Saturday, September 21, 2024

KIGUU NA NJIA sehemu ya tatu


 #ANNA: (Wakiwa darasani Siku liyofuata). Eeh! Shoga yangu wacha we! Unasema kuwa ulilala kitanda kimoja na yule handsome aitwaye Ben?

AMINA: Sikufichi shoga yangu, nakwambia ilinibidi nimlazimishe ku do naye, yaani kijana alionekana mgeni haswa, mara nimshike hapa, utakuta anatetemeka, mara nimpapapse pale, angelitoa mikono yangu, lakini yote tisa kumi nilimuweka pale alipopaswa kuwekwa.ANNA: Teh! Teh! Teh! Teh! Yaani shoga yangu kuku mgeni hakosi kamba, huyo keishaingia kiulaini laini, na kwa jinsi nijuavyo mie atakulilia huyo, hakuachi ng’o, atakuwaza iwe usiku iwe mchana, hawezi kula kulala, wala kusoma juu yako.

AMINA: ( Anakomboa mafuta ya ku
jipaka midomoni mwake kunako kopo dogo alilobeba kisha anajipaka paka midomo yake). Swala keishaingia mitegoni.

SUZZANA: (Alikuwa bize anajisomea somea vitabu). Lakini rafiki yangu, ukumbuke kuwa mshika mawili moja humponyoka, mdharau mwiba mguu huota tende, mapenzi na shule wapi na wapi? Yakupasa ushikilie elimu kwanza, mapenzi yapo, nawe utayapata ukiisha kuolewa, mara baada yaw ewe kumaliza chuo kikuu na kupata kazi laazizi.

ANNA: Huyu naye asitutibulie maongezi yetu, kila siku yeye anajifanya ni mshauri nasaha, kila siku yeye anajifanya ni Bingwa wa kutoa hoja kuhusu elimu, kama unaona mawazo yetu ni finyu basi ushauri wetu ni wewe kuwa mwalimu tu itatosha iwapo utakuwa mwelimishaji wa jamii.

AMINA:  Tena wengine tumeshachoka na hiyo elimu ambayo yeye anaitilia mkazo, wala hatuoni faida yoyote ile zaidi ya  kupoteza muda wetu wa kufundwa mada zile Zile za kurudiwa rudiwa. (Anajibu kwa kebehi).

ANNA: Umesikia wewe Kimburukutu!

SUZANNA: (kimya). Anaendelea kujisomea.

AMINA: Yaonekana huyu Bibiye bado ni kifaranga, hajapata kumjua mtu mume ndio maana, yupo Zubezube, haoni mbele wala nyuma, kutwa kucha anakazania elimu, elimu, elimu…Elimu ndio nini?

ANNA: Tena kwa taarifa yako kuna msemo mmoja wa Wazungu unaosema. ‘Money is everything, education is nothing…. Money is better than education” Sijui hupo hapo?

AMINA: Yupo hapo na tena yeshamshuka, anajishaua shaua bure. (Mara ile Mwalimu Grace anaingia, darasa linasimama kumsabahi, naye anawaitikia kama kawaida yake.)

MWALIMU GRACE: (Anafundisha). Leo tutaimalizia ile mada ya ugonjwa wa kipindu pindu. (Mara kwa ghafla Amina alijisikia Kichefu chefu, anatoka mbio mbio kuelekea nje kutapika).Eeeh! (Mwalimu Anashangaa). Nyie wanafunzi mbonqa ni wa ajabu sana, yaani nimewafundisha  msiende kula vyakula vichafu, tayari mmekwisha bugia. (Analalamika). Niliwakataza kunywa maji yasiyochemshwa, niliwakataza kula matunda yasiyooshwa, niliwaambia ni marufuku kunywa maji ya mitoni. Mwe! Lakini bado tu hamnisikii. (Anamwendea Amina pale alipoinama kutapika). We Amina, vipi una tatizo gani?

AMINA: Najisikia kichefu chefu madam, nahisi ndio hizo dalili za Kipindu pindu, maana tangu kizuke hapa jijini Dar es Salaam, kila mtu ana hofui na kuogopa.

MWALIMU GRACE: Oooh! (Anapumua kwa kasi kidogo). Pole sana mwanafunzi wangu, kama unajisikia vibaya waweza kwenda kulala pale kwenye bustani ya shule. Mwalimu Grace alimpatia ruhusa ya kwenda kupumzika). (Amina Alikwenda kupumzika angali ana wingi wa hofu na wasi wasi juu ya afya yake, kwasababu huu ni mwezi wa pili sasa, amekuwa akitapika tapika ovyo, mate yanamjaaa Mdomoni mwake, kuchooka kusiko kwa kawaida, mara angelitamani kula udongo, mambo kede kede yanamchanganya.

****************

Uvumilivu ulimshinda Amina, akajikuta anaelekea hospitalini kumwona Daktari, akiwa yeye na mama yake walifika hospitalini salama, walimweleza Daktari shida iliyowapeleka, naye Daktari alichukua vipimo vya damu yake Amina, mara baada ya vipimo, majibu yalitolewa.

DAKTARI: Umesema upo kidato cha ngapi vile? (Dakta aliuliza).

AMINA: Nipo kidato cha tatu Dakta.

DAKTARI: Na huyu ni mama yako mzazi au mwalimu wako.

AMINA: Mmmh! Daktari nawe una maswali mengi kama Polisi, huyu ni mama yangu mzazi.

DAKTARI: Ok, kuuliza sio ujinga bali ni kutaka kujua. Ni hivi binti, vipimo vinaonesha kuwa wewe ni m…aaah!, wewe ni mjamzito, na tena huu ujauzito wako ni wenye miezi miwili hivi. (Dakta aliongea).

MAMA AMINA: Yallah! Toba! (Alipigwa na mshangao).

AMINA: Mimi nina mimba Daktari? (Bado amebaki anashangaa, kinywa wazi, haamini yale yasemwayo na Dakta).

DAKTARI: Ndio mdogo wangu, wewe ni mjamzito, tena ujauzito wako ni wa miezi miwili, mimi binafsi nashangaa kwanini unajihusisha na suala la mapenzi katika umri huu mdogo ulionao!

MAMAYE AMINA: Au umekosea kupima bwana Daktari, mwanangu yungali bado mwanafunzi, atawezaje kushika mimba akiwa shuleni?

DAKTARI: Suala la yeye kushika mimba akiwa shuleni sio tatizo, tatizo ni yeye kujihusisha na suala la mapenzi akiwa shuleni.

AMINA: (Akilia machozi). Jamani Daktari, nitafanya nini mimi, bado shule naipenda, ninataka kusoma, elimu ndio ufunguo na ukombozi wangu.

DAKTARI: Sina chas kukushauri mdogo wangu, cha muhimu ni wewe kwenda kuongea na walimu wako, labda watakushauri vema na pia watajua jinsi ya kukusaidia.

AMINA NA MAMAYE: Machozi yaliwafunika, wakalia kama vile wamepatwa na msiba.

************

Amina pamoja na mamaye walikwenda Shuleni kwao Amina ili wapate kuomba ushauri wa mwalimu kuhusu tatizo la Amina. Walipokelewa vizuri, mwalimu Grace aliwasikiliza kwa upole zaidi.

