Monday, November 25, 2024

MY BODY SHAPE, MY BENEFITS

 


MUME WANGU ALINIPA TARAKA 📃 ATI KWA SABABU NINA SHAPE🕴️ MBAYA NILICHOKUJA KUMFANYANYIA HATOKAA ASAHAU.


        Sydney aliporejea kutoka kazini alirejea akiwa amevaa sura ya chuki 😠usoni ile furaha iliyozoeleka  siku zote hakuwa nayo tena. Siku ya Leo alirudi amekunja ndita👊 Yale macho yake yenye mboni nyeusi iliyokooza yakawaka moto🔥, kinywa chake kilichozoeleka kwa upole na tabasamu kikawa ni kinywa kikali kama katafuna lundo la pilipili kichaa mdomoni

       "Nimechoka Abigair, nimechoka kuishi na wewe Tena nimekuchoka. Mwanamke haunivutii Wala haunipendezi"Aliongea Kwa jaziba. Mie nalifikiria yamkini mwenzangu kabanwa kiu ya maji nifanye hima kumletea maji baridi💦 🥛lakini maji yangelisaidia Nini kupooza hasira za Mume wangu!? 😔

        "Shida Nini my sweet husband Sydney🙍?" Nilijaribu kumsogelea pale sofani alipoketi lakini bila kutegemea alinionesha ishara ya kustop✋ kusogelea Huba langu.

       "Umepoteza mvuto wako ule mvuto wa msichana mbichi umekuwa tufe, bonge nyanya🍅 kama mti wa mbuyu🌳, umbo lako limekua baya halinivutii tena maana umekorogeka, hautamanishi mahabani. Ajabu mapenzi hauyawezi siku hizi" Kauri za mume wangu hazikua na mashiko nilihisi utoto, ujana na ujinga umemrudia.

        "Ni Hilo tu au kuna la mno linakukera?" Nilimuhoji.

        "Mapenzi huyawezi na yamekushinda Abigair unene wako kama kitimoto 🐷🐖🐽aliyenona unanifanya nipoteze hisia na hamu ya kufanya mapenzi na wewe. kila siku Moyo wangu unakuchukia. Ujinga wako umeendekeza tabia ya kubugia mayai,🥚🐣pizza 🍕, maziwa🐄🥛, Baga🥯 na vyakula vyenye mafuta 🐷" Alinikemea.

       "Sydney Mume wangu mbona silioni tatizo hapo! nipe siku mbili tatu nianze kufuatilia mlo kamili, balance diet 🥩na mazoezi ya mara 🚶‍♀️🏋️🏊🚴kwa mara umbo langu litarejea na kuwa normal yaani chembamba ukipendacho" Nilijaribu kujitetea.

      "Ushachelewa Abigair naomba Leo iwe ovar yaani penzi lifikie kikomo. Taraka hii hapa📃📜 ikikupendeza Saini ✍️📝leo au Kwa muda wako." Alinishitua.🧟lna maana umbo na mwonekano wangu ndio upelekee afanye jambo la kipuuzi kwenda Mahakamani👨‍⚖️ kuchukua taraka? Jamani! Mbona hajawai kuniambia kuhusu ubaya wa umbo langu? Mbona hatujawai jadiliana kuhusu mwonekano wangu?  Mume wangu mekurupuka kufanya maamuzi.

     "Ninakupenda Mume wangu siwezi kuishi pasina wewe, please futa mawazo hayo, mawazo ya kuniacha hayapendezi katika ndoa. Ndoa ni uvumilivu na mapatano yanayoendana na maelewano." Nilimwaga chozi niliposikia Mume niliyempenda alinitaka nisaini taraka.📝 Mbona ghafla.

       "Sina muda wa kupoteza, Leo ninaondoka, naondoka na Shebimu👠 Secretary wangu yupo ndani ya Gari ananisubiri."Aliongea. Akaendeleza.

      "Mtoto slim, slim, English figure ni mrefu wa asili ya mti wa mkaratusi, mwembamba kama kiuno cha nyigu, mapenzi anayaweza na mapenzi yake ni matamu kuliko asali."Alimsifia na kugamba sifa za Secretary wake.

      "Ina maana Kwa muda wote huo tukiwa ndoani wewe uliishia kuchepuka  na Secretary wako?" Nilimuuliza.

      "Sasa kumbe! Ulitaka nichepuke na nani?"Alinijibu ovyo. Akaingia chumbani kwetu na kupanga panga nguo zake na vikorokoro mbalimbali Kisha akatoka na Begi kubwa la nguo.

      "Sikiliza wewe nguruwe chibonge nataka ufanye hima kutia Saini yako kwenye hio karatasi ya Taraka, siku yoyote ile nitakuja kuichukua." Sikuamini kauri alizotoa Mume wangu nilihisi utani, nilihisi ndoto lakini kumbe mwenzangu alimaanisha.

       "Sydney Mume wangu tafadhali badili maamuzi ya moyo wako sababu jambo ulifanyalo sio sahihi Kwa wanaondoa."Nilipiga magoti chini anisikilize lakini wapi! Mwenzangu hakunisikiliza, alichofanya yeye ni kuufungua mlango wa sebule akatoweka kimya kimya Kwa kuliburuta lile Begi lenye nguo na vikorokoro vyake. Nikamsindikiza Kwa machozi yaliyojaa mapenzi.😢💧

Nje Nilimuona huyo Secretary wake Shebimu akija Kwa mapozi na madaha ya Mbuni mbungani akampokea lile Begi lenye nguo. Gari ikawashwa moto na kutoweka.

         *********
Tangu siku ile Mume wangu Sydney aondoke sikuwa na amani, furaha na Raha. Nilijinyima kupika na kula chakula changu kitamu, nikageukia unywaji wa pombe Kali na uvutaji wa sigareti kali nikijiaminisha kuwa vitu hivyo vitaupooza Mtima 💔ulioachwa. Ghafla nikaja kukikumbuka kisa cha rafiki yangu  LOVE 💕 WA JUAKALI. Rafiki yangu aliyeolewa takribani miaka Mitano iliyopita, kisa chake na changu vilishabihiana.
    
      Love alikua ni mfanyajazi wa kampuni ya Airtel Tanzania. Yeye ni Bi. Dada mwenye umbo tipwatipwa kibonge mwenye kilo zake miambili na hamsini, kusema kweli rafiki yangu huyu alikumbwa na unyanyapaa mkubwa kutoka Kwa marafiki zake wengi wakimcheka Kwa kudai kuwa hakupendeza. Shingo yake Nene hata ashindwe kutazama miguu yake, mikono yake minene na mizito yenye minyama uzembe, tumbole lenye kitambi lilimsaliti na kuimba shape ya tako lake ambalo lilionekana kama karatasi, yaani hakuwa na tako zaidi ya kitambi.

      Basi rafiki yangu Love wa Jua Kali akaanza kupendwa na kijana mmoja aitwaye Zeidi, Zeidi akamwambia Love Mama yangu mpenzi anatarajia kusheherekea siku yake ya kuzaliwa tarehe 20 mwezi October, karibu uungane nasi. Kama alivyomweleza kweli tarehe 20 ya October ilifika lakini sijui Zeidi hakutaka kuisherekea ile sherehe pamoja na Love!? Basi akampigia simu Love📲 akamwambia samahani siku ile asingelisheherekea ile sherehe ya mama yake maana amepata dharula ya kwenda Zanzibar 🇹🇿 Kuna shuhuli Bosi wao amemkabidhi.

Love alihuzunika lakini Mtima wake ukamwambia haitakua vema iwapo atakaa tu Bure pasina kumwandalia mama wa boyfriend wake ZAWADI. Basi Love wa Jua Kali akaenda Sokoni Kariakoo, akachagua vitenge viwili vitatu na batiki Moja akafikiria kuvipeleka vile vitu nyumbani kwao Zeidi, amkabidhi mamaye Zeidi. Ingawaje aliambiwa na Zeidi hatokuwepo nyumbani alichofikiria yeye ni kueleka nyumbani kwao Zeidi kupeleka zawadi.

      Alipofika nyumbani kwao Zeidi aligonga mlango na mamaye Zeidi akaja fungua.
   
         "Hallow!" Love Alimsabahi mama Zeidi.

         "Hallow! Karibu sweet heart." Ma Zeidi aliitikia salamu.

         "Naitwa Love, 💕 ni mchumba wa Zeidi aliniambia unasheherekea furaha ya birthday nimeona heri nikuletee zawadi" Love akamkabidhi mama Zeidi ile Zawadi ya birthday 🎈 🎊🥳🎉

      "Love 💕!!? Mchumba wa Zeidi!!?" Mama Zeidi alionekana Kupigwa butwaa.🙃🤔

     "Yes Mama. Je, Zeidi hajakwambieni?"Aliuliza.

      "Sio hajatuambieni! Ila Binti wanishangaza sababu Zeidi yupo ndani na Binti aitwaye Love 💕" Mama aliongea maneno yaliyomshangaza Love wa Juakali.

      "Nitaamini vipi!? Embu nimuone huyo Love. Ingawaje Mimi ndiye mchumba wake Zeidi."
     
      "Ingia ndani ujihakikishie." Love wa Juakali akaingia sebuleni, macho yake yalipogota mbele ya macho ya Zeidi, Zeidi alishituka😰 kombe alilolitumia kunywea wine ya Mzabibu 🍷lilidondoka chini puu🥂 likavunjuka mdomo wazi hadi lnzi 🐝walitamani kuingia walambelambe juisi tamu ya Mzabibu. Macho pima kama Jusi lililobanwa mlangoni, pembeni yake aliketi demu mmoja mrembo , mwembamba wa umbo, mrefu mwenye figa ya kizungu alionekana kumkumbatia Zeidi kimahaba.👩‍❤️‍💋‍👨.

      "Zeidi huyu ni nani?!" Love wa Juakali aliuliza Kwa Mshangao.

    "Nitaeleza Love...... nitaeleza please!"Zeidi akatetemeka.

      "Nieleze Please😡🗯️"

      "Huyu ni Love...... Ni......!"Alishindwa kuimaliza sentensi yake.

        "Ni mchumba wako si ndio? Ina maana Mimi unanichezea sababu ya umbo na mwonekano wangu."Juakali alipayuka.

       "Samahani Love, samahani please. Zeidi alitetemeka mamaye alishangaa, love chembamba alishangaa pia.

      "Basi Love chibonge aliondoka pale sebuleni Kwa hasira huku nyuma Zeidi alijaribu kumkimbilia lakini wapi! Aliitisha Uber akaipanda na kutoweka.

