Friday, April 25, 2025

WATABAKI NA LABDA

 




MIPASHO YA MAMSAPU

WATABAKI NA LABDA


Sehemu ya nne


Bwaga moyo wako chini, ubwage huo moyo wa tamaa, bibi litafute ‘solution’  juu ya tatizo la mumeo. Kwanini USIMRUDIE MUNGU? Mwaya, MUNGU NI PENDO, APENDA WOTE. Wenye madhambi na waso na madhambi mbele ya mungu wote ni waja wake, Vijori wake na kondoo wa malisho yake. Basi bibie yasije yakakufika shingoni mwenzetu ukazama. Jijue kuwa bado unayo nafasi ya kumuokoa mumeo. Anza sasa, anza leo, wakati ni mida na mida ndio sasa.”

 

 Ngoja nikupe mfano mmoja Sophia wangu. Ni hivi bibie, huko ZAMBIA kuna mwanamama alijaa wivu na gere, maneno ya majirani, wambea na washambea yalimpatia Stress isiyokwisha. Mara wamtonye, ooh, mumeo hajatulia, ooh, mumeo yupo na huyu yupo na yule, ooh, mumeo…..oh, mumeo……. Ndo ikawa hivyo Mzambia huyu alibaki na Labda, akijisemea moyoni mwake, Labda kweli jamoni, lisemwalo lipo kama halipo langojewa. Pasina kufanya uchunguzi wa dhati bibie Mzambia akapata wazo, wazo lililomsukuma afunge Safari kwenda kwa waganga wa kienyeji, ati, Kusaka dawa ya kumtuliza mumewe,  ‘Teeh teeh teeh,’ Bibie Mzambia alibaki na labda, ai! Jamani, ati tangu lini mume atulizwe kwa dawa za Kienyeji?

            Jamani mapenzi hayatafutiwi dawa kwa waganga wa kienyeji, mapenzi ni maelewano, mapatano na makubaliano, maagano na masikilizano, dawa ya mapenzi ni kutenda kile ulichonena, kwenda kwa waganga wa Jadi ni kuyavuruga mambo na kujiongeza matatizo nyumbani.

            Eh, ikawaje? Kama wahenga walivyosema mwanzo wa hadithi kuna mwisho wa hadithi. Hadithi yaweza kufurahisha au kuchukiza kuonya au kukosoa, yalomkuta Mzambia Mwaya enenda kawaulize Wazambia, kamwe wasisite kukudodosa mawili matatu waliyoyaona huko. LIMBWATA , jina baya kama shetani, alipewa akarikoroga kwenye mlo wamlo wa mumewe, mtoto akafanya kama alivyo ambiwa, sasa kumbe alisahau ule msemo wa watasha “TOO MUCH IS HARMFUL” Ikizidi inaua, ikizidi ni hatari hatarishi.

            Mzambia akazidisha madawa, ati apendwe sana na mumewe, Shoga yaliyomkuta ni aibu na fedhea, Ghafla bin vuuu mara baada ya mumewe kubugia matonge mawili ya NGUNA,  papo hapo akajikunja kunja akabadirika na kuwa Nyoka, lolioooh!  Mbona nyoka sio nyoka bali ni Chatu jeusi tii kama chungu. Lile Joka likamwandama Mzambia Popote pale aendapo wacha na lenyewe liende, Jamani aibu woga na fedhea, kila dawa aliyoitumia ili kumrudisha mumewe katika hali yake ya ubinadamu haikuzaa matunda na ajue fika kuwa ALIYEMSAIDIA KUMROGA MUMEWE TAYARI AMEKWISHA KUFA, sijui kama atafufuka.

            Maji yakamwagika, ndugu, jamaa na marafiki wakapigilia msumari ili kieleweke, liwalo na liwe tunamtaka ndugu yetu, tena umrudishe katika hali ya ubinadamu. Ikawa hivyo tena, MASENGENYO na MANENO VUNDO MNUKO yakapamba moto, tena yakafika mbali na kudondokea kwenye Vyombo vya Habari, Mwanamke akachafuka sana hata ashindwe kujua ni dawa gani aitumie ili kumrudisha mumewe katika hali yake ya ubinadamu. Ndo’ ikawa hivyo tena SOPHIA shogangu wivu mwingine uwe ni wivu wa kutafakari, waganga wengine Noma. Angalieni jamani waliomsaidia Sophia  kumroga Mumewe tayari wesha kufa, Oooh! Sijui ataipata wapi dawa ya kumrudisha mumewe kutoka kwenye ujoka kwenda kwenye  ubinadamu

            ‘Teeh teeh teeh,’ Mzambia alibaki na labda, aibu na fedhea, ndo maana kusema  maneno mengine yanafirisi, maneno mengine hasara.

Safari yangu mie Mamsapu mlo wa mumewe, mtoto akafanya kama alivyo ambiwa, sasa kumbe alisahau ule msemo wa watasha “TOO MUCH IS HARMFUL” Ikizidi inaua, ikizidi ni hatari hatarishi.

