keisha kutambuliwa na wazazi wangu kule Tanga Aloo! Jamani! Kakubaliwa na kupokelewae vema ukweni washampa baraka zote wenyewe wam’tambua.


Pompo akafanya Juhudi akajituma zaidi na zaidi akajibidisha, Mungu wake Mungu wa Ibrahimu, Isack na Jacob akamtangulia mbele ya safari ya Maisha yake, akamsaidia na kumuwezesha. Pompo hakuzichoka zile kazi zake kazi za kusaka tonge la maisha akivuja majasho na maumivu tele, leo akichimba makaburi kesho akifukua vyoo, kesho kutwa akiuza kahawa na kashata siku zingine akijitafutia riziki yoyote ile Riziki popote Mwenyezi Mungu anagawa. Mwanaume wangu hakusahau kuwekeza pesa zake Benki tena hakusahahu kuendelea kujenga nyumba yake huko Kigamboni.


             Kasemaje kasema ati muda si mrefu ataniweka ndani, basi mie nikacheka na kufurahia, kwake mie ni malaika hao wengine ni magubegube na uzuri wa Pompo haraka akaniweka ndani mie nikapata nafasi ya kuwa karibu karibu na yeye, akanipenda zaidi sababu nyumbani kwetu Tanga washamkubali wanamtambua na uzuri wake weshampa Baraka zote za mie Toto la kitanga kuishi na yeye. Tanga ni kwetu kule mapenzi yalikozaliwa. Basi mwaya mie nikastarehe nikajibidisha kwa shuhuli za kijungu jiko nikifua , nikipuguta deki, nikikosha vyombo nikiufwagia uwanja na pia nikijibidisha kujitwika shughuli za kufuma vitambaa, kudalizi na kupamba.


                   ###########################

            “Ninataka niunue Gari, Pompo aliongea na kunishitua siku moja tukiwa chumbani kwetu tumetulia tuli juu ya kitanda chetu chenye mahaba.

              “Ebo🙄! Mwanaume we, mbona wanishitua?”


              “Ndio hivyo tena wangu, pesa nilizozitunza Benki zatosha kununua Tax.”


                “Kama una lengo zuri wangu mie ninakupa hongera, hiyo ndiyo njia ya mafanikio.” naliongea kisha nikanena tena.


                “Lakini wangu si ungelijifunza namna ya kuliendesha ilo Tax.” Nilimshauri Pompo.


                “Hainipi shida, kuna rafiki yangu pale Magomeni jinale Fred Chirstopher, amenipa Idea ya kunifunda namna ya kuiendesha Gari,”


             “Wanipa furaha Mume,we fanya utakavyo tupate mafanikio maishani mwetu.” Naliongea moyoni n'nacheka.😆


              “Ipo siku ile nyumba yetu ndogo tunayoijenga Kigamboni itakamilika, tena…..” Pompo alinitizama kwa matabasamu.


            “Ongea wangu,” nalimsistizia.


            “Tena kwa nguvu za Mwenyezi Mungu sie tutalishusha horofa hapa Kigamboni,” pompo alinishitua roho yangu kwa maneno yale.😟


                “Wanishitua Pompo,” Naliongea domo bumbuwazi.🫢


               “Mungu atupe pumzi wangu,” Naliongea.


               “Ninaona mbali Pompo,” naliongea, Pompo akalivuta shuka la kitanda chetu, akanifunika nayeye akajifunika, tukawa ndani ya hilo shuka gubigubi tunatizamana.

          

        “Mbali sana, mbali kwenye mafanikio”, akanishika kiuno changu, nikampapasa usoni kwake, nikamsikiliza.


               “Ninaiona biashara, ninafikiri ipo siku nitakuja kufanya biashara kubwa huko ng’ambo; Dubai, South Afrika, Amerika, China na Japan.” Akanibusu😘😚 akanibusu midomoni mwangu na mie nikampokea kwa mabusu yake kimya nikamsikiliza.


             “Biashara itatutua, iwe isiwe, tutafanya mengi makubwa zaidi ili sie wawili tunaopendana tuzidi na kuzidia,” Maneno yale matamu yaliingia masikioni mwangu, akanitia hamu ya Mahaba. Aki! Mwanaume wangu anatamani na pia ananitamnisha mapenzi.


              “Ninakuombea mapenzi, ninakuombea mafanikio, wangu upite njia za salama, njia za salama ndizo zitakazo kufanikisha ufike pale tunapotarajia kufika.” Naliongea.


              “Asante wangu basi ujue kuwa mie ninakupenda sana.” Pompo aliongea.


               “Unishindi love, 💕 mie nakupenda zaidi ya sana,” Niliongea Pompo akanigawia mabusu yake, akazidisha na kuzidisha wawili tukawa hoi Bini taabani.


          ##########################


Basi miezi kadhaa kupita 'chai wa moyo wangu' alifanikiwa kuipata Tax nzuri ya kuendesha, akafundwa na huyo Fred Chirstopher rafikiye wa Magomeni, wangu akafanya kujibidisha tusikose tena pesa ya mbogamboga nyumbani, maisha yakaendelea tena uzuri wa maisha hayo, yakawa ni maisha matamu yenye unaafu, Mie shoga yenu Mamsapungo nikaona fahari isiyo na kipimo, nikajisikia sana, nikafurahia kupendwa, nikayapata mahita yangu yote, yaani raha na furaha, nimempata wa kunipenda tena yeye mwenyewe kanipenda, nina haki ya kujivunia mie ni mwanamke na mwanamke lazima nipendwe.