********
Siku iliyofuata Love alipokwenda kazini alishangaa kuwaona wafanyakazi wenziwe wote wamejikusanya ukumbini wanamshangaa Zeidi aliyekua amepiga goti akilia. Aliposogelea zaidi ndipo akakutana na bango kubwa limeandikwa kwa herufi kubwa:

 'NINAKUPENDA 💖 PEKEE YAKO LOVE 💕 WA JUAKALI.💘'. 

Alipolisogelea zaidi ndipo wafanyakazi wenza wakampisha na kumpa nafasi ya kumuona Zeidi aliyekua akilia Kwa uchungu wa machozi ya damu. Zeidi alipomuona Love akamkimbilia na kumpigia goti 🧎akamuomba 🤲 msamaha akilia😭.

      "Nisamehe Love, nisamehe mpenzi. Nilifanya uamuzi mbaya kukubagua kutokana na umbo lako nene lakini Leo nimekuja kugundua wewe ndiye mpenzi wangu sahihi."Alilia Zeidi hadi kamasi 🤧kumtoka.

      "Sikupaswa kukubagua Love, nilipaswa kuwa na mapenzi ya dhati, nilipaswa kukupenda na sio kuupenda mwili ambao unaweza kubadilika nyakati zozote. Please nisamehe love😥🙏"Juakali alimsikiliza Zeidi.

      "Yule Love uliyemkuta nyumbani amenisusa na kuniacha 💔baada ya kugundua kuwa Nina uhusiano na wewe. Please ninaomba tulirudishe penzi letu liendelee. Ninakupenda sana love.Zeidi alililia😿😿 Basi Love akamnyanyua Zeidi pale
sakafuni alipopiga goti akamwambia:

      "Maamuzi yako hayakuwa sahihi Zeidi, kama ulilipenda umbo kuliko moyo wenye mapenzi ungeliniambia mapema Ili nijijue naelekea wapi na njia ipi niishike"

      "Nisamehe 💕 "Zeidi Aliomba tena.

      "Sawa nimekusamehe mpenzi, usirudie tena sababu ubaguzi uwatenganisha watu"Love wa Juakali akamkumbatia Zeidi naye Zeidi akamkumbatia Kwa nguvu zote Hadi wafanyakazi wote wakafurahia Kwa kupiga makofi na kushangilia.👏👏👯‍♀️.

**********

Ngo' ngo' ngo👊 nilisikia sauti ya mtu akigonga mlango🚪 wa sebule yangu. Wakati huo nalikua katikati ya mawazo juu ya kisa cha Love wa Juakali na Zeidi, nikaacha kunywa vileo vyangu vikali🍺nikaeleka kuufungua mlango. Oh! Nilipoufungua mlango nilikutana na sura ya shogangu Sabienjo. Waooo! 😹🙋🫂🤗Nilimfurahia.

      "Karibu shogangu karibu mwaya!😗" Nilimkaribisha Sabi.

       "Unaniweka tumbo joto Abigair."Alianza kunichamba👌pasina salamu wakati huo mie kilevi kishashiba tumboni.

      "Nimepiga simu🤳 mara Mia lakini mwenzangu hupokei, ninatuma meseji Fb na Wasap lakini sijibiwi. Jamani Abi! Wanifanya nihisi mazito yamekukamata." Aliongea kihasira 🤕fulani kimemkwama shingoni.
      
     "Jamani Sabi!!🤔" Niliongea kilevilevi.

     "Umeanza kunywa pombe kali lini?!🍾"

      "Nina mazito yanayonichanganya."Nilimjibu.

 Tukaelekea sebuleni tukaketi nikaanza kumueleza Sabi matatizo yaliyonikuta.

    "Mwenzio nimeachwa💔." Niliongea kilevi levi.

    "Unasemaa!🧟 Sabienjo alishituka kidogo chupa ya bia aliyojichukulia kwenye Jokofu almanusura impokonyoke na kudondoka, na kwa jinsi ilivyokua ya baridi ingemtetemesha.

        "Hivyo hivyo kama ulivyosikia👂" Nikajimiminia kilevi kwenye Birauli Sabi alinitazama tu.

     "Abi, tafadhali wacha kunywa pombe yamkini pombe inakupumbaza."Alinishauri.

    "Nimefall in love 💕 with pombe." Nikacheka Kwa sauti kuu kisha nikaongea serous.
   
    "Sabi shogangu shemejio anadai siyajui mapenzi na nipo ovyo. Umbo langu halimvutii mapenzini tena halimpendezi kama alivyonikuta zamani nikiwa Kuku wa kizungu, slim body, English figure. Amenichukia, amenidharau, hajaupenda mwili wangu, amenikataa na taraka ameniachia niitie Saini. Nikubali tuyamalize."

      "Maria mama wa Yesu!🤯 Sabienjo aliishia kushangaa kisha akaongea.

      "Nilijua mapenzi yatoka moyoni, mapenzi uvumilivu, mapenzi maelewano na mapenzi ni vile mtu anavyokupenda na kukubali. Inakuaje Sasa alichukie umbo ambalo laweza kubadilika iwapo unania ya kulibadilisha.🥴

     "Ndo' hivyo Sabi moyo wa mtu umeficha mengi, mie nilimpenda Kwa dhati kumbe mwenzangu kapenda kidogo." Nikachomoa pisi ya Sigareti na kuiwasha kwa kutumia kiberiti cha gesi, pisi nyingine nikamgea Sabi, akaivuta. Uzuri ni kama vile alianza kunogewa na kunoga kwa ile story akaacha kunywa kale kabia kake akachukua Birauli na kujimiminia Jack Daniel pale mezani tukawa sawa mwendo wa kugugumia zile pombe Kali.

      "Kwahiyo hiyo Taraka chafu ushaisaini?"Aliniuliza.

      "Nangoja mwenzangu aje kuibeba. Sina jinsi, ninampenda lakini kitendo cha yeye kuniletea Secretary wake nyumbani kwangu ni dharau na kunishusha cheo cha kuitwa mama wa nyumbani."


     "Jamani! Jamani! Yaani Kwa upumbavu wake kaamua kukuletea mwanamke mwingine nyumbani" Sabi alizidi kuudokoa dokoa ule umbea uliokolezwa na kuchagizwa na vilevi vilivyotuweka huru kuondoka aibu na stress.
   
      "Nakwambia mwanaume yule ni kama Umbwa🐕 alidhani ukewenza👩‍❤️‍💋‍👩 nitauweza"Teh teh teh 😂😹🤣🤭Nilicheka Kwa sauti kuu.

     "Mmh! Sasa mwaya usikae kizembe ukazidi kuugua kwa stress na ukafa kizembe. Mwenzio ningali bado sijaingia ndoani 💍lakini ninamfrahia Mr. wangu James ambaye hanibagui Wala hanichagui. Embu tufanye jambo moja la faida."Sabi aliichukua simu yake nzuri na njema machoni, Samsung Galaxy 📱 simu ya bei gharama. Kisha akaniambia.

      "Niruhusu tufanye mchakato wa kutafuta Boyfriend mtandaoni" Mmmh!☺️ shogangu alinishangaza.

        "Mmh!🤭 Mwenzangu mbona umeenda mbali ina maana unataka wanaume wote Duniani wanifikirie Mimi kama Malaya ninayejiuza mitandaoni 🌍?"

     "Sio kwamba unajiuza Abi, move on dear, usikae kizembe. Achana na Shemela Sydney huu ni wakati wa kumuonesha kama yeye anasema chanini hiki wewe mjibu Dhahabu hii💛🌟" Maneno ya Sabi yakaniamsha na kunifariji mie niliyeachwa kizembe.

     "Aya mwaya tufanye jambo la faida💰" Tukazama mitandaoni🌏 tukazifungua zile channel za watafutanao, wale watafutao wapenzi, wachumba, mashangazi , maanko na faraja ya moyo. Basi Sabi akanifungulia Account yangu akanipiga mapicha na kuposti mtandaoni. Babu 😂😂  mie tipwatipwa chibonge nyanya niliyeachwa nilijiachia Kwa mapozi mbali mbali. Tena sie wawili siku ile tukaendekeza starehe, tuliipiga mitungi na Sigareti hadi mitungi na Sigareti ziliomba poo😂😂🤣😗.

******
Asubuhi ya siku iliyofuata nilijidamsha kivivu, Sabienjo alikwisha chukuliwa na Boyfriend wake James. Mie niliamshwa na mlio wa simu yangu, macho yalinijaa tongotongo, mekundu kama nilijipakaza pilipili kichaa nywele tipwatipwa hazitamaniki. Bado pombe ya Jana ilikua ikivuruga vuruga kichwa changu. Basi nikaichukua simu yangu iliyokua ikiita pasina kupokelewa. Video call!!🤔Wasap! Mie huyo nikaiwasha.

Nikatazamana na mwanaume mtu mzima mwenye kadirio la miaka harobaini na tano, mwanaume yule alinipungia mkono 🙋‍♂️Kwa tabasamu mwanana. Aibu ilinijaa, mwanaume safi kama yule kutazamana na mwanamke mwenye tongotongo nzito machoni, nywele tipwatipwa, mwanamke mwenye macho mekundu ya kilevi na baya zaidi ningali nimetoka kudamka kitandani. Oohsh!!😤 Nikaizima ike video call Kisha nikaingia mesenja kuandika ujumbe.

     'Tafadhali nipe dakika kumi nijisafishe, ninaona aibu kutazamana.' Nilipoituma ile meseji jibu likaja haraka haraka.

   "Usijari rafiki yangu, Nina mengi ya kuongea nawe" Oh! Nilifarijika kibonge mie haraka haraka nikaingia bafu kuswaki ovyoovyo, nikazititimua nywele zangu ndefu Kwa maji ya vuguvugu kisha nikazama ndani ya sinki la kuogea nikaukosha mwili wangu ule mchovu ulionogewa vilevivya jana Ili kupunguza stress.

      Dakika kumi kupita nilikwisha maliza kujikwatua pale Dressing table, 👗 nikametameta kwa  kujiremba na kupendeza. Mie mshamba baada ya kujilipstick nikajimwagia marashi ya Pemba na Unguja: Udi, iriki, mdalasini na vumba.... Teh tah teh🤣🤣 sikutaka kupoteza muda nikarejea ile video call nikatazamana na yule mwanaume mtanashati.

     "Niite Dakta Dario" Alijitambulisha.

