Saturday, August 23, 2025

BEKA

 




BEKA


(ANA SURA YA MAUZO.)


SURA YA KWANZA.

“SIIONI KAZI YOYOTE YA KUFANYA DINGI.”

Ile Beka anamuona Bella akipita pita barabarani, Sultan Hoteli, moyo wake ulikuwa ukiugua, ukiugua ndani kwa ndani, ukiugua kwa mapenzi, ukiugua kwa kumpenda msichana mdogo aitwaye Bella, mwenye kadirio la miaka kumi na mitisa, Beka ana umri wa miaka Therathini na moja ni mtu mzima mzima wa umri mwili akili na majaliwa.


        Jina lake halisi anaitwa BAKARI ARMOUR lakini alipoingia KIWENGA alibadili jina akajiita BEKA ARMOUR sijui kwanini aliamua kufanya hivyo au ni kwa sababu ya ujana na kupenda mabadiliko?  Labda! Lakini ndani ya vyeti vyake vya elimu ya msingi, Sekondari na kile alichokipata alipokuwa amehitimu mafunzo ya Ulinzi kwenye kampuni ya SIGA, jina lake bado litabaki kuwa ni lile lile, BAKARI ARMOUR.


        Ni Mzaramo kwa kabila, kijana wa Jiji la DAR ES SALAAM, amesoma shule ya Msingi Buguruni Moto, akabahatika kwenda shule ya Sekondari Msimbazi, matokeo ya mitihani yake hayakuwa mazuri, upepo ukabadilika, akawa ni mtu wa kuketi Vijiweni, akijifunza uhuni na tabia zingine mbaya zinazotendwa na vijana wa Jiji la Dar es salaam.


Beka hakuwa na jambo lolote lile la msingi  au la maanaa kulitendea haki, ili apate maendeleo, ajiotambue kuwa yeye ni kijana wa kiume, hapaswi kufanya mambo ya ajabu yaliyojaa uhuni. Bbabaye mzee Armour kipato chake ni kidogo, kidogo hiki kilitosheleza mahitaji ya familia, biuashara yake ya kuuza Mboga mboga haikumlipas sana, japo ilimtoa kimaisha ilimsaidia katika malezi ya watoto wake watatu BEKA, Aisha na Tunu.


        Mzee armour alipoona mwanaye anakoenda ndiko siko, huruma juu ya Beka ziliongezeka, alimuonea huruma mwanaye na hatimaye akafanya juu chini kumketisha chini, akamtaka mwanaye yeyue na moyo wake atamke  ni aina gani ya kazi ambayo ingelikuwa naafu ya maisha yake , kukaa bure hakutoshi, kuomba omba wapitao njia hakuridhishi, kuiba, kutapeli au kutumia nguvu za lazxima huo ni uvunjifu wa sheria, na uvunjifu wa sheria ni makosa, makosa yana adhabu yake. Sio haba baba alihisi anaweza kumpoteza mwanaye, akafanya juu chini, hana Budi kumnusuru mwanaye na majanga ya dunia.

Beka angali akikuna kuna kichwa chake kilicho jaa Umba, viroboto, chawa na kungtuni, nywere zake ni ndefunamezisokota sokota, midomo yake imekomaa na kuonesha rangi ya kijivu ni kutokana na moshi wqa bange macho yake mekundu kama pili pili iliyo ivaa yamezoea kupora, kunyang’anya, kubaka, kulawiti na kudhurumu kwa kutumia silaha zenye ncha kali. Beka Yule wa vijiweni tayari alikwisha haribika.


“Sioni kazi yoyote ile ya kufanya dingi wacha mie niendelee kusota kijiweni.” Beka alimjibu mzee Armour kijeuri jeuri pasina kutafakari vema.

“Beka mwanangu, Dunia ni nzuri lakini  lakini wanadamu sisis ni wabaya, yatazame maisha yako yalivyo haribika na kukongoroka, utamlilia nani kipindi cha dhiki kuu, mateso na maumivu, kumbuka ukimtegemea ndugu utakufa masikini, ukidharau mwiba utakuchoma, mdharau Jembe si mkulima. Tafakari ni aina gani ya kazi unayoweza kufanya ili mimi baba yako nifanye juu chini kukutafutia. Mzee Armour aliongea.


“siioni kazi yoyote ile ya kufanya Dingi, niache nitulie kijiweni nile raha za duniaq,, nile ujana kwa mudaa wangu, maisha ni mafupi, uzee hauko siku hizi tofauti na  zamani.”  Beka aliongea kwa dharau.

“majuto ni mjukuu mwanangu,asiyefundwa na babaye ulimwengu utamfunda, kiburi sio maungwana, kumbuka hiyo ni misemo tu lakini ukweli ujapodhiirika wewe utalia na kusikitika.kazi ni maisha ni kufanya kazi, mwenda bure hakai bure ataokota, mgaa gaa na pwa hali wali mkavu, fanya juu chini ufikirie aina yoyote ile ya kazi ambayo wewe unaweza ukaitendea haki.” Mzee Armour alimsihi mwanawe.


“mwanangu, ndani ya Jiji la Dar es salaam kuna kazi nyingi sana, ukitaka utoke vizuri unaweza ukajiajiri kwenye kilimo cha mboiga mboga, biashara ya kuuza maji, chakula cha migahawani, sokoni na kadharika, utatoka tu mwanangu, Binafsi sidharau kazi za kuajiriwa, zinaweza kukutoa kimaisha, lakini kujiajiri ni bora zaidi ya kuajiriwa. Sema ni kazi gani unaipenda na pia unaweza kuitendea haki.” Babaye Beka alimhoji Beka aina mbali mbaliu za kazi ambazo zingelimsaidia katika kuyaboresha maisha yake.
Beka alikataakata kata, alidai kwamba aina za kazi ambazo baba yuake anamtaka afanye ni kazi  zinazowafaa wanawake, yeye ni kijana wa kiume hawezi kuuchoshaa mwilio na akili zake kujishughurisxha na shughuri kama zile.

                        ##########

BENTEN BENITHO



HADITHI YA MAMSAPU



BENTEN BENITHO



 

Sehemu ya 1

Teh teh teh eeeh, 😂 nacheka mie, nacheka Mamsapu nacheka mama wa Kitanga, nafurahia siku njema asubuhi Majogoloo, uhai nipewe pumzi shukrani kwake Mola, nafsi niitumie vema fursa tele bado zanisubiria. Mie niliyependwa ndani nikawekwa navuna nipandacho nala jasho langu mie mwenyewe. Mume kanipenda Moyoni haondoki anaifurahia Luba ya mahabati tena nakuambieni huyu Pompo ninamtunza kama mboni ya jicho langu, kan’torosha Peponi kan’jengea Paradiso Mbingu yangu Mbinguni.


Wahenga wanasema uzuri wa mwanamke sio sura, sio mvao wa mawigi yake kichwani wala sio maringo na madaha kama Twiga mbungani. Uzuri wa mwanamke huonekana Machoni, Macho udhiirisha uzuri au wema wa mwanamke. Kwa bahati nzuri sie wanawake tumejaliwa uzuri wa kuvumilia, kusamehe kuhurumia na kusaidia. Any way sijisifu kwa maneno na makeke!! Niwaachieni nafasi nyie wachambuzi mchambue chambue maneno yangu kama Karanga, makapi mkiyaswaga mbali na mema mkiyakusanya mkiyatunza na kuyahifadhi ili kizazi kijacho kifaudu.


Mama wa kitanga nimekujieni na simulizi moja iliyonitia machozi huzuni na majonzi makuu ninashindwa kumsahau Mwanawangu Laazizi wangu wa kufikia Benito. Mwana wa mke mwenzangu MAUA,  Mwanamama niliyempokonya tonge mdomoni.  Bi. Dada aliyetema pipi kwa maonjesho ya karanga. Nakumbuka nilikwisha wagea hii simulizi ya huyu Mwanadada kwenye ile simulizi yangu pendwa  MWENZENU N’SHAPENDWA sioni raha ya kuyarudia matapiko niliyoyatema miaka mingi iliopita acheni nisonge mbele, mbele kuna mafanikio


Bi. Mkubwa nikampokea mwanangu wa kufikia Benito, katoka masomoni Kenya huko ndiko mwanetu kakulia, kaishi sana huko kala na kulala Hostel. Mume wangu Pompo hana shida aligharamia. Ajabu kizazi hiki kizazi cha Bongo fleva ni shida! Hakipingwi wala hakipigiwi maweTeh teh teh (Nacheka mie)  Mtoto karejea na Satifiketi yake ya Form four ina Divisheni ziro. Mmh! Nipewe pole mie mwanamke. Mwana wa mwenzangu kakaa shule ya Bweni miaka kama yote leo hii arejee nyumbani na Divisheni ziro, niliumia.


Basi Benitho mwana wa mwanamke mwenzangu kaketi nyumbani ni mwaka wa pili sasa, hataki kwenda Chuo japo babaye ana pesa zake, kamfanyia mpango aende Chuo,  mtoto wa mwenzangu hataki kusoma! Kutwa kuchwa kajifungia chumbani kwake akipigisha Muziki mzito wa Singeli, Muziki unaoniudhi mie, Muziki unanichukiza masikioni sio haba Muziki huo umejaa maneno makali ya nguoni.


Nitawachukia vibaya wale Mashuga Mamy, wale wanawake wazee waliomzidi umri mwanangu Benito, kwa waliyonifanyia Mungu anawaona, Mungu awasamehe. Wamenivuruga mie na Pompo wangu, washatutesa sana juu ya Kibenten wangu Benito kijana aliyehitimu kidato cha nne miaka miwili iliyopita sie tulitumaini mwanetu angeliibukia Bingo kunako matokeo yake ya kidato cha nne lakin mmh! Yalituchoma. Mwana karudi na FFFF, GGGG, HHHH, ZZZZ, Ziro kwenye kila mtihani alofanya


Mmmh! Makubwa haya kijana aliyeketi Hostel miaka kama yote kuanzia darasa la kwanza hadi kuhitimu kidato cha nne anafanya vibaya kwenye matokeo yake ya kuhitimu elimu ya Sekondari. Je, yule anayekaa Dei? Kulea mtoto ni kazi nzito inayotaka moyo, mie binafsi ninamlaumu Pompo Dume langu la ukweli mapungufu yetu kama wazazi yanachangia kwa kiasi kikubwa sana kufeli kwa Mtoto darasani. Kutwa kuchwa sie tulikuwa tukizisaka pesa ili mtoto asome, ale vizuri, anywe vizuri, ajisikie kwamba na yeye yupo nyumbani. Kumbe tulijisahau, tulisahau kwamba pesa pekee haitoshi kumfanya mtoto afanye bidii darasani. Tulipaswa kumfuatilia mtoto ili tuyajue maendeleo yake kitaaluma, tujue ni wapi alipopunguka tumsaidie sababu uhuru ukizidi mtoto anaharibika, tubaki tukikumbuka wahenga walisema; Samaki ukunjwa akiwa mbichi ajapokauka hakunjiki.


