Saturday, August 23, 2025

CASH MADAME



CASH MADAME.


 SEHEMU YA KWANZA


STEVEN BIKO

            Suzanna ndio jinale halisi, lakini wacha tumpatie jina la  Cash Madame, mama mwenye pesa zake, kama yeye binafsi anavyopenda kuitwa. Yeye ni mama la mapesa, hapa mjini mama kama yeye  vijana wengi utawasikia wakimwita ‘pendeshee’ yaani mama la mapesa kama nilivyo kueleza mpenzi msomaji, Suzann ana pesa mapesa, pesa nyingi kama mchanga wa bahari Suzanna hana shida kama unavyodhani weye mwenye kijicho cha ukapera yeye ni Cash madame mama mwenye pesa zake.

 Jumamosi ya leo ni wikiend moja tulivu, Suzi au tumwite kwa jina alipendalo Cash madame (Mama mwenye pesa zake) anateremka ngazi mbili tatu za hiyo Benk ya NMB tawi la Mwalimu house Ilala boma, ametoka kazini na sasa anaelekea nyumbani kwake, Magomeni mapipa huko ana mjengo wake, bonge la mjengo aliojengewa na mumewe marehemu Mheshimiwa Abdul Kadiri.

                  Suzanna aliteremka chini kwenye ngazi ya Benk ya NMB Mwalimu house, amevalia moja ya sketi fupi yenye rangi ya bluu ikionesha asilimia kubwa ya maungo yake, mapaja manono malaini ya kunenepa, yeye mwenyewe ni mweupe wa rangi ya chungwa la kitanga nakwambieni mwanamama ni mwenye mg’ao wa  dhahabu mnene wa kuridhika, wigi lake jeusi kichwani, kajipaka wanja kwenye kope zake, lipstick midomoni mwake, basi mwanamama anatembea kwa maringo na kwa madaha anaelekea kunako gari yake, gari moja zuri aina ya  Prado. Nadhani gari hiyo mwanamama kaigharamia si chini ya milioni hamsini au milioni themanini na ushee, hiyo ni kazi ya mumewe Bwana Abdul Kadiri kumfanya mkewe mrembo anapata furaha sio mdomoni pekee kunako tabasamu pia moyoni kunako hifadhi hisia za mapenzi ya dhaati

                 Suzi aliifikia gari yake, mara baaada ya kuteremka ngazi mbili tatu za ile Bank ya NMB Mwalimu house, akaingiza mkono wake wa kuume kunako moja ya pochi  zake nene zilizo jaa maburungutu ya pesa, noti mpya mpya zenye rangi nyekundu (Elfu kumi kumi) kama sikosei zilikua yapata milioni saba. Ndio tabia yake,  yeye na pesa pesa na yeye anatembea siku zote na maburungutu ya pesa mikononi mwake, hana shida yeye si ni mtumishi wa Benki na baya zaidi mumewe Marehemu Abdul kadiri hakua mtu mdogo hapa Tanzania mtu  maarufu mwenye cheo chake mwenye mshahara wake, tena mumemewe ni fisi la mafisadi, ashindwe nini? Kama ni pesa na utajiri vitu hivi havikumpa shida.

                Suzi akaitoa Remote ndani ya pochi yake ya mkononi na baada ya kuichomoa hiyo Rimoti akabinya binya vitufe fulani akiwa amesimama pembezoni mwa gari yake na hata baada ya kubinya binya vitufe hivyo gari yake ikatoa mlio wa ‘piiiiiii piiiiiii piiiiiii’ mlio wenye sauti ya chini,  mlango wa gari yake mlango wa mbele, mbele kwa dereva ukafunguka akajitoma ndani, akaingia kwa madaha akisindikizwa na macho pamoja na vimacho vya wanaume vijana wanaouza mitumba hapo soko la Ilala boma yangali yanamtizama kwa matamanio makubwa miongoni mwa macho ya hao vijana  mengine yakijisemea “nitampataje mwanamama mzuri huyu.” Suzi yupo very simple hana magumashi yaani hazingui wala hapotezei akikupenda kakaangu basi ujue kuwa amekupenda balaa, amekupenda penzi la dhaati hakuachi, au labda umuache wewe na roho yako, roho ya wivu na tamaa, roho ya……. Mmmh!  sijui utayaweza? Ushindwe mwenyewe! Teeh teeh teeh (Nacheka mie).

                  Basi ndo hivyo tena, mara baada ya Suzi kuingia ndani ya ile prado yake nyeupe, harufu nzuri ya marashi aliyoyanunua kule Pemba na Unguja yakalipamba gari lake, gari ikanukia na kupendeza zaidi Suzi akaiwasha gari yake naye akaondoka pale Ilala Boma.

                  “Dah! Sijui niende wapi siku ya leo nikajirushe?” Suzi aliwaza yeye na moyo wake yungali yupo round about, kati kati ya makutano ya  barabara ya Uhuru na  Kawawa, gari yake imesimama taa zimeruhusu gari zinazoenda Kawe, Kigogo ya Mburahati, Mabibo, Manzese na Makumbusho.

               “Aaah! Wacha niende beach, nikaangaze angaze macho yangu leo.” Suzi alihitimisha matamanio yake, sasa amebadiri nia badala ya kwenda nyumbani kwake Magomeni ameona wacha aende beach kupunguza mawazo pamoja na kupepewa na upepo mzuri wa baharini.

                      “Beach!” Suzi aliwaza tena, taa za kuruhusu magari, zilimruhusu apite.

                      “Magogoni beach, Kawe beach, Mahaba beach, Kunduchi beach, Kigamboni beach……. Ooooh beach…beach…beach….!!!’ Suzi aliongea kama mwendawazimu, gari yake iliendelea kutembea, mara jicho lake likatua juu ya uso na mwili wa kijana mmoja aliyekua akitembea pembeni ya bara bara, mtaa wa Congo, moyo wa Suzanna ulishituka na kudunda kwa kasi ya ajabu, ndu ndu ndu ndu moyo wake ukaendelea kwenda kasi, hakutaka kwendelea mbele.

 Akaisimamisha gari yake pembeni ya bara bara ya ule mtaa wa Congo, macho yake yalitua kwa yule mwanaume kijana mweusi hivi, mrefu kiasi, sio mrefu sana, ana mwili wa mazoezi,(body bulder) mwili wake umejengeka vizuri, amevalia singled inayo onesha wazi misuri ya mikono yake, misuri mizito minene ana kifua kipana kinachovutia, ana sura nyamvuto yaani sura inayovutia mwanamke, ukimwona mwenyewe utampenda, labda utakubaliana na mie kuwa asilimia kubwa ya wanawake wanaona aibu ndio maana wanashindwa kumtongoza japo wanamtamani sana.

                  Baada ya Suzanna kuisimamisha gari yake hakutaka macho yake yazibwe kwa pazia, kama wasemavyo wahenga bahati haiji mara mbili mbili, chelewa chelewa mwana sio wako, hakutaka apitwe na wakati ndio maana alikuwa macho kodo ili kujua wapi na wapi yule kijana hand some ana elekea.

                 “Ooooh!” Cash madame alivuta pumzi ndefu iliyotaka kumtoa kijasho, kiyoyozi kilicho ndani ya gari yake kilimpooza naye akalainika na kuregea kijike jike, yule kijana alivuka bara bara, kutoka kushoto kuelekea kulia sehemu ambayo gari ya madame imeegeshwa. Kijana yule mwenye body builder alitembea kwa nguvu zake zote wakati huo huo Cash madame alikua akitizama ujio wa yule kijana kupitia kioo cha gari yake, moyoni asitake kuona yule kijana anampita kama gari bovu.

                “Holla! Hallow brother!” Suzanna alimwita yule mwanaume kijana mwenye macho makubwa kama mayai ya bata, makubwa kama mfano wa mwanamke aliyetafuna kungu manga, ana nywele nyingi za kichotara wa kipemba, ni mzuri sio wa sura pekee, jinsi anavyotembea, anavyosimama na anavyomtizama Cash madame. je akifungua kinywa chake apate kuongea? Mmmh! Hiyo sauti yake tamu nakwambieni madame atachanganyikiwa, hiyo sauti yake tamu itampooza madame, italipooza joto alilo nalo, haki ya Mungu! Madame atazimia kwa furaha, presha, presha, presha ya kupanda na kushuka itampalia madame, mama mwenye pesa mapesa.

                  “Yeah madame.” Yule kijana aliitikia, macho ya hawa wawili yakatazamana.

                  “Unaelekea wapi nikupe lift?” Suzi aliongea kwa kujiamini, Keisha toka ndani ya gari yake yupo ‘out’ kisiketi chake kidogo, kilaini, kimepanda juu kinayaacha mapaja yake yakiwa wazi yanaonekana, meupeee pee, si mkorogo wala si mchina ( sio yale ya kutengeneza kwa madawa na makemikali) ni yale ya asili.

                   “Naelekea Posta ya zamani, asante kwa lift.” Yule kijana akaelekea lango la mbele kushoto, akajifungulia na kuingia, sijui kwanini hakusita sita? Yeye mwenyewe alijishanga shangaa na kujikuta tayari amejitoma ndani ya ile gari ya yule mwanamama mrembo aitwaye Suzanna. Wawili wale hawakukumbuka hata salamu zaidi ya kutizamana tizamana kama vile misukule isiyojua nini kinachoendelea.

                  “Namie naelekea Posta,” Suzi alijishaua shaua, akimtizama yule kijana aliyeketi, mbele ya gari yake.

                  “Niite Suzanna, watu wengi upendelea kufupisha Suzi.” Suzi alijitambulisha.

                  “Oooh jina zuri kulitamka lapendeza machoni, lavutia moyoni.” Yule kijana mwenye kifua kipana na mikono ya mazoezi pamoja na mwili ulio jengeka kisawa sawa aliongea, madame alifurahi kusifiwa na yule mwanaume kijana hand some.

                 “Mie ninaitwa Steven Biko lakini watu wengi wanapenda kuniita Steven power, body builder, kwa sababu ya mwili nilionao, mwili wa mazoezi.” Steven alijitambulisha wakati huo huo bado Cash madame angali ni mwingi wa tabasamu, tabasamu pana kama mlango wa pango la kale.

              “Vip umeoa Steven power?” Madame aliuliza.

              “La! Asha, sijaoa.” Steven hakushangazwa na lile swali aliloulizwa na yule mwana mama mtu mzima.

             “Na wewe je umeolewa, una mtu pembeni?” Steven power alimuuliza Madame.

           “Sijaolewa bado.” Madame alimjawabia yule kijana mwenye mwili wa mazoezi.

           “Mmmh!” Steven aliguna mguno ambao Cash madame aliusikia.

                     “Mbona waguna?” Suzi alimtwanga swali Steven Biko.

                   “Siamini kama kweli haujaolewa, kwa uzuri ulio nao utakosaje mwanaume hapa Dar es saalam.” Steven alionesha wasi wasi wake.