      "Niite Abigair." Nilijitambulisha pia.
     
        "Waooo! Jinalo zuri, mwaaa😘."

        "Lako pia 😋"

        "Nimeichukua Nambari yako kule Dating network. Nimeipenda introduction yako, nimependa kila kitu kinachokuhusu wewe, zaidi nimelipenda umbo lako. "

 Woyooo!🤣😗 Mambo si ayo! Mie nikatabasmu

     "Asante Dakta Dario." Aibu 🙈kidogo ilinivaa.

     "Dear, naomba kama Leo utakuwa na muda tuonane LAMADA HOTEL. Tutafurahia Dinner."🍝🍽️ Mtanashati wangu aliniomba Leo tutoke.

        "Mh!" Niliguna Kwa aibu.

         "Ninaheshimu mawazo yako."Aliniambia Lugha
 tamu kutamka.

        "Sawa, Dakta Dario. Jioni ya Leo nitakua na muda mzuri wakuonana LAMADA HOTELI " Nilimjibu Kwa kiaibu kidogo kilicho nifunika, Kisha nikamuaga na kuikata simu. Moyoni  nikichekelea, mwili wangu ukarukaruka na kufarijika. Sauti ya Dakta ilitosha kuniponya stress zangu, sura yake tanashati ilizuia ugonjwa wowote kunivamia. Umbo lake jembamba na mavazi yake nadhifu yalinipendeza. Nikajiambia bahati nasibu haiji mara mbili mbili kwahiyo nisiichezee.

 ''''''''’''''''''''''''''''''''''''''''''

Saa kumi na mbili jioni niliingia bafu kukoga kisha niliyabadili mavazi yangu nami nikapendeza kwa mtoko wa jioni. Basi mie Abi nikiwa nataka kutoka sebuleni kwangu akaingia Mume wangu wa zamani, mtaraka wangu Sydney,  akanitizama kuanzia kiguu Hadi unyweleni.😶

       "Nyooo! ☹️😖 Unadhani ukivaa hivyo ndo' utapata mwanaume wa kukupenda!?"Aliniponda lakini mie sikumjibu nilimkalia kibubu.

       "Ninakuapia juu ya Jua 🌞na Mwezi ☪️hutopata mwanaume wa kukupenda kwa umbo lako hilo baya kama Andazi la kihindi." Alinikashifu lakini bado sikumjibu.

     "Hupendezi lakini unang'ang'ania kupendeza! Nimeifata Barua yaTaraka, ushaisaini!!?" Bado sikumjibu nikaingia chumbani na kutoa ile Barua ya Taraka Kisha nikamkabidhi.

        "Huna adabu Nguruwe  wewe, yaani ninaongea na wewe lakini haunipi majibu! Kibonge mpumbavu wewe"Aliingia chumbani kisha akatoka na makoti yake matatu aliyoyasahau ile siku anaondoka na Secretary wake Shebimu.

     "It's over now Sydney. N'shapata kipepeo🦋💗 wangu wa kunipendeza usitegemee kama nitayabadili maamuzi."Alinitazama Kwa Jicho la dharau Kisha akaubamiza mlango na kutoweka. Nilimshukuru Mola wangu hajaharibu jambo ingawaje alinipoteze muda wa kuonana na Dakta Dario.


###########

       Saa Moja kamili, mida ya usiku nilifika LAMADA HOTEL moyoni nikijuta kuchelewa maana sikumuona Dakta Dario. Nikamuita mhudumu nikamuuliza iwapo amemuona mwanaume wangu,mwenye sura ya Kiarabu, nyele ndefu Singa za kichotara, mwenye mustach wa kihindi, sauti tamu ya kizungu tena kavalia miwani ya glass.👨‍🏫🤓🥸 Mhudumu alimtambua Kisha akaniambia: 'huyo alikuwepo hapa muda si mrefu kaondoka' Yallah!🧟  Niliumia na kulialia mtimani🥲. Nilichelewa siku tamu ya kuonana na Dakta Dario. Huzuni ikanikumbata.

    "Wacha niondoke."Nilijisena moyoni,

     "Au nimpigie simu." Mtima ulipata wazo. Ile natoa simu yangu ya mkononi nikasikia sauti nyuma ya mgongo wangu. Alikua ni Dakta Dario.

     "Sweet  heart❤️ umefika mapema." Niligeuka, nikamkumbata na kumpiga kiss shavuni.😘 Hmmwaaa

        "Nilifikiria haitapendeza mrembo kama wewe kuja na kuondoka pasina zawadi ya Maua 🌹🌷🌺. Alinikabidhi lundo la Maua ya Rose, mie nikatabasmu, tabasamu la bahati.

   "Asante Daring💞🥀", Tuliketi pale mezani, manwyaji na malaji yakaandaliwa, tulianza kula kunywa na kutambulishana. Nilimweleza mie ni Mama wa Nyumbani niliyeachwa Kwa Taraka na yeye akanieleza ni Dakta aliye Singo Hana mtu, Hana kitu zaidi ya kunipenda mie. Nikamkubali basi tuliendelea kula, kunywa na kucheza Muziki🎺🎻🎶💽 baada ya hayo yote Dakta wangu akafanya kunirudisha nyumbani kwangu.🏘️

      Ikawa hivyo Tena mapenzi kati ya mie Abigair na Dakta Dario yakapamba moto, yakaiva na kututosha kushiba na kunenepa tulinenepa. Nilianza kimsahahu mtaraka wangu Sydney yule aliyedai kamwe sintakuja kumpata mwanaume mzuri kutokana na umbile langu ambalo halikumpendeza.

Basi siku Moja tukiwa pale LAMADA HOTEL Dario Mpenzi wangu alienda kaunta kuagiza wine ya Mzabibu mie niliachwa pale mezani nikinyofoa nyofoa vipande vya nyama ya kuku kwa mrija. 🐓🍹Ghafra akaja na kusimama mwanaume aliyenikera  na kunifanya nijisikie kichefu chefu na kutapika. Nilimtazama jinsi alivyokonda na kudhoofika, nilimtazama alivyoisha kisaikolojia. Hakuwa yule Sydney niliyemzoea Mwaka mmoja uliopita, tangu tutarikiane. Alipoona nikamtazama Kwa utulivu akaniambia.

        "Ninaomba unisamehe Abigair mpenzi wangu ninajua nilikukosea lakini sikupaswa kufanya hivyo." Kama kawaida yangu Nilimsikiliza kimya na kumkalia kibubu.

          "Nisamehe Abi mwenzio niliingia choo cha kike🚻 na Sasa majuto yamenivaa na yanalazimisha niyabebe. Nilikudharau my ulipokua mke wangu na nikakuapia kwamba hutokuia kupata mwanaume atakayekuja kukupenda kumbe viapo vile nilijiapia mie. Shebimu amenikataa 💔na tena ameenda kuolewa na mwanaume mwingine. Chozi lilitamani kumdondoka.😿

     "Kisa Nini mwenzangu au na wewe hauyajui mapenzi?" Nilimtania.

       "Bora nisiyajue mapenzi lakini sio Kwa dharau hii ya kunikataa kisa tu nimefirisika. Sina hella na sifai kuitwa mwanaume, imagine starehe zote tumezifanya kama pesa kutumia tumetumia pesa nyingi alafu baada ya kuona zimeisha ndipo mwanamke ananikataa na kunikimbia." Safari hii chozi lilidondoka naye akachukua leso akajifuta.

          "Pole," Niliongea Kwa ufupi.

          "Sijapoa Abigair Nina donda moyoni. Ninakuomba unipe nafasi turudiane tena na tupendane tena, tuishi wote Kwa furaha kama zamani." Aliitamani kunipigia goti,🧎‍♂️ viganja vya mikono yake amevikunja ishara ya kuniomba na kunisihi.🙏

      Teh teh teh, 😁🤣 nilicheka Kwa dharau.

      "Wewe usiyeyajua mapenzi na Mimi nisiyeyajua mapenzi tutaendana vipi? Nyota 🌠 zetu hazifanani lazima mmoja wetu awe anayajua zaidi ya mwingine. Mpendwa Ex naomba usijisumbue." Nilimwambia wakati huo Dakta wangu, Dakta Dario alirejea pale mezani

     "Niite Dakta Dario, huyu ni Abigair my sweet heart,💘 wangu wa moyoni kufa na kuzikana." Akanibusu Kinywani na mie nikamshikiria ili aendelee kunipa ndimi 👩‍❤️‍💋‍👨 kitendo kile kilimkera EX wangu.

     Mie na Dario wangu tukasimama pale tulipoketi tukajiandaa kuondoka, Dario alivyo na roho nzuri akakitoa kikadi 💌 cha mwaliko wa harusi yetu kisha akamkabidhi Ex wangu.

       "Wiki ijayo mie na Abigair tunatarajia kufunga ndoa,👰💍👰‍♂️ karibu sana tusheherekee pamoja. Dakta Dario aliongea. Tuliondoka pale mezani kuelekea nyumbani tukamuacha Sydney amesimama palepale mezani, abubujika machozi, hakika majuto yalimsumbua.




..................
TCHAO 💌 👋👋






   

     ,








    


      

Thursday, November 21, 2024

GOLDEN DIGGER HUSBAND




 INTO LADIES ROOM


(NDANI YA CHOO CHA KIKE)

      Niite Tunda au ukipenda refusha, Matunda🍎🤣 ninacho kisa kinachoelimisha na kufundisha wanawake na mabinti wanaokimbilia kuolewa pasina kujua mwenza (Mwanaume) uliyempenda anania mbovu, tamaa, matamanio na ubaya kwa mwenza wa kike.  Ninakubali pia ninaunga mkono pale mtu akisema mapenzi ni upofu, mapenzi ni kupendana💕 na mapenzi kukubaliana lakini yaliyomkuta Binti yangu Semi kama ningelichelewa kuyavulia nguo sijui nani angeliyaoga. 

     Semi Binti yangu kesho anaweza kutimiza miaka ishirini na mitano pia miaka mitatu ya kuachwa na Teo mwanaume aliyemdanganya kupitia kigenzo cha ndoa. kweli alimuoa lakini moyo unaficha mengi na mengi hayo ni mazito ya Dunia. 

