Friday, August 8, 2025

I MISS YOU CHUGA

 CHOMBEZO: I MISS YOU CHUGA



SEHEMU YA PILI


(ILALA DAR ES SALAAM)


       Nikarudi chumbani nikamkuta Jerome amelala mie sikutaka kulala sababu nilitibuliwa na mawazo lukuki juu ya mchepuko wangu Obi basi nikafanya hima hima kuzikusanya nguo chafu za mie na Jerome nikaelekea kuzifua Faster faster mawazo hayaishi juu ya Obi mchepuko wangu nilipomaliza kufua nikakusanya vyombo vichafu nikavikosha na pia nikapuguta deki faster faster saa moja juu ya alama kazi zangu zote za pale nyumbani zilifikia tamati.


Jerome tayari alikwisha kuondoka akaelekea kazini kwake Posta, anabiashara zake, kwanza anaduka moja kubwa anauza simu za kila gharama, pili ana duka lingine kubwa la vipuri vya magari, mie na Jerome hatunaga shida sema bado tunakaa uswahilini sababu Mzee baba (Jerome) anafanya kujenga nyumba yetu sie wenyewe huko CHANIKA nje kidogo na mji wa Ilala. Mie na Jerome hatunaga shida sababu pesa ipo na uzuri wa pesa Jerome ananikatia kingi, na ubaya wa mie Sonia hicho kingi ninampatia Obi Mchepuko wangu. kutokana na mazoea ya kumpatia Obi pesa mingi, Obi amejenga tabia na mazoea ya kuni ‘distrub’ ati nimpe zaidi na zaidi nikimyima pesa nayeye ananinyima penzi lake tamu kuliko asali.

Alright, mie nilipomaliza kazi za pale nyumbani, Sharifu shamba, nikatoka na kuufunga vizuri mlango wa chumba chetu kimoja tulichopanga hapo Sharifu nikawaaga majirani zangu, jamani eeh mie ninatoka sintakawia kurejea.

Bajaji ilinidondoshea hapo kituo cha Polisi Pangani, nikafanya faster kumlipa dereva mwendesha Bajaji, nikaingia ndani ya kituo cha Polisi Pangani nimebeba pesa za kutosha angarau moyoni nilijisemea wakihitaji Pesa ili Obi atoke hapo kituoni nipo radhi kuwapa kidogo kidogo.


“Hallow, Aunty habari yawewe, pole na majukumu yote,” nilimsalimia Polisi wa kike, ameshiba vizuri yule mwanamke mwenzangu weupe wake amenizidi, mzigo huko nyuma nimemzidi, kazisuka vizuri nywele zake, ana miwani machoni, yupo kuandika andika ndani ya daftari la kuandikia kesi zinazoletwa pale kituoni.


“Habari ya mimi nzuri, kimajukumu nimepoa, nikusaidie nini Aunty?”


“Ninashida Aunty, kuna mtu wangu wa karibu anaitwa Obi, nimepigiwa simu alfajiri ya leo nimeambiwa amekamatwa, ana kesi ya kujibu, hivyo nimekuja kusikiliza Tatizo lake nini haswa?”


“Ok Auny embu nipe dakika sifuri nicheki cheki kwenye Buku la kesi ili nijue tatizo la mtu wako wa karibu, maana mimi nimeingia shift muda si mrefu, kesi kama hii iliandikwa na Askari wenzangu waliokuwepo ‘On duty’.” Yule Aunty alichukua daftari lenye kesi za watuhumiwa mbali mbali akaanza kulitafuta jina la Obi Mchepuko wangu akalipata, akanisomea kesi ya Obi kisha akaniambia.


“Jana usiku yapata muda wa saa tano, Obi alivamia chumba cha Bi.dada mmoja jinale Rehema, Bila ruhusa Obi aliingia, Jirani walimuona. Na kwa sababu muda ule Rehema hakuwepo nyumba Jirani walihisi Obi ni mwizi, hivyo wakamvamia mule chumbani na kumtoa nje, Jirani wakamhoji Obi ana shida gani kuvamia chumba cha mtu ambaye hayupo ndani?”