                   Teeh teeh teeh teeh! Madame alicheka kicheko cha maringo na madaha.

                  “Kuolewa ni bahati Steven au unataka kunioa wewe?” Madame aliropoka, Steven aliishia kutabasamu, hakutaka kulijibu lile swali la Madame haraka namna ile. Gari ya Madame iliendelea kukata mitaa.

                 “Vipi je tunaweza kupitia Hoteli tukapate Lunch?” Suzi aliongea wakiwa karibu karibu na Serena Hoteli, moja ya Hoteli za kifahari ndani ya jiji la Dar es salaam.

                  “No problems, hakuna matata, binafsi nina njaa kali.” Steven aliongea, gari ilisogea mbele na kwa bahati nzuri wawili wale walifika Serena Hoteli wakaingia wakaketi mbele ya moja ya meza za Hoteli ile, wakimsubiria mhudumu afike awahudumie mahitaji yao. Ala za muziki zilisikika masikioni mwao, magitaa pamoja na vinanda viliwaburudisha wageni waingiao na wale watokao ndani ya ile Hoteli wasijisikie wapweke wajisikie wapo nyumbani wankaribishwa tena na tena

                  Mhudumu aliitwa na kujongea pale walipoketi wale wawili, mhudumu huyu alikua ni msichana mmoja mzuri, mzuri wa kumtosha Steven Biko, waliendana kiujana ujana, yule msichana hakuling’oa jicho lake mbele ya yule mtanashati aitwaye Biko hali ile ilimpa kero na kumtia gere Cash madame, lakini hata hivyo hakujari alihitaji kupotezea, hana shida, kama ni pesa anazo, na kama ni kumpata Steven power sidhani kama atashindwa.

                  “Karibuni wapendwa hapa ndio Serena Hoteli, kuna kila aina ya vyakula na manywaji mtakayo.” Mhudumu aliongea wakati huo huo akaitoa Menyu yenye lundo la vyakula vya bei gharama akawapatia wale wageni Hotelini.

                  “Mie nipe samaki wa kukaanga wakubwa wawili, nyama iliyopigwa rosti, kuku mzima wa kunitosha pamoja na supu ya mbuzi, mtori wake uwe mwingi bakurini.” Steven Biko aliagiza mara baada ya kuisoma Menyu.

                  “Mie niletewe kuku rost wa kunitosha, maziwa mtindi pamoja na wali maini tena unijazie maini bakurini nile nishibe.” Madame alitoa oda yake. Mhudumu aliondoka na kwenda kuwachukulia, hakukawia alirejea na vile vyote alivyo agizwa, mapocho pocho kamili, manywaji ya bei ghari kutoka Ulaya na South Africa.

Basi Madame na yule Kibeni teni wake (dogo dogo) aitwaye Steven Biko, mwanaume mwenye mwili wa mazoezi, aliyejazia, aliye shiba, mzuri wa sura chotara wa kipemba na kiarabu. Waliendelea kula taaratibu taaratibu wakinyofoa nyofoa na kutafuna vipande vya nyama walizoagiza. Malaji pamoja na manywaji ya Bei gharama.

                 “Je, unakunywa Pombe?” Suzi alianza kumchokoza chokoza handsome wake aliyemuokota mtaa wa Congo.

                 “Yeah, niko safi katika unywaji wa pombe kari za kisasa.” Biko alideka.

                 “Good, nitakununulia siku ya leo, unywe utosheke, hata ukipenda agiza kreti mia, nipo tayari kukununulia.” Suzi aliongea.

                  “Waooo! Napenda sana bia pamoja na mizinga ya konyagi.” Biko aliona sasa ni fursa ya kuagiza kila atakacho. Wakati wote ule wangali bado wananyofoa nyofoa minofu ya kuku na samaki.

                   “Biko.” Suzi alimwita Biko.

                   “Naam Madame,” Biko aliitikia, Suzi akiwa ni mwingi wa tabasamu akanena.

                   “I love you so much Biko, nimetokea kukupenda sana, naomba uniamini tena unielewe mie moyo mpweke.” Suzi aliongea akimaanisha.

                   “I love you too Suzi, nimekupenda my.” Biko pasina kupepesa macho, aliongea na kujishaua.

                   “It’s true, ni kweli love?” Suzi alihitaji uhakika kutoka kwa Biko.

                    “Yes my,I mean it…..nina maanisha.” Biko hakuchelewesha jawabu.

“Waitress! Leta bia hapa.” Steven Biko alimpigia kelele mhudumu yule aliye wapokea, yule mhudumu mrembo ambaye mara kwa mara hachoki kumtazama Steven Biko kwa matamanio makuu, japo anashindwa kuelewa atampataje pataje, maana anajua fika kuwa mwanaume yule ana mtu wake, na mtu huyo ni mwanamama mwenye pesa zake.

                  Bia zililetwa, kreti zima, pamoja na konyagi mizinga, meza yao ikasheheni chupa kibao za pombe. Biko hakulaza damu aliendeleza makamuzi, alizishambulia zile bia kwa pupa ni kama vile hajapata kunywa pombe miaka na miaka mingi iliyopita.

                   “Duh! Kumbe yupo konki, konki liquid, konki master. Mnywaji mzuri wa pombe.” Suzi aliongea yeye na moyo wake mara alipomwona Steven Biko akigugumia bia mbili tatu kwa pupa.

                   “Mbona wewe haujinafsi kwa bia mbili tatu?” Biko alimuuliza Madame ambaye wakati wote huo alikua kinywa mvinyo,

                   “Aaah! Love mie tena sio mtumiaji wa kileo chochote kile, mie ni wa vinywaji baridi, soft drink,” Suzi alimjibu Biko.

                    “Jaribu kidogo sweet heart.” Biko alianza kmshawishi Suzi.

                    “Asante, nitajaribu siku nyingine, si unajua fika kuwa mwenzio ninaendesha gari.” Suzi alijitetea. Biko hakuwa na neno zaidi ya kuendelea kunywa kwa mapozi yake yote, vilevi vilipopungua hakusita kuongeza, aliagiza, aliagiza, aliagiza, aliagizaaaa, hadi alipotosheka, akawa bwii’ amelewa chakari.

                     “Mhudumu.” Suzi alimwita yule mhudumu wa ile Hoteli ya kimataifa.

                     “Abee Madame.” Mhudumu alikuja haraka haraka pale alipo Suzi.

                      “Je tunaweza kupata chumba cha kulala?” Suzi alimuuliza yule mhudumu.

                      “Ndio Madame, chumba kizuri kipo horofa ya tano, mlango nambari 25.” Mhudumu alimjibu Suzi

                      “Ok. Kamata hii shilingi laki tatu ni zawadi yako, asante kwa kutuhudumia.” Suzi alimpatia fedha yule mhudumu, mhudumu alizipokea hakukosa shukrani, tabasamu pana lilimpanuka alikenua na kuchekelea moyoni kwa furaha, ile shilingi laki tatu ni pesa nyingi kwake, ni nani mwingine aliye wahi kumpa hiyo zawadi? Mmmh! Hakuna, leo kapokea bahati, bahati kubwa kweli kweli.

                      Steven Biko alikua bwiii amelewa hajielewi, yupo juu ya meza anapepesuka pepesuka macho yake yameregea regea, mwili umeregea hawezi wala hajiwezi, Cash madame akamzoa zoa pale alipoketi na kumpeleka kwenye lift iliyowatua horofa ya tano, wakajitoma ndani ya chumba nambari 25, kufika huko, Suzi akambwaga Steven Biko juu ya kitanda kimoja nadhifu, bora kiloichoboreshwa, na baada ya Suzi kumbwaga Biko juu ya kitanda Madame alianza kumchojoa chojoa viwalo vyote ndani ya mwili wa steven Biko alimchojoa kama vile kuku anaye nyonyolewa manyoya, na baada ya kumaliza kumnyonyoa nyonyoa nguo zake, sijui nini kilicho endelea, sie hatujui, wanajua wao wenyewe kile kilichoendelea.

                              #####################

                     Mapenzi ni ua chanua, mapenzi kikohozi, hayana siri mapenzi wala hayafichiki, ndio hivyo tena ikawa hivyo lile penzi la Cash madame pamoja na Steven Biko yule kijana mwenye mwili wa mazoezi, penzi lao likachanua na kupendeza, tizama leo Cash madame anamtoa Out steven Biko anampeleka Mlimani City anaenda kumfanyia Shopping moja ya nguvu, nguo si nguo bali ni nguo za bei gharama, mashati mawili ya bei gharama, suruali tatu za bei gharama, viatu vya bei ya juu hata ile saa anayoivaa Steven Biko ni saa ya bei gharama, haki! Steven Biko kwa sasa ameanza kujiona tayari amefika pale anapotarajia kufika.

                     Ule umasikini wake wote tayari umekwisha kuyeyuka, tena sasa body builder anaishi kwenye raha na starehe, awali alikua akifanya kazi ya kubeba ‘ndwika’ (mizigo) magunia na mizigo mingine ya wachuuzi soko kuu la Ilala boma, leo kama zari ameangukiwa na bahati nasibu, yeye binafsi anajiuliza aiwache au? Mmmmh! Never, impossible, acheni ajilie vyake vimekuja kama Mana ndani ya jangwa lenye njaa na kiu.

                     Miezi miwili mbele, penzi kunoga, penzi kunogela, mama mwenye pesa zake akamfanyia suprizement yule kijana mzuri mwenye mwili wa mazoezi, akamnunulia bonge la gari Land cruser pajero gari moja jeusi la kupendeza, haki! Steven Biko aliruka ruka kama mwendawazimu kwa yeye kupewa ile gari haijatokea maishani mwake, ni kama ndoto japo ni kweli. Msela akajiona sasa hapo amefika, patamu hapo, hameguki wala hadondoki, hapo panamtosha sana, hapo amefika pengine hapaoni.

                   Basi Steven Biko akaanza kudeka na yeye akadekezwa, Steven Biko akaringa na kujiona yeye ni bora zaidi ya rafiki zake wale wabeba ndwika, wale aliotoka nao mbali kimaisha, wale wasakatonge, wale alioumia pamoja nao alio hangaika nao, haki! Mbona alijiona na tena alijigamba.

                   Miezi miwili mbele, akanunuliwa kiwanja apate kujenga nyumba yake binafsi, maeneo ya kigamboni, ramani ya nyumba yake ikachorwa, haraka haraka nyumba yake ikasimama, nzuri ajabu, nzuri mfano wa zile nyumba zilizojengwa Mbagara kama unaelekea Chamanzi, uzuri wa nyumba hizo zipo ndani ndani, zinapendeza, zimejengwa kisasa, ni za wenye pesa zao matajiri wafanyao biashara zao.