Binti yangu alipendana sana na Boyfriend wake Mateo au kwa kifupi Teo, Hatimaye walikubaliana ndoa, harusi nzuri ndani ya Kanisa la mtakatifu Maiko, baada ya harusi mie Tunda mamaye Semi, Semi Binti yangu, Teo mkwe wangu pamoja na Sesi: best woman (Msindikizaji wa BIBI harusi) tulielekea ROYAL HANDZABE HOTEL kufurahia Sherehe. 💃🕺🎶

     Wahudhuriaji walikula, walikunywa na Muziki mwororo walicheza, macho yangu yalitua na kumuona Teo akimnong'oneza Sesi sikioni jambo fulani ambalo yamkini walipatana kwenda pahali kunena jambo wakati huo Binti yangu Semi alikua akiserebuka na kufurahia Muziki pamoja na waalikwa.💃🕺 Ghafra mkojo ulinibana pwiiii nikapata wazo la kwenda Washing room kujisaidia haja ndogo. Wakati huo Muziki uliendelea furaha na pongezi zililiminika. 

       LADIES ROOM 🚺 maandishi makubwa yalisomeka mlangoni mie Tunda nikaufungua ule mlango nikaingia kujisaidia.  Ningali bado ninatabasamu 'sasa Binti yangu mpendwa anaolewa na Bwana wa mtima wake💖.' Taa zilimulika vizuri room ikapendeza lakini ghafla macho yangu yalikua mbele ya watu wawili niwajuao tena waliniachia mshangao🙄 nilipowaona tu nilijificha kona moja ya chemba ya kuhifadhia vifaa vya usafi wa choo, moyo wangu ulienda ndu ndu ndu! Mapigo maana nilichokiona kilinistaajabisha. 

Mateo alikua amepitisha mikono yake mizito kiunoni kwa Sesi naye Sesi aliizungusha mikono yake kwenye shingo ya Teo. Walikua wakipeana ndimi💏 wakadendeka. Moyo ulinienda mapigo, pumzi zilinitoka kama vile mwanariadha Usain Bolt alivyochoka baada ya Kukimbia masafa marefu. Niliichomoa Enka yangu nikaziba mdomo pumzi zisiendelee kunitoka kwa kasi.

   'Jesu! Teo mkwe wangu anafanya nini Restroom?' Nilijiuliza.🤔

   'Teo anamsaliti mwanangu Semi kwa kupigania mabusu na Sesi rafiki wa Semi' Nilijiambia.🤭

    'Jamani kumbe Mateo mkwe wangu hajajivika ngao ya uaminifu!!'🫣 Nilishangaa na pia nilijishangaa. wakaacha kudendeka Kisha wakaongea maneno ambavyo hadi leo hii naapa kama nisingeliyafanyia juhudi zangu hakika ningelifirisika.

       "Mpenzi fanya hima umuue Tunda Bibi mama mkwe wako ili Semi aachiwe urithi wa familia na baada ya kumuua Bibi mama mkwe utauamishia utajiri wote mikononi mwako tuwe matajiri wa kutupwa" Rafiki wa Bi. Harusi aliongea.

    "Sesi ninakupenda 😘kuliko Semi kile kinyago cha mpapure. Pale ndoa hamna ninajifanya kuzuga tu, wewe nipe miezi michache jambo letu litatimia" Teo yule ninayemwita mkwe wangu aliongea.

      "Unachelewa nini Dear?😒😬 Mbona unakuwa kama mwanaume wa Dar!😡 Hauyaoni yale magari kumi ya fahari na bei ya kutupwa? Hauyaoni yale mashamba mkubwa ya mpunga kule Mbeya? Hauoni Malodge, mahotel na kumbi nyingi za starehe? Au hauoni biashara na pesa nyingi anazozimiliki mamaye Semi. Ukiisha muua Tunda mamaye Semi muue pia Semi Kisha fanya kubadilisha Majina ya urithi kwenye documentary.... Jiandikie majina yako Kisha tuanze kuyachezea mahella. " Sesi alimshauri Teo.💰💸

      "Usijari mpenzi nitafanya yote kwa ajili yako mapema ndani ya mwezi huu" Teo alimjibu Sesi. Mie mapigiti ya moyo yalinienda kasi nikiwa ningali nimefichama pembeni ya chemba ya kuhifadhi vifaa vya usafi wa choo nikawaona Sesi na Teo wakiondoka mule Restroom.

Nikakitoa kitambaa nilichokiweka kinywani ili kuzuia presha iliyonipanda, nikawaza kuondoka Ladies room maana hata mkojo uligoma kutoka baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa Teo na Sesi rafiki wa mwanangu.

      'Umdhaniaye ndiye kumbe sie' Niliwaza.🤨

      'Heri nusu Shari kuliko Shari kamili' Niliwaza tena.🙂‍↕️

      'Yakimwagika hayazoleki.' 😶‍🌫️Nilijiambia lazima niizuie tufani inayotaka kupiga chombo kiende mlama nikatembea nikiwa natetemeka.

*******

Siku iliyofuata Teo Mkwe wangu pamoja na Semi mwanangu walinisindikiza uwanja wa Ndege wa Arusha lnternational Airport kwa ajiri ya Safari ya kurejea Dar es saalam. Nilikata tiketi Lever ya juu yaani High class. Niliwaomba waniache Airport Kisha warudi makwao.

Mwanangu Semi aliniaga akisema ataelekea Ofisini kwake kukata keki🎂 ya pongezi ya kuolewa, angeliikata na rafiki zake. Teo alimwomba Semi kurejea 🏕️ nyumbani Kuna shuhuli ya kiofisi alidai angelienda kuimaliza. Niliwaaga kila mmoja alienda njia zake. 

        Lakini kumbe mie nilikua na mpango wangu, mpango wa kumuokoa Binti yangu mpenzi Semi kutoka kwenye mikono ya Tapeli anayetaka kuniua ili amdanganye mrithi wa mali zangu, Mali zangu ziandikwe kwa jina lake Mateo na sio kama Documentary mbalimbali zinavyolitaja jina la Binti yangu Semi. 

Sikuipanda Ndege niliyokodisha siku ile nilichofanya mimi ni kuichukua Uber🚗 iliyonipeleka moja kwa moja hadi nyumbani kwa Binti yangu Semi pahali anapoketi yeye na Mumewe tapeli Teo. Nilifika na baada ya kufika kwenye ile nyumba nikamuona Mkwe wangu Teo akiteremka kutoka Garini ameambatana na Sesi wanapigana mabusu na kutomasana kama wanandoa.

      Nilikereka na kuudhika kuona Binti yangu anahujumiwa na Best friend wake pamoja na mumewe tapeli aliyekula njama ya kuniua ili hapo baadae mali zangu zihame kutoka kwa Binti yangu kwenda kwa mpuuzi Teo baada ya kuniua na kumuua Binti yangu. 

       Nikiwa ningali ndani ya ile Uber niliyokodisha nikaichukua simu 📳yangu ya mkononi na kumpigia Semi mwanangu aliyekuwa Ofisini akifurahia pongezi kutoka kwa watumishi na wafanyakazi wengine wa kampuni yake.

        "Hallow! Binti yangu mpendwa Naomba uje Nyumbani kwako haraka iwezekanavyo."🏃

      "Mama si wewe upo ndani ya Ndege✈️ na waelekea Dar es saalam, jambo gani limekusibu hadi uende nyumbani kwangu?" Binti yangu aliuliza.

      "Nimepata homa ya ghafra Binti 🤒💊💉 yangu imenibidi kuongea na uongozi wa Ndege kwamba leo sintasafiri, nimehairisha."
 
      "Sawa mama basi niruhusu muda huu niutumie🎂🍰 pamoja na marafiki Kisha baada ya hapo nitakuwepo nyumbani."

     "Hapana mwanangu mimi ni mama yako Naomba unijali Nina tatizo tafadhali fanya hima."

    "Sawa mama nipe dakikachache nitakuwepo hapo." Semi aliliheshimu wazo langu. Ndani ya dakika kumi na tano aliisimamisha gari🚘 yake pembeni ya ile Uber niliyokodisha Karibu na nyumba yake.

*********

      "Samahani Binti yangu🙏" Nilianza kumueleza Semi.

     "Kuna jambo nilitamani kukueleza usiku wa Jana kwenye ukumbi wa🏰 sherehe  lakini niliona haitapendeza, basi leo nataka nikueleze yote." Nilimwambia, nikaanza kumpasha. 

     "Teo sio mume wa kumuamini, Teo ni muuaji aliyekula njama ya kutaka kuniua ili mali zote nilizoziandika kwa jina lako ziwe zake akiisha kukusonga na kukushawishi." Semi hakunielewa.

     "Najua haunielewi lakini nakuambia Binti yangu muda huu mumeo Teo na rafiki yako Sesi wapo sebuleni wanafanya mapenzi. Amini usiamini Jana niliwafumania wakiwa chooni wakipigana mabusu na kupanga mipango ya kutuua na kutuangamiza ili mali zetu ziwe zao.

      "Mama bado sikuelewi."Binti yangu hakunielewa kwa maneno 🔊ilibidi nimueleweshe kwa vitendo.📚📖💥

    "Twende ndani na tuwafumanie." Tulitoka ndani ya geti kuu la kuingilia nyumba ya Binti yangu tukaelekea ukumbini huko nilisikia sauti za miguno baini ya Teo na Sesi hakika nilighadhibika, Binti yangu aliisikia lakini alinyamaza kimya kimya kama bubu🧏😵 kiziwi.

     Kwiyoooo Lango la sebuleni lilifunguka, nilikua wa kwanza kuingia nadhani hapa nilifanya kosa, Binti yangu alinifuata nyuma ghafra Teo na Sesi waliponiona wakaacha kunyonyana ndimi haraka haraka kama mshare 🏹 waliikimbilia meza iliyojaa madokumentary na makabrasha ya Ofisi wakajifanya wanaandika andika.

    "Umeona mwanangu? 👀Umeona washenzi hawa wakinyonyana ndimi" Niliropoka ingawaje Sesi alichelewa kuliona lile tukio.

     "Bibi mama mkwe unataka kusema nini juu ya uongo wa macho yako?" Teo aliropokwa

      "Teo nilikuheshimu sana nilikuchukulia na kukuhesabia wewe kama mkwe wangu na mwenza💑 kwa mwanangu Semi, lakini kauri nilizozisikia Jana usiku Restroom 🚺ninaapa sintakusamehe" Niliongea kwa kujiamini.

     "Unataka kusema nini Bibi mama  mkwe mbona sikuelewi?"🙄 Teo aliongea akivifungafunga vifungo vya juu vya Shati yake nyeupe iliyopata mikunjo kutokana na upuuzi waliokua wanaufanya pale ukumbini.