MWALIMU GRACE:Ulikuwani mtoto mwenye tamaa kiasi hicho, daima nilikuona ukiwa mtiifu na mwenye uvumilivu darasani, ajabu leo umeshika ujauzito, hembu nieleze huo ujauzito ni nani aliyekupatia. (Amina kimya kwa aibu.) Nakuuliza tena Amina, unieleze huo Ujauzito  ulionao ni nani aliyekupatia ili nayeye achukuliwe sheria na hatua kali kwa  uharibifu huu uliofanyika.

AMINA: (Kimya).

 MAMAYE AMINA: Usijitie ububu shuleni, umesikia mwana we! Mpatie jibu mwalimu wako naye ataweza kutoa ushauri wake.

AMINA: (Anajibu kwa hofu.)Yawezekana ni Ben.

MWALIMUI GRACE: Ben yupi tena huyo.

AMINA: Yupo kidato cha nne B.

MWALIMU GRACE: Ok, vema, suala hili sio la kitoto, mimi kama  Mwalimu wa nidhamu nitalichukua hili suala na kulipeleka kwa mkuu wa shule, yeye ndiye mwenye uamuzi wa mwisho, nadhani atajua nini atakachoamua na kukushauri. (Mwalimu Grace alimruhusu Amina aende darasani, mamaye Amina alirudi nyumbani kwake, Mwalimu Grace tayari alikwenda Ofisini kwa mkuu wa shule ili kutoa taarifa juu ya lile jambo.)

******************

Amina akiwa darasani ameketi pamoja na shogaze wawili Anna na Suzanna, ilimbidi awatobolee ile siri ya yeye kuwa mjamzito).

ANNA: Eeeh! Mwaya, unasema kweli?

AMINA: Yamenikuta mwenzenu.

SUZANNA: Yaani kutaopika kote kule, kichefu chefu cha mara kwa mara, kulala lala ovyo darasani, Kupenda maji na udongo, nani asijue kuwa tayari mwenzetu umekwisha nasa? nilikwambia mimi cheza na elimu, uisicheze na pesa ama mapenzi, hivyo ni vitu hatari katika masomo.

ANNA: Eh! Eh! Bibiye, huu sio muda wa kumlaumu shosti wetu, huu ni wakati wa kumfariji, maana tatizo alilonalo sio dogo ni zito kama Mlima. 

SUZANNA: TEH! Teh! Teh! Teh! (Anacheka kwa dharau) nicheke mie, ni bora angelifeli mitihani, mie ningelikuwa mstari wa mbele kumfariji, kumtia moyo na kumtakia ajibidishe zaidi, lakini kwa hilo suala la ujauzito nasema siliwezi, nitajifariji kwenye elimu, elimu ndio msingi wa maisha yangu, mbona wahenga walisema kama unaona elimu ni gharama basi jaribu ujinga ili uione hasara yake.

ANNA: Kwenda zako huko, unajiona wewe ndiye  mwenye akili sana ndani ya darasa hili,  kumbe bichwa zero, huna huruma msichana wewe, lakini ukae ukijua matatizo ni sehemu ya maisha ya kila siku, hatuyakaribishi matatizo bali matatizo ndio yanatuvamia.

SUZANNA: Aaah! (Anacheka kidogo). Ati hatuyakaribishi matatizo bali  yenyewe ndio yanatuvamia. Napingana na wazo lako kwa sababu asiyesikia la mkuu huvunjika guu, asiyefundwa na mamaye hufundwa na ulimwengu. Amina amelilia wembe ameshapewa, tangu mwanzo nilitoa ushauri wangu tujihadhari kabla ya kuzuka kiwa hatari lakini sikio la kufa kamwe halisikii dawa. Ndio hivyo sasa, leo mmenikumbusha usemi mmoja wa Wahenga waliposema Masikio hayazidi kichwa. (Suzanna aliongea kwa kirefu).

ANNA: Nitakuponda vibaya wewe binti wa kilokole tena ni heri ungelihama pahali hapa tulipotulia, unazidi kutuharibia ishu na mishe zetu, mchawi mkubwa we! (Anna anataka kumpiga Suzanna, lakini  Amina aliyeketi katikati ya dawati alizuia yasitendeke).

SUZANNA: Usipoziba ufa utajenga ukuta, maji yakimwagika hayazoleki, mfa maji haachi kutapa tapa. Pokea huo ujumbe bibie Anna, zubaa uchekwe, hapa ndio mjini bibie. Ukijipendekeza kidogo tu tayari na wewe unaondoka na huo mzigo wa mwenzio, mie nakushauri acha kabisa hayo mambo ya kupenda penda wanaume watu wazima pamojqa na wanafunzi wenzio, watakuharibia maisha yako bure, utashindwa kutimiza ndoto na malengo uliyojipangia, itakuwa ni sawa sawa na kuupanda muda hatimaye ukavuna upepo, mbona walisema wenye hekima, cheka na Nyani uvune mabua. (Leo Suzanna aligeuka mhubiri)

AMINA: (Machozi yanamtoka). Yote ayasemayo Suzanna ni ukweli mtupu, Anna rafiki yangu, majuto ni mjukuu, kila mtu hujuta, tufuate ushauri alioutoa Suzanna, Suzanna ni rafiki bora aliyefaa kuigwa katika jamii, amefundwa akafundika, anaelewa nini kinachoendelea, anajua pia matokeo ya kile kinachoendelea. (Analia).-Looh! Tamaa mbele mauti nyuma, sijuik hatima yangu itakuwaje, jamani kile kipindi cha raha na furaha sikuipenda elimu lakini wakati huu wa shida, tabu na misukosuko ndio roho yangu imeanza kuipenda Elimu, hembu tizameni daftari zangu zote, tangu naanza kidato cha kwanza hadi hiki cha tatu, sijapata kuandika neno na ukitegemea walimu wetu walivyo wazembe hawafuatilii, hawachunguzi, hawasahishi wala hawatoi tamko la ukusanyaji wa haya madaftari yetu wapate kukagua kagua mienendo yetu ya kimasomo. (Aliongea akilia zaidi na zaidi).

ANNA: (Anamfuta machozi Amina kwa kutumia kitambaa chake). Usilie sana Amina, acha yaliyopita si ndwele tuuyagange yajayo lakini si unamjuua alieyekugeia huo ujauzito?

AMINA: Mwaya, nipo njia panda, kutwa kuchwa kutembea na mijibaba mijitu mizima kama Zeee la PutaPuta. Kutwa kucha kutembea na wanafunzi wenzangu kama vile Ben, utadhani hapo nitamtaja nani aliyenisababishia huu ujauzito…Yaani nipo Njia panda.sina mbele, sina nyuma, sina ae wala bae). Mara wakasikia monitor wa darasa akimwita Amina aliyehitajika Ofinini kwa mkuu wa shule. Huko nako akakutana na macho yake Ben aliyekuwa akilia kwa uchungu ati asifukuzwe  shule kwa kosa la kumtia Mimba Amina. Mkuu wa shule alikuwa mkali kama Pili pili,. Hatimaye Amina alipewa barua ambayo aliambiwa aipeleke nyumbani kwa wazazi wake naye akafanya kama alivyoambiwa)

###

Itaendelea

JUTO sehemu ya pili


                                    JUTO

  Sehemu ya pili

             Basi nakwambieni mara baada ya Kungwi Uaridi kumaliza Semester  yake akalipwa ujira naye akaondoka akaenda zake, tayari keisha mfunda huyu Bibie Maisha ya Mjini, kamfunda mafundo yote, kamfunda uvumilivu, ustahilivu, unyenyekevu, utulivu, upendo, mahaba na vyote muhimu katika ndoa. Tayari Bibie kafundika hata Mumewe akafurahi na kujisifu kwa kuchukua hatua njema, uamuzi bora na wenye busara kumtafutia mkewe Mwalimu wa kumfunda mafundo ya Mwanamke.