           Sasa shoga zangu ikawa siku moja mie nipo barazani nachambua chambua mboga ya harage kwetu twaiita Nguniani , nikitwanga twanga kipome au kwa kifupi karaga za kuchanganya kwenye Nguniani, nikatembelewa na ugeni nyumbani. kanijia huyu mwanamke anitishaye surani, mmh! kwa mwonekano wake si ningelimwita chizi mwenda wazimu, lakini aka! yatanikuta mie, nizibe mdomo wangu, sio kila neno kuropoka.


Itaendelea sehemu ya saba.


   

Saturday, July 19, 2025

OBIMO CHETA

 



OBIMO CHETA


REMEMBER MY LOVE 💕 


Sehemu ya nne


Hakuwa na pahali pazuri pa kulala, hakuwa na maji, hakuwa na chakula, alilala kwenye majengo mabovu ambayo hayajakamilika kujengwa, alilala popote pale akitanga tanga na njia, akiomba omba chakula na maji huko Arusha Mjini, haja jinsi Derila, maisha ya wale waliokuwa pamoja naye hayapo tena, wamemkataa, oooh! Masikini, Derila hana furaha na ujauzito wake nao unakuwa kila siku, unakuwa mkubwa ajabu.


        Mbu hawachoki kumfyonza damu, chawa nao hawachoki kumtembelea, sio yule binti mweupe wa rangi ya chungwa kwa sasa, amebadilika rangi amekuwa na rangi ya kaki, ukimtazama mara mbili mbili waweza kusema kuwa yule sio Derila uliyemzoea miaka na miaka, kama unamjua basi waweza ukalia na kumuonea huruma.


                *************************

        Kuna kijana mdogo wa umri, mdogo wa umbo lakini kwa kipaji cha kuimba nyimbo yupo vizuri, tatizo alilo nalo  yule kijana ndilo tatizo alilo nalo Derila, Frank alifukuzwa nyumbani kwao kikatili, alifukuzwa mara baada ya kufeli masomo yake ya sekondari, alifeli kidato cha pili, alifeli kutokana na mapenzi yake kwenye burudani, muziki ndio burudani yake, yeye ana kipaji chake kizuri sana, anaimba japo hapewi sapport, ni kama vile Frank anaupoteza muda wake mzuri wa kujibidisha na masomo, ingawaje amefeli, tena kufeli kwake kuna nafuu, yote kwa sababu anayo nafasi nyingine ya kurudia darasa japo hataki kurudia, wazazi wake walipoona wamembembeleza bembelezo lisilozaa matunda hawakuwa na jinsi, waliamua kumfukuza, tena walimfukuza kama mbwa, mbwa mwizi, wazazi wa kipindi hiki daima hawakuwa na mashauri bali walikuwa na maamuzi, na maamuzi yao daima ni kuwafukuza watoto wao pale wanapoona hawaafikiani kabisa.

        Frank akawa omba omba la jiji, maisha yalipomtupa mkono, ugumu wa hayo maisha ndio uliomfanya Frank awe ombaomba la Jiji, uzito wa maisha ndio uliomfanya Frank ashindwe kupata mahitaji yake muhimu, chakula kwake ni kama ndoto kukipata, maji au mahali pa kulala ni taabu na taabiko, wazazi wake hawamtaki. Ndugu, jamaa na marafiki hawana cha kumpa.

        Ombaomba, Frank akaungana pamoja na ombaomba na mwenzie Derila, tena huyo Derila angali ni mwingi wa majonzi, kilio na masikitiko, analia na kuhuzunikia juu ya penzi lake, penzi alilolipenda Derila. Frank akawa faraja kwake, alimfariji kwa nyimbo nyingi zilizojaa mapenzi na kumbukumbu za kweli.

        Tendo la Frank kumuimbia Derila nyimbo, lilikuwa ni tendo lililomfariji sana Derila akawa sio mtu wa kulialia tena, sasa akawa ni mtu wa kuimba pamoja na Frank, watu wenye moyo wa kutoa chochote walitoa pale walipoburudishwa na nyimbo tamu alizoimba Frank pamoja na Derila, tuseme uzuri wad Derila alikuwa na sauti nzuri ya kuimba, sauti ya kumtoa nyoka pangoni, sauti bora kabisa, sauti ya burudani, na uzuri wa sauti hiyo ndiyo iliyowafanya watu wajitolee chochote kile kidogo walicho nacho, iwe pesa, iwe chakula, iwe nguo au ushauri, burudani iliwatosha.

        “Watu wanasema umejaliwa sauti tamu sana Derila.” Frank alimsifu Derila.

        “Ni bahati tu Frank, mimi binafsi sijui kama ninayo sauti nzuri ya kuvutia.”Derila alitabasamu, ndivyo alivyo Derila siku zote hutabasamu.

        “Je. Derila unaonaje siku moja mimi na wewe tuingie studio, tutengeneze Audio moja, wimbo wetu uwe mtamu wenye mavuto.” Frank alishauri.

        “Frank, kwa hali hii ndugu yangu kweli tunaweza kuingia studio, pesa tutapata wapi, maisha yetu yalivyo magumu, sidhani kama tunaweza.”

        “Tunaweza Derila, tunatakiwa kila siku tunapopata kidogo majaliwa tukitunze kwa sababu haba na haba hujaza kibaba, ndo, ndo, ndo sio chururu.” Frank aliongea, wapitao njia walifanya kurusha rusha vijisenti kwenye bakuri zao, kwani walijua kuwa wale wawli ni wahitaji?