                 Mpenzi yao yakanoga na kunogela, kila alichokitaka Biko alikipata, alikipata haraka pasina kuchelewa, pesa mingi alipewa, zawadi mingi aliletewa, maeneo mengi yenye fahari alipelekwa, Steven Biko alijiona kweli kweli, alijiona tayari amefika, tena amefika pale alipotarajia kufika na ule umasikini uliomkumbata hapo awali ulianza kujimegua megua wenyewe ulijimegua kama gamba la nyoka linavyojivua. Umasikini ule ulikiri kumuacha na kumtema kabisa.

ITAENDELEA 

BEKA

 




BEKA


(ANA SURA YA MAUZO.)


SURA YA KWANZA.

“SIIONI KAZI YOYOTE YA KUFANYA DINGI.”

Ile Beka anamuona Bella akipita pita barabarani, Sultan Hoteli, moyo wake ulikuwa ukiugua, ukiugua ndani kwa ndani, ukiugua kwa mapenzi, ukiugua kwa kumpenda msichana mdogo aitwaye Bella, mwenye kadirio la miaka kumi na mitisa, Beka ana umri wa miaka Therathini na moja ni mtu mzima mzima wa umri mwili akili na majaliwa.


        Jina lake halisi anaitwa BAKARI ARMOUR lakini alipoingia KIWENGA alibadili jina akajiita BEKA ARMOUR sijui kwanini aliamua kufanya hivyo au ni kwa sababu ya ujana na kupenda mabadiliko?  Labda! Lakini ndani ya vyeti vyake vya elimu ya msingi, Sekondari na kile alichokipata alipokuwa amehitimu mafunzo ya Ulinzi kwenye kampuni ya SIGA, jina lake bado litabaki kuwa ni lile lile, BAKARI ARMOUR.


        Ni Mzaramo kwa kabila, kijana wa Jiji la DAR ES SALAAM, amesoma shule ya Msingi Buguruni Moto, akabahatika kwenda shule ya Sekondari Msimbazi, matokeo ya mitihani yake hayakuwa mazuri, upepo ukabadilika, akawa ni mtu wa kuketi Vijiweni, akijifunza uhuni na tabia zingine mbaya zinazotendwa na vijana wa Jiji la Dar es salaam.


Beka hakuwa na jambo lolote lile la msingi  au la maanaa kulitendea haki, ili apate maendeleo, ajiotambue kuwa yeye ni kijana wa kiume, hapaswi kufanya mambo ya ajabu yaliyojaa uhuni. Bbabaye mzee Armour kipato chake ni kidogo, kidogo hiki kilitosheleza mahitaji ya familia, biuashara yake ya kuuza Mboga mboga haikumlipas sana, japo ilimtoa kimaisha ilimsaidia katika malezi ya watoto wake watatu BEKA, Aisha na Tunu.


        Mzee armour alipoona mwanaye anakoenda ndiko siko, huruma juu ya Beka ziliongezeka, alimuonea huruma mwanaye na hatimaye akafanya juu chini kumketisha chini, akamtaka mwanaye yeyue na moyo wake atamke  ni aina gani ya kazi ambayo ingelikuwa naafu ya maisha yake , kukaa bure hakutoshi, kuomba omba wapitao njia hakuridhishi, kuiba, kutapeli au kutumia nguvu za lazxima huo ni uvunjifu wa sheria, na uvunjifu wa sheria ni makosa, makosa yana adhabu yake. Sio haba baba alihisi anaweza kumpoteza mwanaye, akafanya juu chini, hana Budi kumnusuru mwanaye na majanga ya dunia.

Beka angali akikuna kuna kichwa chake kilicho jaa Umba, viroboto, chawa na kungtuni, nywere zake ni ndefunamezisokota sokota, midomo yake imekomaa na kuonesha rangi ya kijivu ni kutokana na moshi wqa bange macho yake mekundu kama pili pili iliyo ivaa yamezoea kupora, kunyang’anya, kubaka, kulawiti na kudhurumu kwa kutumia silaha zenye ncha kali. Beka Yule wa vijiweni tayari alikwisha haribika.


“Sioni kazi yoyote ile ya kufanya dingi wacha mie niendelee kusota kijiweni.” Beka alimjibu mzee Armour kijeuri jeuri pasina kutafakari vema.

“Beka mwanangu, Dunia ni nzuri lakini  lakini wanadamu sisis ni wabaya, yatazame maisha yako yalivyo haribika na kukongoroka, utamlilia nani kipindi cha dhiki kuu, mateso na maumivu, kumbuka ukimtegemea ndugu utakufa masikini, ukidharau mwiba utakuchoma, mdharau Jembe si mkulima. Tafakari ni aina gani ya kazi unayoweza kufanya ili mimi baba yako nifanye juu chini kukutafutia. Mzee Armour aliongea.


“siioni kazi yoyote ile ya kufanya Dingi, niache nitulie kijiweni nile raha za duniaq,, nile ujana kwa mudaa wangu, maisha ni mafupi, uzee hauko siku hizi tofauti na  zamani.”  Beka aliongea kwa dharau.

“majuto ni mjukuu mwanangu,asiyefundwa na babaye ulimwengu utamfunda, kiburi sio maungwana, kumbuka hiyo ni misemo tu lakini ukweli ujapodhiirika wewe utalia na kusikitika.kazi ni maisha ni kufanya kazi, mwenda bure hakai bure ataokota, mgaa gaa na pwa hali wali mkavu, fanya juu chini ufikirie aina yoyote ile ya kazi ambayo wewe unaweza ukaitendea haki.” Mzee Armour alimsihi mwanawe.


“mwanangu, ndani ya Jiji la Dar es salaam kuna kazi nyingi sana, ukitaka utoke vizuri unaweza ukajiajiri kwenye kilimo cha mboiga mboga, biashara ya kuuza maji, chakula cha migahawani, sokoni na kadharika, utatoka tu mwanangu, Binafsi sidharau kazi za kuajiriwa, zinaweza kukutoa kimaisha, lakini kujiajiri ni bora zaidi ya kuajiriwa. Sema ni kazi gani unaipenda na pia unaweza kuitendea haki.” Babaye Beka alimhoji Beka aina mbali mbaliu za kazi ambazo zingelimsaidia katika kuyaboresha maisha yake.
Beka alikataakata kata, alidai kwamba aina za kazi ambazo baba yuake anamtaka afanye ni kazi  zinazowafaa wanawake, yeye ni kijana wa kiume hawezi kuuchoshaa mwilio na akili zake kujishughurisxha na shughuri kama zile.

                        ##########

BENTEN BENITHO



HADITHI YA MAMSAPU



BENTEN BENITHO



 

Sehemu ya 1

Teh teh teh eeeh, ๐Ÿ˜‚ nacheka mie, nacheka Mamsapu nacheka mama wa Kitanga, nafurahia siku njema asubuhi Majogoloo, uhai nipewe pumzi shukrani kwake Mola, nafsi niitumie vema fursa tele bado zanisubiria. Mie niliyependwa ndani nikawekwa navuna nipandacho nala jasho langu mie mwenyewe. Mume kanipenda Moyoni haondoki anaifurahia Luba ya mahabati tena nakuambieni huyu Pompo ninamtunza kama mboni ya jicho langu, kan’torosha Peponi kan’jengea Paradiso Mbingu yangu Mbinguni.


Wahenga wanasema uzuri wa mwanamke sio sura, sio mvao wa mawigi yake kichwani wala sio maringo na madaha kama Twiga mbungani. Uzuri wa mwanamke huonekana Machoni, Macho udhiirisha uzuri au wema wa mwanamke. Kwa bahati nzuri sie wanawake tumejaliwa uzuri wa kuvumilia, kusamehe kuhurumia na kusaidia. Any way sijisifu kwa maneno na makeke!! Niwaachieni nafasi nyie wachambuzi mchambue chambue maneno yangu kama Karanga, makapi mkiyaswaga mbali na mema mkiyakusanya mkiyatunza na kuyahifadhi ili kizazi kijacho kifaudu.


Mama wa kitanga nimekujieni na simulizi moja iliyonitia machozi huzuni na majonzi makuu ninashindwa kumsahau Mwanawangu Laazizi wangu wa kufikia Benito. Mwana wa mke mwenzangu MAUA,  Mwanamama niliyempokonya tonge mdomoni.  Bi. Dada aliyetema pipi kwa maonjesho ya karanga. Nakumbuka nilikwisha wagea hii simulizi ya huyu Mwanadada kwenye ile simulizi yangu pendwa  MWENZENU N’SHAPENDWA sioni raha ya kuyarudia matapiko niliyoyatema miaka mingi iliopita acheni nisonge mbele, mbele kuna mafanikio


Bi. Mkubwa nikampokea mwanangu wa kufikia Benito, katoka masomoni Kenya huko ndiko mwanetu kakulia, kaishi sana huko kala na kulala Hostel. Mume wangu Pompo hana shida aligharamia. Ajabu kizazi hiki kizazi cha Bongo fleva ni shida! Hakipingwi wala hakipigiwi maweTeh teh teh (Nacheka mie)  Mtoto karejea na Satifiketi yake ya Form four ina Divisheni ziro. Mmh! Nipewe pole mie mwanamke. Mwana wa mwenzangu kakaa shule ya Bweni miaka kama yote leo hii arejee nyumbani na Divisheni ziro, niliumia.


Basi Benitho mwana wa mwanamke mwenzangu kaketi nyumbani ni mwaka wa pili sasa, hataki kwenda Chuo japo babaye ana pesa zake, kamfanyia mpango aende Chuo,  mtoto wa mwenzangu hataki kusoma! Kutwa kuchwa kajifungia chumbani kwake akipigisha Muziki mzito wa Singeli, Muziki unaoniudhi mie, Muziki unanichukiza masikioni sio haba Muziki huo umejaa maneno makali ya nguoni.


Nitawachukia vibaya wale Mashuga Mamy, wale wanawake wazee waliomzidi umri mwanangu Benito, kwa waliyonifanyia Mungu anawaona, Mungu awasamehe. Wamenivuruga mie na Pompo wangu, washatutesa sana juu ya Kibenten wangu Benito kijana aliyehitimu kidato cha nne miaka miwili iliyopita sie tulitumaini mwanetu angeliibukia Bingo kunako matokeo yake ya kidato cha nne lakin mmh! Yalituchoma. Mwana karudi na FFFF, GGGG, HHHH, ZZZZ, Ziro kwenye kila mtihani alofanya


Mmmh! Makubwa haya kijana aliyeketi Hostel miaka kama yote kuanzia darasa la kwanza hadi kuhitimu kidato cha nne anafanya vibaya kwenye matokeo yake ya kuhitimu elimu ya Sekondari. Je, yule anayekaa Dei? Kulea mtoto ni kazi nzito inayotaka moyo, mie binafsi ninamlaumu Pompo Dume langu la ukweli mapungufu yetu kama wazazi yanachangia kwa kiasi kikubwa sana kufeli kwa Mtoto darasani. Kutwa kuchwa sie tulikuwa tukizisaka pesa ili mtoto asome, ale vizuri, anywe vizuri, ajisikie kwamba na yeye yupo nyumbani. Kumbe tulijisahau, tulisahau kwamba pesa pekee haitoshi kumfanya mtoto afanye bidii darasani. Tulipaswa kumfuatilia mtoto ili tuyajue maendeleo yake kitaaluma, tujue ni wapi alipopunguka tumsaidie sababu uhuru ukizidi mtoto anaharibika, tubaki tukikumbuka wahenga walisema; Samaki ukunjwa akiwa mbichi ajapokauka hakunjiki.