Mmmh! Maelezo yale yalinitia wivu,nilihisi Obi tayari kampata demu mwingine, kwanini avamie chumba cha mtu usiku? Mtu mwenyewe hayupo, je Obi na huyu Rehema wana mahusiano gani? Sikupata jawabu la moyo wangu, Askari aliendelea kunena.


“Aunty inasemekana kuwa Rehema aliupoteza ufunguo wa chumba chake, ndio sababu ya Obi kuingia na kuvamia, ile anatolewa ndani ya chumba cha Rehema Obi alikuwa amelewa chakali, akatumia Lugha chafu kuwatusi wale watu waliomlazimisha kuondoka.”

“Nimekuja KUMF*****Rehema, sina shida na nyinyi, embu niacheni Choko nyie.”Askari aliongea kama vile nayeye alikuwepo mbele ya tukio.


“Bwabwa nini wewe? Unamwita nani CHOKO, wewe ni Jambazi, huwezi kuingia ndani ya ya chumba cha mtu bila ruhusa,” Majirani walimpigia kelele Obi ambaye bado pombe zilimtawala.”


“Nasema sitoki hadi nimfir* Rehema, umbwa nyie msiniharibie Starehe yangu.”


“Nani umbwa? Tumevumilia sana matukano yako, sa’ ngoja tukuoneshe kuwa jeuri yako si kitu. Ghafla majirani wakamshambulia Obi, wakamponda vibaya mno nayeye alivyo jeuri akawarudishia vipondo vyao, mapigano yao yalisababisha Obi aletwe kituoni.”


Oooh! Masikini, hisia zangu zilikuja kuwa kweli, kumbe Obi ana demu mwingine zaidi ya mie.’Mfyuuuu’ nikafyonya kwa hasira. Si bure nimuache tu afie Jela ili huyo Rehema aje kuuzika mzoga wake.


“ Naweza kumuona Aunty?” Nilihitaji kumuona Obi.


“No problem keti hapo kwenye Siti nipe dakika sifuri, Obi atakuwa pamoja na wewe,” Askari aliongea akaenda ‘Cello’ chumba kimoja kidogo ndani y a kile kituo, akafungua mlango wa hicho chumba kisha akaita jina la Obi, Obi akaitikia Askari akamwambia ‘nifuate’,


 Obi akamfuata. Lo! Nillipomwona mchepuko wangu, nilimuonea huruma kwa jinsi alivyo onekana amevimba mwili mzima, damu iliyogandiana mwilini imegandiana pia kwenye nguo zake. Haki Obi alipewa kipondo cha kufunga mwaka.


“Obi pole Mpenzi,” Nilimtia faraja zile chuki za kumchukia Obi ati sababu ampata bibi mwengine ziliyeyuka zikanitoka na kupotea, nikatuliza moyo, huruma na machozi juu ya mchepuko wangu.


“Asante Mpenzi,nimepoa.”


“Obi kwanini unanifanyia hivyo Sweet heart.” Nilimfuta futa Obi damu zilizogandiana mwilini kwa kutumia kanga yangu Moko.


“Nisamehe Sonia, nisamehe lavu pombe, ilinitawala”


“Mbali na pombe kumbe Obi unaye demu mwingine?”Niliongea kwa hasira kidogo.


“ Ni pombe Sonia, ni pombe lavu, pombe zilinipitia. Naomba nisamehe, sintarudi, Obi alinisihi akiwa anatia huruma kibao Usoni.


“ Sonia fanya juu chini mie nitoke hapa kituoni, Umbu wananing’ata balaa.” Obi aliongea.


“Nikikutoa sitaki kusikia habari za huyo Rehema, mwambie nitaua mtu mie nina wivu wangu mwenyewe, sikubali kuibiwa kizembe.” Nilimuonya Obi, Nikasimama pale tulipoketi nikaelekea Kaunta niongee na Polisi yule demu mrembo haswa


ITAENDELEA

No comments:

Post a Comment

ZEE LA ZAMANI

  SEHEMU YA KWANZA. HOTELINI Ndani ya Hoteli Paradiso katikati ya Jiji la Mzizima (Dar es salaam) ZEE LAZAMANI akiwa na Mwanagenzi wake JAN...