        “Mmmh! Tuombe Mungu afanye wepesi Frank, mbele za Mungu yote yanawezekana.” Derila aliongea kwa imani, Frank akatabasamu, naye akafungua kinywa chake akaimba kwa hisia;

                         Milele, milele,
                         Milele, milele,
                         Mapenzi milele,
                         Milele na milele.

                         Tupendane sana,
                         Tupendane tena
                         Milele na milele
                         Mapenzi milele
                         Mi na wewe milele.


           
    ********************************

Itaendelea

NILIHARIBU KIZAZI CHANGU

 


_BAADA YA KUMFUKUZA 🏃‍♀️🏃‍♂️MKE WANGU WA NDOA MAMA NA DADA YANGU WAKAKIHARIBIU💀 KIZAZI🩸 CHANGU.

"Hamza!" Mama aliniita kwenye Rununu yake📲" Nilisikia sauti ya kwikwi😿 Ma. Alikua akimwaga chozi.

"Naam, Ma. Mbona kama nasikia unalia" 🥲Nilimuuliza moyoni nimejaa maswali kibao.⁉️

"Acha nilie my son. Mkeo huyu ni shetani mkubwa, shetani Ibilisi 🦹‍♀️👿kwahaya anitendeayo nimevumilia miaka yote lakini nimeona mvumilivu ninakula mbovu, Bora nikuambie" Safari hii alitoa kilio kikuu, moyo wangu ulinidunda uchungu ulinivaa kusikia kilio cha Mama mpenzi.

"Tatizo Nini Ma, acha kulia."😤😠 Niliongea simuni.📱

"Sijalia miaka mingi tangu baba yako achukuliwe na Mungu🪦⚰️, Leo acha nilie tu sababu Mkeo ananinyanyasa, ananitesa, ananishusha kwa matukano baya zaidi ananidunda mwili wangu umejaa makovu sema nashindwa kukwambia mwanangu. iiiiiiii😿iiiiiiii uwiii 🥲." Alipaza sauti ya kilio.

"Nini👺? Jasimini anakutesa, anakupiga, anakunyanyasa" Nilipaza sauti 🗣️safari hii hasira zilianza kuninyanyasa.

"Nitafanya nini mwanangu zaidi ya kuvumilia, Leo tu ameniambia niondoke nyumbani hapa, ananifukuza na kunitimua ndani ya nyumba uliyojenga mwanangu,🏘️ ananifukuza kama vile ni yeye aliyejenga nyumba hii" Ma. Alinisimulia.

"Nasema haiwezekani Ma, haiwezekani..... Ngoja nije nimuoneshe kwamba anapaswa kukuheshimu, mpumbavu mkubwa huyo." Nilibwata nikiwa Ofisini✍️ kwangu hima hima nikachukua funguo ya Prado 🚗yangu nikaikoki na kutimua vumbi moja kwa moja hadi Oysterbay nyumbani moyoni nikimlaani mke wangu.👩‍❤️‍👨

"Mpumbavu huyu hajui jinsi nilivyoishi na Mama yangu Kwa tabu, shida na maangaiko."

"Mama alikua akiuza mbogamboga, nyanya na vitunguu ili Mimi nisome na nimesoma kwa tabu hadi kupata Diploma yangu ya Sheria ⚖️👨‍⚖️alafu mjinga yule anampiga na kumnyanyasa Mama yangu."Nilivurugwa.

"Leo atanikoma, ama zangu ama zake ni mwendo wa kutimuliwa tu."Nilibwata ndani ya Gari nikaikimbiza ovyo Hadi masikani kwangu, mlinzi wa geti alinifungulia haraka nikaenda moja kwa moja hadi sebuleni.

"Yu wapi huyo mpuuzi anayekunyanyasa Mamangu."Nilifoka.👺

"Amelala chumbani kwake😴, Ma. Alikua Analia Hadi kamasi zilimchuruza.😪 Nikaenda chumbani alipolala mke wangu nikaubamiza mlango mbaaaaa  Mama Jasimini mke niliyezaa naye watoto wawili:Jasimini na Ali alishituka baada ya kusikia sauti kuu ya mlango ule.

"Twende sebuleni,"Nilimvamia pale kitandani nikamvuta mkono wake kinguvu karibia niutengue ukavunjika Nikamburuta na kumtoa nje kuelekea barazani nilipomuacha Mama.

"Kuna Nini Baba Jasimini? Kuna Nini?" Sikuisikiliza sauti yake. Nikamsukumia sebuleni pale Mama alipokua analia Kwa uchungu.

"Bibi Mama mkwe mbona unalia umepatwa na Nini? Mke wangu alimuuliza Mama yangu maana alionekana kushituliwa na kilio cha Mama.

"Unajifanya haujui Mama Jasimini yaani kila siku unanitukana, unanipiga na kuniambia niondoke kwenye nyumba aliyojenga mwanangu Hamza."Ma. Aliongea akilia.

"Mimi!!? Mimi ni wa kukupiga 💪wewe, kukutukana na kukufukuza.🤭😯" Mama Jasimini aliongea kwa mshangao na mshituko. Nilisikiliza tu wakibishana.

"Sasa kumbe! unataka kuniua ndani ya nyumba ya mwanangu wa kumzaa." Mama aliongea Kwa uchungu mzito.

"Bibi Mama mkwe!!" 🤯Mama Jasimini bado alipigwa na butwaa.

"Naomba uingie chumbani na ubebe kila kilicho chako kisha uondoke."🛅🧳🛍️ Nilimwambia Mama Jasimini kwa hasira.

"Baba Jasimini Bibi Mama mkwe haongei ukweli, hakuna jambo kama hilo mimi kumtenda." Mama Jasimini alijitetea.