Kwisha kumaliza kidato cha nne Benito akatua Masikani, anataka uhuru zaidi. Yeye na Muziki, Muziki nayeye. Ndo’ uingie ndani ya Apartment yake haukosi kuvurugwa kwa sauti zile za Maspika makubwa  ya Muziki yakitoa sauti nzito za nyimbo za kizazi cha leo wenyewe wanaita Bongo Fleva. Sikujisikia raha na furaha kuzisikiliza hizo nyimbo ambazo kwa asilimia kubwa hao wasanii wa kizazi cha leo haweshi kuimba utupu wa mwanamke, kumchora na kumharibu mwanamke.


Nyimbo zingine zinamdharilisha Mwanamke, hizo nyimbo za Singeli hazifuati ubora wa Lugha fasaha ya Kiswahili embu tuone mfano mmoja ambao msanii wa Muziki kama kioo cha


jamii anavyowadharilisha wanawake.


Michirizi ya kwenye Nyonga,

Shanga juu ya uno,

Matiti kama mto wa kulalia,

Nipe nikupe raha tupate.

Leta huo mzigo, Mashine nitakugea .


Mmmh! Ashakum si matusi siwezi endelea kusikiliza hizo nyimbo ziso adilifu. Serikali inawajibu wa kutoa elimu kwa kizazi hiki cha sanaa ya Muziki. Kwanza kwa kuanzisha Chuo kitakachowafunda Vijana Muzik na utamaduni wake. Vijana wetu watajua namna ya kuandika mashairi yenye vina na mizani. Nyimbo zenye maneno yenye hekima na adili. La, sio hizi ambazo  Maudhui yake hayafai kusikilizwa na watoto wadogo, wazazi na jamii kwa ujumla.


            Kwa hasira nikateremka juu ya Horofa ya tatu nikafika chini ya flow Apartment nikafanya kuvamia chumba cha Mwanangu Benito, nikaubamiza mlango wa chumba chake ukafunguka. Hasira zikanifanya nimpigie kelele Beni mwanangu wa kufikia.


            “Mwana we! Hembu nizimie hiyo Radio Spika, aina gani ya nyimbo unazosikiliza? Nyimbo ziso na heshima wala adili. Washindwaje kusikiliza nyimbo za dini upate kujifunza neno la Mungu nawe ubarikiwe.” Nilimkemea.


            “Mama wanizingua.” Kijana wangu aliongea kwa sauti kuu, sauti ya ujana wake sio nzito kuibeba, nyepesi, sio laini kama zile za videmu. Akah! Babu we, ninaogopa mwanangu akiwa na sauti za videmu mie nitaambiwa mwanao  nyota yake si riziki. Ninamshukuru Mungu kampendelea Mtoto wangu mrefu kiasi, mweusi wa rangi, mwili wake ni mwili wa mazoezi ‘Body builder.’


            “Sikiliza Beni ushakuwa mtu mzima na uzima wako una maana yake muhimu kuutunza ukutunze. Kumbuka ujana ni kipindi kifupi sana cha wakati, ujapouchezea ujana uzee utashika hatamu. Kwanini wasikiliza nyimbo ziso na maadili mema? Nyimbo zinazokupotosha na kukuharibia njia ya maisha yako.” Nilimkemea tena mwanangu.


            “Oyah Mamangu kama hauna Idea fresh si useme tu, mie nipo na stress kibao naomba uniache nijitulize.” Beni alinijibu kihuni huni nikamtizama akaichukua paketi ya Sigareti juu ya meza,  akaiwasha, akaweka domoni akaanza kuivuta mikupuo miwili mitatu.


            “Mmmh!”  Niliguna, moyoni nikijiuliza ameanza lini kuvuta Sigareti mwana wangu wa kufikia? Hapana. nilikereka. Nikamsogelea usawa wake nikampoka ile pisi ya Sigareti domoni nikaitupa sakafuni nikaikanyaga kanyaga na kuhakikisha haitoi moshi tena.


            “Wanifanyaje Mamangu? Mbona wanipoka uhuru? Je, nimefanya vibaya kurejea nyumbani? Beni aliuliza maswali mfululizo.


            “Uhuru mbaya huo mwana we! Wajua kuwa wewe ni msomi miongoni mwa wasomi  tegemezi katika taifa letu? Hembu sikia. Kupata Divisheni Ziro haimaanishi ati umefeli maisha.  Hapana, kuna maisha mengine baada ya kufeli Mitihani Darasani. Pale ulipoanguka amka tena endelea kukimbia, pale ulipokosea usiliwache kosa libaki kuwa kosa, jaribu kusaka ufumbuzi ili kulitatua kosa.” Niliongea kama mlevi, nisijue niliupata wapi ujasiri wa kumfokea mwanangu. Beni akafanya kutoka ndani ya chumba chake nisijue wapi anakwea, nikakitazama chumba chake kilkikuwa nyang’a nyang’a, shagalabagala, ovyo hakitamaniki kwa uchafu wa vikorokoro na vikorombwezo kibao vilivyozagaa chumbani.


 Kijana kabandika ukutani picha za utupu, tupu ya wanawake wa Kizungu, picha zingine zikionesha faragha ya mume na mke. Mmh! Nilikereka nikajiuliza Mtimani ni nani anayemharibu Beni wangu? Je, ni Shule aliyosoma? Ni marafiki na makundi ya marafiki? Mmh! Nilibaki na Labda.


            Njiiiiiii…..mmmmmuuu. Mlio wa gari ikiondoka ulisikika Beni alikuwa anaelekea pahali, sikutia shaka uhuru wa kuitumia gari anao, tushamuachia aitumie gari popote pale atakapo kuenenda.


            Nitamwita Haika mtumishi wangu wa ndani, azinyofoe hizi picha za utupu na kuzibwaga jahani kisha azitie kiberiti, hazifai wala hazipendezi machoni. Kazipata wapi hizi picha? Hakika dunia sio ndogo ina mengi ya kuhadithia. Nilijisemea mie na moyo wangu.


            Benito kasema ana stress, mawazo. Nalikumbuka kauli ile aliyoitoa Benito mwana wangu wa kufikia.


            Stress gani zamsumbua? Kwanini nimeruhusu aondoke na Gari? Mmh! Asijepata ajari, asije gonga Waja wa Maanani huko barabarani. Kwa sababu ya stress asije kamatwa na polisi wa barabarani! Hapana jamani yasimpate mabaya mwanangu Benito…… Ewe Mola umwepushe. Mwanangu na dhiki za ulimwengu. Nilimwombea mwanagu Beni nikapanda ngazi za Horofa ya tatu nikamfate Haika Mtumishi wangu nimpashe kazi ile ndogo anayopaswa kuifanya ndani ya chumba cha Benitho


TUENDELEE KESHO

WATOTO WANGU FREDO NA NELISO ๐Ÿ’•๐Ÿ˜ฟ

 



NILIWASOMESHA WATOTO WANGU KWA TABU SANA,๐Ÿ“š๐Ÿ“‘ WALIPOISHIWA ADA๐Ÿ’ฐ YA CHUO๐Ÿ‘จ‍๐ŸŽ“ WAKANITIMUA NYUMBANI KAMA PAKASHUME๐Ÿˆ‍⬛.


WEMA WA MUNGU ULIPONIZUNGUKA GHAFRA NIKAWA BILLIONEA๐Ÿฆ๐Ÿ’ฐ๐Ÿ’ธ๐Ÿ’ฒ WALIPOSIKIA ๐Ÿ‘‚KUWA NIMEKUA BILLIONEA WAKAANZA KUNITAFUTA ATI NIWASAMEHE.๐ŸงŽ‍♂️๐ŸงŽ๐Ÿ›


    "Maua ๐ŸŒนpamoja na wewe Adam  kuanzia Leo hamtakiwi kuonekana hapa shuleni,๐Ÿšท kosa mlilolitenda ni kosa kubwa, kufukuzwa kwenu Shule ๐Ÿซ๐ŸŽ’iwe fundo Kwa wengine."Mwalimu mkuu Bwana Chikoko๐Ÿ‘จ‍๐Ÿซaliongea kwa ukali.


      "Tunaomba utusamehe Mwalimu mkuu, hatukujua kama lile tendo lingelipelekea matokeo haya." Adam alilia,na mimi  Maua pia nililia.๐Ÿ˜ข๐Ÿ˜ฟ Ilikua ni lazima tuondoke pale shuleni sababu baada ya mie Maua kukutwa na ule ujauzito nililazimishwa kumtaja aliyenipa ule ujauzito.


    "Hamkuwekeza akili zenu kwenye elimu mkombozi wa maisha mkawekeza elimu kwenye tamaa za mwili zinaa na ujinga. Bodi ya Shule haiwezi kuwaacha mkasababisha Samaki mmoja aoze na wengine wafuate kuoza. Kamateni Barua๐Ÿ“ƒ zenu, wapelekeeni wazazi wenu na muwaambie hamtakiwi Tena kuwepo hapa Shuleni." Mwalimu mkuu alipaza sauti.


      "Please forgive us Sir." Tulipiga goti chini ndani ya Ofisi ya Mwalimu mkuu lakini Mwalimu mkuu hakutujali wala kutusikiliza, tukaondoka kuelekea nyumbani kwetu, tumejaa machungu, majuto na masikitiko.Tulipofika majumbani kwetu, nyumba hazikukalika, fimbo hazikutulia, fimbo nzito ziwakazo moto zilitua makalioni mwetu. Tulifinywa kwa visu vilivyopakwa mapilipili. Tulitukanwa na kuonekana kuwa hatuna maana ndani ya jamii iliyotuzunguka


Mateso hayakukoma, ilikua kila siku tunateswa na ukitegemea mie Maua nalikua tayari mjamzito, nalihitaji amani na utulivu sio stress ambazo kwa bahati mbaya zingelipelekea mimba kuchoropoka. Adam akanishawishi  tuutoroke Mkoa wa Bongo na kuelekea Lushoto Tanga. Ikawa hivyo basi tuliiba nauri na vijipesa kidogo vilivyotusaidia kuingia Lushoto Kijiji cha Magamba. 