Miezi miwili mitatu mara baada ya Kungwi Uaridi kuondoka pale nyumbani kwa Bwana Denis, nasema nyumbani kwa sababu Denis tayari kashajikamilisha, ana nyumba yenye kila kitu muhimu ndani, hakipungui kitu, ukitaka unga, mchele, mafuta, nazi, hoho, nyanya nakadhalika Bibie hukosi hapo, vyote hivyo huletwa na huyu Mume aliyezaliwa Pemba akalelewa Pemba na kuja kuishi Dar es salaam. Zamani, zama za utoto na utu uzima alikuwa akiitwa Ally Hassan, lakini mapenzi, mapenzi jamani yakamfanya huyu Mpemba abadili Dini kutoka kwenye U-Ally Hassan akaenda kwenye U-Denis.

Lily alijiona mpweke, mpweke aliyepungukiwa kitu kimoja muhimu maishani mwake, Mtu wa kuongea naye, mtu wa kucheka naye, mtu wa kubadilishana naye mawazo. Nyumba yao ni kubwa ina vyumba sita, Sebule (Sitting room) Jiko, Choo na Bafu ndani kwa ndani, pasina kusahau chumba cha stoo na chumba cha faragha (maongezi). Miezi mitatu aliyoitumia kufundwa na huyu binti (kungwi) aitwaye Uaridi tayari ilikwishafikia tamati, alimzoea sana Kungwi Uaridi ajabu leo hamwoni mtu wa kumzoea. Masikini, unyonge, upweke na mawazo yalimtibua Lily.

Kama nilivyokwambieni hapo awali, mumewe ni mtu wa ‘Mishe mishe’ (Mizunguko ya hapa na pale) hana muda wa kutulia nyumbani ili apate kuzungumza na Mkewe, hata siku za Jumamosi na Jumapili Mwanaume yupo bize kutafuta pesa. Kwa bahati nzuri pesa anazipata, Bosi anamlipa kitita chake, ndio maana amejenga nyumba yake mwenyewe, kilichobaki ni kuwekeza haba na haba ili anunue Coster yake mwenyewe aimiliki na kuizungusha ndani ya Jiji. Upweke! Upweke binti aliuona ni kama sumu, hajazoea upweke, alizoea kuketi Pahali na watoto wenziwe zama zile bado hajaolewa akicheza cheza rede, akiruka boi, akifukuzana na mabinti wenziwe. Wakicheza kombolela, wakienda kisimani kuchota maji au kufua nguo mtoni, tena wakikata kata kuni Mwituni wakiokota okota Mayai ya Ndege na matunda Mtini. Loh! Hajazoea upweke japo ndani ya nyumba yake kuna Televisheni, hata hiyo Televisheni anaona haimbadilishi fikra zake. Televisheni inazungumza na kujijibu yenyewe, yeye ana maswali kedekede ambayo Televisheni haiwezi kumjawabia. 

‘Aaagh’ alijichukia, yanini kukaa kibubu wakati Dunia sio ndogo, Dunia ina watu wengi ajabu. Basi Mwanamke akatoka ndani mchana wa siku moja Jumapili tulivu, siku hiyo Soko la Ilala hufurika watu wenye hitaji la mahitaji mbali mbali ya kimaisha, hajatoka ndani muda mrefu tangu Kungwi Uaridi aondoke hivyo leo ameona acha atoke kidogo akanyooshe nyooshe miguu na mikono yake , akaangaze angaze apate kinachoangaza.

        “Hi” Kashikwa bega lake la mashoto, ile anageuka tu uso kwa uso kakutana na mabinti watatu warembo haswa, warembo ajabu, wamejikoroga usoni wakakorogeka, kwa mapambo, kwa marashi, kwa manukato na kwa mavazi. Lily aliwatazama ashindwe kujifananisha nao, kwanza wao ni watoto wazuri wa Mjini, weupe wa mapodozi, wazuri wa maumbo. Tena maumbo yenyewe hawakosei wanatumia madawa ya kuyaongeza hayo maumbo. Embu tizama makalio yao yalivyo makubwa ya nesanesa, hembu tizama macho yao, macho kungu  na hayo matiti yao? Loh! Sitaki kusema kwamba yanafanana na mto wa kulalia. Ni makubwa balaa.

Lily Cheusi mangara, tena cheusi Chungu ni mrefu kama alivyo Mumewe Denis, nywele zake asilia hajapata kuzipaka dawa, azionapo hizo nywele za hao wadada wampao ‘hai’ mwenyewe anazitamani, japo tuseme mwenyewe hajui wala hajazoea kuvaa mawigi marefu kama mkia wa Farasi. “Hi.” Lily aliitikia ile salamu.“Naitwa Elizabeth.” Yule mkubwa kuliko wote mwenye kadirio la miaka Ishirini na mitano alijitambulisha. Ajabu hata hajaombwa afanye hivyo, papara tu ndio zamsumbua.  “Huyu ni Shoga yangu anaitwa Lisa na huyu mwenye kidoti puani ni Shoga yetu anaitwa Anjelina.” Elizabeth aliwatambulisha Shogaze wakati wote huo Lily alikuwa amesimama pembeni ya Barabara hao Dada watatu walikuwa wakimfuatilia pale walipomwona. Kumbe ni zube, zube la Jiji. Teh teh teh. (Nacheka mie) Hachoki kuangaza angaza huku na kule kama Tochi kizani, tembea yake yenyewe binti bado ana mguu wa Kijiji japo amefundwa kafundika, amefundwa na Kungwi Uaridi, Kungwi aliyevumilia yote.

“Asanteni sana kwa utambulisho wenu, mie ni Liliani watu wengi hupenda kuniita kwa kifupi Lily, nimeolewa ninaishi Buguruni Malapa.” Lily alijitambulisha kwa ufupi. “Oooh! Unakaa Malapa, wacha we! Hata sie twatoka huko Shosti.” Anjelina binti mwenye kidoti puani alionge amejaa tabasamu, meno yake mema yaonekana.

        “Sie tungependa uwe Shosti wetu, tumekupenda sana tumependa jinsi ulivyo mpole mwenye huruma tele machoni.” Anjelina aliomba urafiki.

“Hakuna tatizo nipo tayari nawakaribisha nyumbani, nimefurahi kujuana nanyi mmekuja kipindi kizuri kwangu.” Lily alichekelea, furaha ya kupata marafiki ni moja ya mambo anayoyapenda Maishani.

“Asante sana Shosti, tutakuja hata kesho, hembu chukua Nambari zetu za rununu  nawe utupe Nambari yako ili kurahisisha Mawasiliano.” Lisa aliyeketi kimya muda wote alitia neno.