"Mama yangu hawezi kudanganya, Mama amenilea katika tabu, shida, na maumivu makuu leo hii kimburukutu wewe unampiga na kutaka kumuua." Nilimfokea Mama Jasimini.

"Siwezi kufanya jambo kama hilo Mume wangu, wallai! Bilali! Ninakuapia."Alijitetea machozi yakitaka kumdondoka lakini mie sikusikiliza, kwanza yeye sio damu yangu na sio ndugu yangu kuna baya gani nikimtimua?❓

"Kabebe nguo zako zote utoweke." Nilimsukumia chumbani.

"Nisikilize Baba Jasimini nisikilize Dear!"Machozi yalimdondoka.

"Namsikiliza Mama yangu sikusikilizi wewe mpumbavu." Nilipoona anachelewa kuingia chumbani kubeba vigagula vyake nikaingia Mimi na kutoa kila kila chake na kumfukuzia nje kama Jibwa🐕 lisilotakiwa nyumbani

"Nisikilize Baba Jasimini naomba nipe nafasi nijieleze."Lakini wapi sikumtetea niliegemea upande wa Mama tu.

"Ondoka na Tena ondoka nyumbani kwangu,"Niligeuka mnyama mwenye hasira.🐉🦍🦁

"Basi nipe nafasi ya kuondoka na wanangu."z👨‍👦 Alilia.

"Neva eva, hauna watoto hapa. Watoto Hawa ni wa kwangu ulikuja mikono mitupu na uondoke mikono🙌 mitupu." Nilikua namsukuma aende nje ya Geti, baada ya kumtoa nje nikamuacha pale Analialia na kugonga geti ahurumiwe.⛩️ Sikujali. (I didn't care)

--------*****--------*****

Mama Jasmin hakukata tamaa kila siku akawa ni mtu ni wa kuja Ofisini ✍️akilia kwa uchungu akidai hajawai kumtendea Mamangu ubaya, aliomba aonane na wanangu. Lakini bado sikumpa nafasi hiyo. Basi akafanya kwenda ustawi wa jamii kudai haki ya kuwaona watoto tuliozaa pamoja, Hilo nalo sikulitaka kabisa na kwa vile mie ni Hakimu 👨‍⚖️na pia nina pesa nyingi 🤑🪙💲💰nikatoa rushwa kubwa kubwa wamnyime haki hiyo, kwa asilimia kubwa wale watu wa ustawi walipokea rushwa na kumnyima ile haki ya kuwaona watoto.

       Mwanamke hakuchoka bado tu aliendelea kunisumbua Ofisini na nyumbani. Nikacheka kwa ule usumbufu wake nikaanza kumtisha kwa kumwambia iwapo ataendelea kunisumbua nitamfanyia 🥷kitu kibaya ambacho hatokuja kukisahau maishani mwake. Akanywea na kuogopa..... Nilidhamiria kumwaribia maisha yake sababu pesa ninazo na cheo ninacho.

Baada ya miezi sita kupita baada ya kuachana na mke wangu Dada yangu Aisha alihamia nyumbani kwangu maana alikua amegombana na Mume wake na Taraka juu aliachiwa. 📝📜Aisha hakuwa na pahali pa kukimbilia zaidi ya nyumbani kwangu akaambatana na Jumanne mwanaye mwenye umri wa miaka kumi na Mitano. Wakati huo wanangu hawakukoma kuniuliza kuhusu pahali alipokwenda mama yao, niliwajibu uongo nikawaambia Mama yenu hawapendi, amewakimbia, hawataki na pia hataki kabisa kuwasikia. Wanangu waliamini hivyo hivyo nilivyowadanganya.

     Kwa vile Mimi ni mtu mwenye pesa zangu basi nikafanya kuwaajiri vijana wawili wawe wanamfuatilia mke wangu na kumchunguza:anafanya Nini?Anapanga mpango gani? Anatembea na nani? Miaka ilivyozidi kwenda nilikuja kuambiwa tayari ameolewa hapo ndipo nilipopata mwanya wa kumwandalia Taraka. Akala Taraka yake na tena sikujali nilipokuja kuambiwa amejifungua mtoto wa kiume. kwani anafaida gani kwangu, ⁉️❓sikuona umuhimu wake.

     -------------------------------

Nilikua ni mtu wa bize bize kazini, mtu wa kazi kazi.kama ningeliondoka saa kumi na moja Alfajiri basi ningerejea saa sita au saba usiku, muda huo ningeliwakuta watoto wangu wamelala, Mama na Dada yangu wamelala pia moyoni Nilifurahia nikijua kuwa familia yangu inaishi kwa furaha. Nilitembea na Ufunguo wangu wa nyumba, nirejeapo kutoka kazi ningelifungua mlango kwa Ufunguo wangu na niondokapo kurejea kazini ningelifunga kwa Ufunguo wangu. Mama na Dada pia walikua na funguo zao za akiba
   
        Ilipita miaka Saba pasina mke niliyempa Taraka kunifuatilia. Siku moja nilijisikia kuumwa mwili💉🥵 wangu wote nikaaga Ofisini mapema yapata saa tatu usiku,🌆 nikaeleka nyumbani kwangu Tabata nipate kupumzika. Kama kawaida niliutumia Ufunguo wangu kuingia nyumbani kwangu nikalilaza Gari langu na kuelekea chumbani kwangu.

      Ile napita karibu na mlango wa chumba cha Dadangu nikayasikia maongezi ya majibizano kati ya Mama na Dadangu, nikatega sikio nisikilize nini wanachobishaniana.