"""""""""""""""""""""""""""

      Miezi Tisa kutimu mie Maua nilikuja kujifungulia nyumbani watoto pacha ๐Ÿ‘ฌ Fredo na Nelso, wavulana Wazuri tuliowalea katikati ya maadili, uvumilivu, heshima, utii na kuipenda elimu. Kilimo kwetu kilikua ni utukufu tuliipanda miti ๐ŸŒด๐ŸŒณndani ya shamba kubwa alilolinunua Adam, tuliipanda pia viazi, ๐Ÿฅ”karroti,๐Ÿฅ• makabeji ๐Ÿฅฌna matunda kama ma tufaa ๐Ÿ na mapeas๐Ÿ. Kila senti tiulioipata kutokana na kilimo tuliitunza kununulia mifugo ya nyumbani: Ng'ombe๐Ÿ‚, mbuzi๐Ÿkondoo ๐Ÿ‘kuku๐Ÿ“๐Ÿˆ๐Ÿ–๐Ÿฐ na mabata๐Ÿฆ†. Kidogo kidogo maisha ya uvumilivu yalitukubali.



    Fredo na Nelso  walikuwa na kuongezeka haraka sana. Tuliwapeleka Shule na kuwataka wasome sana Ili siku moja waje kuwa Madaktari bingwa waje kuwasaidia binadamu maana kusaidia binadamu ni wajibu wa kila mwenye moyo na roho nzuri. Hatukuwashauri wajiingize kwenye kilimo maana kilimo kilivyokua kigumu sijui kama wangeliweza.



      Ghafla janga zito likaibuka na kuikumba familia yetu, Adam akiwa Shambani akilima kwa kutumia Jembe la mkono alishituka kumwona Ng'ombe aliyepandwa wazimu akimwendea kwa kasi na kumfuata pale alipokua akilima. Adam wangu Aliogopa akaacha kilimo akaanza kukimbia lakini walisema wahenga mbio za sakafuni uishia ukingoni, hakuna marefu yasiyo na ncha Adam aligongwa kwa pembe ya yule Ng'ombe kichaa akapigishwa huku na kule tena akapiga kelele za kuomba msaada, wakulima wenziwe waliposikia kelele zake wakaacha kulima na kwenda kumpa msaada mwenzao.


     Yule Ng'ombe๐Ÿ„ kichaa tayari alikwisha toweka, wakulima walipofika pahali alipolala Adam wakamkuta Adam wangu anakata roho. Tumboni damu ๐Ÿฉธzimejaa na utumbo umetoka nje ya tumbo maana yule Ng'ombe alimbutua tumboni. Wakulima wakiwa ni wenye uchungu na majonzi wakambeba Adam na kumleta nyumbani. Huku kilio kikuu kilipasua anga. Nililia mie Maua, walilia wanangu pacha Fred na Nelson.


Kumpoteza Adam Mume bora na Baba bora kwetu tulihisi tufe la Dunia limetuangukia.๐ŸŒ Uchungu mzito ulituvaa miilini tukajivisha magunia na kujimwagia majivu kama tumepandwa Maruhani.๐Ÿ˜ˆ๐Ÿ‘น


         Baada ya mazishi ya Adam Mume na kichwa cha familia yule mbeba majukumu ya nyumbani, nyumba yetu ikapooza sababu mahitaji mengi yalikosekana tofauti na Kipindi alichokuwepo Adam tuliyafurahia maisha ya uvumilivu sio haya ya mie kuitwa Singo mama, mengi mazito kupambania.


Ilinibidi nianze kufanya kazi mbili kwa nyakati tofauti angarau nipate pesa za kuhudumia familia, nikapambana na kilimo wakati huo huo nikaanza kufanya vibarua vya kusafisha nyumba za mabosi: kupuguta deki, kufua na kuhudumia meza. Hakika Jua๐ŸŒž lilinikomesha.


     Nilihitajika nyumbani kuandaa chakula, nilihitajika Shambani kulima, bado vibarua vidogo vidogo viliniita na kunifuata. Nilihakikisha watoto wanakula, kunywa na kuvaa.Tena watoto wanasoma kwa bidii Ili watimize ndoto zao za kuja kuwa Madaktari bingwa na Mola wetu asivyo mbahiri wala choyo wanangu walikaza kamba hadi kuingia Muhimbili university kusomea mambo ya Udaktari.๐Ÿฉบ⚕️๐Ÿ’Š


     Maisha ya Chuo yalikua magumu sana, ada ya Chuo ilikua mzigo ingawaje walikubaliwa kupata mikopo ya masomo lakini bado tu mahitaji yao yaliongezeka ukijumlisha starehe na anasa zao za ujanani. Wakati Mama yao nikipambana na kilimo pamoja na kusafiri masafa marefu hadi Tanga mjini kusafisha majumba ya mabosi na majumba ya wenye pesa zao, huku nyuma wanangu walifanya anasa na starehe za ujanani. Hatimaye sasa pesa sabuni ya roho ziliwaishia vibaya wakakosa ada ya Chuo na kurejeshwa nyumbani.



     Walipofika nyumbani nilimwambia acheni Mama yenu nipambane lazima mtarudi Chuo kuendelea na masomo. Kweli kweli walikubali kubaki nyumbani kunisaidia kilimo๐Ÿช“๐Ÿ…๐Ÿฅ” na shuhuli za ufugaji, ๐Ÿ‚๐Ÿ๐Ÿ„๐Ÿwakati huo mie Mama yao ninafanya vibarua kwenye majumba ya mabosi na watu wenye pesa zao.


     Siku moja niliporudi kutoka kwenye vibarua vyangu niliwakuta wanangu wanajadiliana kuhusu shamba lile kubwa ambalo Adam baba yao alipanda miti:๐ŸŒณ๐ŸŒฒ๐ŸŽ‹


    "Maisha ni magumu Mama tukiendelea kukaa hivi hivi tutapoteza nafasi ya kusoma Chuo" Fredo aliongea.


     "Vumilieni wanangu, pesa zitapatikana tu. Mbali na kufanya vibarua nitawaomba mabosi wanipe mikopo itakayowawezesha mrudi Chuo." Niliwapooza Kwa maneno ya matumaini.


     "Mama hatuwezi na kamwe hatuwezi kuendelea kusubiri masomo yaaendelee kutupita." Nelso aliongea.


     "Wanangu Mimi kama Mama yenu nimewaambia msubirie na nyie hamtaki kwahiyo nifanye nini?"๐Ÿ˜” Niliwauliza.


     "Huna la kufanya Mama lakini sisi tutafanya jambo la maana." Fredo aliongea maneno ambayo sikuyaelewa.


     "Mtafanya kitu gani? Mnataka kurejea Chuo mikono mitupu." Nilihoji.


      "Pesa zipo Mama na pesa lazima tuondoke nazo." Fredo alijibu.


       "Unajua sikuelewi Fredo au siku hizi mmeanza kuvutwa bangi mchana kweupe? Pesa ๐Ÿ’ฐ๐Ÿ’ดziko wapi?" Nilianza kuzichukia akili za vijana wangu.


    "Baba si alituachia shamba, Hilo Hilo litatutosha kurejea Chuo." Neliso alinishitua.


     "Nini!? Mnalitaka shamba aliloliacha marehemu Baba yenu liuzwe? Haitawezekana, shamba Hilo ndilo litupalo kula na kutuweka hapa kijijini." Niliwaonya wasithubutu kuligusa shamba aliloliacha Baba yao Adam.


     "Huwezi kutuzuia Mama elimu ni bora kuliko kilimo kinachoumuza migongo na mikono. Lazima shamba liuzwe Ili turejee Chuo ili hapo baadae tuje kuwa msaada kwako." Fredo alitilia mkazo wa kuliuza shamba.


     "Never Fredo, never. Mkitaka nitoe radhi na kuwakasirikia jaribuni kuligusa Shamba aliloliacha Baba yenu." Niliwapiga kibuti kisha waliketi kimya. Muda si mrefu waliondoka kwenda  Bar ๐Ÿป, Ili kupooza koo zao kwa moja moto, moja baridi. Sikujali maana ujana ulianza kuwasumbua. Miaka ishirini na mitatu sio umri mdogo ni umri wa kijana kuanza kutamani vingi.

  
                                 ๐Ÿง‍♂️๐Ÿง‍♂️

Toba! Baada ya siku tatu kupita nilishangaa wanangu Nelso na Fredo wameongozana na Mzee mmoja aliyejulikana Kwa jina la Mzee Kapusi.๐ŸˆWaliponifikia waliamuru niache kulima lile Shamba ambalo Baba yao Adam alilinunua miaka 23 iliyopita.


       "Niache kulima ili iweje?" Niliwahoji.❓


       "Shamba tushaliuza Mama na Hati ๐Ÿ“ƒya shamba hii hapa. Bahati nzuri Baba kabla hajaaga Dunia aliandika majina yetu kwenye Hati kama walinzi wa hili Shamba. Fredo ambaye ndiye mkubwa aliongea.


        "Mmeliuza Shamba." Nilipata mshituko.

        "Hatukupi nafasi ya kusikiliza mara mbili mbili Mama, kuanzia Leo hili shamba sio lako au letu tushaliuza  kwa huyu Bwana Kapusi."

    
      "Wanangu mmeniua." Machozi na kilio cha kwikwi kilinitoka.


       " Mmeniua wanangu, mmeua rasilimali ya pekee inayotupa maisha hapa kijijini, tutakuwa wageni wa nani. Ooh! Nilijitupa juu ya shamba langu na kuanza kujigaragaza.


     " Sasa wewe ukitegemea tukae tu kusubiri iyo mikopo unayokopa Kwa mabosi? Tutasubiri Hadi lini? Jua likizama na siku kuyoyoma" Fredo aliniita uchungu na hasira


     "Mgekua na Subira wanangu lakini sio kuuza Shamba ambalo ndilo tegemeo la maisha yetu."


      "Hatuwezi kukitegemea kilimo, hatukuzaliwa kuwa wakulima. Tulizaliwa kuwa wasomi na Madaktari" sikutaka tena kuendelea kusikiliza ule upuuzi wa watoto wangu. Nikafanya kuondoka pale Shambani nikaeleka mtoni huko Nililia sana, machozi YANGU yakawa sawa sawa na maji ya mto. Jioni ilipoingia sikutaka kurejea nyumbani sababu nilikua nikilia tu na kumkumbuka Adam Mume wangu aliyeniachia watoto wasiokithamini kilimo.

Kiza kilipoanza kuingia niliona sio vema kuketi mtoni umbu wakinisumbua na kuninyanyasia damu yangu. Nikafanya kurudi nyumbani.


     Nilipofika nyumbani nilishituliwa na sauti za maradio๐Ÿ“ป๐Ÿ”˜☢️ spika yaliyokua yakitoa sauti za Muziki mzito wa Bongo freva. Sauti zilipanda juu Hadi ikawa kero kwa majirani hali ambayo haijazoeleka nyumbani kwetu.