      "Kubali au kataa wewe na Sesi ni wapenzi, 💏Jana niliwaona Restroom mkipeana ndimi na kupanga njama za kuniua na kumuua Binti yangu ili mpate kurithi mali nyingi nilizochuma kwa jasho langu" Niliongea kwa hasira hasara

     "Samahani Bibi mama mkwe ninakuheshimu, yote unayoongea ni uongo pamoja na hilo umedhamiria kunigombanisha🥷🗯️ na mke wangu Semi." Teo aliongea, Semi mwanangu akamsogelea mumewe.

      "Teo ni kweli wewe na rafiki yangu Sesi ni wapenzi wa siri?" Semi alimuuliza Teo.

      "Semi ninakupenda lakini kwa hili aliloongea Bibi mama mkwe ni uongo. Tazama Documentary hizi hapa Mimi na Sesi tulikua tunajadiliana juu ya nyumba. Mpya niliyokununulia kwa sapraizment." Teo akatoa funguo🗝️🔐 za nyumba anayodai kuwa ni mpya amemnunulia Semi.

    "Waooo! ☺️🙌Asante My Daring husband." Semi alimrukia Teo na kunyakua kwa furaha zile funguo za nyumba ambayo Teo alidai amemnunulia.

      "Niamini mpenzi ninakupenda hadi kukufanyia Sapraizment, 🙀kama utaendelea kusikiliza maneno ya Bibi mama mkwe niruhusu niondoke nirudi kwenye nyumba yangu nikuacheni." Teo aliongea.

      "Hapana, siwezi kukuacha mume wangu mpenzi, ninakupenda. maneno ayaongeayo mama siwezi kuyaamini sababu hata ushahidi wa picha📷, video📹au audio Hakuna. Nitaaminije." Mwanangu Semi aliongea.

   "Sawa mwanangu kama hauniamini lakini kumbuka majuto ni mjukuu, mimi ninarejea Dar es saalam siku utakapozinduka akili Nina imani utanikumbuka." Niliongea kwa hasira na kutoka ndani ya nyumba ya mwanangu nikaichukua Uber yangu na moja kwa moja nikaelekea Arusha lnternational Airport🛬 nilale hapo ili kesho nirejee Dar es salaam.🌆
============

Lilipita juma moja sikuwasiliana na Semi mwanangu lakini bado moyo uliniuma kuona mwanangu ameolewa na muuaji ☠️🏴‍☠️ tena mwenye tamaa. Sikupendezwa, basi nikampigia simu Semi wangu.

     Ngriii Ngriii ngroooo📞📲 Simu iliita mara tatu. Kisha Semi aliipokea baada ya salamu na maamkizi Nilimuuliza.

       "My daughter🧖bado Unataka kuishi ndani ya ndoa ya huyo mpuuzi muuaji mwenye tamaa, Mateo?"

     "Siwezi kumuacha mama, ninampenda💘. Mimi na Teo tumetoka mbali, tumedumu mapenzi kwa zaidi ya miaka saba hadi hapa tulipofika ninamjua vizuri pia ninamuelewa kama anavyonijua na kunielewa." Semi mwanangu aliongea.

    "Semi mapenzi kila mtu anayataka na kuyalilia lakini kuishi na huyo Bwana msaliti mwenye tamaa naomba nikuambie vunja nazi 🥥chini maji yamwagike, achana naye tafadhali."😢 Nilimshawishi tena na tena.

     "l'cant mama💔, siwezi tafadhali ninampenda Teo, he his charming man, mwanaume wa kipekee." Alinijibu.


    "OK, Semi ninajua mapenzi yana nguvu za kuvunja vunja milima au kupasua anga la Dunia basi ninaomba nikuambie muda huu ninamwita Mwanasheria wangu nitamwambia alifute jina lako kwenye Documentary za urithi ambao kama ningeliitwa na Mungu ☁️⚰️wewe ungelirithi kila kitu ambacho nimevuna kwa jasho langu. "Nilimwambia.

   "Jamani mama!!!" 🙄Aliongea kwa mshangao mkuu.

     "Tena mali zangu zote ninaelekeza iwapo nitachukuliwa na Mola ziwaendee watoto yatima, 🧒👶watoto wa mitaani, wajane na wenye shida. Wewe hutopata hata mia mbili." Nilimwambia Binti yangu ambaye hakuonesha darili za kumwaga chozi Wala kuniomba niubadilishe uamuzi wangu.

**********

Miezi sita baadae nilikuja kusikia mtu akigonga mlango wa nyumba yangu nzuri iliyopambwa maua. 🌺🌹🌸💐🌻🥀 Nikaenda kumfungulia mgongaji kidogo nilishituka nilipomuona Semi amesimama Langoni 🚪nywele zake tipwa tipwa zimekosa mafuta yaani hazitamaniki. Nguo alizovaa kama visepe au vigagula. Binti alidhofika, machozi abubujika. 😭

     "Nisamehe mama🙊🙏🙈, Nisamehe mwanao" Alikimbilia kunikumbatia🫂 akilia chozi zito la ndimu, chozi lililojaa tongotongo.

    "Sikukusikiliza kumbe ni kweli Teo alikua ananidanganya, amenitimua ndani ya nyumba anayodai ameninunulia, amemuweka rafiki yangu Sesi kama mkewe mimi ananiona takataka na uchafu nyumbani." Alilia Binti yangu.

      "Kisa nini? Si ni wewe uliyesema unamjua na yeye anakuja vema mmedumu kwa zaidi ya miaka misaba tangu mkiwa chuo hadi ndoa imepamba moto?"

    "Mama asiyesikia la mkuu atavunjika mguu. Kila neno uliloniambia miezi sita iliyopita lina ukweli. Siku Teo alipokuja kugundua kuwa mali zote ulizoziandika kwa jina langu zimefutwa na kuwahamishia kwa yatima, wajane na wenye shida ndio siku niliyokuja kugundua rangi yake halisi, makucha yake na tamaa zake.👿Amenifukuza kama Umbwa 🐕‍🦺nisiye na mbele Wala nyuma" Semi mwanangu alibwaga chozi.😿😿🥹

      "Pole mwanangu Zimwi 🧞likujualo litakukula kidogo kidogo likumalize, heri mie mamayo nililijua Zimwi mapema kabla halijatumaliza."  Nilimfariji mwana mpotevu nikamkaribisha tena nyumbani lakini nafasi ile nono ya kupata urithi wangu hana tena na sintaibadili nia kamwe never, ever and forever."

**********
 TCHAO. 👋

Wednesday, November 20, 2024

BWANA HARUSI TAPELI

 



MASIKINI MAMA YANGU ALIITAFUNA AIBU. 


      Daegy ni jina langu na kwa bahati nzuri mie Egy Nina kazi nzuri inayoniweka mjini, kazi niliyoiridhia mimi wenyewe. Nimeajiriwa katika shirika la Ndege la Ndege, Tanzania Air way. Nimeajiriwa kama muhudumu yaani Fry attendant, kazi yangu ni kuhudumia wasafiri (Air traverer) wanaoenda kwenye mataifa mbali mbali ya Dunia:China, lndia, Australia, South Africa, Uganda, Rwanda, Burundi na Commorrow. 

Mie Daegy ninacho kisa kimoja Naomba kushea nanyi wapendao visa na Mikasa.

      Kisha changu kinaanzia mwezi September mwaka 2024 siku hiyo Mwanamama tajiri Africa Mashariki Bi. Shyrose alikodisha Fry jet, Ndege ndogo binafsi kwa lengo la kujifurahisha angani. Hakuwa pekee bali aliambatana na kijana mmoja mzuri shababi wa sura na sauti ya kipekee, nilikuja kumjua kwa majina Amboni Ambrose. Usiniulize niliwajuaje hawa wapendanao nitakujibu mimi ni Fry attendant lazima ni wajue wateja wetu.

     "Daegy keti hapa tuikate keki yetu ya furaha" Mwana a matajiri Shyrose alikua akifanya shereh ndani ya ile Ndege ndogo binafsi.

      "Asante madame, niliketi Karibu na dirisha upande wa kushoto wao aliketi upande wa kulia. Kipande cha keki, 🎂🍰kilikatwa Kisha Mwanamama akanilisha kwa tabasamu nono.

    "Happy birthday madame." 🎂Nilimwambia.

     "Thanks🥰🙏 Daegy Naomba nikutambulishe kwa mchumba wangu tarajiwa Amboni Ambrose," Alimgeukia yule kijana mzuri wa sura.

     "Please my sweet Ambrose meet Our fry attendant Daegy."

     "I'm pleased to meet you Daegy." Ambrose alinijibu kimomboo akanipiga kiss😘 mkononi, ishara ya upendo na kujali.

      "I'm pleased to meet you too nilimrudishia kiss ya upendo mkononi. Shyrose akamwambia Amboni:

    "Leo ni siku yangu ya kuzaliwa lakini pia anataka nikufanyie sapraiziment ambayo hufanywa na wanawake wachache Duniani" 

    "Waooo! Daring 😍nitaifuraia." Amboni alijidekeza.

    "Fumba macho yako Baby" Amboni alitii. Akayafumba macho yake. Shyrose akakitoa kibox kimoja kidogo kwa umbo alikifungua na kutoka na Pete moja mashallah😘yenye madini ya Almasi 💎 katikati. Taratibu na kwa madaha Shyrose akamvisha ile Pete bwana Amboni. Kisha kwa mwingi wa tabasamu Mwanamama akasema.

      "Sasa yafumbue macho yako mume wangu tarajiwa."
   
       "Waoo😻💖!" Amboni alipoiona ile Pete yenye kito cha Almasi alimkumbatia Shyrose kwa furaha wakapigana kiss😘 na kuibadilishana ndimi😉😊🥰 baada ya lile tendo la furaha wine ya Mzabibu ilifunguliwa, birauri zilimiminwa ile wine sie tukanywa kwa furaha, raha na tabasamu, watatu sie tulijihisi kama tunaelekea Jerusalem kuijenga mbingu☁️🌤️ ya raha starehe na sherehe kwa jinsi furaha zetu zilivyonoga.