        "Sophia nilikuambia lile tendo la kumfukuza Jasmin mke wa kaka yako lingelileta matatizo ni Bora tungelimwacha alee watoto wake."

      "Lakini Mama hata wewe ulishiriki kusababisha Jasimini mke wa kaka Hamza afukuzwe nyumbani hapa."Dada alimjibu Mama.

       "Kumbuka ni wewe ndiye uliyenishawishi nitunge uongo na kujifanya naigiza mbele ya kaka yako Ili kumpumbaza aamini kuwa Jasimini alikua ananipiga, ananitukana na kunidharau." Mama aliongea Mimi niliyekua nimetega sikio pale mlangoni nilishangaa maongezi yao.

       "Sasa Mama ningelienda wapi ikiwa Mume wangu alinifukuza na pahali pa kukimbilia sikua napo zaidi ya nyumba ya kaka Hamza."Sophia Dadangu alimjibu Mama.

        "Haya Sasa tuachane na hayo maji yashamwagika hayazoleki, ⛲embu niambiwe Sasa tunafanyaje kuhusu Ali mwana wa kaka yako? Je ataendelea kujinyea hivi hivi hadi lini? Tena la zaidi nimekuomba sana mchunge mwanao Riziki tendo la kufanya mapenzi na Aisha mwana wa kaka yako litasababisha majanga mazito ikiwemo kuharibu kizazi cha Aisha au kubeba mimba katika umri madogo."Uwii! Maongezi yao yalinipa Presha.😤🥶🥵

      "Mama punguza lawama, Riziki alianza michezo ya ngono tangu akiwa Shule ya Boarding🏫 walimu walipomgundua wakapelekea afukuzwe Shule na Mimi kupewa Taraka na Mume wangu. Sasa Mama ningefanya Nini ikiwa sikuwa na pa kukimbilia zaidi ya hapa nyumbani kwa Kaka."Dada alijitetea.

      "Nimesema tuachane na hiyo Topic yakuachwa na Mumeo, tujadiliane kuhusu hali mbaya ya Ali mwana wa kakayo kutokwa na choo kikubwa bila speed, 🚽mkanye Riziki kuendeleza mchezo huo pia muamishe Riziki ndani ya chumba alalacho na Ali, kumbuka Ali ni mtoto madogo mwenye umri wa miaka nane tu."Maneno ya Mama yalinifanya nianze kuona kizunguzungu na kuanguka.

     "Nimemkanya Riziki mara ngapi wala asinisikie!?"

    "Na Kaka yako akifahamu itakuaje??"
   
    "Tutatunga uongo mama....." Sikutaka kuendelea kusikiliza maongezi yao nilikwishajua kuna kitu hakipo sawa pale nyumbani. Nikausukuma mlango wa chumba cha Dadangu nikaingia kwa fujo ile wananiona tu walishituka na Ili kutoonesha darili ya kwamba wameyasikia maongezi yao wakajifanya kuibadilisha Topic, wakaanza kujadiliana mambo mengine.

    "Nielezeni vizuri kuhusu Mtoto wangu Ali na Dada yake Aisha." Nilipaza sauti, hawakuamini kama nilikwisha yasikia maongezi yao wakajitetea kwamba hawajui jambo lolote linaloendelea. Nikawabana sana Ili waongee ukweli wa mambo hatimaye mwisho wakajieleza. Mama akaeleza ukweli kwamba yeye na Dada walipanga njama mke wangu atimuliwe pale nyumbani kwangu Ili Dada aje aishi pale nyumbani maana Dada alipewa Taraka na mumewe kwahiyo hakuwa na pahali pa kukimbilia.

Wakaeleza Riziki  mtoto wa Dada mwenye umri wa miaka kumi na Tisa umwingilia Aisha Binti mwenye miaka kumi na moja umbaka mwanangu Hadi aridhike na tena hatosheki umwingilia kinyume na maumbile mwanangu Ali ambaye tayari ameharibika anajinyea.     We! Nilicharuka nikawa Mbogo mnyama wa porini nilitamani niwapige Dada na Mama yangu nilichofanya ni kuwafukuza pale nyumbani kwangu wote waondoke warudi kijijini. Hasira zilinipanda baada ya kujua kumbe mama na Dadangu walipanga njama chafu Ili nimfukuze mke wangu mpenzi wao waishi kama Malaika pale nyumbani kwangu. Moyo uliumia na kusikitika.

      Nikafanya mpango wa kuwatafutia Madaktari wanangu. Mishipa ya haja kubwa ya Ali mwanangu iliregea na kusababisha kinyesi kiwe kinamtoka ovyo. Aisha mwanangu alikua kama teja la ngono kila alipokua ameketi peke yake alilia anataka mtu amwingilie wafanye ngono. Hali ile iliniumiza sana maana ukikaa nae tu angelilia mwanaume wa kusex nae inaonekana Riziki alimzoesha ule mchezo mchafu

Niliwaomba Madaktari 🥼🩺👨‍⚕️wanisaidie, nikatafuta wataalamna Wanasaikolojia. Loh! Masikini majuto yaliniandama.

      Ikawa sasa ninautumia muda mwingi wa kukaa na wanangu, 🕐nilitamani kutafuta wasichana wa kazi lakini sikuwaamini kabisa, nilitamani kuacha kazi Ili niwe karibu na wanangu nikaona haitoshi wacha nimtafute Mama yao nimuombe turudiane. Mama yao niliyempa Taraka alikwisha olewa na mtu mwingine. Nilipompa taarifa juu ya kile kisa cha Mama na Dada Wala hakuumia au kusikitika alichosema yeye alisema: "Sasa Mimi nifanye nini kama watoto wameharibika basi pambana warejee kama zamani. Ulikataa katakata nije niwaone na kuwasabahi na sasa imepita miaka Saba ndo' unadai turudiane? Haiwezekani mie nina maisha yangu."