Kwisha kumaliza kidato cha nne Benito akatua Masikani, anataka uhuru zaidi. Yeye na Muziki, Muziki nayeye. Ndo’ uingie ndani ya Apartment yake haukosi kuvurugwa kwa sauti zile za Maspika makubwa  ya Muziki yakitoa sauti nzito za nyimbo za kizazi cha leo wenyewe wanaita Bongo Fleva. Sikujisikia raha na furaha kuzisikiliza hizo nyimbo ambazo kwa asilimia kubwa hao wasanii wa kizazi cha leo haweshi kuimba utupu wa mwanamke, kumchora na kumharibu mwanamke.


Nyimbo zingine zinamdharilisha Mwanamke, hizo nyimbo za Singeli hazifuati ubora wa Lugha fasaha ya Kiswahili embu tuone mfano mmoja ambao msanii wa Muziki kama kioo cha


jamii anavyowadharilisha wanawake.


Michirizi ya kwenye Nyonga,

Shanga juu ya uno,

Matiti kama mto wa kulalia,

Nipe nikupe raha tupate.

Leta huo mzigo, Mashine nitakugea .


Mmmh! Ashakum si matusi siwezi endelea kusikiliza hizo nyimbo ziso adilifu. Serikali inawajibu wa kutoa elimu kwa kizazi hiki cha sanaa ya Muziki. Kwanza kwa kuanzisha Chuo kitakachowafunda Vijana Muzik na utamaduni wake. Vijana wetu watajua namna ya kuandika mashairi yenye vina na mizani. Nyimbo zenye maneno yenye hekima na adili. La, sio hizi ambazo  Maudhui yake hayafai kusikilizwa na watoto wadogo, wazazi na jamii kwa ujumla.


            Kwa hasira nikateremka juu ya Horofa ya tatu nikafika chini ya flow Apartment nikafanya kuvamia chumba cha Mwanangu Benito, nikaubamiza mlango wa chumba chake ukafunguka. Hasira zikanifanya nimpigie kelele Beni mwanangu wa kufikia.


            “Mwana we! Hembu nizimie hiyo Radio Spika, aina gani ya nyimbo unazosikiliza? Nyimbo ziso na heshima wala adili. Washindwaje kusikiliza nyimbo za dini upate kujifunza neno la Mungu nawe ubarikiwe.” Nilimkemea.


            “Mama wanizingua.” Kijana wangu aliongea kwa sauti kuu, sauti ya ujana wake sio nzito kuibeba, nyepesi, sio laini kama zile za videmu. Akah! Babu we, ninaogopa mwanangu akiwa na sauti za videmu mie nitaambiwa mwanao  nyota yake si riziki. Ninamshukuru Mungu kampendelea Mtoto wangu mrefu kiasi, mweusi wa rangi, mwili wake ni mwili wa mazoezi ‘Body builder.’


            “Sikiliza Beni ushakuwa mtu mzima na uzima wako una maana yake muhimu kuutunza ukutunze. Kumbuka ujana ni kipindi kifupi sana cha wakati, ujapouchezea ujana uzee utashika hatamu. Kwanini wasikiliza nyimbo ziso na maadili mema? Nyimbo zinazokupotosha na kukuharibia njia ya maisha yako.” Nilimkemea tena mwanangu.


            “Oyah Mamangu kama hauna Idea fresh si useme tu, mie nipo na stress kibao naomba uniache nijitulize.” Beni alinijibu kihuni huni nikamtizama akaichukua paketi ya Sigareti juu ya meza,  akaiwasha, akaweka domoni akaanza kuivuta mikupuo miwili mitatu.


            “Mmmh!”  Niliguna, moyoni nikijiuliza ameanza lini kuvuta Sigareti mwana wangu wa kufikia? Hapana. nilikereka. Nikamsogelea usawa wake nikampoka ile pisi ya Sigareti domoni nikaitupa sakafuni nikaikanyaga kanyaga na kuhakikisha haitoi moshi tena.


            “Wanifanyaje Mamangu? Mbona wanipoka uhuru? Je, nimefanya vibaya kurejea nyumbani? Beni aliuliza maswali mfululizo.


            “Uhuru mbaya huo mwana we! Wajua kuwa wewe ni msomi miongoni mwa wasomi  tegemezi katika taifa letu? Hembu sikia. Kupata Divisheni Ziro haimaanishi ati umefeli maisha.  Hapana, kuna maisha mengine baada ya kufeli Mitihani Darasani. Pale ulipoanguka amka tena endelea kukimbia, pale ulipokosea usiliwache kosa libaki kuwa kosa, jaribu kusaka ufumbuzi ili kulitatua kosa.” Niliongea kama mlevi, nisijue niliupata wapi ujasiri wa kumfokea mwanangu. Beni akafanya kutoka ndani ya chumba chake nisijue wapi anakwea, nikakitazama chumba chake kilkikuwa nyang’a nyang’a, shagalabagala, ovyo hakitamaniki kwa uchafu wa vikorokoro na vikorombwezo kibao vilivyozagaa chumbani.


 Kijana kabandika ukutani picha za utupu, tupu ya wanawake wa Kizungu, picha zingine zikionesha faragha ya mume na mke. Mmh! Nilikereka nikajiuliza Mtimani ni nani anayemharibu Beni wangu? Je, ni Shule aliyosoma? Ni marafiki na makundi ya marafiki? Mmh! Nilibaki na Labda.


            Njiiiiiii…..mmmmmuuu. Mlio wa gari ikiondoka ulisikika Beni alikuwa anaelekea pahali, sikutia shaka uhuru wa kuitumia gari anao, tushamuachia aitumie gari popote pale atakapo kuenenda.


            Nitamwita Haika mtumishi wangu wa ndani, azinyofoe hizi picha za utupu na kuzibwaga jahani kisha azitie kiberiti, hazifai wala hazipendezi machoni. Kazipata wapi hizi picha? Hakika dunia sio ndogo ina mengi ya kuhadithia. Nilijisemea mie na moyo wangu.


            Benito kasema ana stress, mawazo. Nalikumbuka kauli ile aliyoitoa Benito mwana wangu wa kufikia.


            Stress gani zamsumbua? Kwanini nimeruhusu aondoke na Gari? Mmh! Asijepata ajari, asije gonga Waja wa Maanani huko barabarani. Kwa sababu ya stress asije kamatwa na polisi wa barabarani! Hapana jamani yasimpate mabaya mwanangu Benito…… Ewe Mola umwepushe. Mwanangu na dhiki za ulimwengu. Nilimwombea mwanagu Beni nikapanda ngazi za Horofa ya tatu nikamfate Haika Mtumishi wangu nimpashe kazi ile ndogo anayopaswa kuifanya ndani ya chumba cha Benitho


TUENDELEE KESHO

WATOTO WANGU FREDO NA NELISO 💕😿

 



NILIWASOMESHA WATOTO WANGU KWA TABU SANA,📚📑 WALIPOISHIWA ADA💰 YA CHUO👨‍🎓 WAKANITIMUA NYUMBANI KAMA PAKASHUME🐈‍⬛.


WEMA WA MUNGU ULIPONIZUNGUKA GHAFRA NIKAWA BILLIONEA🏦💰💸💲 WALIPOSIKIA 👂KUWA NIMEKUA BILLIONEA WAKAANZA KUNITAFUTA ATI NIWASAMEHE.🧎‍♂️🧎🛐


    "Maua 🌹pamoja na wewe Adam  kuanzia Leo hamtakiwi kuonekana hapa shuleni,🚷 kosa mlilolitenda ni kosa kubwa, kufukuzwa kwenu Shule 🏫🎒iwe fundo Kwa wengine."Mwalimu mkuu Bwana Chikoko👨‍🏫aliongea kwa ukali.


      "Tunaomba utusamehe Mwalimu mkuu, hatukujua kama lile tendo lingelipelekea matokeo haya." Adam alilia,na mimi  Maua pia nililia.😢😿 Ilikua ni lazima tuondoke pale shuleni sababu baada ya mie Maua kukutwa na ule ujauzito nililazimishwa kumtaja aliyenipa ule ujauzito.


    "Hamkuwekeza akili zenu kwenye elimu mkombozi wa maisha mkawekeza elimu kwenye tamaa za mwili zinaa na ujinga. Bodi ya Shule haiwezi kuwaacha mkasababisha Samaki mmoja aoze na wengine wafuate kuoza. Kamateni Barua📃 zenu, wapelekeeni wazazi wenu na muwaambie hamtakiwi Tena kuwepo hapa Shuleni." Mwalimu mkuu alipaza sauti.


      "Please forgive us Sir." Tulipiga goti chini ndani ya Ofisi ya Mwalimu mkuu lakini Mwalimu mkuu hakutujali wala kutusikiliza, tukaondoka kuelekea nyumbani kwetu, tumejaa machungu, majuto na masikitiko.Tulipofika majumbani kwetu, nyumba hazikukalika, fimbo hazikutulia, fimbo nzito ziwakazo moto zilitua makalioni mwetu. Tulifinywa kwa visu vilivyopakwa mapilipili. Tulitukanwa na kuonekana kuwa hatuna maana ndani ya jamii iliyotuzunguka


Mateso hayakukoma, ilikua kila siku tunateswa na ukitegemea mie Maua nalikua tayari mjamzito, nalihitaji amani na utulivu sio stress ambazo kwa bahati mbaya zingelipelekea mimba kuchoropoka. Adam akanishawishi  tuutoroke Mkoa wa Bongo na kuelekea Lushoto Tanga. Ikawa hivyo basi tuliiba nauri na vijipesa kidogo vilivyotusaidia kuingia Lushoto Kijiji cha Magamba. 