“Hamna shida Shosti, hembu ngoja niwape,” Lily alitoa rununu yake aina ya NOKIA, akaandika andika hizo Nambari za Marafiki waliokuwa wakitumia hizo simu zinazoitwa SAMSUNG GALAX-6, IPAD na INlFIX. Mmh! Vitu vya bei gharama. Basi huo ndio ukawa mwanzo wa urafiki mwema kati ya hawa Mashosti wanne, Elizabeth, Lisa, Anjelina, na Lily, kutwa kuchwa hao wakina Elizabeth, Lisa na Anjelina, walikesha wakila na kunywa nyumbanmi kwake Lily, muda mzuri ambao Mumewe hayupo. Kutwa kuchwa wakipiga simulizi za hapa na pale, simulizi zimejaa umbea, zinachosha na kuumiza vichwa kuzisikiliza, kutwa kuchwa kumtoa Lily Out na kwenda kumtembeza sehemu mbali mbali za Jiji. Lily akainjoi kula Bata na raha. Pesa zipo, zile Pesa alizoachiwa na Mumewe yeye alizitumia na hao Mabesti wake. Akajisikia Mtoto Lily, akajisikia raha kuwa na Mabesti wanaompunguzia mawazo, upweke na unyonge. 

Kumbe! Kumbe binti hakujua kuwa wenzie wapo kazini, pale wanamchota akili, kilichofunikwa binti anaona kimefunuliwa na kilicho funuliwa anaona bora kifunikwe ni kama Mazingaombwe, yeye mwenyewe haelewi nia na malengo ya hawa Mashosti, Mabesti na Mashoga zake.

Hakushtuka wala hakushtukia kuwa hao wenziwe anaowaona kuwa ni wafariji wake kimawazo wamemtamani Mumewe Denis, maana Denis mwenyewe hatulii nyumbani ni kiguu na njia, yupo bize kusaka pesa, kutwa kuchwa yupo ndani ya Coster anasaka hella ya Bosi ili apate kidogo dogo ambacho ni haki kwake. 

Au labda hawa Mashosti walimuona Denisi hapo Malapa? Labda, maana Denis ni Dereva na Dereva lazima akutane na makumi ya watu kila siku iitwayo leo. Jamani hisi na hisia hazitoshi, tusilolijua litatusumbua, tusilolijua lipo kizani.

Itaendelea  



DONDA LA WIVU sehemu ya pili


 

 SURA YA PILI

TUNU.

                 Kwisha kupata mlo wa mchana, mzee Jamali akapata nguvu, afya na uzima, mkewe mdogo ni mjuzi wa kuyapika mahanjumanti, madiko diko, mapocho pocho manono manonozi, mlo ule ulimpatia sio nguvu pekee bali pia matumaini ya kuishi kwa raha na furaha , yote haya ni mapenzi apewayo na mkewe Tunu mke wa pili mara baada ya mke wake wa kwanza kuaga dunia.

                 Mzee Jamali alifanya uamuzi wa kuoa mke wa pili ili kujiondolea mawazo na uchovu, Tunu alimpendeza machoni, basi  mzee Jamali akamuweka ndani, akampamba, akamremba na kumkwatua, kabla ya kuwa hivi alivyo sasa mzuri  wa kunenepa binti alikua yu dhaifu, amekonda na kukondeana. Amekonda na kuchakaa kama gofu lililoachwa na Mkoloni. Haki! Huko nyumbani kwao Lukozi Tunu aliiishi maisha ya kifukara sana. Nikwambieni mpenzi msomaji kwa mara ya kwanza kama ungelipata nafasi ya kumuona, jamani! Usingeli mtamani, mmmh! Kukonda huko sio haba, maisha magumu Vijijini.

                 Kwa juhudi za mumewe, Mzee Jamali Tunu alianza kuboreka kimwili, afya yake iliyoporomoka kwa sasa ilianza kuimarika na kujengeka yote sababu Tunu hakupata kulala njaa hata siku moja ndani ya nyumba ya Mzee Jamali kila kitu alichokihitaji Tunu alikipata, hakuna  alichoomba Tunu akakikosa. Uzuri wa nyumba ya Mzee Jamali kuna bustani ya mboga mboga na matunda ambayo yamekuwa msaada  mkubwa katika kuiboresha afya ya Tunu.

                 Lukozi kijijini kwa babaye na mamaye shida ziliwatafuna, umasikini uliwameza, tabu ziliota mizizi, mahangaiko yaliota mashina masumbuko yalichipua na kumea Maua, mara leo wangelibahatika kupata mlo, mara kesho wangelikosa, leo wanywe kesho wasinywe, leo waumwe kesho wapone, leo wavae kesho je? Tabu juu ya tabu, pesa ngumu kupatikana,  mahitaji yao muhimu ngumu kuyapata, umasikini nao tayari umekwisha gonga hodi na kuingia kwa lazima.

                  Looh! Umasikini mbaya, yaani umeamua kugonga hodi hadi kwenye kijumba nyasi chao Tunu, kijumba nyasi kilicho shikiliwa na makuti pamoja na mbavu za Umbwa, dhiki tupu. Ingawaje wazazi wake Tunu walimshukuru Mwenyenzi Mungu muweza wa yote mara baada ya Mzee Jamali kujitokeza kumposa yule binti.

                     Kuolewa kwa Tunu kuliyapooza yale machungu ya umasikini wa familia ya baba na mama Tunu, kuolewa kwa Tunu ilikua ni  kupunguza mzigo wa kumlea Tunu ambaye wazazi wake waliokumbwa na umasikini ulio wakalia hadi visiginoni sasa waliutua ule mzigo mzito wa kumwangaikia Malaika wao.

                     Ndio maana ninasema walimshukuru sana Mwenyezi Mungu maana baada ya dhiki faraja tabu na shida ni jambo la mapito. Wanadamu hawakuumbiwa maumivu ya milele. Uzuri wake  mara baada ya Tunu kuolewa amekua ni msaada mkubwa sana  kwa wazazi wake, akihitaji chochote kile cha kuwapelekea wazazi wake huko Kijijini kwao Lukozi binti hanyimwi,  binti anapewa tena anazidishiwa mara mbili zaidi ya kile alichoomba. Anapewa pesa, anapewa nafaka, anapewa zana za kilimo, anapewa zawadi nyingine nyingi  za kuwapelekea wazazi wake, baba na mamaye, huko kwao kijijini Lukozi kijiji kilicho ndani ya mji mzuri wa Lushoto Tanga.

                     Kwisha kupata mlo mchana wa leo, mzee Jamali alitoka ndani ya chumba chake cha kupumzikia. Alikua amejilaza kwa zaidi ya masaa mawili alipata wazo la kwenda kulitizama shamba lake, shamba alilopanda karoti nyanya na kabeji, ana hamu ya kuliona shamba lake, ana hamu ya kuona namna gani shamba lake linavyomea na kupendeza, yeye ni mkulima kilimo kwake ni utukufu anajua tena anatambua kuwa kilimo ni uti wa mgongo, asiefanya kazi asile, jembe halimtupi mkulima, asie na shamba kwake kuna njaa.

                     Keisha ukosha mwili wake kwa maji safi salama maji yenye umoto moto, kapambwa kwa kanzu nzuri yenye rangi ya kijivu tena uzuri wa Bi. Mdogo Tunu kampamba mumewe kwa kumvisha koti  jeusi alilo linyosha vizuri  kwa pasi ya makaa, ajabu hata kulipiga pasi lile koti la mumewe Tunu kashirikiana na Ally mwanae.

                    Karibu njia yote Mzee Jamali aliyawaza mapenzi manono apewayo na yule binti aitwaye Tunu binti aliyefundwa kafundika kwenye unono wa mahaba. Kati kati ya mawazo yake mzee wa watu anabadirika na kumshuku kimoyo moyo mkewe Tunu anamshuku kuwa Tunu anamsaliti tena anamsaliti kwa kutembea na mwanae  wa kumzaa Ally.