      Kilio kilinitoka nilimpoteza mke mwema kwa ujinga wa kumsikiliza Mama yangu, Mama yangu na Dada wamekula njama na kushiriki kuniharibia kizazi changu. Masikini mimi ni Bora kama ningelimpa mke wangu Jasimini nafasi ya kujieleza kuhusu lile sakata lakini ubaya wake nilimsikiliza Mama yangu.

""""""""""""""""""""""""'""


TCHAO


🥲😥😢🤧😭


""""""""""'"""""""""""""""""
 

Friday, July 18, 2025

MWENZENU N'SHAPENDWA

 


MIPASHO YA MAMSAPU 

MWENZENU N'SHAPENDWA 

Sehemu ya tano

Jina zuri kutamka, lapendeza machoni, lanivuta moyoni, nitaliweka kifuani.” Pompo kajishaua na kuchombeza maneno yaliyozidi kunifanya niweuke, n’shituke na kupandwa na hisia za kumhitaji, japo simjui lakini kanivuta macho yangu kumpenda.


                 “Shidayo nini kakangu? Je nikufungashiye matunda yepi?”

                 “Nifungashie yote na yote nitayalipia.”   

                  “Eeeh! Toba! Mwanaume we! Sijapata kufanya biashara kiwepesi kama hivyo,” nalifurahishwa na manenoye.

                   “Leo lazima upende na ukipendwa pendwa ufurahie? Pompo kaongea.

                   “Nimependa kakangu, nimependa sana tena nafurahia kwa jinsi ulivyopenda pia.” Naliongea kwa raha tele. Nikitamani kuendeleza maongezi na mwanaume huyu kijana.

                    “Kama umependa na mie pia nimependa, twaweza kuungana ili tupende zaidi.” Pompo katamka

                    “Mmmh! We mkaka una mambo, huchoki kunena.”  Ilikua ni zamu yangu mie kujishaua kwa Pompo.

                    “Naomba unielewe na pia unifikirie zaidi.” Pompo katamka.

                   “Nitakuelewa pia nitakufikiria zaidi, nipe mida mirefu, muhimu mawasiliano.” Nilikuwa mwepesi kumjibu Pompo. Akafanya kuchagua chagua matunda aliyoyataka mara ile katoa noti ya shilingi elfu kumi, kanigea, mie n’kagomea, n’kamwambia, n’kamwambiaje, n’kasema

              “Chukua hayo matunda kama zawadi yako, weye nimekupendelea.” Pompo kashangaa ule wema niliomfanyia na yeye alivyo mtani kanishika mkono wangu wa kulia kanipiga busu. Ooosh! Mie kutetemeka, jamani aibu kwa mie Bi. Dada, japo raha n’kajisikia maana yule fundi alinipendeza usoni.

              “Asante, njoo tena kesho  nitakuona Mamsapungo tuongee mengi ya maisha.” Maneno yale nilitamani yaendelee kuwepo na mie muda wote wa kukutana na yule kijana mzuri wa kunipendeza. Nilitamani nisimwache na yeye asiniwache niwe pamwe na yeye milele.

                “Nitakuja rafiki, nitakuja nikusikilizeni,"

                “Nina hadithi nyingi nyingine kwa ajili yako,” Pompo kaniambia.

                “Ninapenda sana hadithi uniwekee moja yenye umoja nipate kuburudika.” Nilimwambia Pompo kwisha kunena maneno yale mie nilijitwika kapu langu nikafanya kumuaga na yeye akaniaga akinitizama  ninavyopotea mbali na upeo wa macho yake, nisiweze kujizuia kugeuka geuka nyuma ili nimuone tena yule mwanaume kijana

##########################

               “Nina nini mie, mbona  naweweseka  weseka kitandani, ndoto nyingi nyingine juu ya huyu mwanaume kijana niliyepata kumuona mchana wa jana?” Naliongea mie na moyo wangu, ni usiku wa manane, usiku mzito ajabu ndoto nyingi nyingine juu ya huyu Pompo zilinigutusha, nimelowa jasho ajabu kama mgonjwa wa Maralia.

                 “Mkaka huyu!” Naliwaza mie Bi.dada wa kumi na 19 (19 age)

                 “Nisimpite asije kuniona mbali na peo za macho yake, nisitoweke mbali na peo za macho yake, lazima nifanye hima niwe karibu na yeye, niutue moyo pale ninapoona pafaa kutuliwa. Niridhie kwa moyo wote, moyo mmoja, nisione kinyongo  na mtima nyongo ukae mbali na mie, nahitaji furaha sihitaji sumu, sijawahi kupenda kwake huyu nitafanya maamuzi sahihi”  

Mie Mamsapu niliwaza na moyo wangu, ilikuwa ni usiku mzito, mvua sio mvua, kila tone lililodondoka lilinipa  matumaini ya kuujaza moyo wangu mafuriko, na mafuriko hayo ni mafuriko ya mapenzi.

              Hata siku ya pili tulipoonana mie na Pompo tukanena zaidi wakati huu ulikuwa ni wakati mzuri kwetu, sio tena kariakoo kule nalikomkuta pompo akijenga majumba ya watu, leo kanichukua na kunipeleka ufukweni, tena kaaga kule saiti kasema  ‘angependa kupumzika,’ ruhusa ilikubaliwa.