"""""""""""""""""""""""""""

      Miezi Tisa kutimu mie Maua nilikuja kujifungulia nyumbani watoto pacha 👬 Fredo na Nelso, wavulana Wazuri tuliowalea katikati ya maadili, uvumilivu, heshima, utii na kuipenda elimu. Kilimo kwetu kilikua ni utukufu tuliipanda miti 🌴🌳ndani ya shamba kubwa alilolinunua Adam, tuliipanda pia viazi, 🥔karroti,🥕 makabeji 🥬na matunda kama ma tufaa 🍏 na mapeas🍐. Kila senti tiulioipata kutokana na kilimo tuliitunza kununulia mifugo ya nyumbani: Ng'ombe🐂, mbuzi🐐kondoo 🐑kuku🐓🐈🐖🐰 na mabata🦆. Kidogo kidogo maisha ya uvumilivu yalitukubali.



    Fredo na Nelso  walikuwa na kuongezeka haraka sana. Tuliwapeleka Shule na kuwataka wasome sana Ili siku moja waje kuwa Madaktari bingwa waje kuwasaidia binadamu maana kusaidia binadamu ni wajibu wa kila mwenye moyo na roho nzuri. Hatukuwashauri wajiingize kwenye kilimo maana kilimo kilivyokua kigumu sijui kama wangeliweza.



      Ghafla janga zito likaibuka na kuikumba familia yetu, Adam akiwa Shambani akilima kwa kutumia Jembe la mkono alishituka kumwona Ng'ombe aliyepandwa wazimu akimwendea kwa kasi na kumfuata pale alipokua akilima. Adam wangu Aliogopa akaacha kilimo akaanza kukimbia lakini walisema wahenga mbio za sakafuni uishia ukingoni, hakuna marefu yasiyo na ncha Adam aligongwa kwa pembe ya yule Ng'ombe kichaa akapigishwa huku na kule tena akapiga kelele za kuomba msaada, wakulima wenziwe waliposikia kelele zake wakaacha kulima na kwenda kumpa msaada mwenzao.


     Yule Ng'ombe🐄 kichaa tayari alikwisha toweka, wakulima walipofika pahali alipolala Adam wakamkuta Adam wangu anakata roho. Tumboni damu 🩸zimejaa na utumbo umetoka nje ya tumbo maana yule Ng'ombe alimbutua tumboni. Wakulima wakiwa ni wenye uchungu na majonzi wakambeba Adam na kumleta nyumbani. Huku kilio kikuu kilipasua anga. Nililia mie Maua, walilia wanangu pacha Fred na Nelson.


Kumpoteza Adam Mume bora na Baba bora kwetu tulihisi tufe la Dunia limetuangukia.🌍 Uchungu mzito ulituvaa miilini tukajivisha magunia na kujimwagia majivu kama tumepandwa Maruhani.😈👹


         Baada ya mazishi ya Adam Mume na kichwa cha familia yule mbeba majukumu ya nyumbani, nyumba yetu ikapooza sababu mahitaji mengi yalikosekana tofauti na Kipindi alichokuwepo Adam tuliyafurahia maisha ya uvumilivu sio haya ya mie kuitwa Singo mama, mengi mazito kupambania.


Ilinibidi nianze kufanya kazi mbili kwa nyakati tofauti angarau nipate pesa za kuhudumia familia, nikapambana na kilimo wakati huo huo nikaanza kufanya vibarua vya kusafisha nyumba za mabosi: kupuguta deki, kufua na kuhudumia meza. Hakika Jua🌞 lilinikomesha.


     Nilihitajika nyumbani kuandaa chakula, nilihitajika Shambani kulima, bado vibarua vidogo vidogo viliniita na kunifuata. Nilihakikisha watoto wanakula, kunywa na kuvaa.Tena watoto wanasoma kwa bidii Ili watimize ndoto zao za kuja kuwa Madaktari bingwa na Mola wetu asivyo mbahiri wala choyo wanangu walikaza kamba hadi kuingia Muhimbili university kusomea mambo ya Udaktari.🩺⚕️💊


     Maisha ya Chuo yalikua magumu sana, ada ya Chuo ilikua mzigo ingawaje walikubaliwa kupata mikopo ya masomo lakini bado tu mahitaji yao yaliongezeka ukijumlisha starehe na anasa zao za ujanani. Wakati Mama yao nikipambana na kilimo pamoja na kusafiri masafa marefu hadi Tanga mjini kusafisha majumba ya mabosi na majumba ya wenye pesa zao, huku nyuma wanangu walifanya anasa na starehe za ujanani. Hatimaye sasa pesa sabuni ya roho ziliwaishia vibaya wakakosa ada ya Chuo na kurejeshwa nyumbani.



     Walipofika nyumbani nilimwambia acheni Mama yenu nipambane lazima mtarudi Chuo kuendelea na masomo. Kweli kweli walikubali kubaki nyumbani kunisaidia kilimo🪓🍅🥔 na shuhuli za ufugaji, 🐂🐍🐄🐐wakati huo mie Mama yao ninafanya vibarua kwenye majumba ya mabosi na watu wenye pesa zao.


     Siku moja niliporudi kutoka kwenye vibarua vyangu niliwakuta wanangu wanajadiliana kuhusu shamba lile kubwa ambalo Adam baba yao alipanda miti:🌳🌲🎋


    "Maisha ni magumu Mama tukiendelea kukaa hivi hivi tutapoteza nafasi ya kusoma Chuo" Fredo aliongea.


     "Vumilieni wanangu, pesa zitapatikana tu. Mbali na kufanya vibarua nitawaomba mabosi wanipe mikopo itakayowawezesha mrudi Chuo." Niliwapooza Kwa maneno ya matumaini.


     "Mama hatuwezi na kamwe hatuwezi kuendelea kusubiri masomo yaaendelee kutupita." Nelso aliongea.


     "Wanangu Mimi kama Mama yenu nimewaambia msubirie na nyie hamtaki kwahiyo nifanye nini?"😔 Niliwauliza.


     "Huna la kufanya Mama lakini sisi tutafanya jambo la maana." Fredo aliongea maneno ambayo sikuyaelewa.


     "Mtafanya kitu gani? Mnataka kurejea Chuo mikono mitupu." Nilihoji.


      "Pesa zipo Mama na pesa lazima tuondoke nazo." Fredo alijibu.


       "Unajua sikuelewi Fredo au siku hizi mmeanza kuvutwa bangi mchana kweupe? Pesa 💰💴ziko wapi?" Nilianza kuzichukia akili za vijana wangu.


    "Baba si alituachia shamba, Hilo Hilo litatutosha kurejea Chuo." Neliso alinishitua.


     "Nini!? Mnalitaka shamba aliloliacha marehemu Baba yenu liuzwe? Haitawezekana, shamba Hilo ndilo litupalo kula na kutuweka hapa kijijini." Niliwaonya wasithubutu kuligusa shamba aliloliacha Baba yao Adam.


     "Huwezi kutuzuia Mama elimu ni bora kuliko kilimo kinachoumuza migongo na mikono. Lazima shamba liuzwe Ili turejee Chuo ili hapo baadae tuje kuwa msaada kwako." Fredo alitilia mkazo wa kuliuza shamba.


     "Never Fredo, never. Mkitaka nitoe radhi na kuwakasirikia jaribuni kuligusa Shamba aliloliacha Baba yenu." Niliwapiga kibuti kisha waliketi kimya. Muda si mrefu waliondoka kwenda  Bar 🍻, Ili kupooza koo zao kwa moja moto, moja baridi. Sikujali maana ujana ulianza kuwasumbua. Miaka ishirini na mitatu sio umri mdogo ni umri wa kijana kuanza kutamani vingi.

  
                                 🧍‍♂️🧍‍♂️

Toba! Baada ya siku tatu kupita nilishangaa wanangu Nelso na Fredo wameongozana na Mzee mmoja aliyejulikana Kwa jina la Mzee Kapusi.🐈Waliponifikia waliamuru niache kulima lile Shamba ambalo Baba yao Adam alilinunua miaka 23 iliyopita.


       "Niache kulima ili iweje?" Niliwahoji.❓


       "Shamba tushaliuza Mama na Hati 📃ya shamba hii hapa. Bahati nzuri Baba kabla hajaaga Dunia aliandika majina yetu kwenye Hati kama walinzi wa hili Shamba. Fredo ambaye ndiye mkubwa aliongea.


        "Mmeliuza Shamba." Nilipata mshituko.

        "Hatukupi nafasi ya kusikiliza mara mbili mbili Mama, kuanzia Leo hili shamba sio lako au letu tushaliuza  kwa huyu Bwana Kapusi."

    
      "Wanangu mmeniua." Machozi na kilio cha kwikwi kilinitoka.


       " Mmeniua wanangu, mmeua rasilimali ya pekee inayotupa maisha hapa kijijini, tutakuwa wageni wa nani. Ooh! Nilijitupa juu ya shamba langu na kuanza kujigaragaza.


     " Sasa wewe ukitegemea tukae tu kusubiri iyo mikopo unayokopa Kwa mabosi? Tutasubiri Hadi lini? Jua likizama na siku kuyoyoma" Fredo aliniita uchungu na hasira


     "Mgekua na Subira wanangu lakini sio kuuza Shamba ambalo ndilo tegemeo la maisha yetu."


      "Hatuwezi kukitegemea kilimo, hatukuzaliwa kuwa wakulima. Tulizaliwa kuwa wasomi na Madaktari" sikutaka tena kuendelea kusikiliza ule upuuzi wa watoto wangu. Nikafanya kuondoka pale Shambani nikaeleka mtoni huko Nililia sana, machozi YANGU yakawa sawa sawa na maji ya mto. Jioni ilipoingia sikutaka kurejea nyumbani sababu nilikua nikilia tu na kumkumbuka Adam Mume wangu aliyeniachia watoto wasiokithamini kilimo.

Kiza kilipoanza kuingia niliona sio vema kuketi mtoni umbu wakinisumbua na kuninyanyasia damu yangu. Nikafanya kurudi nyumbani.


     Nilipofika nyumbani nilishituliwa na sauti za maradio📻🔘☢️ spika yaliyokua yakitoa sauti za Muziki mzito wa Bongo freva. Sauti zilipanda juu Hadi ikawa kero kwa majirani hali ambayo haijazoeleka nyumbani kwetu.