                   Akawaza na kuwaza tena Mzee Jamali, usiku wa jana, usiku wa mahaba yao, Tunu alikua akimpepea pepea Mzee Jamali, akimpepea kwa kutumia ungo mzuri safi wa kupepetea mchele ili Mzee apate usingizi alale unono.. ….Leo tena kabla hajaondoka kwenda kulitizama shamba lake Mzee Jamali anakumbuka heshima na adabu ya huyu binti, ile anamvisha Baraka shea yake, binti alipiga goti chini akamsihii mumewe waende pamoja huko kwenye bonde la Kidundai lilipo shamba la Mzee Jamali, ajabu Mzee Jamali hakutaka kuongozana na mkewe, akamweleza Tunu akamwambia, sio mbaya kama atabaki nyumbani apumzike, hatochelewa kurejea.

                   “Lakini binti anaonekana kuyajua mapenzi kwangu mie, nilie mtoa Kijijini kwao kwenye umasikini wa kutupwa?” Yalimjaa mawazo Mzee Jamali, akachanganywa changanywa  na hayo mawazo hatimae akachanganyikiwa.

                  “Mmh! Hivi ndivyo walivyo mabinti wa siku hizi? Yawezekana Tunu analazimisha mapenzi kwangu, ajifanya kunipenda wakati huo huo  hataki kuonesha darili za kunitema. Je, Tunu ananipenda kweli  au anampenda Ally? Mmmh! Hapana sikubali kuona hali inavyoendelea lazima niwakomeshe wawili hawa wanao nipumbaza akili zangu.”  Aliwaza Mzee jamali , aliwaza akiendelea kupanda na kuteremka kilima cha Kidundai.

Itaendelea

Friday, September 20, 2024

MBOSSO Sehemu ya tano


 

Tulipoishia

"Mtoto tayari ametuunganisha, sidhani kama baba na mama yangu watakuwa na pingamizi juu ya hilo.” Diva alijipa tumaini.  

          “Tutegemee mengi, mazuri, mema na yenye kukubaliwa, pia tumtangulize Mwenyezi Mungu atakayetuwezesha na kutufanikisha katika safari yetu ya kurejea nyumbani Dar es salaam.”  Mbosso alitia neno, wakaendelea na shughuli ya kilimo, kuvuna viazi vyao vingi vyenye afya na siha njema, vilivyoshiba mbolea na rutuba ya kutosha.

***      

Tuendelee hapa Leo.   

   Safari ya Diva, Mbosso na Lavu kurejea nyumbani Dar es salaam iliiva, ndani ya ile Prado aliyoimiliki Diva, waliketi hawa wanafamilia wakiwa na furaha, raha na imani ya kwamba sasa mambo ndio yanaenda kuwa sawa sawa. Yanini kuandikia mate wino ukiwepo? Wacha waende nyumbani kwa baba na mamaye Diva japo kuyaweka mambo sawa ili sasa waishi kwa amani kwa sababu bado walijiona wamekosa baraka pale tu wazazi wao wakiwa na pingamizi.  

          Waliwasili salama salimini ndani ya Jiji la Dar es salaam, wamebeba zawadi tele kutoka Shambani, mikungu ya ndizi, viazi vitamu, mihogo, magimbi, kabichi na vinginevyo vingi vya bei gharama, tena uzuri wake wawili hawa hawakutumia gharama yeyote ile, bali walitumia hekima zao kupata mazao  ya shambani.   

                                    #####      

       Baada ya kuwasili  walitegemea labda wangelipokelewa kwa furaha, bashasha, raha na vicheko, lakini bila ya kutarajia walikumbana na zile sura zenye chuki kutoka kwa wazazi wa Diva, vitisho na maneno ya kuvunja moyo, japokuwa walijitahidi kuomba msamaha, walijitahidi kuomba huruma, tena waliwaeleza wazazi  kwamba ni mapenzi ndio yaliyowafanya watoroke na kwenda kuishi pamoja, hilo halikusaidia, hasira za wazazi wake Diva ziliiva.

            “Ulishindwa kutuheshimu pamoja na kuyaheshimu mawazo yetu, mawazo ambayo kwa uzuri wetu tulikuhelimisha tukijua kwamba yatakusaidia katika maisha yako.” Babaye Diva akiwa ni mwingi wa hasira, amefura kama mbogo aliyejeruhiwa, aliongea mate yakimtoka kwa fujo mdomoni.”

            “Biblia takatifu inasema ‘Waheshimu baba na mama yako, ili siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi akupayo Mwenyezi Mungu’. Lakini Diva umetuvunjia heshima, umetudharu sie wazazi wako, umetuona sie kama takataka, umetufananisha na vyombo vibovu vilivyoharibika hata ufikie hatua ya kujikabidhi kwa mwanaume asiye wa hadhi yako.” Mamaye Diva aliongea.   

         “Baba na mama, tumekuja kuomba mtusamehe, yaliyotokea tunajua ya kwamba yaliwavunja mioyo yenu, lakini yote tisa kumi tunajuta na pia kwa sababu ya mapenzi tunaomba mtusamehe, tunapendana, tumepanga maisha ya pamoja milele hadi kifo.” Diva aliyatetea mapenzi yao. Wakati huo hawa wapendanao wameketi juu ya sofa moja kubwa pale sebuleni wakiwa na nyuso za huzuni, tegemeo lao ni kuyaweka mambo sawa kama walivyoyaona yanaenda kombo.    

        “Diva, nakumbuka kabla ya haya yote kutukia niliwahi kukuambia mwanangu, niliwahi kukuambia kuwa wewe ni msomi tena sio msomi jina bali ni msomi wa chuo kikuu, msomi mwenye Degree ya Sheria, ulishindwaje kuitumia Degree yako kumtafuta mume kijana msomi mwenzio. Tazama jinsi wazazi wako tulivyo na upendo, upendo wa dhati, tulifanya hima hima kukutafutia mapenzi tukampata kijana msomi mwenzio tukategemea mtapendana na kuishi pamoja, ajabu iliyoje Diva mwanangu umetuangusha na kukutia aibu mbele a jamii.” Mamaye Diva alitia neno.  

          “Mama naomba nirudie kusema yote niliyoyatenda niliyatenda kwa sababu ya mapenzi yangu kwa huyu mwanaume niliyempenda, moyo ndio unaoanza kupenda sababu hiyo moyo wangu ulitua kwa Mbosso acha niseme ukweli kwamba ningali bado ninampenda, Mwenyezi Mungu ametujalia Binti mzuri huyu hapa mbele zenu, matokeo ya mapenzi na kupendana naomba yaliyopita wazazi mtusamehe mtupatie Baraka zenu ili tuishi kwa nguvu za haya mapenzi.” Diva aliyatetea mapenzi yake. 

           “Wazazi tambueni kuwa tumependana na kuachana kamwe isiwezekane.” Mbosso aliyekuwa kimya sasa alitoa neno.  

          “Diva ni mwanamke mwenye hekima , hekima nyingi za kisomi, mimi nilikuwa ninatabia nyingi mbaya kuzitamka katika jamii, leo hii Diva amenibadilisha nami leo ni mwingi wa utulivu, amani na mipango mizuri katika maisha. Pasina Diva mimi leo hii ningeliharibika ningeliuawa na wananchi wenye hasira, ningelifungwa Jela kwa sababu ya tabia zangu chafu zisizofaa katika jamii.” Mbosso alinena.  