____________

Madame Shyrose alitokea kunipenda na kuniamini sana siku ile baada ya sherehe aliniachia kitita cha shilingi million tano pamoja na nambari yake ya rununu.🤳📞 Aliniambia zile pesa alizonipa ni kama Asante kwa kampani. Jamani🤭 nilijiona siku ile hadi nikaanza kumuonea Gere yule hensam wake Amboni, moyoni nilijisemea 'Huyu anafaudu vingi kutoka kwa madame Shyrose'🤪

       Shuhuli ile fupi ilipofika kikomo nikafanya kurejea nyumbani kwangu kigamboni huko nikajibwaga kitandani na kulala kwa furaha. Siku mbili baadae Mama yangu Bi. Benedetha alinipigia simu akaniita nyumbani na kuniambia Kuna jambo zuri angelipenda kushea Nami. Hima hima 🏃nikaichukua Prado yangu rangi ya kijivu niliyoinunua kwa mshahara wangu mwenyewe.

Nilifika Oysterbay ndani ya mjumba wa mama yangu mwenye pesa zake, sema Baba yangu aliaga Dunia na kutuachia mali nyingi na pesa nyingi ndani ya Bank, kiwanda kidogo cha kutengenezea mikate na sabuni huko Pugu, Super market ndogo kule Barabara ya Kamata, aliacha pia majumba sita katikati ya Jiji, pia aliacha magari yake.

      Mama alinipokea kwa bashasha,☺️ tukaelekea sebuleni tuketi na kuongea mengi. Nilipoingia tu sebuleni nilishangaa kumkuta Bwana Amboni ameketi sofani kapigisha pozi miguu yake nambari nne anakunywa Whsky🍷 Bila wasiwasi kama yupo nyumbani kwake.

"Mpenzi mwanangu mimi mama yako ile miaka yote ya upweke imefikia kikomo leo nimeona nikutambulishe kwa mchumba wangu na Mume wangu tarajiwa Bwana Amboni Ambrose" 😷Jesu! Nilipigwabutwa

'Mpenzi na mchumba mtarajiwa!?' Nilijiuliza mtimani.

'Jamani huyu Amboni ana akili kweli au amerogwa!?' Sikupata jawabu. Niliishia kumtazama yule Bwana Amboni kwa jicho lamshangao sema yeye hakutaka kukutanisha macho yake yakutane na yangu. Aliishia kutazama Tv na kugugumia mafunda ya ile Whsky.

     "Ninampenda sana Bwana Ambrose tumekubaliana tufunge ndoa mwezi ujao." Mama alizidi kunishangaza. 🤭😶🤥
   
    "Mimi pia ninampenda sana mama yako Bi. Benedetha, Mungu bariki ndoa yetu ipendeze" Alipoongea hivyo mama alifurahi sana akijua Bwana Amboni yupo siriasi na hatanii.

    "Mama mbona wanishangaza yaani ukutane na mtu ndani ya wiki kisha ndoa ifanyike mwezi ujao? 🙄" Nilimuuliza Mama.

      "Ninampenda sana Bwana Amboni, ameniondolea upweke, huzuni na majonzi ya kufiwa na baba yako." Mama alijibu

    "Kwahiyo ninataka ndoa👰 ya haraka haraka, tukae ndani tuyafurahie maisha." Mama aliongea. 

     "Ma, Naomba tutoke twende pahali tukaongee." Nilimwambia mama aliyenisikiliza tukatoka na kwenda chumbani kwake.

     "Mama unamjua vizuri huyu Bwana Ambrose?" Nilimuuliza.

     "Mwanangu nimefall in love💕😍💖💞💘 sisikii Wala sielewi kwa ajili ya Ambrose. He is kind of charmistick man. Nitamjua vizuri tukiwa ndoani."

     "Mama nadhani umeingia ndani ya pango la Simba na mdomo wa Mamba bado  kidogo utaliwa." Niliongea fumbo tungali tumeketi kitandani, chumbani kwa mama.

    "Unamaanisha nini mwanangu?"🤔 Benedetha mamangu aliuliza.

  "Usolijua ni kama usiku wa kiza, huyo bwana Ambrose ana mchumba wake jinale Shyrose Mwanamama tajiri Afrika Mashariki." Nilianza kumtobolea mama siri.

    "Nini!?" 😶‍🌫️🫥 Mama alianza kubadilika, hasira juu ya komwe lake zilionekana kutuna

    "Belive me or not my Mom huyu mwanaume yawezekana ni tapeli. Anawafuata wanawake wenye pesa zao ili awaingize mitini akiisha laghai na kuwatapeli." Niliendelea kuongea.

   "Majuzi nimewahudumia Shyrose na Bwana Amboni ndani ya private fry jet, Shyrose alikua na birthday akanitambulisha kwa bwana Amboni kama mchumba wake akamvisha Pete yenye kito cha Almasi na uzuri Shy ameniambia ndoa lazima ifungwe mwezi ujao." Nilimfunulia mama ukweli. 

   "Stapenda kusikia uongo huo Daegy,😒😵‍💫 tangu lini mwanaume akavishwa Pete ya uchumba? Mbona hiyo Pete yenye kito cha Almasi hajavaa kidoleni? 🤷Wanionea wivu eeh! Wanionea wivu sababu tu nimependwa na kijana mzuri wa sura ya kupendeza machoni? Mama  aliwaka hasira.😡

     "Sio hivyo mama..... 😢" 

     "Ila... Ila unataka kunitenganisha na mpenzi wangu? Nakwambia ushindwe🤢 uregee. Ninampenda, amenipenda mapenzi motomoto huyu simuachi ng'o hadi nirogwe" 👌 Nilimshangaa mama anavyoongea 🙌

    "Tena haya mazungumzo yafie hapa hapa Usije ukamuudhi mpenzi wangu na kuniharibia mipango yetu. Kama hauniungi mkono juu ya kumpata mwanaume mzuri kama Ambrose Naomba niache na maisha yangu. Mama has life mama need to live. Mama pia ana maisha, mama pia anahitaji kuishi. " Alinifokea na kuniacha chumbani kwake akarejea sebuleni kule alikomuacha yule Conman (Tapeli) Ambrose. 

************

Ilipita wiki moja mamangu hakuongea na mimi binafsi nilikua nawaza nitamsaidiaje mamangu atoke kwenye mikono ya yule mwanaume Tapeli. Yamkini ndio tabia na mazoea yake  kuwalaghai wanawake wenye pesa zao akiisha kuwachezea angeliwabwaga na kuwaachia maumivu. Hapana kama anataka kumchezea mama yangu hapa amebuma, hafiki mbali kipungu hata angeenda mbinguni. Niliwaza lazima nimuokoe mama. 

      Ghafla nikapata wazo nikamkumbuka Shyrose yule Mwanamama tajiri Afrika mashariki, roho yangu ikaniambia fanya hima umtafute Kuna mazuri utayapata kutoka kwake aweza kuwa msaada tosha. Nikampigia simu madame Shyrose tukakubaliana tukutane LAMADA HOTELI iliyopo Msimbazi Center. Kama wazungu vile tulikutana tukaongea. 

     "Juzi hapo ameniomba millioni hamsini amedai anaenda kununua Shamba lakini bado hajanipa data juu ya shamba hili. Binafsi nimeanza kuingiwa wasiwasi juu ya Ambrose ananiomba pesa nyingi ambazo hata sijui anavyozitumia." Madame Shyrose alionesha wasiwasi wake 

   "kwanini tusimchunguze, tumchunguze ili tujue labda Kuna wanawake wengi wengine amewachezea na bado tu anaelekea kuwachezea wengine." Nilitoa wazo. 

    "Wazo lako zuri sana Daegy, mwanaume huyu atakua Conman haiwezekani anipe proposal ya kunioa mwezi ujao wakati huo huo unaniambia anataka kumuona mama yako. 🙄 Haiwezekani Daegy huyu ni tapeli." Shyrose aliongea kwa hasira. 

    "Tuliza komwe madame nimepata wazo kama utaliafiki yamkini litakua msaada kwetu." Wazo zuri liliniingia kichwani. 

     "Wazo gani hilo uniambie hata kama Lina gharama Nipo tayari kugharamia" Madame hakunivunja moyo. 

     "Fanya kumwita mimi nitajifanya mhudumu wa hii hoteli, lazima tupate majina ya wanawake wote anaowatapeli kupitia simu yake. Kisha tutamkomesha kupitia hao wanawake." Niliongea yangu. 

"Bright and beautifully. Nimelipenda wazo lako lazima tumuaibishe na kila pesa au mali aliyotapeli Lazima ataitema na kutapika mbele ya Polisi, Mahakamani au Magereza. Madame alipendezwa na wazo langu. Amboni alipigiwa simu akuje pale LAMADA. Madame akaongea na meneja wa ile hoteli juu ya mpango wetu, pesa ilifanya kazi faster nikavaa mavazi ya wahudumu wa ile Hoteli nikajifanya na mimi kama muhudu.

Ambrose walifika pale Hoteli akiwa amejaa tele, Pete ile yenye kito cha Almasi imetulia chandani, wakapiga story mbili tatu Kisha wakaagiza manywaji mie niliyebadilika mwonekano nikaenda kuwahudumia. Nilipofika tu nikafanya ujanja nikajitegesha mezani ile wine iliyokuwa ndani ya Bilauri la Bwana Amboni ikatenguka na kumwagikia Ambrose, akaghafirika. Sikupoteza muda niliiwai simu yake aliyoiwacha pale meza pasina yeye kuniona nikajifanya Naomba msamaha. Aliponiona alishangaa nimefuata nini Hotelini.

        Haraka haraka nikaenda Restroom (Choo cha kike) karatas na karamu yangu mkononi na uzuri wa simu yake haikua rocked nikafanya faster kuiba nambari za wanawake wote aliowasave. Walikua wengi yapata miamoja mama yangu akiwa miongoni mwao. Nikasave zile nambari kwenye karatasi yangu Dakika therathini kupita nikashangaa bwana Amboni yupo miguu kwangu.

     "Pumbavu 😡nilijua tu ni wewe uliyeichukua simu yangu" Alinifokea na kunipokonya ile simu.📱

    "Unadhani sintamuoa mama yako? Lazima nimuoe, nyau 🐈‍⬛wewe hauwezi kunizuia." Alinifokea tena.

     "Haya Bana tapeli tutaona kama utafanikiwa." Nilimjibu nyodo. 

    "Nimefanikiwa mengi hili  nitashindwa?" 🤪😜😛 Alijigamba.