     Ngo' ngo' ngo' 🤛🤛🤛. Niligonga mlango Kwa hasira  mara baada ya kuchungulia dirishani na kuwaona vijana wangu Fredo na Nelson wakinywa vilevi vikali vilivyojazana juu ya meza  iliyopo sebuleni baya zaidi vijana wangu waliwakodi wasicha warembo kutoka mjini waje kucheza Muziki wakiwa nusu utupu.


    Ngo' ngo' ngo🤜🤜🤜' niligonga Tena lango la sebuleni.

       
    "We nani? "Fredo aliipunguza sauti ya Muziki na kuja mlangoni akiwa amelewa apepesuka.


    "Tafadhali Fredo nifungulie mlango muda si mrefu mvua itanyesha." Niliongea.


  "Mama hauna chako hapa nyumbani, shamba sio lako na nyumba sio yako pia." Neliso alipaza sauti wangali wameufunga mlango, Safari hii wote wamesimama Dirishani.


   "Nini nyie vijana? Mmerogwa nyie! Mnazipata wapi kauri hizi za kumvunjia Mama yenu heshima? Ama Kwa vile Adam Baba yenu aliwapa kipaumbele cha kuwaachia urithi? Urithi huo haukupaswa kuuzwa Mama yenu nikiwa hai."


    "Ukiwa hai au usipokua hai haitatusaidia sababu nyumba ni yetu na Shamba ni letu. Uzuri tushaliuza na nyumba hii tupo mbioni kuiuza." Fredo aliongea Kwa sauti Kali ya makaripio.


    "Fredo na Neliso, Mimi ndiye Mama yenu niliyewatunza ndani ya tumbo langu Kwa zaidi ya miezi Tisa ni Mimi ndiye niliyewalea Kwa tabu na Kwa shida Hadi mfike Chuo, Chuoni mnafundwa kuwadharau wazazi wenu?" Niliongea chozi likinibubujika.🥲🥹


     "Tafadhali ondoka Mama hapa hauna chako, kama ni suala la kututunza au kutusomesha tunasema Asante hata sisi tutazalisha, tutalea na kusomesha." Wanangu walitumia Lugha Kali sana.



     "Wanangu naomba mfanye utu na kufikiria Mama yenu asiye na baya, angalieni mtapata radhi na laana juu ya yule aliyewatabikia na kuwaangaikia. Tafadhali nifungulieni." Wanangu hawakutaka kunisikiliza, mvua kubwa ilianza kunyesha⛈️, wakayafunga madirisha na kuniacha nje. Tayari walikwisha kunitupia nguo zangu na vitu vichache muhimu, hawakutaka Mama yao niingie nyumbani kwangu.


       Nililia sana, Nililia machozi ya ndimu, Nililia na kumlilia adam Mume wangu aliyenijali na kunithamini inashangaza mara baada ya kifo chake watoto wananitia aibu. Oh! Masikini niliendelea kulia pale mlangoni.


       Watoto wamekataa kuniheshimu, watoto wamekataa kuwa watiifu yote sababu ya ujana, pesa, pombe na wanawake,wamenidharau Mama yao na kuniacha nje mvua ikiniadhibu. Loh! Kosa langu Nini mie?🥲 Nilijiuliza lakini sikupata jawabu.



                        🌧️🌧️🌩️⛈️


Ile mvua kubwa uliendelea kunyesha, radi nzito ilipiga, niliogopa sana, niliogopa radi inaweza kuniua, watoto wangu hawakujali wala kunionea huruma. Nilifikiria labda niende kuomba msaada kwa majirani. Lakini nilihisi wazo hilo laweza kuwa ni usumbufu kwa majirani. Nikakimbilia kule shambani kwangu, kule shamba lishapigwa maokoto.


Nilijificha migombani, nikajizuia kwa kutumia majani ya migomba, baridi ilinitesa, mvua ilinitesa hadi pale ilipokata mbu nao waliona wamepata chakula, wakanifyonza damu yangu hakika ile ilikua siku nzito tena kwangu.


     Hasubui pambazuko ilinikuta nimepooza kwa kukesha shambani bila kupata lepe la usingizi, akili zilinitumaa kurudi nyumbani kwa watoto wangu nikaongee kiustaarabu na watoto wangu yamkini ni ujana ndio unaowasumbua, sio wale niliowazoea miaka yote ya furaha na huzuni. Basi mie huyo nikajibeba na kuelekea nyumbani kwangu nguo zangu zikiwa tipwa tipwa kwa kuliwa maji ya mvua.


     Nilipofika nyumbani kwangu 'eh!🤔' nilijikuta nashangaa kumkuta Mzee kapusi🐆 akiwa katika hatua za mwisho za kufunga milango ya Nyumba yangu. Baada ya salamu nilimuuliza:


     "Kulikoni Mzee kapusi uifunge milango ya Nyumba yangu?" Mzee kapusi akanijibu kwa ufupi.


       "Haujui, au watoto wako hawajakushirikisha!?"⁉️


     "Sijui nini na wao kunishirikisha Nini?!"😕


     "Mama Nelso usijizime data na kujitoa ufahamu tafadhali. Watoto wako wameniuzia hii nyumba na tayari wameondoka kurudi Dar es saalam, Ina maana hawajakushirikisha."



    "What!?⁉️" Presha ya taratibu ilianza kupanda na kushuka, mwili wangu ulichoka nilikua kama mzigo mzito ulio karibu kudondoka. Lo! Nguvu ziliisha, nilidondoka chini puui! Kama gunia la mapumba.



     "Nilikuja kuzinduka nikiwa nimezingirwa na majirani kibao wakinipulizia pulizia kwa vitenge vyao wengine wakilia wakidhani tayari nimeaga Dunia. Kumbukumbu ziliponijia nilianza kulia kama mtoto nikiwalaani watoto wangu Fredo na Neliso kwa ubaya walonitendea Mama yao mzazi.