          “Ukweli Diva ni mwanamke mwenye hekima, tizama ndie yeye aliyenishawishi mie niingie kwenye Kilimo na uzuri wa Kilimo tumevuna tulichopanda, tumejenga nyumba nzuri huko Lushoto,Tanga. Tumenunua Mashamba mengi makubwa kwa ajiri ya mazao yetu.  Tumefuga mifugo mingi, tungali bado tuna mipango mingi ya kimaendeleo, wazazi tafadhali mtusamehe na pia mtubariki ili tuyadumishe mapenzi yetu.” Mbosso aliongea akiwatizama  wazazi wake Diva, wazazi ambao bado wamefura kwa hasira.  

          “Kama mnataka Baraka zetu mtazipata…… Lakini poleni.”Babaye Diva aliongea, wakati huo alitoka pale Sebuleni na kuelekea chumbani kwake, mkewe (mamaye Diva) alimfuata. Sebuleni pale walibaki Diva, Mbosso na Lavu mwanawao kipenzi.     

                                           *****    

        “Tupige simu Polisi ili waje wamkamate  huyu mshenzi mpuuzi Diva na hiki Kimburukutu chake Mbosso.”  Mamaye Diva aliongea wakiwa chumbani yeye na mumewe.

            “Wazo zuri sana hilo my wife, umenikumbusha tulikwisha ripoti Polisi juu ya kutoroka kwa Diva miaka miwili iliyopita, wazo hili litatusaidia kuwaweka ndani ili walione joto la Jiwe.” Babaye Diva aliongea.   

         “Sharti tuyavunje mapenzi yao.”        

    “Uzuri Samsoni kijana anayefanya kazi Benki ya CRDB angali bado hajaoa, lazima amchukue Diva, haijalishi hata kama Diva amekwisha zaa mtoto.” Baba alinena. 

           “Tufanye juu chini kulivunja penzi lao Diva.” Mama aliongea tena. 

           “Hembu nipe simu yako ya kiganjani niwapigie Polisi, niwataarifu juu ya uwepo wa hawa haramia ndani ya nyumba yetu.”Babaye Diva aliomba simu, mamaye Diva akampatia, na baada ya kumpatia simu ilipigwa Polisi, Polisi waliahidi kufika nyumbani kwa babaye Diva haraka sana iwezekanavyo.  

          Nusu saa baadaye, polisi walikwisha kufika nyumbani kwao Diva (nyumba ya babaye Diva bwana Zine), Diva na mumewe wakiwa hawana hili wala lile wanajipa tumaini la kupewa msamaha kwa kadri ya juhudi zao. Walishtuka kuwaona Polisi wawili wakiwatia pingu mikononi mwao. Babaye Diva na mamaye Diva walifurahia lile tendo. Diva na Mbosso wakapelekwa kituo cha Polisi kwa kosa la kutoroka miaka miwili iliyopita. 

           “Lavu aliachwa mikononi mwa babu na bibiye, wakati baba na mamaye wakiwa chini ya mikono ya Polisi. Ubaya wa wazazi wake Diva tayari walikwisha panga mpango wa kumficha  Lavu hadi pale watakaposikia kuwa Diva amelivurugavuruga penzi la yeye na Mvosso.Diva anayavurugavuruga mawazo na tena Diva anakata tamaa ya kuishi na Mbosso. 

 Uzuri wa mipango yao walijipa matumaini kwamba Diva angelikubali kuolewa na Msomi mwenzie mwenye kazi nzuri, mwenye maisha mazuri, mwenye cheo na sifa njema katika jamii.     

                               *****       

    Leo ni siku ya tatu, siku  ambayo Diva ametupwa ndani ya Jela ya Segerea, Mbosso naye pia ametupwa Jela, kila mmoja amewekwa ndani ya chumba chake, Diva amewekwa hapo akilalamikiwa kwa kosa la kuwaweka wazazi wake kwenye wakati mgumu mara baada ya kutoroka miaka miwili iliyopita, wakati Mbosso amewekwa hapo akilalamikiwa kwa kosa la kumtorosha Diva akijua kuwa kufanya hivyo ni kuvunja Sheria,  akakumbushwa miaka miwili iliyopita aliiba, alimwibia mkoba mwana mama mmoja Kariakoo. Mkoba ulikuwa na pesa nyingi, vito vya dhahabu pamoja na mavazi ya huyo mwanamama.   

         Itakumbukwa kwamba yule mwana mama alikwenda kuripoti Polisi ndio maana Polisi walipata nguvu ya kumshitaki kwa makosa haya mawili. Kosa la kumuibia mwanamama vito vya thamani na pesa ni kosa ambalo Mbosso aliliona kuwa laweza kutibika haraka, japo yupo hatarini. Ule mkoba wenye mali za bei gharama ulikuwepo bado ungali umehifadhiwa kwenye gari ya mkewe mpenzi bibiye Diva. Pesa walizokwisha kuzitumia hawakuwa na budi kuzirudisha  mara baada ya wao kufanya kazi kwa bidii na maarifa.     

        Kosa la kumtorosha Diva kutoka  Dar es Salaam kwenda Kijijini Lushoto lilikuwa ni mzigo kwa Mbosso, japokuwa alijipa matumaini, liwalo na liwe, yote tisa kumi angelijitetea awezavyo. Mawazo juu ya Diva na mwanaye Love yalikiteka kichwa chake, alihuzunika na kusikitika. Kwa upande wa Diva angali yupo selo hataki kula wala kulala, anasikitika moyoni mwake mara baada ya yeye kufanya maamuzi ya kuja Dare es Salaam, anajilaumu na pia anailaumu nafsi yake, afanyeje basi? Hana la kufanya, anakubali kwamba amekosea japo anajipa matumaini  kwamba atatoka tu, yeye na mwanaume wake mpenzi Mbosso. Mawazo yake Diva yanatua kwenye sura ya mwanaye Lavu na mumewe mpenzi Mbosso, mara anajikuta akiimba kwa hisia.     

                               “Nimekumiss mpenzi wangu,

Nimekupenda mpenzi wangu,

Nitakuwa pamoja nawe,

 wakati sio muda,`  

                     Navumilia, 

matatizo yana muda wake,

Nayo yatakwisha, 

tuvumilie,

Navumilia,

Furaha ina muda wake, 

nayo itakuja, 

tuvumilie.

Kumbe wakati huo, wakati ambao Diva alikuwa bize akiimba kwa huzuni, akiimba taratibu kwa uchungu wa kutenganishwa na Mbosso pamoja na mwanaye mpenzi, ndio wakati ambao Mbosso pia alikuwa akiimba kwa uchungu ndani ya chumba cha gereza.

Nimekumisss Mpenzi wangu,

Nimekupenda penzi langu,

Nitakuwa pamoja nawe,

Wakati sio muda,

Navumilia,

 matatizo yana muda wake,

Nayo yatakwisha,

 tuvumilie,

Furaha ina muda wake,

Nayo itakuja,  

Tuvumilie. 


Kilikuwa ni kipindi kimoja kigumu sana kwao, kipindi cha huzuni ya kutenganishwa, hata wasijue hatima yao.      