               “Moyo hauwezi kuishi pekee, moyo wahitaji faraja na mfariji, ujue Mamsapu maji ya moto yaliyochemka mtu hawezi kuyaoga, ila tu yakipoozwa kwa mchanganyo wa maji baridi.” Pompo aliongea tukiyatazama maji mazuri ya bahari yenye mawimbi madogo madogo.

              “Mie pia ninafahamu.” Nalimjibu Pompo kwa ufupi

              “Vizuri wafahamu, tena wajua Babu yetu Adam hakuweza kuuvumilia upweke hata Mwenyezi Mungu alipompatia mali na fahari.” Pompo alieleweka.

              “Ndio kamleta Bibi Hawa ili Adam apate furaha, mali na fahari ni vitu vya kupita tu ila wawili wenye Mapenzi walidumu.” Mie nikaongeza maneno.

               “Ninapata raha kusikia hivyo.” Kidogo Pompo aliona aibu kuendelea kuongea, muuza vinywaji alipita Pompo akaagiza soda mbili , Fanta orange baridi. Tukaendelea kunywa taratibu.

               “Rangi nyekundu yamaanishani Mmsapungo?” Pompo aliitazama ile rangi ya Fanta orange.

               “Hiyo ni rangi ya moyo Pompo.” Mie nilijibu.


              “Umejibu vema, kwa hiyo moyo wangu na moyo wako ni mwekundu eti eeh? Ok. Niambie na moyo nini?” Pompo kwa maswali ni mtu mbele za watu.

               “Moyo ni mapenzi, tena mapenzi ya dhaati yale yasiyochuja, yale mapenzi ya kumpenda akupendaye kumvumilia kwa hali zote iwe shida iwe raha na mola atajalia.”

               “Napenda unavyo jibu kwa ufasaha, acha nikuambie mie niliwahi kupenda, lakini sikubahatika kupendwa pendo la dhati kwa yule niliyempenda. Maneno ya mashoga wambea na majirani yalipozidi nguvu za moyo wake akanifanyia vibweka vituko na mikasa, hatimaye mara baada ya kunizalia mtoto mmoja wangu niliyempenda akatoweka kama upepo nisijue ni wapi alipokimbilia . Pompo aliongea kwa huzuni.

              “Je, ungali bado wamsubiria?” Mie nilihoji.

              “Sidhani kama itakuwa fair kumsubiria.” Pompo alisikitika

               “Na ikiwa hivyo?” Nikamtwaga swali jipya.

               “Maua amenitesa, Maua atanitesa yule ni msaliti na msaliti nimfayie nini Mamsapu?” Pompo aliniuliza nikacheka kidogo kisha nikamjibu.

               “Huyo ni sumu, mteme, mfute tena mtupe, usimuweke moyoni.”

               “Na baada ya hayo yote?” Pompo alinitega.

               “Tulia, mwombe Mola, fanya ibada, maisha kutafuta, umempata mwengine.” Nikajitongozesha.

                “Teh teh teh! Mamsapungo wanichekesha,” Oh! Kumbe Pompo anapenda kucheka.

                “Ongea nisikie tena,” Nilihitaji kumsikiliza.

                “Nimemwomba  sana Mola, nimetulia huu ni mwaka wa saba sasa tangu yule niliyempenda nimfute, nimteme, nimtupe nisimtake tena, nikafanya ibada za mara kwa mara na Mungu amenionesha mwanamke mzuri ninampenda.”Pompo aliongea.

               “Hongera, tayari ushampata.”

                 “Nimkose tena Mamsapu, sidhani kama hiyo bahati ni ya kunipita, ninakupenda sana Mamsapu, nimekuweka moyoni.” Akaendelea kunena.

                “Nina kuhitaji, ninahitaji kuishi na wewe.” Mie nalijifanya kushtuka.

                “Simwoni mwingine, wewe ndiwe, tulia kwangu, nitulie kwako tutulizane.”Pompo aliongea.

                “Teeh teeh teeeh,” Nikacheka na kumeza mafunda mawili matatu, moyoni nikawaza “ Asinipite mwanaume huyu, asipotee mbali na peo za macho yangu, ambatane na mie tu. Aki! Sijawahi kupenda, acheni nipendwe nami nipende na kupendeka.”

              “Mmmh! Wasema kweli  Pompo?”Nalijifanya kuuliza.

              “Mia mia, sina mizinguo, mtu mzima kama mie nidanganye tena, wallah! Nipigwe kwa moto wa Mungu.” Alitoa kiapo.

              “Nakuamini Pompo, imani yangu ipo kwako, nisiwe mwingi wa kusita sita, ninajua umenipenda na mie nimekupenda pia, tusipoteze Muda  mambo kuyajadili, tupeane nafsi mapenzi yetu machanga yaanze kuota mizizi .” Naliongea vizuri Pompo akanisogelea karibu na mie nikamkumbatia, akanipiga mabusu elfu na mie nikamrudishia mabusu elfu.

                “Asante sana Mamsapungo, asante kwa kunielewa, acha mapenzi yaote mizizi, mizizi itazaa  shina, shina litazaa matawi na matawi yatazaa maua na maua yatazaa matunda.” Pompo aliongea.

              “Asante nawe pia, asante kwa kunipenda penzi la kupendeka, basi unipe penzi la dhati, usiniwache angani, uniweke moyoni mwako.” Nalimjibu Pompo, akaniomba tufanye kuogelea kwenye maji ya bahari ya Hindi nikamkubalia.tukaeleka kujimwaga hapo Coco beach, hapo mapenzi yetu yalipozaliwa, hapo ngoma za mapenzi zilipodundwa, hapo raha na furaha kunoga.