     Majirani wema walinichukua na kunihifadhi majumbani kwao, kisa changu kiliwahuzunisha sana, wao pia walishangaa wakashindwa kuamini kama kweli Fredo na Neliso wanaweza kunitendea ubaya ule mimi mama yao jamani, ilikua ngumu kumeza.


~~~~~~~~~~~~


    Wiki mbili kupita nilihitaji kurejea kazini Nyumbani kwa Mzee Bushiri, nikafunga Safari hadi Nyumbani kwa Mzee Bushiri, yaani Bosi wangu Mzee yule mpole hakuniuliza Wala kunifokea kwanini nimechelewa kurudi kazini? Niligundua Mzee Bushiri alikua na wasiwasi juu ya mwonekano wangu tangu niliporejea kwake nilikua ni mnyonge, ile furaha na uchangamfu niliiozoeleka kua nao sikua nao tena, lile tabasamu alilozoea kuniona nalo Kila siku likachukua nafasi ya huzuni. Mara nyingi niliinama na kuitazama chini machozi yaishe nibubujika.



       Siku tatu mbele nikiwa ndani ya Mjumba 🏡🏘️wa Mzee Bushiri baada ya kumaliza shuhuli za kila siku nilitoka na kwenda katikati ya bustani huko niliketi pekee yangu nikilia kwa uchungu na kuomboleza juu ya kifo cha mume wangu Adam, pamoja na huzuni waliyoniachia watoto wangu Fredo na Nelso. Kumbe wakati mie namwaga chozi Mzee Bushiri aliniona akanifata.


       "Maua Mtumishi wangu Kwanini unalia, nieleze sababu nini hadi ulie kila siku." Alinishika bega jambo ambalo sikulitarajia kama Kuna mtu anitazama ninalia pale Bustanini.


     Mazito yamenikuta mie Mzee wangu." Nilisitasita kueleza changamoto iliyonisibu lakini 'piga ua' Nilipiga moyo konde na kumueleza changamoto zangu.


      "Mazito gani embu nieleze naweza kukusaidia." Mzee Bushiri Baba aliye jaa wema na hekima hakunibagua zaidi ya kunionesha faraja na upendo.


     "Nilimpoteza Mume wangu ambaye alikua ni nguzo muhimu ya familia hata baada ya kumpotezea mume wangu watoto hawaoneshi kunijali au kunithamini, hawatambui kuwa damu ni nzito kuliko maji, wamesahau uchungu wa Mwana mzazi anaujua, wameuza mashamba aliyoyaacha mume wangu baya zaidi watoto wangu wamenifukuza Mama yao kama Umbwa🐕 koko." Machozi yalishindwa kunivumilia yakarejea tena kunidondoka.😿


     "Dah! Kizuri mpe ng'ombe sio binadamu." Mzee Bushiri aliongea.


     "Nahitaji kukusaidia." Mzee Bushiri aliongea tena. Niliacha kulia,nikamtazama usoni nikiwa nimeivaa sura ya kuonewa huruma.🥹


     "Nitashukuru Baba yangu utakua umenifuta chozi la uchungu maana jasho la mnyonge haliendi tupu, chozi lilinibubujika upya.


     "Usilie kesho jiandae tutoke twende Lushoto pale pale ulipodhurumiwa haki zako, pale ulipotimuliwa na kufukuzwa kama Umbwa. Kila ulichpoteza kitarudi pale pale." Moyo wangu ilianza kuingiwa tumaini, furaha yangu ilianza kurudi kwa kasi. Tabasamu lililopotea lilianza kurudi kwa kasi. Nilihisi zile ni ndoto za akina Abunuwasi, lakini wapi! Kila neno alilonena Mzee Bushiri lilijaa ukweli. Akanikumbatia katikati ya faraja kuu.


                               🤗🥹🤗

Siku iliyofuata tulifunga Safari ya kuelekea Lushoto Kijiji Cha Magamba tulifika pahali pale haki zangu zilipopokonywa kwa nguvu za watoto 🤗🤗wangu. Mzee kapusi aliitwa mbele ya tajiri wangu Bushiri ambaye alimshawishi Kapusi kuiuza upya ile nyumba aliyoinunua kwa watoto wangu Fredo na Neliso. Kapusi mbele ya pesa hakuwa mdogo alishawishika kuipokea offa ya shilingi million Therathini ukitegemea yeye aliinunua ile nyumba kwa kiasi cha shilingi millioni kumi na Tano.  Shamba langu alilolinunia shilingi million Tano Bushiri alimpa offa ya shilingi millioni kumi na Tano.


    Mali zangu zilirudi, furaha yangu iliongezeka Sasa nikawa mmiliki wa zile Mali ambazo Adam alitoa wosia watoto wetu wawe warithi. Pamoja na huruma zote alizonifanyia Mzee Bushiri Bado tu aliingia gharama za ukarabati wa nyumba aliyoninunulia upya. Shamba langu liliboreshwa na uzuri wa yale maboresho Bushiri alininunulia mashamba  mengine matatu na vifaa vipya vya kilimo. Furaha yangu ikarejea, shukrani nyingi na sadaka zenye furaha, Mola wangu alizipokea. Nikajiona mimi ni mwingi wa bahati.

🤛👊👊👊👊


      Miaka mitano ilipita nikiwa ningali ndani ya nyumba ya Tajiri wangu mzee Bushiri, Mwarabu kutoka Omani,🇴🇲 mzee aliyekula  chumvi nyingi, yaani mpole na mwenye huruma kwa watu, mtoa misaada na ufadhiri kwa wenye dhiki, shida na masumbuko. Alianza kuuugua homa za uzeeni na uchovu wa mwili aliugua sana hata macho yake yakawa mazito kufungua. Muda mwingi aliutumia kulala kitandani Mie Maua nikawa bize kumhudumia huduma zote muhimu  ili kuirejesha afya yake iliyoteteleka. lakini ya Mola mengi ya binadamu machache, Mola akamtwaa yule mzee, 🥹🥹 Mzee akaaga Dunia na kuniachia machozi na kilio. Mzee alifariki juu ya mikono yangu, alifariki akiwa tayari amewatendea watu mengi mema na Bado tu alitamani kuendelea mema yake. Watu wengi walilia msibani kwake wakikumbuka mema na mazuri aliyowatendea, mtu mwenye roho ya huruma na kutenda mema pasina kungoja shukrani.


      Yakaanikwa matanga na matanga yakaanuliwa hapo ndipo nilijipapasa na kujua kwamba sina changu na pale nyumbani kwa marehemu Mzee Bushiri sio pangu nilitakiwa kuondoka haraka sana iwezekanavyo. Nikarejea nyumbani kwangu Lushoto Tanga.



   Harobaini kupita baada ya kifo cha Mzee Bushiri nilishangaa kuona magari yaapatayo kumi na tano yanaongoza na kusimama mbele ya nyumba yangu, nyumba alonijengea Mzee Bushiri. Kwanza niliogopa moyoni nilijua ni yale yale waliyonifanyia watoto wangu Fredo na Nelso kuuza nyumba yangu kinguvu pasina kinishirikisha lakini hapa hawawezi maana hati ya nyumba na shamba ina majina yangu.


  Yale malori yalikua yamejaa vitu mbali mbali vya nyumbani, kuanzia masofa, makabati , mafridge,vitanda na vyombo vya gharama. Yalipotua mlangoni kwangu akasimama mwanaume mmoja nadhifu, safi aliyevaa suti nyeusi na kiatu cheusi Cha kupendeza.



      "Bibi Maua huu ni wasia uliachwa na mzee Bushiri aliundika kabla ya kifo chake akikutaka uwe mmiliki wa mali zake zote, utajiri wake, mashamba yake, magari na makampuni."


     "Jesuu! Nilipigwa kelele na kunyanyua mikono juu kumshukuru Mola, majirani pia walishangilia kwa furaha,


       "Mzee Bushiri hakubahatika kuwa na ndugu au jamaa ndani ya Tanzania ndugu zake wote wapo, Oman na ni matajiri wa kutupwa kwahiyo mzee Bushiri aliona Hana mtu wa kumwachia Mali zake nyingi, utajiri na mapesa yaliyovundikwa Banki anakukabidhi wewe Bibi Maua" Nyie mimi ninashindwa kuieleza furaha yangu.



      "Lakini........" Mwanasheria aliyevalia suti safi na kiatu kinachompendeza aliongea.



      "Lakini Mzee Bushiri ameandika ndani ya wosia wake Mali na utajiri wako wote usithubutu hata siku Moja kuwaachia watoto wako, ndugu na jamaa zako. Iwapo Mola atakupenda na kukuchukua⚰️☠️ Mali zako zote zitwaendea watoto yatima. Wajane wagane watotot wa mitaani masikini na wahitaji." Mwanasheria alimaliza kuongea, nilipiga makofi  🙏👏na kufurahia kwa Raha zangu zote. Nikaupokea ule Wosia na kuubariki. Basi yale maroli yakaanza kupangilia Mali zote ndani, nikawa Tajiri na Bilionea wa ghafra.

             💰💴💰💴


Fredo na Nelso walikuja kupata fununu Mama yao amepata Bingo la utajiri, Bilionea wa ghafra. Wakafunga Safari kutoka Dar es salaam hadi Tanga kwa lengo la kumuomba mama yao msamaha. Basi walipofika waliukuta ule mjumba alioniachia Mzee Bushiri getini Kuna walinzi wengi pamoja na mijibwa Mikali  inayotisha na kuogopesha. Waliishia kuogopa pale nje wakamwita mlinzi na kumweleza shida yao, mlinzi alikuja kunipa taarifa na mie niliyeishi kama Malkia👸 nikatoka nje nipate kusikiliza shida zao, niliwakuta wamepiga magoti chini nje ya ule majumba wangu.



       "Karibuni nyinyi ni wakina nani na mnashida gani ambayo naweza kuwasidia."Waliposikia maswali ninayoqauliza walijikuta wanapigwa na butwaam wakanishangaa.


    "Mama umetusahau, mimi ni Fredo na huyu ndugu yangu Neliso. Sisi ni watoto wako tumemaliza Chuo lakini tunatangatanga mitaani kuokota chupa tupu🍼🧴 na makopo tuuze ili tupate pesa ya Dagaa chukuchuku  na ugali. Vijana wangu walionekana kuchoka na kuchakaa tongotongo machoni, nywele tipwatipwa zenye mba chawni viroboto na papasi . Nguo zao zilijaa kunguni, miili yao iliota  ukurutu, visigino vya miguu yao  virijaa funza, fangasi na magamba kama ya Kobe.



         "Siwafahamu nyie na Wala Sina watoto wanaoitwa Fredo na Neliso. "Nikijifanya kuwasahau ingawaje uchungu uliniingia na kuniumiza moyo wangu pale nilipowaona wanangu waliopotea Leo wamepatikana wakiwa wameoza.



       "Mama, Mama, Mama  sisi ni watoto wako Baba yetu Adam alituachia Nyumba na Shamba tuka........" Fredo hakumaliza sentensi yake walianza kulia na kuumwaga chozi.😿😭