     Ngo' ngo' ngo' ๐Ÿค›๐Ÿค›๐Ÿค›. Niligonga mlango Kwa hasira  mara baada ya kuchungulia dirishani na kuwaona vijana wangu Fredo na Nelson wakinywa vilevi vikali vilivyojazana juu ya meza  iliyopo sebuleni baya zaidi vijana wangu waliwakodi wasicha warembo kutoka mjini waje kucheza Muziki wakiwa nusu utupu.


    Ngo' ngo' ngo๐Ÿคœ๐Ÿคœ๐Ÿคœ' niligonga Tena lango la sebuleni.

       
    "We nani? "Fredo aliipunguza sauti ya Muziki na kuja mlangoni akiwa amelewa apepesuka.


    "Tafadhali Fredo nifungulie mlango muda si mrefu mvua itanyesha." Niliongea.


  "Mama hauna chako hapa nyumbani, shamba sio lako na nyumba sio yako pia." Neliso alipaza sauti wangali wameufunga mlango, Safari hii wote wamesimama Dirishani.


   "Nini nyie vijana? Mmerogwa nyie! Mnazipata wapi kauri hizi za kumvunjia Mama yenu heshima? Ama Kwa vile Adam Baba yenu aliwapa kipaumbele cha kuwaachia urithi? Urithi huo haukupaswa kuuzwa Mama yenu nikiwa hai."


    "Ukiwa hai au usipokua hai haitatusaidia sababu nyumba ni yetu na Shamba ni letu. Uzuri tushaliuza na nyumba hii tupo mbioni kuiuza." Fredo aliongea Kwa sauti Kali ya makaripio.


    "Fredo na Neliso, Mimi ndiye Mama yenu niliyewatunza ndani ya tumbo langu Kwa zaidi ya miezi Tisa ni Mimi ndiye niliyewalea Kwa tabu na Kwa shida Hadi mfike Chuo, Chuoni mnafundwa kuwadharau wazazi wenu?" Niliongea chozi likinibubujika.๐Ÿฅฒ๐Ÿฅน


     "Tafadhali ondoka Mama hapa hauna chako, kama ni suala la kututunza au kutusomesha tunasema Asante hata sisi tutazalisha, tutalea na kusomesha." Wanangu walitumia Lugha Kali sana.



     "Wanangu naomba mfanye utu na kufikiria Mama yenu asiye na baya, angalieni mtapata radhi na laana juu ya yule aliyewatabikia na kuwaangaikia. Tafadhali nifungulieni." Wanangu hawakutaka kunisikiliza, mvua kubwa ilianza kunyesha⛈️, wakayafunga madirisha na kuniacha nje. Tayari walikwisha kunitupia nguo zangu na vitu vichache muhimu, hawakutaka Mama yao niingie nyumbani kwangu.


       Nililia sana, Nililia machozi ya ndimu, Nililia na kumlilia adam Mume wangu aliyenijali na kunithamini inashangaza mara baada ya kifo chake watoto wananitia aibu. Oh! Masikini niliendelea kulia pale mlangoni.


       Watoto wamekataa kuniheshimu, watoto wamekataa kuwa watiifu yote sababu ya ujana, pesa, pombe na wanawake,wamenidharau Mama yao na kuniacha nje mvua ikiniadhibu. Loh! Kosa langu Nini mie?๐Ÿฅฒ Nilijiuliza lakini sikupata jawabu.



                        ๐ŸŒง️๐ŸŒง️๐ŸŒฉ️⛈️


Ile mvua kubwa uliendelea kunyesha, radi nzito ilipiga, niliogopa sana, niliogopa radi inaweza kuniua, watoto wangu hawakujali wala kunionea huruma. Nilifikiria labda niende kuomba msaada kwa majirani. Lakini nilihisi wazo hilo laweza kuwa ni usumbufu kwa majirani. Nikakimbilia kule shambani kwangu, kule shamba lishapigwa maokoto.


Nilijificha migombani, nikajizuia kwa kutumia majani ya migomba, baridi ilinitesa, mvua ilinitesa hadi pale ilipokata mbu nao waliona wamepata chakula, wakanifyonza damu yangu hakika ile ilikua siku nzito tena kwangu.


     Hasubui pambazuko ilinikuta nimepooza kwa kukesha shambani bila kupata lepe la usingizi, akili zilinitumaa kurudi nyumbani kwa watoto wangu nikaongee kiustaarabu na watoto wangu yamkini ni ujana ndio unaowasumbua, sio wale niliowazoea miaka yote ya furaha na huzuni. Basi mie huyo nikajibeba na kuelekea nyumbani kwangu nguo zangu zikiwa tipwa tipwa kwa kuliwa maji ya mvua.


     Nilipofika nyumbani kwangu 'eh!๐Ÿค”' nilijikuta nashangaa kumkuta Mzee kapusi๐Ÿ† akiwa katika hatua za mwisho za kufunga milango ya Nyumba yangu. Baada ya salamu nilimuuliza:


     "Kulikoni Mzee kapusi uifunge milango ya Nyumba yangu?" Mzee kapusi akanijibu kwa ufupi.


       "Haujui, au watoto wako hawajakushirikisha!?"⁉️


     "Sijui nini na wao kunishirikisha Nini?!"๐Ÿ˜•


     "Mama Nelso usijizime data na kujitoa ufahamu tafadhali. Watoto wako wameniuzia hii nyumba na tayari wameondoka kurudi Dar es saalam, Ina maana hawajakushirikisha."



    "What!?⁉️" Presha ya taratibu ilianza kupanda na kushuka, mwili wangu ulichoka nilikua kama mzigo mzito ulio karibu kudondoka. Lo! Nguvu ziliisha, nilidondoka chini puui! Kama gunia la mapumba.



     "Nilikuja kuzinduka nikiwa nimezingirwa na majirani kibao wakinipulizia pulizia kwa vitenge vyao wengine wakilia wakidhani tayari nimeaga Dunia. Kumbukumbu ziliponijia nilianza kulia kama mtoto nikiwalaani watoto wangu Fredo na Neliso kwa ubaya walonitendea Mama yao mzazi.