                                          *****

Itaendelea

KIGUU NA NJIA. Sehemu ya tatu


Ben akiwa anajiandaa kucheza mpira pamoja na rafiki zake wawili Kijiko na Kichungu, mara ghafla Kijiko alianzisha maongezi.

KIJIKO: Oya! Ben, ninasikia siku hizi unatembea na mtoto Amina.

BEN: (Kwa aibu Fulani). Mmmh! Ni nani kakwambia?

KICHUNGU: Mzee, mapenzi hayana siri, mapenzi ni kikohozi, usilolijua litakusumbua, shule nzima wanafunzi wote wanajua kuwa wewe una mahusiano na Amina. (Anaongea kwa utani).

BEN: (Anashangaa na kuguna). Mmmh! Ishakuwa balaa, yaani mimi na Amina hatuna hata mwezi mmoja katika mahusiano yetu, nashangaa haya yamevuma kama upepo wa baharini.

KIJIKO: Ndio hivyo mkuu, sisi tumezinyaka tetesi kutoka kwa madenti wa darasa analosoma Amina, wanadai kuwa Amina anawaambia kuwa wewe ni wa kwake, hakutemi wala hakutupi.

BEN: Duh! Nilijua itakuwa siri, sasa naamini kama dunia haina siri, hapana siri ya watu wawili.

KICHUNGU: Yanini kuficha ficha Ben, eeh! Mficha uchi hazai, kula vitu bwana, ondoa aibu inayokutafuna, mchinje yule kuku, ule umtakavyo.

BEN: (Anacheka kwa aibu).

KIJIKO: Vipi huyo kuku ushamla au unasubiria hadi apoe(Anajaribu kucheza mpira wa danadana).

BEN: Wallah! Bado kabisa.

KICHUNGU: Unasubiri nini sasa?

BEN: Mmmh! (Anaguna). Aaah! (Anashindwa kuongea).

KIJIKO: Wakati ndio huu mzee, kula ujana uzee safari ndefu.

BEN: (Anajaribu kucheka).

KIJIKO: Lakini pia ukumbuke kuvaa mpira, si unajua tena zigo likituna tumboni inakuwa kesi, utaiacha shule pasina kupenda, utawakwaza wazazi wanaokusomesha, na baya zaidi utapoteza ndoto zako. (Kijiko alitoa mashauri).

BEN: Poa washikaji, nimewageti, nitafanya kama mnavyonishauri. (Ben, Kijiko, na Kichungu walianza kucheza mpira).

  ****************************


BEN:(Ameketi pamoja na Amina wakiwa Canteen, wanapata chai na mihogo, maongezi yao yanaendelea). Vipi masomo yako yanasemaje?

AMINA: Hata siyapendi.

BEN: (Anashangaa kidogo Amina). Kivipi, mbona sikuelewi mpenzi wangu?

AMINA: (Anarembua rembua macho). Mie sielewi kitu chochote wanachofundisha walimu.

BEN: Hilo sio tatizo kubwa sana Amina, mie nipo radhi kukusaidia somo lolote lile ambalo linakushinda.

AMINA: Ooooh! Jamani Ben. (Anakanyaga mguu wake Ben).Asante sana, nitashukuru.

BEN: (Anajaribu kujiondoa pale alipokanyagwa). Shaka ondoa, binadamu kusaidiana, leo kwangu, kesho kwako, mbona wahenga walisema, ‘Wema hauozi’, tenda wema uende zako, nifae la mvua, nikufae la jua, maisha ni kusaidiana’.

AMINA: (Mwingi wa fahari, japokuwa anachukia masomo yake). Leo nataka uanze kunisaidia somo la Kiswahili, au hauna muda huo.

BEN: Anawaza moyoni mwake). Mmmh! Hadi Kiswahili kinamshinda…au!? Mmmh! Anajua kukiongea, kukiandika hawezi. (Anamjibu Amina). Ninao muda mwingi wa kutosha.

AMINA: Vizuri, basi mie nitakuja geto kwako, si uliniambia umepanga huko Buguruni?

BEN: (Anaingiwa na wasi wasi). Aaah! Ndio…Ka…Ka. Karibu sana, utakuja saa ngapi vile?

AMINA: Usiku ndio mzuri, saa mbili hivi nitamdanganya mama yangu, nitamwambia leo naenda kujisiomea kwa Shoga yangu Anna, nitalala huko huko. (Amina aliongea bila wasi wasi).

BEN: Hapana Amina, usifanye hivyo, basi mie nitakufundisha muda wa mchana tutokapo shule, ili usiku uwahi kurejea nyumbani. (Ben alitia wasiwasi).

AMINA: Hapana Bwana, jua kuwa mie nakupenda, nikubalie ili leo nije nyumbani kwako. (Amina alimlazimisha Ben, Ben hakuwa na jinsi, alijikuta anakubali.)

##

ANNA: (Wakiwa darasani Siku liyofuata). Eeh! wacha we! Unasema kuwa ulilala kitanda kimoja na yule handsome aitwaye Ben?

AMINA: Sikufichi, nakwambia ilinibidi nimlazimishe ku do naye, yaani kijana alionekana mgeni haswa, mara nimshike hapa, utakuta anatetemeka, mara nimpapapse pale, angelitoa mikono yangu, lakini yote tisa kumi nilimuweka pale alipopaswa kuwekwa.

ANNA: Teh! Teh! Teh! Teh! (Anacheka) kuku mgeni hakosi kamba, huyo keishaingia kiulaini laini, na kwa jinsi nijuavyo mie atakulilia huyo, hakuachi ng’o, atakuwaza iwe usiku iwe mchana, hawezi kula kulala, wala kusoma juu yako.

AMINA: ( Anakomboa mafuta ya kujipaka midomoni kunako kopo dogo alilobeba kisha anajipaka paka midomo yake). Swala keishaingia mitegoni.


Itaendelea

DONDA LA WIVU sehemu ya pili.

 


SURA YA PILI

TUNU.
                 Kwisha kupata mlo wa mchana, mzee Jamali akapata nguvu, afya na uzima, mkewe mdogo ni mjuzi wa kuyapika mahanjumanti, madikodiko, mapochopocho manono manonozi, mlo ule ulimpatia sio nguvu pekee bali pia matumaini ya kuishi kwa raha na furaha , yote haya ni mapenzi apewayo na mkewe Tunu mke wa pili mara baada ya mke wake wa kwanza kuaga dunia.

                 Mzee Jamali alifanya uamuzi wa kuoa mke wa pili ili kujiondolea mawazo na uchovu, Tunu alimpendeza machoni, basi  mzee Jamali akamuweka ndani, akampamba, akamremba na kumkwatua, kabla ya kuwa hivi alivyo sasa mzuri  wa kunenepa binti alikua yu dhaifu, amekonda na kukondeana. Amekonda na kuchakaa kama gofu lililoachwa na Mkoloni. Haki! Huko nyumbani kwao Lukozi Tunu aliiishi maisha ya kifukara sana. Nikwambieni mpenzi msomaji kwa mara ya kwanza kama ungelipata nafasi ya kumuona, jamani! Usingeli mtamani, mmmh! Kukonda huko sio haba, maisha magumu Vijijini.