        "Ondokeni hapa kwangu siwajui nyinyi rudini kwenye ile nyumba na Shamba la Baba yenu Adam" Niliongea kwa ukali ulioficha maumivu na uchungu juu ya wale watoto wangu. Nilitoa amri kwa walinzi wangu wafanye haraka kuwafukuza wale ombaomba waliowai kuninyanyasa hapo zamani. Umbwa 🐕🐕wakali walifunguliwa wakawatisha wale ombaomba waokotao chupa, wale omba omba wakatoka nduki na kukimbia kama vichaa wendawazimu.


Nilikua na maumivu makali hata nikajifungia chumbani na kulia  sana, Bado nilikua ninawapenda watoto wangu ingawaje wosia wa mzee Bushiri ulinitaka nisithubutu kuwapa kitu chochote kile alichoniachia.



       Basi nikamwita mmoja wa walinzi wangu nikamwambia enenda ukawatafute wale vijana wangu wawili Fredo na Neliso, wanunulie nyumba ya kuishi yenye kila kitu ndani, waketi humo, wale wanywe, wapewe chakula chao na mavazi tena wahudumiwe huduma zote muhimu, nikamwambia wape pia Pesa za kuwasaidia maishani mwao la zaidi watafutiwe kazi wanayoipenda kuitenda yaani Udakta 🥼🩺lakini wasithubutu kuja kugusa Mali aliyoniachia Mzee Bushiri mali hizi sio mali zao Bali mi Mali zangu pamoja na watoto yatima, wajane., wagane, masikini na wahitaji. Mlinzi wangu akaenda kuwatafuta naye akawapata.



😚😙😗😚

TCHAO

☺️😊😌

Let love 💞 lead.




 

I MISS YOU CHUGA



MISS YOU CHUGA



SEHEMU YA TATU

(ILALA DAR ES SAALAM)


PALE TULIPOISHIA

“ Sonia fanya juu chini mie nitoke hapa kituoni, Umbu wananing’ata balaa.” Obi aliongea.

 “Nikikutoa sitaki kusikia habari za huyo Rehema, mwambie nitaua mtu mie nina wivu wangu mwenyewe, sikubali kuibiwa kizembe.” Nilimuonya Obi, Nikasimama pale tulipoketi nikaelekea Kaunta niongee na Polisi yule demu mrembo haswa

 LEO TUSONGE HAPA

 “ Aunty ninaomba utusaidie ninahitaji kumtoa Obi hapa kituoni.”

 “Unataka nikusaidieje Aunty, ujue kuwa Obi mtu wako wa karibu amefanya kosa na hapa kwenye mafaili inaonekana amefunguliwa kesi za aina mbili, kesi ya kwanza ni kesi ya kuzurura usiku mitaani kama mwendawazimu, kesi ya pili ni kufanya uzembe, kuingia ndani ya nyumba ya mtu pasina ruhusa, akiwa amelewa, kuwatusi na kuwapiga majirani. Yote hayo ni makosa ya mtu wako wa karibu.” Yule Askari mrembo aliongea.

 “ Kwamaana hiyo basi Obi ni lazima apelekwe mahakamani akajibu shitaka la kwanini afanye kuvunja sheri.” Polisi aliongea mie nikamwombea chuga huruma.

 “ Aunty ‘please do us favour’ tusaidie bado ninamhitaji mtu wangu wa karibu,” Nilimsihi yule Askari mrembo.

 “ Haitawezekana kumtoa huyu ni mzembe.”

 “ Aunty nipo tayari kutoa pesa mingi ili Obi aachiwe huru,” Niliteta.

 “Good girl, una pesa mingi, sema una bei gani….. una shilingi laki tatu, ili tuifute hii kesi ya mtu wako wa karibu.” Yule  Askari Mrembo aliongea akiwa amepunguza sauti, ananong’ona ili Polisi wenziwe wasisikie maongezi yetu.

 “ Mmh! Aunty pesa mingi hizo, nipunguzie jamani!”

 “Fanya laki mbili na nusu,”

 “Punguza tena Aunty,”

 “Fanya laki mbili kamili,”

 “Oooh! Polisi punguza tena,”

 “Bull shit!  Pimbi nini wewe? Haya sema haraka una pesa mingi bei gani? Faster tuizike hii kesi kabla haijapelekwa mahakamani” Yule Polisi mwenye uchu wa pesa zangu aliongea.

 “Laki moja na nusu Aunty,”

 “Ok. Fanya presha presha, leta,leta,leta,leta ili nilifute jarida la kesi ya mtu wako wa karibu.” Nilijikuta ninatoa burungutu la pesa haraka hara bila kuzihesabu nikampatia yule Aunty na yule Aunty haraka haraka akazipokea. Akaangaza macho yake kulia na kushoto kuona kama kuna mtu  amemwona akipokea ile RUSHWA aliyoniomba, alipoona hakuna aliyemuona akazificha zile pesa kwenye SINDIRIA yake matitini. Dakika tano baadae akaniita.

 “ Sasa mnaweza kuondoka nimelifuta faili la kesi ya Obi lakini …….. Sikiliza Obi, unapaswa kuishi vizuri na watu, unapaswa kutii kanunini na taratibu za sheria, Pombe itakuponza, utaletwa tena hapa ili ujute kwanini ulizaliwa Tanzania.” Askari aliongea kwa hasira, amemnyoshea Obi mkono wa taadhari

 Tukaruhusiwa kuondokapale PANGANI kituo cha Polisi mie nikakodi Bajaji iliyotupeleka moja kwa moja hadi BUGURUNI KWA MADENGE, sehemu anayoishi mchepuko wangu Obi, amepanga GETTO mie kazi yangu ni kumlipia kodi ya hilo getto, kumnunulia Luku, kumlipia billi za maji nakadhalika. Yaania Obi Mchepuko wangu anaishi kama Malaika, ananitegemea mie na mie namchotea pesa mingi kutoka kwa Dume langu, dume kibamia Jerome.

 Jamani mie namfanyia vyote hivyo huyu Mchepuko wangu Obi, lakini masikini! Ananisaliti, ananitoroka na kwenda kwa KIDOSHO yule aitwaye REHEMA  roho inaniuma lakini sinaga jinsi Obi anakituliza kitumbua changu, Obi ananigusa na kunitekenya pale ninapostahiri kutekenywa, ai! Napata raha za dunia asikwambie mtu, mwanamke lazima akunwe akakunika, mwanamke lazima aridhishwe akaridhika, mwanamke lazima apelekwe pale anapostahiri kupelekwa, yaani tupande wote mlima na kushuka tushuke wote, ngoma dro, hapa kaaaazi!

                ########

 Basi tulipofika Buguruni kwakwa Madenge Magettoni anakoishi Obi Mchepuko wangu, huku ndiko ninakoliaga utamu, sitaki kulia utamu kule nyumbani kwa Jerome maana majirani kwa midomo hawajambo, nakwambieni wanavyo chongaa balaaa. Tukaingia ndani, nikayapasha maji moto kwenye jiko la gesi, jiko nililomnunulia Obi Mchepuko wangu. maji yalipochemka nikaanza kumkanda kanda Obi sehemu mbali mbali zaa mwili wake aliopigwa kama paka mwizi .

  “Aaash! Obi mchepuko wangu alipiga kelele yale maji ya moto pamoja na Spirt yalimuumiza

 “ Unalia nini? SI KITUMBUA CHANGU UMEKICHOKA EEH! Na sasa umeona bora ukaile Sambusa ya Rehema,” Nilimkebehi nikimkanda kanda usoni kwa maji ya moto na ile Spirt, Mchepuko wangu amepigwa balaa, amevimba balaa, amevimba kama kando la maandazi lililotiwa amira.

  “Bebi usiseme hivyo, ujue unaniumiza roho yangu, mie nakuambiaje pombe sio chai, nilipitiwa my.” Obi alijitetea

 “Umeniudhi Obi ujue, ukirudia tena mie namtafuta Mwanaume mwingine, siwezi kuteseka kwa sababu ya Rehema,” Niliendelea kumkanda kanda, hakunijibu kitu. Dakika tano mbeleni nilikwisha maliza kumkanda Obi Mchepuko wangu.

 “Sasa bebi kama vipi naomba unitoe leo buku hamsini nitoke na msosi.” Obi alianza kunisumbua sumbua, akitaka pesa, wakati yeye Binafsi aliona jinsi gani nimefirisika kwa kumpatia Rushwa yule Askari Polisi.

 “Toka huko, Dume surualia, hauna akili weye, umenigeuza Buzi kichuna eeh!? Kila siku nikupe Pesa kama mimi ni Benki ATM.” Leo nilimpa makavu yake

 “Bebi wanijibu hivyo, Poa, kama wanijibu nyodo penzi sikupi.” Mwe eeh! Eeh!😂 Kweli Obi Mchepuko wangu ni Mhuni ajabu anatoa penzi kwa pesa, bila kumpa pesa Penzi silipati ng’o.


 “Haya shika hii shilling elfu Therathini nenda Hoteli ukale, sitaki usumbufu, wanifirisi mie mwanamke.” Nilinywea,  nikaogopa kulikosa penzi, nikaingiza mkono wangu  kwenye mkoba niliotoka nao nyumbani Sharifu Shamba, nikatoa  nyekundu nyekundu tatu nikampatia Mchepuko


` “ Waoooo! Mwaaaa! 😽😘Mwaa! Pesa ni elfu kumi, Ilove you so muchi bebi,” Obi alinikumbatia akanipiga Kiss akinipapasa papasa  ishara ya kwamba anataka kunipa Penzi, Mmmh ananipa hamu, ananipandishia hisia za kulala nayeye, Basi anazidi kuitembeza mikono yake kiunoni kwangu, juu ya matiti yangu, kwenye mapaja yangu meupee peee kama chungwa lililoiva, Aaash! Ananipa hamu ya kutaka kunilala.

 Basi Obi anazidi kuitembeza mikono yake kiunoni kwangu na mapajani kwangu, mmh! Aaaai!  Oooosh! Obi analiingiza dole lake, lile dole refu la kati kwenye kitumbua changu anakitekenya tekenya na kukikuna kitumbua, aaaash! Ai mh! Kitumbua changu kimejaa maji balaaaa!

 Aaaaash! Ooohsh! Nilianza kuweweseka pale juu ya kitanda kikubwa nilichomnunulia Obi, Obi aliendelea kunipapasa papasa, anaivua ile Blauzi yangu nyembamba laini inayoyonesha matiti yangu manene ya kutamanisha, nyembamba laini iliyokichonga kiuno changu, kiuno nambari nane,  aash! Pumzi zilinitoka, presha presha, uuuh! Jamani ananinyonya chuchu zangu, aaaash! Ananinyonya kwa muda mrefu, mie napagawa miguno ya kimahaba haikakuki kunitoka, nazidiwa jamani, presha ya kupumua imenipanda, hamu ya penzi imenivamia, macho yangu makubwa ya kungu yakaanza kuniregea regea sababu Obi kanigea ulimi na ulimi huo ananisafisha safisha kule chini ya uvungu wa mapaja yangu, kule kitumbua kinawasha. Aaash mie napagawa zaidi sababu kanivamia kwa ghafla kaanza kunipa ulimi mdomoni wawili tunabadilishana mate kama vile njiwa wapendanao. Uuuh! Aaaash! Uauuauuu! Traaaaamu, ulimi wa Obi mchepuko wangu ulivyo mtamu bado angali anakikuna kuna kitumbua changu kwa kile kidole chake kirefu cha katikati ya vidole vyote vya mkononi.

  Na mie sikuwa nyuma nilikuwa bize naichezea chezea ile Dudukwe🍆 yake ndefu nyembamba, ipo kama mkono wa mtoto mchanga, hamu ya kulamba Dudukwe ikanivamia, bila kuchelewa nikaiparamia. Nikaitia mdomoni nikaitembeza kwenye ulimi Obi tayari Keisha nivua nguo zake zote na sasa anazichezea chezea shangaa na mikufu ya dhahabu niliyovaa kwenye UNO, anazidisha mipapaso, ananipagaza balaa.