Basi mwaya penzi letu lilizaliwa mtoni, kwenye asali na maziwa yashukayo milimani, hapo mapenzi yetu yalianza kuogelea, Pompo akanipenda sana asiweze kunitema na mie Mamsapu nikamuweka moyoni nisiweze kumtoa rohoni. Hapo sie tukakumbukana kwa yale mapenzi ya kadi na maua, zawadi tele, SMS za mahaba na mapenzi, kutembeleana mara kwa mara na kufurahia pamoja. Mie nikampenda Pompo nikampenda wangu wa mapenzi

Itaendelea kesho.

Thursday, July 17, 2025

l PROMISE YOU



 SURA YA TANO

SIACHI MBACHAO.
Najua fika kuwa Brenda ana mwana wangu pembeni lakini hilo halikomi kuniumiza mtima wangu, hilo haliachi kunichoma na kunifanya niwe na msongo wa mawazo bado ninamuwaza Brenda wangu, bado ninayawaza yale maneno mazuri ya kimomboo niliyotamka siku zile za ulevi wangu.
“Ipromise you brenda, Iwill fulfill all of your wants, you just have to wait, time and moment will come.”
             “Ninamapungufu gani hata nishindwe kufullfill all of  Brenda needs and wants.” Ninasikitika nimezidiwa kete, nimezidiwa ujanja, ujanja wa Fisi, sio ule wa Sungura na huyo Fisi tayari alikwisha poromosha bonge la harusi, harusi ambayo mie Job nilikuja kusikia nikiwa Pretoria, nakitumikia kifungo kilicho sababishwa  na Biko.
               Nimeumia, nimeumia moyoni kwa sababu ya mapenzi yangu kwa yule niliyempenda yule niliye amini kuwa amenipenda kwa dhaati lakini ajabu amenibwaga na kunitelekeza.
Msongo wa mawazo umepelekea kurudia tena asili yangu, nimerudi bungeni, nimerudi bunge la walevi, mwanzo nilikuwa mpwke na mnyonge walevi wenzangu walinionea huruma sana, wakanirejeshea amani yangu, amani iliyopotea, taratibu ndio mwendo pole pole tutafika, nikachepuka mie niliyekuwa meneja wa kiwanda cha TBL , leo hii nimekuwa  mnywaji wa matapu tapu, haki muda ni wakati, wakati ni muda, hakuna marefu yaso na ncha. Basi nikawa supa supa furaha ikarejea, japo sio ile furaha niliyokuwa nayo kipindi kile nikiwa na Brenda wangu.
             Teeh teeh teeh ai! Nacheka mie,nacheka hadi meno therathini na mawili yamenitoka, nikiwa nagugumia lita ya matapu tapu, ati walevi wenzangu wanadai kuwa ifikapo kesho watanivika ufalme, niwe Raisi wa chama cha walevi Tanzania, teeh teeh teeh, vichekesho vingine vyaniacha hoi mie chongo.
Kwa kiasi fulani bado nina majonzi na machozi mazito moyoni mwangu, Nikiwa ningali bado gerezani, babu yangu  aliugua vidonda tumbo, nikapata fununu babu yangu amekwisha twaliwa ameuwacha mwili na roho yake pema peponi.
                Bado nina kidonda moyoni mwangu, kidonda kibichi, bado hakijapata kupona sawa sawa, miezi miwili tena mara baada ya  babu yangu kuaga dunia bibi alipatwa na mshituko wa moyo, akadondokea kwenye moto wa mafiga matatu, siku hiyo alikua akipika ugali mekoni. Vifo vyao viliwasikitisha sana wanakijiji walioomboleza pasina uwepo wangu, sasa mambo yote yamebadirika nimempoteza wangu wa moyoni Brenda, nimewapoteza walezi wangu babu na bibi, nimeachana na  cheo changu ndani ya TBL, nimekuwa mpweke mwenye msongo wa mawazo. Mazuri yaliyonifuata yamekua mazito mtimani. Sio mbaya sana nipo na mwanangu Ayubu wacha adeke deke kwa babaye, mamaye amekwisha pendwa na mwanaume aliyenionesha ukarimu  na ili kumpata mama Ayubu ilibidi atumie mbinu mbadala, ndo’ sababu za mie kulala jera.
                   Ukarimu wa bwana Biko umekua shubiri mtimani mwangu, nimekubaliana na matokea kwamba nilichelewa kutimiza ahadi ya kumpatia Brenda maisha bora, nilichelewa japo nilikua na nia ya kufanya hivyo sababu nilimpatia promise, nikamwambia I promise you……..Ah! ninatizama majira ninagundua kuwa muda umekwenda sana ni saa tisa, ni usiku wa manane, nipo bado napiga mitungi ndani ya bunge letu, bunge la walevi wa kiafrika. Nina cheka cheka pekee yangu, nina cheka cheka kama mwendawazimu, ninafurahia hiyo nafasi ambayo  walevi wenzangu wameniambia ati kesho ndo’ siku yenyewe kesho ndo’ siku ya mie chongo kuvishwa ufalme, ili niwe mfalme wa chama cha walevi Tanzania.  Lakini mmmh! Msema kesho mwongo, lakini……. Lakini…. Lakini…….. Subira yavuta heri.
                 ###############################################
                                              MWISHO 

BEKA

 SURAYA TATU                        “AKIPITA ATAJIPITISHA.” Beka akawa member wa kampuni ya SIGA, akipelekwa hapa na pale kulinda mali za ma...