            Mzambia akazidisha madawa, ati apendwe sana na mumewe, Shoga yaliyomkuta ni aibu na fedhea, Ghafla bin vuuu mara baada ya mumewe kubugia matonge mawili ya NGUNA,  papo hapo akajikunja kunja akabadirika na kuwa Nyoka, lolioooh!  Mbona nyoka sio nyoka bali ni Chatu jeusi tii kama chungu. Lile Joka likamwandama Mzambia Popote pale aendapo wacha na lenyewe liende, Jamani aibu woga na fedhea, kila dawa aliyoitumia ili kumrudisha mumewe katika hali yake ya ubinadamu haikuzaa matunda na ajue fika kuwa ALIYEMSAIDIA KUMROGA MUMEWE TAYARI AMEKWISHA KUFA, sijui kama atafufuka.

            Maji yakamwagika, ndugu, jamaa na marafiki wakapigilia msumari ili kieleweke, liwalo na liwe tunamtaka ndugu yetu, tena umrudishe katika hali ya ubinadamu. Ikawa hivyo tena, MASENGENYO na MANENO VUNDO MNUKO yakapamba moto, tena yakafika mbali na kudondokea kwenye Vyombo vya Habari, Mwanamke akachafuka sana hata ashindwe kujua ni dawa gani aitumie ili kumrudisha mumewe katika hali yake ya ubinadamu. Ndo’ ikawa hivyo tena SOPHIA shogangu wivu mwingine uwe ni wivu wa kutafakari, waganga wengine Noma. Angalieni jamani waliomsaidia Sophia  kumroga Mumewe tayari wesha kufa, Oooh! Sijui ataipata wapi dawa ya kumrudisha mumewe kutoka kwenye ujoka kwenda kwenye  ubinadamu

            ‘Teeh teeh teeh,’ Mzambia alibaki na labda, aibu na fedhea, ndo maana kusema  maneno mengine yanafirisi, maneno mengine hasara.

Safari yangu mie Mamsapu


na roho wangu Pompo ingali bado ndefu, ndefu ya kula chumvi nyingi, kama ni sukari, tayari tushalamba kama ni asali tushalamba sana, sasa nyie akina Mariamu pamoja na Sophia mwatutakia nini sie? Au ndo hivyo tena mnahitaji kubaki na labda, LABDA ETI: pompo atanitupa na kuniacha aje kujipendekeza kwenu nyie viroboto ‘teeeh teeh teeh ‘ kamwe Pompo hawezi kunitema kaniweka moyoni anashindwa kunitapika, kaniijua na mie n’shamjua , kanivaa na mie n’shamvaa, mapenzi maelewano, yenu nyie macho.


            Hana Siri Pompo yeye ni mtu mzima, mzima wa 40 hivi na mie ni mwanamke wa 32 hivi tunayala maisha yenye tunu, tunu za raha na mustarehe, mahaba na mahabati, tushavumilia mengi lakini haya tena ya kuibiana waume zetu hapana jamani hayavumiliki, lazima niseme ukweli toka moyoni na ukweli huo unauma na kuchoma mtima


            Nishasema Pompo hanaga Siri kwangu lazima aseme aseme yalo moyoni mwake ili hao waso na makabati wajichange wakanunue makabati tena makabati yenyewe yawe ni makabati yenye vitasa na funguo nzito zisofunguka. Mbona Mariamu alipojipendekeza kwa mume wangu Pompo , POMPO ALINIMWAGIA MTAMA na mie nikaelewa, ndo hivyo tena Sophia naye kaingia kwenye anga za wenyewe amekuja na gia ya kudai ati Mumewe kibamia chake Kimelegea mlaini kama mrenda, hakiwaki bali kimezima kama mshumaa uliokwisha mafuta yake na suluhisho la yeye kuupooza mtima wake ni kwenda kwenye hayo MADANGURO yaso mbele yaso nyuma


            Bibie hana haya huyu kutwa kuchwa kigulu na njia KUDANGA na KURUKA UKUTA wakati huo huo Issa mumewe yupo, yule mume wa ukweli, dume la zamani halina mbele halina nyuma ni mfano wagari lililokwisha isha mafuta. Teeh teeh teeh sijui Shoga zangu sijui kama hilo gari litakwenda Salama


             Jamoni, mie naumia, ninamwonea huruma Issa angali baddo ni kijana mdogo, kijana wa 30 hivi, ana umbo la kimazoezi ‘Body bulder’ ana sura nzuri ya kutamanisha, amekamilika kila idara, ndo hivyo tena Sophia kaharibu mambo hata asijue nini cha kufanya Ilihali mganga aliyemkorogea mumewe tayari Keisha fariki, kafariki na zile dawa za kumfungua Issa mume wa SOPHIA, kutoka kwenye ULIMBWATA kwenda kwenye UTIMAMAU wake


            Sophia, naanza kumchukia bibi huyu, namchukia kama nini? Ndo’ maana sipiki chungu kimoja na yeye, yeye mwenye roho ya kutu, Si alijifanya yeye ndo nambari one katika kujishaua na kujipendekeza kutongoza waume za watu, basi akafanya KUMTOKEA mume wangu , roho wangu Pompo.

No comments:

Post a Comment

I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...