     Majirani wema walinichukua na kunihifadhi majumbani kwao, kisa changu kiliwahuzunisha sana, wao pia walishangaa wakashindwa kuamini kama kweli Fredo na Neliso wanaweza kunitendea ubaya ule mimi mama yao jamani, ilikua ngumu kumeza.


~~~~~~~~~~~~


    Wiki mbili kupita nilihitaji kurejea kazini Nyumbani kwa Mzee Bushiri, nikafunga Safari hadi Nyumbani kwa Mzee Bushiri, yaani Bosi wangu Mzee yule mpole hakuniuliza Wala kunifokea kwanini nimechelewa kurudi kazini? Niligundua Mzee Bushiri alikua na wasiwasi juu ya mwonekano wangu tangu niliporejea kwake nilikua ni mnyonge, ile furaha na uchangamfu niliiozoeleka kua nao sikua nao tena, lile tabasamu alilozoea kuniona nalo Kila siku likachukua nafasi ya huzuni. Mara nyingi niliinama na kuitazama chini machozi yaishe nibubujika.



       Siku tatu mbele nikiwa ndani ya Mjumba ๐Ÿก๐Ÿ˜️wa Mzee Bushiri baada ya kumaliza shuhuli za kila siku nilitoka na kwenda katikati ya bustani huko niliketi pekee yangu nikilia kwa uchungu na kuomboleza juu ya kifo cha mume wangu Adam, pamoja na huzuni waliyoniachia watoto wangu Fredo na Nelso. Kumbe wakati mie namwaga chozi Mzee Bushiri aliniona akanifata.


       "Maua Mtumishi wangu Kwanini unalia, nieleze sababu nini hadi ulie kila siku." Alinishika bega jambo ambalo sikulitarajia kama Kuna mtu anitazama ninalia pale Bustanini.


     Mazito yamenikuta mie Mzee wangu." Nilisitasita kueleza changamoto iliyonisibu lakini 'piga ua' Nilipiga moyo konde na kumueleza changamoto zangu.


      "Mazito gani embu nieleze naweza kukusaidia." Mzee Bushiri Baba aliye jaa wema na hekima hakunibagua zaidi ya kunionesha faraja na upendo.


     "Nilimpoteza Mume wangu ambaye alikua ni nguzo muhimu ya familia hata baada ya kumpotezea mume wangu watoto hawaoneshi kunijali au kunithamini, hawatambui kuwa damu ni nzito kuliko maji, wamesahau uchungu wa Mwana mzazi anaujua, wameuza mashamba aliyoyaacha mume wangu baya zaidi watoto wangu wamenifukuza Mama yao kama Umbwa๐Ÿ• koko." Machozi yalishindwa kunivumilia yakarejea tena kunidondoka.๐Ÿ˜ฟ


     "Dah! Kizuri mpe ng'ombe sio binadamu." Mzee Bushiri aliongea.


     "Nahitaji kukusaidia." Mzee Bushiri aliongea tena. Niliacha kulia,nikamtazama usoni nikiwa nimeivaa sura ya kuonewa huruma.๐Ÿฅน


     "Nitashukuru Baba yangu utakua umenifuta chozi la uchungu maana jasho la mnyonge haliendi tupu, chozi lilinibubujika upya.


     "Usilie kesho jiandae tutoke twende Lushoto pale pale ulipodhurumiwa haki zako, pale ulipotimuliwa na kufukuzwa kama Umbwa. Kila ulichpoteza kitarudi pale pale." Moyo wangu ilianza kuingiwa tumaini, furaha yangu ilianza kurudi kwa kasi. Tabasamu lililopotea lilianza kurudi kwa kasi. Nilihisi zile ni ndoto za akina Abunuwasi, lakini wapi! Kila neno alilonena Mzee Bushiri lilijaa ukweli. Akanikumbatia katikati ya faraja kuu.


                               ๐Ÿค—๐Ÿฅน๐Ÿค—

Siku iliyofuata tulifunga Safari ya kuelekea Lushoto Kijiji Cha Magamba tulifika pahali pale haki zangu zilipopokonywa kwa nguvu za watoto ๐Ÿค—๐Ÿค—wangu. Mzee kapusi aliitwa mbele ya tajiri wangu Bushiri ambaye alimshawishi Kapusi kuiuza upya ile nyumba aliyoinunua kwa watoto wangu Fredo na Neliso. Kapusi mbele ya pesa hakuwa mdogo alishawishika kuipokea offa ya shilingi million Therathini ukitegemea yeye aliinunua ile nyumba kwa kiasi cha shilingi millioni kumi na Tano.  Shamba langu alilolinunia shilingi million Tano Bushiri alimpa offa ya shilingi millioni kumi na Tano.


    Mali zangu zilirudi, furaha yangu iliongezeka Sasa nikawa mmiliki wa zile Mali ambazo Adam alitoa wosia watoto wetu wawe warithi. Pamoja na huruma zote alizonifanyia Mzee Bushiri Bado tu aliingia gharama za ukarabati wa nyumba aliyoninunulia upya. Shamba langu liliboreshwa na uzuri wa yale maboresho Bushiri alininunulia mashamba  mengine matatu na vifaa vipya vya kilimo. Furaha yangu ikarejea, shukrani nyingi na sadaka zenye furaha, Mola wangu alizipokea. Nikajiona mimi ni mwingi wa bahati.

๐Ÿค›๐Ÿ‘Š๐Ÿ‘Š๐Ÿ‘Š๐Ÿ‘Š


      Miaka mitano ilipita nikiwa ningali ndani ya nyumba ya Tajiri wangu mzee Bushiri, Mwarabu kutoka Omani,๐Ÿ‡ด๐Ÿ‡ฒ mzee aliyekula  chumvi nyingi, yaani mpole na mwenye huruma kwa watu, mtoa misaada na ufadhiri kwa wenye dhiki, shida na masumbuko. Alianza kuuugua homa za uzeeni na uchovu wa mwili aliugua sana hata macho yake yakawa mazito kufungua. Muda mwingi aliutumia kulala kitandani Mie Maua nikawa bize kumhudumia huduma zote muhimu  ili kuirejesha afya yake iliyoteteleka. lakini ya Mola mengi ya binadamu machache, Mola akamtwaa yule mzee, ๐Ÿฅน๐Ÿฅน Mzee akaaga Dunia na kuniachia machozi na kilio. Mzee alifariki juu ya mikono yangu, alifariki akiwa tayari amewatendea watu mengi mema na Bado tu alitamani kuendelea mema yake. Watu wengi walilia msibani kwake wakikumbuka mema na mazuri aliyowatendea, mtu mwenye roho ya huruma na kutenda mema pasina kungoja shukrani.


      Yakaanikwa matanga na matanga yakaanuliwa hapo ndipo nilijipapasa na kujua kwamba sina changu na pale nyumbani kwa marehemu Mzee Bushiri sio pangu nilitakiwa kuondoka haraka sana iwezekanavyo. Nikarejea nyumbani kwangu Lushoto Tanga.



   Harobaini kupita baada ya kifo cha Mzee Bushiri nilishangaa kuona magari yaapatayo kumi na tano yanaongoza na kusimama mbele ya nyumba yangu, nyumba alonijengea Mzee Bushiri. Kwanza niliogopa moyoni nilijua ni yale yale waliyonifanyia watoto wangu Fredo na Nelso kuuza nyumba yangu kinguvu pasina kinishirikisha lakini hapa hawawezi maana hati ya nyumba na shamba ina majina yangu.


  Yale malori yalikua yamejaa vitu mbali mbali vya nyumbani, kuanzia masofa, makabati , mafridge,vitanda na vyombo vya gharama. Yalipotua mlangoni kwangu akasimama mwanaume mmoja nadhifu, safi aliyevaa suti nyeusi na kiatu cheusi Cha kupendeza.



      "Bibi Maua huu ni wasia uliachwa na mzee Bushiri aliundika kabla ya kifo chake akikutaka uwe mmiliki wa mali zake zote, utajiri wake, mashamba yake, magari na makampuni."


     "Jesuu! Nilipigwa kelele na kunyanyua mikono juu kumshukuru Mola, majirani pia walishangilia kwa furaha,


       "Mzee Bushiri hakubahatika kuwa na ndugu au jamaa ndani ya Tanzania ndugu zake wote wapo, Oman na ni matajiri wa kutupwa kwahiyo mzee Bushiri aliona Hana mtu wa kumwachia Mali zake nyingi, utajiri na mapesa yaliyovundikwa Banki anakukabidhi wewe Bibi Maua" Nyie mimi ninashindwa kuieleza furaha yangu.



      "Lakini........" Mwanasheria aliyevalia suti safi na kiatu kinachompendeza aliongea.



      "Lakini Mzee Bushiri ameandika ndani ya wosia wake Mali na utajiri wako wote usithubutu hata siku Moja kuwaachia watoto wako, ndugu na jamaa zako. Iwapo Mola atakupenda na kukuchukua⚰️☠️ Mali zako zote zitwaendea watoto yatima. Wajane wagane watotot wa mitaani masikini na wahitaji." Mwanasheria alimaliza kuongea, nilipiga makofi  ๐Ÿ™๐Ÿ‘na kufurahia kwa Raha zangu zote. Nikaupokea ule Wosia na kuubariki. Basi yale maroli yakaanza kupangilia Mali zote ndani, nikawa Tajiri na Bilionea wa ghafra.

             ๐Ÿ’ฐ๐Ÿ’ด๐Ÿ’ฐ๐Ÿ’ด


Fredo na Nelso walikuja kupata fununu Mama yao amepata Bingo la utajiri, Bilionea wa ghafra. Wakafunga Safari kutoka Dar es salaam hadi Tanga kwa lengo la kumuomba mama yao msamaha. Basi walipofika waliukuta ule mjumba alioniachia Mzee Bushiri getini Kuna walinzi wengi pamoja na mijibwa Mikali  inayotisha na kuogopesha. Waliishia kuogopa pale nje wakamwita mlinzi na kumweleza shida yao, mlinzi alikuja kunipa taarifa na mie niliyeishi kama Malkia๐Ÿ‘ธ nikatoka nje nipate kusikiliza shida zao, niliwakuta wamepiga magoti chini nje ya ule majumba wangu.



       "Karibuni nyinyi ni wakina nani na mnashida gani ambayo naweza kuwasidia."Waliposikia maswali ninayoqauliza walijikuta wanapigwa na butwaam wakanishangaa.


    "Mama umetusahau, mimi ni Fredo na huyu ndugu yangu Neliso. Sisi ni watoto wako tumemaliza Chuo lakini tunatangatanga mitaani kuokota chupa tupu๐Ÿผ๐Ÿงด na makopo tuuze ili tupate pesa ya Dagaa chukuchuku  na ugali. Vijana wangu walionekana kuchoka na kuchakaa tongotongo machoni, nywele tipwatipwa zenye mba chawni viroboto na papasi . Nguo zao zilijaa kunguni, miili yao iliota  ukurutu, visigino vya miguu yao  virijaa funza, fangasi na magamba kama ya Kobe.



         "Siwafahamu nyie na Wala Sina watoto wanaoitwa Fredo na Neliso. "Nikijifanya kuwasahau ingawaje uchungu uliniingia na kuniumiza moyo wangu pale nilipowaona wanangu waliopotea Leo wamepatikana wakiwa wameoza.



       "Mama, Mama, Mama  sisi ni watoto wako Baba yetu Adam alituachia Nyumba na Shamba tuka........" Fredo hakumaliza sentensi yake walianza kulia na kuumwaga chozi.๐Ÿ˜ฟ๐Ÿ˜ญ


        "Ondokeni hapa kwangu siwajui nyinyi rudini kwenye ile nyumba na Shamba la Baba yenu Adam" Niliongea kwa ukali ulioficha maumivu na uchungu juu ya wale watoto wangu. Nilitoa amri kwa walinzi wangu wafanye haraka kuwafukuza wale ombaomba waliowai kuninyanyasa hapo zamani. Umbwa ๐Ÿ•๐Ÿ•wakali walifunguliwa wakawatisha wale ombaomba waokotao chupa, wale omba omba wakatoka nduki na kukimbia kama vichaa wendawazimu.


Nilikua na maumivu makali hata nikajifungia chumbani na kulia  sana, Bado nilikua ninawapenda watoto wangu ingawaje wosia wa mzee Bushiri ulinitaka nisithubutu kuwapa kitu chochote kile alichoniachia.



       Basi nikamwita mmoja wa walinzi wangu nikamwambia enenda ukawatafute wale vijana wangu wawili Fredo na Neliso, wanunulie nyumba ya kuishi yenye kila kitu ndani, waketi humo, wale wanywe, wapewe chakula chao na mavazi tena wahudumiwe huduma zote muhimu, nikamwambia wape pia Pesa za kuwasaidia maishani mwao la zaidi watafutiwe kazi wanayoipenda kuitenda yaani Udakta ๐Ÿฅผ๐Ÿฉบlakini wasithubutu kuja kugusa Mali aliyoniachia Mzee Bushiri mali hizi sio mali zao Bali mi Mali zangu pamoja na watoto yatima, wajane., wagane, masikini na wahitaji. Mlinzi wangu akaenda kuwatafuta naye akawapata.