    "Lazima ushindwe, usishindwe wewe kama nani tapeli la mapenzi😵‍💫" Nilimfokea Kisha nikaondoka na kumuacha anakodoakodoa macho ndani ya Choo cha kike. 
                   --------------
Sie wawili tukashirikiana kuwapigia simu wale wanawake mia moja tuliohisi na kudhania ni wahanga wa utapeli kutoka kwa bwana Ambrose. Walijikusanya na kwa kilio kikuu wakaeleza machungu yao ya kutapeliwa na mwanaume mtanashati mwenye ahadi nono kumbe ahadi na promise zote zimejaa uongo. Hatimaye mwisho wa mipango yetu tulikubaliana tumuumbue Bwana Amboni Ambrose siku ya harusi yake na mama yangu Bi. Benedetha. 

     Siku ya harusi ilipofika wale wanawake mia wahanga wa kutapeliwa na bwana Amboni walijipanga, wengi wamebeba mafimbo, mijeledi, mawe, kuni, chupa, viatu na kila aina ya bakora ili kumtia adabu yule mpuuzi anayewadanganya wanawake kwa kisingizio cha ndoa Kisha kuwatapeli na kuwatelekezea umasikini. 

Madame Shy pamoja na mimi tulijitenga ili tuwe watazamaji tujionee video ya bure, video ya kufunga mwaka video ya kumwaibisha bwana harusi tapeli. 

      Mbele ya mchungaj mama yangu na bwana Ambrose walikua wanajiandaa kula kiapo cha ndoa ndipo kanisa lilishituliwa na ujio wa wanawake walioshika silaha za maangamizi waliingia kanisani wakipiga kelele:

    'Bwana Amboni, bwana harusi tapeli, tapeli mkubwa' 

    'Turudishie mamilioni ya pesa zetu ulizotutapeli ukituahidi ndoa' 

    'Magari yetu, nyumba zetu, mshamba yetu umetutapeli.' Walipiga kelele nyingi mno mama yangu aliishia kutetemeka. 🤣🤑. Bwana Amboni alitazama chini kwa aibu, mchungaj na wahudhuriaji wa harusi walishangaa kelele zile. 🔊

    'Utazirudisha au hautazirudisha???💰💸 " Walimuuliza. Kwani aliweza kujibu zaidi ya kutetemeka. Lile kundi la wanawake lilianza kumpiga kwa mawe, mangumi, fimbo na kuni. Walimchania suti yake nzuri aliyonunuliwa na mama yangu. Waliendelea kumpiga na kumfedhehesha, Japokuwa mchungaj aliwasihi wasifanye hivyo lakini wapi! Hawakumsikiliza roho ziliwauma mno. 

Wakamtoa nje ya kanisa wakaendelea kumpiga kipigo cha paka mwizi bahati nzuri  madame Shyrose aliwapigia simu POLISI walifika na kumsomba hadi kwenye Diffenda lililompeleka hadi kituo cha POLISI huko nako akaandikiwa tarehe ya kupanda Mahakamani.

'' '' '' '' '' '' '' '' '' '' " '' '' '' '
Tukio lile kanisani lilimwaibisha sana mama yangu, alijifungia chumbani kwake akilia na kujutia 😢😭🥹kwanini hakunisikiliza nilipomwambia yule Bwana ni tapeli, Baya zaidi ile HABARI ya bwana harusi kula kichapo kanisani iliandikwa sana juu ya magazeti na kusambaa vibaya mno  kama moto wa nyikani 🔥. Kwenye mitandao ya kijamii, wapendao UMBEA wakayakuza yakawa marefu yaliyojaa chumvi na ndimu. 

Picha za mama zilizagaa mitandaoni📡🛰️, alishindwa kuishika simu yake azisome zile HABARI maana aliaibishwa. 

Binafsi namshukuru Mola wangu nimemuokoa mama kutoka kwenye makucha ya Simba 🦁na mdomo wa mamba.🦛 Mama yangu kama angelizubaa Angelikua miongini mwa wale wanawake wanaolia kutapeliwa mashamba yao, majumba yaliyouzwa kinyemela na magari yaliyoibwa yakauzwa black market (Magendoni) 


####### Tchao
*********
     

Sunday, November 10, 2024

BlNTI MADEKEZO

 


    "Sabi." Mama wa kambo aliniita kwa sauti ya juu yenye kuniogopesha. 

     "Abee Mama." Nilimwitikia Mama wa kambo. 

     "Embu nenda ukaoshe vyombo, upugute deki, ufue nguo na ukiisha maliza ukateke maji Kisha upige pasi nguo za Fatuma mdogo wako. Mama wa kambo aliongea kwa ukali. 

      "Sawa Mama nilitii kwa unyenyekevu. Ndivyo ninavyoishi na Mama wa kambo tangu Mama yangu aage dunia miaka kumi na misaba iliyopita sijawai pata amani, ni mwendo wa kazi na makazi lukuki  tena kazi nzito kutamka pale nyumbani. 
  
      "We Sokwe embu rudi hapa," Aliniita jina baya la wa nyama wa Porini

       "Abee mama," Niliitikia na wakati huo huo nilikua nishafika  mlangoni ilibidi nirudi maana kama ningelikaidi mwenzenu ningelikiona kilichomtoa Kanga manyoya, 

        "Nataka ufanye kazi haraka ukiisha maliza kazi nilizokugea haraka uende Sokoni kununua mahitaji ya nyumbani pia utaenda mashine kusaga yale mahindi uliyoyaloweka Jana." Duh! Sabina  mie Binti wa kazi na makazi

    "Sawa Mama" haraka haraka nilienda kujishuhulisha na kazi za pale nyumbani. 

       Wakati Fatuma anajisomea na kudekezwa na mama wa kambo mie ambaye hata baba yangu hakutaka kunilinda niliishia kuteseka kwa kazi nzito, mapigo na mapigiti kama ngoma, matukano makali kama sauti za redioni. 

Nilipomweleza baba yangu mzazi kuhusu kadhia anifanyiayo mama  wa kambo kwani baba mzazi alijali kilio changu aliishia kunipa adhabu kali ya kufinywa mashavu yangu kwa kutumia kisu kikali kilichonitoa makovu mazito ambavyo hadi leo nikijitizama kwenye kioo ninalia masikini. Embu niambieni jamani kama baba tu ameshindwa kunilinda na kunitetea ni Nani atakayeweza kunilinda na kunitetea?

Fatuma mdogo wangu alikula vizuri, alivaa vizuri, alideka mtoto akadekeka na kupendeza. Zawadi nyingi zilimiminika chumbani kwake akajiona Malaika pendwa.

 Basi siku moja mie Sabina baada ya kuchoshwa na mateso ya pale nyumbani roho yangu ikaniambia 'Toroka mwaya utaendelea kuishi katikati ya haya mateso hadi lini? Vaa yako tu inakunyanyasam, utavaa kaukanikuvae hadi lini? Miguu imepigwa Jua hadi imeota sagamba. Tumbo launguruma njaa na kiu, haupakai mafuta au sabuni mwilini zaidi ya kupakaa tongotongo na machozi.' Jaman!! Chozi lkanimwagika mie Sabina. 

           Binti nilidhamiria kutoroka na kutoroka huko nitaenda popote pale penye maisha. Labda Posta, Mnazi mmoja au Ferry nikajiunge na machokoraa na ombaomba nijenge urafiki nao. Labda  Kariakoo, Gerezani Muhimbili au, Manzese nikajiunge na magenge ya wauzao Unga (teh teh teh 😅😅😂 SIO Unga wa ngano au Sembe bali ni Unga special).  Labda nikimbilie Buguruni Sheli, Tandika Sokoni au Mwananyamala nikajiunge na Dada poa niuze uchi wangu. Uwii!! 😭😭Naogopa kukufuru Mungu, Mwili wangu sio hazina ya Ibilisi mwovu mwili wangu ni Hekalu takatifu la Bana Yesu. 

    Basi mie huyo hima hima kupanga vinguo na vigangura vyangu nikajiwekea kwenye fuko la Maliboro Kisha niondoke Oysterbay. 

      Vuuuuu,  Mlango wa chumba changu ulifunguliwa ovyo. Kha! Nilishituka na kutetemeka nilipokuja kugundua mbovu aliyeingia ni Fatuma moyo wangu ulisuuzika Maana Angelikua ni Step mother ningelikoma kutoroka, ningelichomwa na kuiva kwenye maji moto yanayochemwa ndani ya pipa, Ningelipigwa kwa vigigi, vigogo na kuni nzito hadi maji niyaite Maa! Ningelikesha naosha na kuogesha  kuta za mjumba wetu wote kuanza sakafu hadi juu ya Dari We! Naogopa mie. 


       "Sabina nipo njia panda mie. " Alianza kuongea mara baada ya kunibamizia mlago wa chumba changu

    "We naye ndio nini kunishitua na kuniweka roho yangu juu  tipwa tipwa hadi nidondoke chini puuu povu kinywani kama nina kifaa" Nilimjibu kihasira  kwambalii kilinichota. 

     "Wewe embu nisikilize mimi kisha unipe ushauri sitaki mahasira yako" Binti wa kumi na saba alinijibu mie  wa ishirini na tatu. 

    "Embu ongea haraka mie nina kazi za kufanya" Sikutaka mengi maana ningeliyaleta mengi angeyapeleka kwa Mamaye na Kwa jinsi alivyo domo la uongo na umbea atafurahia akiona ninapigwa, ninatukanwa na kufedheheshwa. Jaman ndani ya nyumba ya baba yangu niliishi kwa hofu na amani kupotea.

   "Sabi mie Nina mimba ya Dani  Boyfriend wangu na Dani kaikataa" Aliongea akiyaregeza macho ili kuyabembeleza yatoe chozi na kamwe macho yake hayakumuunga mkono

   "Toba! Fatuma" Nilishituka. 

    "Ndo' Maana nimekwambia Nipo Dillema nisijue lakufanya nipe ushauri au niitoe?" Binti madekezo aliropokwa na kujikurupusha. 

     "Fatuma wewe Binti wa kumi na saba tayari ushabeba mimba? Yote ni shauri ya deko na madekezo kutoka kwa mama" Nilimjibu yeye kaketi kimya na kujilaza kitandani atazama juu darini kitopu chake chaonesha kitovu alichokibana kwa hereni yenye kito cha Almasi. Suruali yake aina ya Jeans ina michano chano mfano wa tambaa la deki. 

    "Sielewi Sabi nasema Sielewi" 

     "Kwani Baba na mama wanasermaje?" Nilimuuliza

     "Hawajui, they know nothing about it" Aliongea kiswahili kilichochangizwa kimomboo. 