Ooh! Asikwambie mtu Dudukwe ya Obi ilivyo tamu inamwaga mwaga ute mweupee kuashiria kuwa Mzee baba anahamu kinoma, ana hamu ya kucheza YOPE na akimaliza kucheza YOPE ya kwanza lazima tufanye Remix MBILI, TATU. Obi anahamu ya kucheza SEBENE, ana hamu ya kupiga NGOMA ya zilipendwa wake mie nikaendelea kulamba Dudu ‘nywa nywa nywa nywa’. Mara ghafla tukasikia sauti ya mlango wa getto ukigongwa.

 ‘Ngo ngo ngo ngo,’ 👊“Hodi” sauti nzito ya kiume ilitutibulia starehe yetu.

 ‘Ngo ngo ngo ngo’ “Hodi,” Ile sauti iliita tena. Mie moyoni niliichukia kwanini niharibiwe starehe yangu.😡

 “Nani tena huyo Bebi anayetutibulia starehe za Dunia?” Nilimuuliza Obi, amabye Safari hii aliachana na mie, akatoka pale kitandani, akavaaa boksa yake akaulaza ule mdude wake juu kuelekea kitovuni, maana kwa hamu zile bado Mchepuko alikua ananihitaji sana tuicheze ngoma hadi ipasuke.

 “ Ni huyu Msenge CHUGA, sijui kafata nini?” Obi alielekea mlangoni kuufungua, mie wakati huo tayari nimejifunika Kanga Moko kiunoni, Kuziba matiti na mzigo wangu huko nyuma mgongoni, maana kwa mzigo nilionao mwenzenu sijambo, nina mzigo balaa, mzigo kama ule wa NICOLE JOLLY BEBE, Mwanamitindo, Shosti ake’ WEMA SEPETU.

 “CHUGA?” Nilijihoji moyoni, jina geni sana masikioni kwangu. Nimetulia juu kitanda cha Banko, kitanda kinacho nesa nesa na kupiga kelele za ‘Twa, twa , twa, twa’ kelele za mahaba. Hamu ya kumuona huyo Chuga ilinivamia. Obi akaufungua mlango

 “Oya mshikaji vipi?” Obi alimpa ‘hai’ Chuga

 “Baridi mwanangu. Uko biee? Chuga ambae bado sijamuona, alimjibu Obi salamu yake, sauti ya Chuga ilinipendeza

 “ Mkaribishe mgeni ndani, Obi kwanini mgeni akae nje,” Ghafla niliropoka.

ITAENDELEA


Friday, August 8, 2025

ZEE LA ZAMANI

 



SEHEMU YA KWANZA.


HOTELINI


Ndani ya Hoteli Paradiso katikati ya Jiji la Mzizima (Dar es salaam) ZEE LAZAMANI akiwa na Mwanagenzi wake JANE wameketi wanapiga Soga, vinywaji baridi juu ya Meza vinasuuza koo zao. Zee anamshawishi Jane, Moyoni Jane anasuasua kumpatia jibu Mwalimu Zee. Ghafla BRAZA JERO akaingia ndani ya Hoteli Paradiso, aliwaona vizuri wale wawili wanaojadiliana kuhusu mapenzi. Jero akajibanza kunako kona moja ya ile Hoteli pasina kuonekana, yamkini Braza Jero anawafuatilia kwa udi na kwa vumba. Sijui kwanini? Tutajua mbele ya Safari.


            “Kama ni kukupenda usiusamehe Moyo wangu Jane, Moyo haujafanya kosa kukupenda sababu kupenda sio kosa kila Mwanadamu ana Haki ya kupenda na kupenda huko Mwanadamu mwenye tamanio la mapenzi humchagua yule wa kumpenda sababu hiyo nimekupenda sana Jane.” Zee lazamani alimchombezea mtoto Jane, Kinda sawa sawa na mwanaye wa kumzaa.


            “Akah! We Zee mie bado Kifaranga sihitaji kuyaharibu Maisha yangu.” Jane binti wa Kidato cha tatu Shule ya Sekondari Benjamini alijishaua mbele ya Zee lazamani.


            “Waogopani? Je, waogopa ati utatimuliwa Shule? No no no, Jane hakuna wakukutimua kama vumbi pale Benjamini.Tafadhali niamini mimi, mimi ndio Zee lazamani Mwalimu mkongwe wa wakongwe, Mwalimu mkuu wa wakuu, mtetezi wako, pendo lako na Sabuni ya Moyo ukichafuka. Sidhani kama kuna mwingine zaidi ya mie.” Zee alijigamba.


            “La, hasha! Siogopi kufukuzwa pale Benjamini, binafsi sina interesting ya kuendelea na masomo sababu siyapendi nafanya kulazimisha tu ilimradi kulisukuma Gurudumu liende kama vile Ng’ombe apelekwaye chinjioni. Hofu yangu ni kuingia penzini na matokeo ya kuingia penzini ninayajua mie.” Jane alijifarangua akionesha sura iliyojaa wasiwasi na woga kwa mbali.


            “Mie ndiye Mlinzi wako, Malaika mwema, ninaahidi kukulinda. Sema je, wanipenda? walipokea ombi la Mtima wangu? Tuanze kuyadumisha mapenzi yakadumu na kudumika, tupendane daima.” Zee akagugumia funda mbili tatu za kinwaji chake baridi akaachia tabasamu na kufurahia.


            “Moyo wangu bado haujahamasika, sioni kama umenishawishi nikashawishika au labda ningerejea tena masomoni, uniache nitulie nisiyafikirie sana mapenzi, nirejee Darasani nikajikite ndani ya dimbwi la masomo.” Jane alichanganya maneno.


            “Wanipa muda tena!? Je, ninapaswa kukusubiri umalize Kidato cha Nne? Miaka miwili ni muda mrefu sana. Mmmh!” Zee aliongea kwa sauti ya deko na miguno.


            “Mwalimu mpenzi, sioni baya sababu mvumilivu hula penzi bivu. Je, una shida nyingi zinazousumbua Moyo wako? Mke unaye, Bi. Mkubwa. Hawara pia unaye na mie Jane wanitaka niwe miongoni mwa wakezo? Huna haya weye, ‘mfyuuuu.’ Jane akambitulia domo Zee lazamani.


            “Watakaje kwa mfano? Je, utaniruhusu nimuache Bi. Mkubwa ili nikuoe weye? Au nimteme na kumtapika Hawara wangu ili niwe na mtoto nyanya, mchele mchele kama weye? Tambua nina haja ya kuishi nawe ili nikurithishe Mali na fahari za uzee wangu. Nina Mali nyingi sidhani kama waweza kuzikadiria kwa siku moja.” Zee alitoa kiapo Jane akacheka pasina kujua kuwa Braza Jero anayasikia maongezi yale Jane akanena.


            “Sijataka Mali zako Mwalimu, sijakushauri unipe Mali, hayo ni maamuzi ya ghafla. Ningependa nikuombe uniache kwanza ili nitulie masomoni niitafute elimu na mafanikio yanifuate.”


            “Ninakusikiliza lakini ninaomba wewe pia unisikilize tulianzishe penzi haba haba, ndo! Ndo! Ndo! Mdogo mdogo taratibu tutafika.” Zee alijaribu tena kuitupa Karata yake kwa huyu Binti wa kumi na saba.


            “Ni bora niyaogope mapema Zee langu. Nijuavyo mie Mwonja Asali haonji mara moja ataonja tena na matokeo ya lamba lamba ni kulichonga Gogo la Asali. Mie ninaisikiliza vema sauti yako lakini nawe pia yaheshimu sana mawazo yangu.” Jane aliongea Zee alishindwa kuendelea kunena, aliyapima maneno ya Jane yakapimika. Kwanza maneno ya Jane yana msimamo legelege pili maneno ya Jane yanayumbayumba, hapo ndipo Zee aligundua Jane anafeli. Mtimani Zee alikuwa akiyatengeneza maneno ambayo kwake binafsi alihisi yatamchochea na kumshawishi Jane aingie kwenye Hamsini zake.


Kama ni suala la uharibifu Zee amewaharibu sana Mabinti wa Shule, amewarubuni na kutumia kila aina ya vishawishi, vizawadi na pesa zake za Posho. Kwa muda ule mfupi aliweza kumsoma Jane, alimsoma kama Binti aliyekubali ingawaje anayachanganya maneno. Anadhiirisha kuwa amekubali ombi lake na wakati huo huo anakataa kwa visingizio kedekede viso na nguvu ya kuyashinda maneno ya Zee.


            Braza Jero akiwa amejibanza Koridoni asionekane na Mtu akaiwasha Kamera ya Simu yake, Samsung Galax 7 akapiga Picha mbili tatu, Moyo wenye wivu ukamfunika, akajisika gere. Je, atafurahia vipi akimuona Jane wa Moyo wake akipangiwa mipango dhalimu na ya kulichuja penzi lao? Jero akachukizwa na yale maongezi aliyoyanyaka. Naam, Jero alifanikiwa kupata picha halisi ya kila kinachoendelea miongoni mwa Mwanafunzi na Mwalimu wake. mmoja akishawishi ili apate yale anayotamani wakati mwingine akiyakataa mashawishi ingawaje anaonesha dalili za kuyatamani hayo mashawishi. Basi Jero akalitega sikio lake asipitwe na maneno.


            “Utanifurahia nikileta Posa nyumbani kwa Baba na Mamayo?” Zee aliuliza.


            “Jamani Mwalimu, mbona papara!? Wamaanisha umedhamiria kunioa kabisa!?” Jane aliuliza kwa mshituko kidogo.


            “Sikutanii mtoto nimekupenda, uzuri wa umbo lako na mabadiliko ya mwili wako ni moja ya vitu vinavyo nishawishi na kunihamasisha nikupende.Wacha nifanye hima nisichelewe sababu Waswahili wanasema chelewa chelewa wakuta Kuku sio wako.” Zee aliongea na kucheka.


            “Mmmh!” Jane aliguna akanyanyua Bilauri pale mezani akagugumia funda moja taratibu kwa madaha, akaitwaa Tishu akafanya kuyafuta mabaki ya ile Sharubati mdomoni.


            “Katika mapenzi umbo la nje na mwonekano wake ni vitu ambavyo vinaushawishi mkubwa kuliko umbo la ndani ambalo ni Moyo.” Zee aliongea kipuuzi.


            “Sio kweli Zee wan’danganya.”Jane alimkosoa Zee.


            “Nakudanganyaje? Embu nieleze nikuelewe ili nami nipate kufafanua maana ya kauli yangu.” Zee alimpa Jane nafasi ya kujieleza.


            “Moyo ndio wenye nguvu na ushawishi mkubwa mapenzini, mwili umejaliwa tamaa. Kwa maana hiyo Moyo huanza kupenda mwili hufuata matakwa ya Moyo. Je, umenipenda Moyoni au umenitamani mwilini?” Jane hakumpa nafasi Zee ajieleze badala yake akamuachia swali ambalo Zee hakulipatia jawabu stahiki.


            “Nisikilize Jane umbo la nje ni zaidi ya matamanio ya Moyo, umbo la nje linabeba na kukumbata Sura nzuri yenye umbo la Yai ling’aaro kama Taa, Ngozi nyororo yenye rangi ya Dodo lililoiva, Macho ya Kungu yanayomvuta Mwanaume tamaa. Ujaponitazama ninayaona mapenzi mazito yenye rangi ya Dhahabu iliyokooza. Umejaaliwa kinywa chenye maneno yanayomtoa Chatu Pangoni, Shingo ndefu ya Twiga mbungani kiuno bila mfupa hicho ni kiuno cha Nyingu jike, tumbo jema bichi lisilochoka na kuchosha, mapaja mazito yaliyonona na kutononoka kama nyama nono ya Nguruwe bado sijakusifia Makalio yako yanesanesa kama Tanda la Banko, haki! Mbona Mtoto wanitamanisha Mie…… Uwii! Nimesahau kukusifia chuchu zako bora kama Zabibu na Divai. Basi Mrembo usinipe tabu nikachoka, fanya kuniruhusu niingie Mtimani nitalii vigeni vilivyo ndani.” Zee alimmwagia sifa Jane, Jane akacheka na kuchoka.