๐Ÿ˜š๐Ÿ˜™๐Ÿ˜—๐Ÿ˜š

TCHAO

☺️๐Ÿ˜Š๐Ÿ˜Œ

Let love ๐Ÿ’ž lead.




 

I MISS YOU CHUGA



MISS YOU CHUGA



SEHEMU YA TATU

(ILALA DAR ES SAALAM)


PALE TULIPOISHIA

“ Sonia fanya juu chini mie nitoke hapa kituoni, Umbu wananing’ata balaa.” Obi aliongea.

 “Nikikutoa sitaki kusikia habari za huyo Rehema, mwambie nitaua mtu mie nina wivu wangu mwenyewe, sikubali kuibiwa kizembe.” Nilimuonya Obi, Nikasimama pale tulipoketi nikaelekea Kaunta niongee na Polisi yule demu mrembo haswa

 LEO TUSONGE HAPA

 “ Aunty ninaomba utusaidie ninahitaji kumtoa Obi hapa kituoni.”

 “Unataka nikusaidieje Aunty, ujue kuwa Obi mtu wako wa karibu amefanya kosa na hapa kwenye mafaili inaonekana amefunguliwa kesi za aina mbili, kesi ya kwanza ni kesi ya kuzurura usiku mitaani kama mwendawazimu, kesi ya pili ni kufanya uzembe, kuingia ndani ya nyumba ya mtu pasina ruhusa, akiwa amelewa, kuwatusi na kuwapiga majirani. Yote hayo ni makosa ya mtu wako wa karibu.” Yule Askari mrembo aliongea.

 “ Kwamaana hiyo basi Obi ni lazima apelekwe mahakamani akajibu shitaka la kwanini afanye kuvunja sheri.” Polisi aliongea mie nikamwombea chuga huruma.

 “ Aunty ‘please do us favour’ tusaidie bado ninamhitaji mtu wangu wa karibu,” Nilimsihi yule Askari mrembo.

 “ Haitawezekana kumtoa huyu ni mzembe.”

 “ Aunty nipo tayari kutoa pesa mingi ili Obi aachiwe huru,” Niliteta.

 “Good girl, una pesa mingi, sema una bei gani….. una shilingi laki tatu, ili tuifute hii kesi ya mtu wako wa karibu.” Yule  Askari Mrembo aliongea akiwa amepunguza sauti, ananong’ona ili Polisi wenziwe wasisikie maongezi yetu.

 “ Mmh! Aunty pesa mingi hizo, nipunguzie jamani!”

 “Fanya laki mbili na nusu,”

 “Punguza tena Aunty,”

 “Fanya laki mbili kamili,”

 “Oooh! Polisi punguza tena,”

 “Bull shit!  Pimbi nini wewe? Haya sema haraka una pesa mingi bei gani? Faster tuizike hii kesi kabla haijapelekwa mahakamani” Yule Polisi mwenye uchu wa pesa zangu aliongea.

 “Laki moja na nusu Aunty,”

 “Ok. Fanya presha presha, leta,leta,leta,leta ili nilifute jarida la kesi ya mtu wako wa karibu.” Nilijikuta ninatoa burungutu la pesa haraka hara bila kuzihesabu nikampatia yule Aunty na yule Aunty haraka haraka akazipokea. Akaangaza macho yake kulia na kushoto kuona kama kuna mtu  amemwona akipokea ile RUSHWA aliyoniomba, alipoona hakuna aliyemuona akazificha zile pesa kwenye SINDIRIA yake matitini. Dakika tano baadae akaniita.

 “ Sasa mnaweza kuondoka nimelifuta faili la kesi ya Obi lakini …….. Sikiliza Obi, unapaswa kuishi vizuri na watu, unapaswa kutii kanunini na taratibu za sheria, Pombe itakuponza, utaletwa tena hapa ili ujute kwanini ulizaliwa Tanzania.” Askari aliongea kwa hasira, amemnyoshea Obi mkono wa taadhari

 Tukaruhusiwa kuondokapale PANGANI kituo cha Polisi mie nikakodi Bajaji iliyotupeleka moja kwa moja hadi BUGURUNI KWA MADENGE, sehemu anayoishi mchepuko wangu Obi, amepanga GETTO mie kazi yangu ni kumlipia kodi ya hilo getto, kumnunulia Luku, kumlipia billi za maji nakadhalika. Yaania Obi Mchepuko wangu anaishi kama Malaika, ananitegemea mie na mie namchotea pesa mingi kutoka kwa Dume langu, dume kibamia Jerome.

 Jamani mie namfanyia vyote hivyo huyu Mchepuko wangu Obi, lakini masikini! Ananisaliti, ananitoroka na kwenda kwa KIDOSHO yule aitwaye REHEMA  roho inaniuma lakini sinaga jinsi Obi anakituliza kitumbua changu, Obi ananigusa na kunitekenya pale ninapostahiri kutekenywa, ai! Napata raha za dunia asikwambie mtu, mwanamke lazima akunwe akakunika, mwanamke lazima aridhishwe akaridhika, mwanamke lazima apelekwe pale anapostahiri kupelekwa, yaani tupande wote mlima na kushuka tushuke wote, ngoma dro, hapa kaaaazi!

                ########

 Basi tulipofika Buguruni kwakwa Madenge Magettoni anakoishi Obi Mchepuko wangu, huku ndiko ninakoliaga utamu, sitaki kulia utamu kule nyumbani kwa Jerome maana majirani kwa midomo hawajambo, nakwambieni wanavyo chongaa balaaa. Tukaingia ndani, nikayapasha maji moto kwenye jiko la gesi, jiko nililomnunulia Obi Mchepuko wangu. maji yalipochemka nikaanza kumkanda kanda Obi sehemu mbali mbali zaa mwili wake aliopigwa kama paka mwizi .

  “Aaash! Obi mchepuko wangu alipiga kelele yale maji ya moto pamoja na Spirt yalimuumiza

 “ Unalia nini? SI KITUMBUA CHANGU UMEKICHOKA EEH! Na sasa umeona bora ukaile Sambusa ya Rehema,” Nilimkebehi nikimkanda kanda usoni kwa maji ya moto na ile Spirt, Mchepuko wangu amepigwa balaa, amevimba balaa, amevimba kama kando la maandazi lililotiwa amira.

  “Bebi usiseme hivyo, ujue unaniumiza roho yangu, mie nakuambiaje pombe sio chai, nilipitiwa my.” Obi alijitetea

 “Umeniudhi Obi ujue, ukirudia tena mie namtafuta Mwanaume mwingine, siwezi kuteseka kwa sababu ya Rehema,” Niliendelea kumkanda kanda, hakunijibu kitu. Dakika tano mbeleni nilikwisha maliza kumkanda Obi Mchepuko wangu.

 “Sasa bebi kama vipi naomba unitoe leo buku hamsini nitoke na msosi.” Obi alianza kunisumbua sumbua, akitaka pesa, wakati yeye Binafsi aliona jinsi gani nimefirisika kwa kumpatia Rushwa yule Askari Polisi.

 “Toka huko, Dume surualia, hauna akili weye, umenigeuza Buzi kichuna eeh!? Kila siku nikupe Pesa kama mimi ni Benki ATM.” Leo nilimpa makavu yake

 “Bebi wanijibu hivyo, Poa, kama wanijibu nyodo penzi sikupi.” Mwe eeh! Eeh!๐Ÿ˜‚ Kweli Obi Mchepuko wangu ni Mhuni ajabu anatoa penzi kwa pesa, bila kumpa pesa Penzi silipati ng’o.


 “Haya shika hii shilling elfu Therathini nenda Hoteli ukale, sitaki usumbufu, wanifirisi mie mwanamke.” Nilinywea,  nikaogopa kulikosa penzi, nikaingiza mkono wangu  kwenye mkoba niliotoka nao nyumbani Sharifu Shamba, nikatoa  nyekundu nyekundu tatu nikampatia Mchepuko


` “ Waoooo! Mwaaaa! ๐Ÿ˜ฝ๐Ÿ˜˜Mwaa! Pesa ni elfu kumi, Ilove you so muchi bebi,” Obi alinikumbatia akanipiga Kiss akinipapasa papasa  ishara ya kwamba anataka kunipa Penzi, Mmmh ananipa hamu, ananipandishia hisia za kulala nayeye, Basi anazidi kuitembeza mikono yake kiunoni kwangu, juu ya matiti yangu, kwenye mapaja yangu meupee peee kama chungwa lililoiva, Aaash! Ananipa hamu ya kutaka kunilala.

 Basi Obi anazidi kuitembeza mikono yake kiunoni kwangu na mapajani kwangu, mmh! Aaaai!  Oooosh! Obi analiingiza dole lake, lile dole refu la kati kwenye kitumbua changu anakitekenya tekenya na kukikuna kitumbua, aaaash! Ai mh! Kitumbua changu kimejaa maji balaaaa!

 Aaaaash! Ooohsh! Nilianza kuweweseka pale juu ya kitanda kikubwa nilichomnunulia Obi, Obi aliendelea kunipapasa papasa, anaivua ile Blauzi yangu nyembamba laini inayoyonesha matiti yangu manene ya kutamanisha, nyembamba laini iliyokichonga kiuno changu, kiuno nambari nane,  aash! Pumzi zilinitoka, presha presha, uuuh! Jamani ananinyonya chuchu zangu, aaaash! Ananinyonya kwa muda mrefu, mie napagawa miguno ya kimahaba haikakuki kunitoka, nazidiwa jamani, presha ya kupumua imenipanda, hamu ya penzi imenivamia, macho yangu makubwa ya kungu yakaanza kuniregea regea sababu Obi kanigea ulimi na ulimi huo ananisafisha safisha kule chini ya uvungu wa mapaja yangu, kule kitumbua kinawasha. Aaash mie napagawa zaidi sababu kanivamia kwa ghafla kaanza kunipa ulimi mdomoni wawili tunabadilishana mate kama vile njiwa wapendanao. Uuuh! Aaaash! Uauuauuu! Traaaaamu, ulimi wa Obi mchepuko wangu ulivyo mtamu bado angali anakikuna kuna kitumbua changu kwa kile kidole chake kirefu cha katikati ya vidole vyote vya mkononi.

  Na mie sikuwa nyuma nilikuwa bize naichezea chezea ile Dudukwe๐Ÿ† yake ndefu nyembamba, ipo kama mkono wa mtoto mchanga, hamu ya kulamba Dudukwe ikanivamia, bila kuchelewa nikaiparamia. Nikaitia mdomoni nikaitembeza kwenye ulimi Obi tayari Keisha nivua nguo zake zote na sasa anazichezea chezea shangaa na mikufu ya dhahabu niliyovaa kwenye UNO, anazidisha mipapaso, ananipagaza balaa.

Ooh! Asikwambie mtu Dudukwe ya Obi ilivyo tamu inamwaga mwaga ute mweupee kuashiria kuwa Mzee baba anahamu kinoma, ana hamu ya kucheza YOPE na akimaliza kucheza YOPE ya kwanza lazima tufanye Remix MBILI, TATU. Obi anahamu ya kucheza SEBENE, ana hamu ya kupiga NGOMA ya zilipendwa wake mie nikaendelea kulamba Dudu ‘nywa nywa nywa nywa’. Mara ghafla tukasikia sauti ya mlango wa getto ukigongwa.

 ‘Ngo ngo ngo ngo,’ ๐Ÿ‘Š“Hodi” sauti nzito ya kiume ilitutibulia starehe yetu.

 ‘Ngo ngo ngo ngo’ “Hodi,” Ile sauti iliita tena. Mie moyoni niliichukia kwanini niharibiwe starehe yangu.๐Ÿ˜ก

 “Nani tena huyo Bebi anayetutibulia starehe za Dunia?” Nilimuuliza Obi, amabye Safari hii aliachana na mie, akatoka pale kitandani, akavaaa boksa yake akaulaza ule mdude wake juu kuelekea kitovuni, maana kwa hamu zile bado Mchepuko alikua ananihitaji sana tuicheze ngoma hadi ipasuke.

 “ Ni huyu Msenge CHUGA, sijui kafata nini?” Obi alielekea mlangoni kuufungua, mie wakati huo tayari nimejifunika Kanga Moko kiunoni, Kuziba matiti na mzigo wangu huko nyuma mgongoni, maana kwa mzigo nilionao mwenzenu sijambo, nina mzigo balaa, mzigo kama ule wa NICOLE JOLLY BEBE, Mwanamitindo, Shosti ake’ WEMA SEPETU.

 “CHUGA?” Nilijihoji moyoni, jina geni sana masikioni kwangu. Nimetulia juu kitanda cha Banko, kitanda kinacho nesa nesa na kupiga kelele za ‘Twa, twa , twa, twa’ kelele za mahaba. Hamu ya kumuona huyo Chuga ilinivamia. Obi akaufungua mlango

 “Oya mshikaji vipi?” Obi alimpa ‘hai’ Chuga

 “Baridi mwanangu. Uko biee? Chuga ambae bado sijamuona, alimjibu Obi salamu yake, sauti ya Chuga ilinipendeza

 “ Mkaribishe mgeni ndani, Obi kwanini mgeni akae nje,” Ghafla niliropoka.

ITAENDELEA


BEKA

 SURAYA TATU                        “AKIPITA ATAJIPITISHA.” Beka akawa member wa kampuni ya SIGA, akipelekwa hapa na pale kulinda mali za ma...