                 Kwa juhudi za mumewe, Mzee Jamali Tunu alianza kuboreka kimwili, afya yake iliyoporomoka kwa sasa ilianza kuimarika na kujengeka yote sababu Tunu hakupata kulala njaa hata siku moja ndani ya nyumba ya Mzee Jamali kila kitu alichokihitaji Tunu alikipata, hakuna  alichoomba Tunu akakikosa. Uzuri wa nyumba ya Mzee Jamali kuna bustani ya mboga mboga na matunda ambayo yamekuwa msaada  mkubwa katika kuiboresha afya ya Tunu.

                 Lukozi kijijini kwa babaye na mamaye shida ziliwatafuna, umasikini uliwameza, tabu ziliota mizizi, mahangaiko yaliota mashina masumbuko yalichipua na kumea Maua, mara leo wangelibahatika kupata mlo, mara kesho wangelikosa, leo wanywe kesho wasinywe, leo waumwe kesho wapone, leo wavae kesho je? Tabu juu ya tabu, pesa ngumu kupatikana,  mahitaji yao muhimu ngumu kuyapata, umasikini nao tayari umekwisha gonga hodi na kuingia kwa lazima.

                  Looh! Umasikini mbaya, yaani umeamua kugonga hodi hadi kwenye kijumba nyasi chao Tunu, kijumba nyasi kilicho shikiliwa na makuti pamoja na mbavu za Umbwa, dhiki tupu. Ingawaje wazazi wake Tunu walimshukuru Mwenyenzi Mungu muweza wa yote mara baada ya Mzee Jamali kujitokeza kumposa yule binti.

                     Kuolewa kwa Tunu kuliyapooza yale machungu ya umasikini wa familia ya baba na mama Tunu, kuolewa kwa Tunu ilikua ni  kupunguza mzigo wa kumlea Tunu ambaye wazazi wake waliokumbwa na umasikini ulio wakalia hadi visiginoni sasa waliutua ule mzigo mzito wa kumwangaikia Malaika wao.

                     Ndio maana ninasema walimshukuru sana Mwenyezi Mungu maana baada ya dhiki faraja tabu na shida ni jambo la mapito. Wanadamu hawakuumbiwa maumivu ya milele. Uzuri wake  mara baada ya Tunu kuolewa amekua ni msaada mkubwa sana  kwa wazazi wake, akihitaji chochote kile cha kuwapelekea wazazi wake huko Kijijini kwao Lukozi binti hanyimwi,  binti anapewa tena anazidishiwa mara mbili zaidi ya kile alichoomba. Anapewa pesa, anapewa nafaka, anapewa zana za kilimo, anapewa zawadi nyingine nyingi  za kuwapelekea wazazi wake, baba na mamaye, huko kwao kijijini Lukozi kijiji kilicho ndani ya mji mzuri wa Lushoto Tanga.

                     Kwisha kupata mlo mchana wa leo, mzee Jamali alitoka ndani ya chumba chake cha kupumzikia. Alikua amejilaza kwa zaidi ya masaa mawili alipata wazo la kwenda kulitizama shamba lake, shamba alilopanda karoti nyanya na kabeji, ana hamu ya kuliona shamba lake, ana hamu ya kuona namna gani shamba lake linavyomea na kupendeza, yeye ni mkulima kilimo kwake ni utukufu anajua tena anatambua kuwa kilimo ni uti wa mgongo, asiefanya kazi asile, jembe halimtupi mkulima, asie na shamba kwake kuna njaa.

                     Keisha ukosha mwili wake kwa maji safi salama maji yenye umoto moto, kapambwa kwa kanzu nzuri yenye rangi ya kijivu tena uzuri wa Bi. Mdogo Tunu kampamba mumewe kwa kumvisha koti  jeusi alilo linyosha vizuri  kwa pasi ya makaa, ajabu hata kulipiga pasi lile koti la mumewe Tunu kashirikiana na Ally mwanae.

                    Karibu njia yote Mzee Jamali aliyawaza mapenzi manono apewayo na yule binti aitwaye Tunu binti aliyefundwa kafundika kwenye unono wa mahaba. Kati kati ya mawazo yake mzee wa watu anabadirika na kumshuku kimoyo moyo mkewe Tunu anamshuku kuwa Tunu anamsaliti tena anamsaliti kwa kutembea na mwanae  wa kumzaa Ally.

                   Akawaza na kuwaza tena Mzee Jamali, usiku wa jana, usiku wa mahaba yao, Tunu alikua akimpepea pepea Mzee Jamali, akimpepea kwa kutumia ungo mzuri safi wa kupepetea mchele ili Mzee apate usingizi alale unono.. ….Leo tena kabla hajaondoka kwenda kulitizama shamba lake Mzee Jamali anakumbuka heshima na adabu ya huyu binti, ile anamvisha Baraka shea yake, binti alipiga goti chini akamsihii mumewe waende pamoja huko kwenye bonde la Kidundai lilipo shamba la Mzee Jamali, ajabu Mzee Jamali hakutaka kuongozana na mkewe, akamweleza Tunu akamwambia, sio mbaya kama atabaki nyumbani apumzike, hatochelewa kurejea.

                   “Lakini binti anaonekana kuyajua mapenzi kwangu mie, nilie mtoa Kijijini kwao kwenye umasikini wa kutupwa?” Yalimjaa mawazo Mzee Jamali, akachanganywa changanywa  na hayo mawazo hatimae akachanganyikiwa.

                  “Mmh! Hivi ndivyo walivyo mabinti wa siku hizi? Yawezekana Tunu analazimisha mapenzi kwangu, ajifanya kunipenda wakati huo huo  hataki kuonesha darili za kunitema. Je, Tunu ananipenda kweli  au anampenda Ally? Mmmh! Hapana sikubali kuona hali inavyoendelea lazima niwakomeshe wawili hawa wanao nipumbaza akili zangu.”  Aliwaza Mzee jamali , aliwaza akiendelea kupanda na kuteremka kilima cha Kidundai.

Itaendelea 

Thursday, September 19, 2024

DEAR UGANDA

 MPENZI WANGU UGANDA




Amani iwe na wewe, mpenzi wangu Uganda,

MOYO WAKO UKUNJUWE, UNIPOKEE  Buganda

Mikononi mwako nituwe, tukae wote Buganda.

 



Hapa ninaranda randa mapenzi yamenipanda,

Tazama nilivyokonda, sababu ninakupenda,

Kwako mesalenda, kamwe sintaja kutenda.

 

Uganda urembo wako, ni zaidi ya mapambo,

Mapenzi wanipa sisimko, kwa zako tamu nyimbo,

Ningali ni Burudiko, faraja punde nkitambo.,

 



Mapenzi utamaduni, nayalilia ya kwako,

Haya mapenzi sabuni, yanasafisha chafuko,

Nitakatishe mwilini, nimwagie manukato.

 


Nakupenda sana Uganda, nakupenda moyo wote,

Na ahidi kukulinda salama uende popote,

Kama wingu nitakutanda, wengine wasikupate,

Mpenzi wangu Uganda, nakupenda sana Uganda.

 


Uganda tulia kwangu, mapenzi tuyaboreshe,

Hata wakija wazungu, ya kwetu tusioneshe,

tupike kimoja chungu, nilishe nami nikulishe.




 

Bernbdera yenye mapenzi,ipeperushe Uganda,

Yenye nguvu yetu mapenzi, wayatamani wanyarwanda,

Dunia uwe kiongozi, Malkia wangu Uganda



 love is all Given and found,🌹 It's all around,πŸ₯° It's hard to tell about,😍 Easy to show,🀩 One sure thing when you feel it You kn...