            “Ungali bado haujanijibu swali langu. Je, umenipendea mwili au umenipenda pendo la Moyo wa dhati? Zee akaona isiwe tabu ngoja amjibu mtoto Jane.


            “Wataka nirudie kunena? Nipo tayari. Basi nikueleze, mie nimekupendea pendo la nje, penzi la mwili na matamanio ya raha za kimwili ndiyo shida yangu kuu. Macho hayana pazia kionekanacho wazi ndicho kinizuzuacho Machoni hata nishindwe kula au kulala. Ninasema kweli siwezi kupenda visoonekana sababu mie sio Jini mie ni Binadamu mwenye mapungufu na madhaifu yangu.”


            “Mmmh! Sawa nimeilewa nia yako Mwalimu Zee hauna haja ya kunipenda mimi wataka penzi la kunichezea na kuniacha kapa mwenye hasara isiyoweza kubebeka.” Jane alionesha wazi kuchukizwa na kukasirishwa na yale maneno ya Mwalimu wake akanyanyuka Kitini na kutaka kuondoka.


            “Umewaza tofauti Jane.”


            “How come? Kivipi?”


            “Uhalisia wa mapenzi ni kuchunguzana ili hapo baadae wawili turidhiane. Hivi je, bado haujaona ninavyokuchunguza mwendo na mwenendo wako? Acha niseme tayari nimeridhia ndio maana matamanio yangu ni kuleta Posa nyumbani kwa Baba na Mamayo haraka iwezekanavyo ili ukimaliza Kidato cha Nne nikuweke ndani, niwatimue wale Wanawake Wazee na wachovu Mahabani, nikupe miliki na urithi wa wanangu, nikupe raha na fahari zote unazozitamani.” Maneno yale yalimfurahisha sana Jane akatabasamu tabasamu lake zuri kama Uaridi likampendeza Zee.


            “Nayafurahia maneno yako basi acha niondoke, Jumamosi ya Leo imekuwa ni siku njema kwangu yamkini nitalala na kuamka vema. Maneno yako yameanza kupooza hisia zangu mbaya juu yako.”


            “Usinichukie Mtoto Jane, basi niambie ni lini tena tutatapata nafasi ya kunena mazuri kama haya? Je, waniacha upwekeni nilikose busu lako shavuni ili mie nijisikie kweli wanipenda?” Zee alimbembeleza Jane, Jane akatabasamu.


            “Jumamosi twaweza kukutana Mikadi Beach, Kigamboni. Busu langu kamwe sikupi hadi siku utakaponitolea Posa, hatua itakayofuata ni kufunga ndoa na Sherehe kubwa ya bei gharama itadondoshwa, tule, tunywe, tusaze Majogoloo.” Maneno ya Jane yakamfurahisha Zee, Zee akamshuhudia yule Tausi mwenye maringo na madaha akijongea na kupotea mbali na peo za Macho yake. Zee akaendelea kunywa kinywaji chake kwa taratibu, Moyoni akijipongeza sababu Ndege mzembe hunasa mtegoni.


 Itaendelea



I MISS YOU CHUGA

 CHOMBEZO: I MISS YOU CHUGA



SEHEMU YA PILI


(ILALA DAR ES SALAAM)


       Nikarudi chumbani nikamkuta Jerome amelala mie sikutaka kulala sababu nilitibuliwa na mawazo lukuki juu ya mchepuko wangu Obi basi nikafanya hima hima kuzikusanya nguo chafu za mie na Jerome nikaelekea kuzifua Faster faster mawazo hayaishi juu ya Obi mchepuko wangu nilipomaliza kufua nikakusanya vyombo vichafu nikavikosha na pia nikapuguta deki faster faster saa moja juu ya alama kazi zangu zote za pale nyumbani zilifikia tamati.


Jerome tayari alikwisha kuondoka akaelekea kazini kwake Posta, anabiashara zake, kwanza anaduka moja kubwa anauza simu za kila gharama, pili ana duka lingine kubwa la vipuri vya magari, mie na Jerome hatunaga shida sema bado tunakaa uswahilini sababu Mzee baba (Jerome) anafanya kujenga nyumba yetu sie wenyewe huko CHANIKA nje kidogo na mji wa Ilala. Mie na Jerome hatunaga shida sababu pesa ipo na uzuri wa pesa Jerome ananikatia kingi, na ubaya wa mie Sonia hicho kingi ninampatia Obi Mchepuko wangu. kutokana na mazoea ya kumpatia Obi pesa mingi, Obi amejenga tabia na mazoea ya kuni ‘distrub’ ati nimpe zaidi na zaidi nikimyima pesa nayeye ananinyima penzi lake tamu kuliko asali.

Alright, mie nilipomaliza kazi za pale nyumbani, Sharifu shamba, nikatoka na kuufunga vizuri mlango wa chumba chetu kimoja tulichopanga hapo Sharifu nikawaaga majirani zangu, jamani eeh mie ninatoka sintakawia kurejea.

Bajaji ilinidondoshea hapo kituo cha Polisi Pangani, nikafanya faster kumlipa dereva mwendesha Bajaji, nikaingia ndani ya kituo cha Polisi Pangani nimebeba pesa za kutosha angarau moyoni nilijisemea wakihitaji Pesa ili Obi atoke hapo kituoni nipo radhi kuwapa kidogo kidogo.


“Hallow, Aunty habari yawewe, pole na majukumu yote,” nilimsalimia Polisi wa kike, ameshiba vizuri yule mwanamke mwenzangu weupe wake amenizidi, mzigo huko nyuma nimemzidi, kazisuka vizuri nywele zake, ana miwani machoni, yupo kuandika andika ndani ya daftari la kuandikia kesi zinazoletwa pale kituoni.


“Habari ya mimi nzuri, kimajukumu nimepoa, nikusaidie nini Aunty?”


“Ninashida Aunty, kuna mtu wangu wa karibu anaitwa Obi, nimepigiwa simu alfajiri ya leo nimeambiwa amekamatwa, ana kesi ya kujibu, hivyo nimekuja kusikiliza Tatizo lake nini haswa?”


“Ok Auny embu nipe dakika sifuri nicheki cheki kwenye Buku la kesi ili nijue tatizo la mtu wako wa karibu, maana mimi nimeingia shift muda si mrefu, kesi kama hii iliandikwa na Askari wenzangu waliokuwepo ‘On duty’.” Yule Aunty alichukua daftari lenye kesi za watuhumiwa mbali mbali akaanza kulitafuta jina la Obi Mchepuko wangu akalipata, akanisomea kesi ya Obi kisha akaniambia.


“Jana usiku yapata muda wa saa tano, Obi alivamia chumba cha Bi.dada mmoja jinale Rehema, Bila ruhusa Obi aliingia, Jirani walimuona. Na kwa sababu muda ule Rehema hakuwepo nyumba Jirani walihisi Obi ni mwizi, hivyo wakamvamia mule chumbani na kumtoa nje, Jirani wakamhoji Obi ana shida gani kuvamia chumba cha mtu ambaye hayupo ndani?”


Mmmh! Maelezo yale yalinitia wivu,nilihisi Obi tayari kampata demu mwingine, kwanini avamie chumba cha mtu usiku? Mtu mwenyewe hayupo, je Obi na huyu Rehema wana mahusiano gani? Sikupata jawabu la moyo wangu, Askari aliendelea kunena.


“Aunty inasemekana kuwa Rehema aliupoteza ufunguo wa chumba chake, ndio sababu ya Obi kuingia na kuvamia, ile anatolewa ndani ya chumba cha Rehema Obi alikuwa amelewa chakali, akatumia Lugha chafu kuwatusi wale watu waliomlazimisha kuondoka.”

“Nimekuja KUMF*****Rehema, sina shida na nyinyi, embu niacheni Choko nyie.”Askari aliongea kama vile nayeye alikuwepo mbele ya tukio.


“Bwabwa nini wewe? Unamwita nani CHOKO, wewe ni Jambazi, huwezi kuingia ndani ya ya chumba cha mtu bila ruhusa,” Majirani walimpigia kelele Obi ambaye bado pombe zilimtawala.”


“Nasema sitoki hadi nimfir* Rehema, umbwa nyie msiniharibie Starehe yangu.”


“Nani umbwa? Tumevumilia sana matukano yako, sa’ ngoja tukuoneshe kuwa jeuri yako si kitu. Ghafla majirani wakamshambulia Obi, wakamponda vibaya mno nayeye alivyo jeuri akawarudishia vipondo vyao, mapigano yao yalisababisha Obi aletwe kituoni.”


Oooh! Masikini, hisia zangu zilikuja kuwa kweli, kumbe Obi ana demu mwingine zaidi ya mie.’Mfyuuuu’ nikafyonya kwa hasira. Si bure nimuache tu afie Jela ili huyo Rehema aje kuuzika mzoga wake.


“ Naweza kumuona Aunty?” Nilihitaji kumuona Obi.


“No problem keti hapo kwenye Siti nipe dakika sifuri, Obi atakuwa pamoja na wewe,” Askari aliongea akaenda ‘Cello’ chumba kimoja kidogo ndani y a kile kituo, akafungua mlango wa hicho chumba kisha akaita jina la Obi, Obi akaitikia Askari akamwambia ‘nifuate’,


 Obi akamfuata. Lo! Nillipomwona mchepuko wangu, nilimuonea huruma kwa jinsi alivyo onekana amevimba mwili mzima, damu iliyogandiana mwilini imegandiana pia kwenye nguo zake. Haki Obi alipewa kipondo cha kufunga mwaka.


“Obi pole Mpenzi,” Nilimtia faraja zile chuki za kumchukia Obi ati sababu ampata bibi mwengine ziliyeyuka zikanitoka na kupotea, nikatuliza moyo, huruma na machozi juu ya mchepuko wangu.


“Asante Mpenzi,nimepoa.”


“Obi kwanini unanifanyia hivyo Sweet heart.” Nilimfuta futa Obi damu zilizogandiana mwilini kwa kutumia kanga yangu Moko.


“Nisamehe Sonia, nisamehe lavu pombe, ilinitawala”


“Mbali na pombe kumbe Obi unaye demu mwingine?”Niliongea kwa hasira kidogo.


“ Ni pombe Sonia, ni pombe lavu, pombe zilinipitia. Naomba nisamehe, sintarudi, Obi alinisihi akiwa anatia huruma kibao Usoni.


“ Sonia fanya juu chini mie nitoke hapa kituoni, Umbu wananing’ata balaa.” Obi aliongea.


“Nikikutoa sitaki kusikia habari za huyo Rehema, mwambie nitaua mtu mie nina wivu wangu mwenyewe, sikubali kuibiwa kizembe.” Nilimuonya Obi, Nikasimama pale tulipoketi nikaelekea Kaunta niongee na Polisi yule demu mrembo haswa


ITAENDELEA

 love is all Given and found,🌹 It's all around,🥰 It's hard to tell about,😍 Easy to show,🤩 One sure thing when you feel it You kn...