    "Ndo' uwaambie kwanza na uwasikilize wanasema nini" 

     "Kwahyo wewe hautaki kunishauri eti eeh! Sawa" Yallah! Fatuma hakunipa nafasi ya kuongea neno akafanye hima kutoka chumbani kwangu haraka haraka nikamsikia akishuka kwa kasi ngazi za horofa ile ya pili kuelekea sebuleni. Moyoni nilihisi anaweza fanya ubaya maana Binti mcharuko yule hajatulia. Nikaacha na na mpango wangu wa kutoroka nikamfuata. 

     "Baba na mama Kuna jambo ni Naomba niwaeleze" Mh! Kwangu yamemshinda ndo' ayakimbize Sebuleni kuwaeleza wazazi. Fatuma mdogo wangu kweli kuishi kizungu Kuna shida. 

     "Eleza Binti yetu, Our gorgeous, Our beautiful life and Our everything" Mama wa kambo aliporomosha kimomboo kumsifia bintiye. 

     "Baba na mama mie nimekamta mimba ya Dani Boyfriend wangu na Dani Boyfriend ameikataa." Aliongea maneno yaliyowashitua Baba na mama wa kambo, wakati huo mie Sabina nimejibanza moja ya kona ya pale sebuleni ninasikiliza. 

      "Unasema kweli Fatu" Unasema kweli wewe una Mimba? " Baba alimuuliza Fatuma

    "Nilete kipaza sauti nipaze sauti au nilete Sabufa nifungulie sound ya juu?" Binti madekezo alimjibu vibaya baba Kisha kwa madekezo akaongea tena. 

    "Mama nitoe au niilee? " Mama wa kambo akamjibu Binti madekezo

     "Hapana Binti yangu usiitoe hiyo mimba sie wazazi wako tutakusaidia kuibembeleza" Sikuyategemea yale maneno yaliyomtoka step mother, nilitegemea angemkaripia na kumponda hadi mtoto ajinyee tumboni. 

        "Itunnze mwanangu mtunze huyo Malaika ni Zawadi yako, Zawadi hadimu." Baba aliunga mkono. Ikawa hivyo basi Mie Sabina nikalifuta wazo la kutoroka safari hii nikachukua jukumu la kumlea Fatuma mjamzito. Kila shughuli au tamanio lililohitajika nililihangaikia, Grocery, dukani, Sokoni au kumsindikiza Clinick. Iwe kumpikia atakacho  na kunimwagia usoni kimkeracho akinilaumu nampikia uchafu, dikodiko rojorojo na tope. Ah! Iogopeni mimba baguzi, 

     Kumfulia kila alichochafua au kutapikia kumuogesha na kumhadithia soga za kina Sungura na Fisi ilimradi tu mdogo wangu aridhike, Hatimaye siku ya kuingia Leba ilifika akajifungua mtoto wa kiume akampa jinale Patrick bado tu mie Sabi niligeuzwa nyanya wa kumlea yule mtoto, Nikimwogesham nikimfulia nikimbadilishia Pampasi, nikimlisha na kumbembeleza hadi mwili wangu ukanichukia kwa jinsi nilivyojitoa ajiri ya Fatuma na Patrick mwanaye. 

_____________

   Basi baada ya mwaka mmoja kupita nikiwa nakabembeleza katoto tayari kulala, aya sasa nikakalaze kitandani.  Nilipoingia chumba cha Fatuma mamaye P nilikutana na Mastaajabiko, Binti deko alikua akipanga na kuzipangua nguo zake alizoziweka kwenye begi, alizozihitaji na kuziondoa zile asizozihitaji

      "Eh! Nambie mwenzangu kupanga na kupangua Safari ya wapi Sasa?" Nilimuuliza?"

    "Sikiliza Sabi. " Aliongea kwa haraka. 

    "Hivi sasa mie nishatimiza umri wa miaka kumi na minanae, umri wa kula Raha na starehe za ujana, nilichukia sana kitendo Cha kubeba mimba iliyoniharibia starehe zangu. Sasa Wacha nikazamie Nairobi nikaponde Raha na Boyfriend wangu Dani." Aliongea Kwa kujiamini.

  Dani Tena!!🥺 Nilishangaa.

      "Fatuma umerogwa wewe si mzima. Yaani unataka kuondoka uende Nairobi na huyo Dani aliyemkataa Patrick, baya zaidi tangu Patrick amezaliwa hakuna siku ambayo Danny amekuja kumtazama sembuse kumletea Pampasi na visepe" Nilimfokea madogo wangu ambaye hakuonesha darili za kujali.

   "Tafadhali Sabi usinifokee" Alielekea dressing table kujichora chora lips rangi nyekundu mdomoni.

    "Nakuachia Patrick umtunze, umlee akue apendeze. Ole wako nikirudi nisikie ati ulikuwa unamtesa " Teh teh teh, 🤣 nacheka kama ni mazuri. Binti deko yamkini alirogwa akachanganyikiwa.

     "Unaongea Kwa kutumia amri na mamlaka, Mama gani wewe unayemtelekeza mwanao kwasababu ya mapenzi ya kinafki. Fatuma rejesha akili ubongoni usitumue uchi wako kufikiria" Nilimtusi.

     "I don't care." Alinikoromea. Akaitazama saa  yake mikononi "Ninachelewa, ndege ya kwenda Nairobi itaniacha." Aliongea haraka haraka kama Mwendawazimu. Akalikokota kokota Begi lake haraka haraka akashuka ngazi za horofa ya pili, Uber ilikua ikimsubiri, Dani alikua akimsubiri pia. Akapakia na kutoweka hata kumbusu mwanae alishindwa. Mie Sabina nikaeleka Sebuleni pale Baba na Mama wameketi.

     "Baba na Mama hivi mnajua Fatuma amebeba Begi lake la nguo na kutoweka?" Nilipaza sauti Baba na Mama wa kambo wakatazamana Wala hawakujishuhulisha kunijibu.

      "Baba na Mama Fatuma ameondoka na kumuacha mwanaye mikononi mwangu." Nilirudia kuongea.

    "Hivi wewe nguruwe mweusi hauoni kama tupo kujadili jambo muhimu." Mama alifoka.

    "Tafadhali ondoka ustuharibie project zetu. Mambo ya Fatuma hayana umuhimu Kwa Sasa" Baba alifoka pia wakaendelea kusaini saini Document ambazo hata sikujua zinahusu Nini? Nikaondoka pale sebuleni  nikaeleka chumbani kwangu na kuubamiza mlango wa chumba changu 'Mbaaa'  mtoto alishitukana kuanza kulia aliposikia sauti ile kubwa ya mlango.

      "Nyamaza mwanangu nyamaza kuanzia Leo wewe na Mimi, Mimi na wewe. Nitakua mama yako milele. Nilimwambia Patrick. Basi kuanzia siku ile Patrick Akawa wangu na Mimi wake, nikahangaikia ili na lile Kwa ajiri yake. Akisikia njaa mama yake nilimwandalia uji, maziwa, maji safi, matunda na juisi. Nilimwogesha mwanangu, Nikimfulia, nilimbadili Pampasi, nikamlea mwanangu aliyekua taratibu.

          Bahati nzuri Sabina mie Nina akili za maisha, nikafungua ubanda  yaani Gengela mahitaji ya jikoni nikauza nyanya, vitunguu, hoho karroti, mbogamboga, mkaa na pia nilipika mabumunda wateja wale wafurahie kazi ya mikono yangu.

Mungu hamtupi mja akajitokeza huyu mkaka jinale Thomasi mie namwitaga Mwanasheria.' Yeye ni Hakimu wa Mahakama ya mwanzo Ilala.  Ati Toma akasema ananipenda. Teh teh  teh🤓 😘🤣🥰 Mie bila kinyongo nilimkubalia na Kwa jinsi nilivyoyachoka maisha ya pale nyumbani Acheni tu. Toma akanitaka tuishi wote tupike na kupakua.

      Ulikuwa ni wakati wangu, wakati wa maringo kumuonesha Baba na Step mother kwamba na mie n'shapendwa. Sikuwaambia goodbye bin kwaheri nikabeba vyangu na kumbeba Patrick mwanangu tukahamia nyumbani Kwa Mwanasheria. Maisha matamu yakanifuata.

________________
   Miaka mitano kupita nikaja kusikia mtu akigonga ovyo  mlango wa sebule yangu mie niliyekua namenya matoke. Nikadamka pale sebuleni kitumbo ndiii🤰 bado miezi mitatu tu niingie Leba. Nilielekea kuufungua mlango Patrick mwanangu akiwa amenishikilia miguu asitake kuniacha.
   
     'Eh! Toba!' Nilishangaa 🥺🤭Fatuma huyu huyu Binti madekezo karejea  baada ya miaka Mitano ya kuponda raha na starehe. Karejea kawa mkondefu asitamanike, kadhoofu tena kapooza  hata inzi wasitamani kumsogelea.

        "Nimekuja kumfuata Patrick mwanangu." Hata salamu haijui yeye anachojua ni jina la Patrick tu.

      "Patrick yupi au umekosea njia." Nilimuuliza Binti deko.

    "Si huyo chini ya miguu yako, tafadhali Sabi usinizuie kumuona mwanangu, ni haki yangu" Alibwata.

     "Haki hiyo kwioooo!😹😹 Nilimbetulia mdomo na kumfyonya mxiuuuu😣.

    "Hakuna mtoto aitwaye Patrick hapa, labda huyo unayemtaja alikufa zama za kale za mawe." Nilimpa vidonge vyake.


"Mpumbavu wewe miaka Mitano imepita sasa hujawai kumkumbuka mwanao Leo hii baada ya starehe kukutema ndio umeona Bora uje uteme mate yako mlangoni kwangu, Bibi umechelewa.👌

       "Sabi nitaenda kumuona Mwanasheria." Aliropokwa.

        "Eeh muone na ukae ukijua na mie ninaye Mwanasheria wangu" Sikutishika na yule nguruwepori. Akaondoka amejaa hasira.

____________

        Niliitwa Mahakamani, yule mshenzi Fatuma eti alinifungulia kesi akidai ati nimekataa kumruhusu amuone na kumchukua mwanaye Patrick. We! Mbona mjadala uliiva mahakamani nilizipika kelele Hadi zilipikika, nilitema cheche Hadi moto uliwaka, nilimpandishia ruhani👿👾 Hadi shetani 👹wake akaomba poo, yaishe. Mahakama ilinielewa na Fatuma akaambiwa ingawaje mtoto amemzaa lakini sio wake. Hakuna mama mwenye akili ambaye angefanya maamuzi ya kijinga kumtelekeza mwanaye ati kutafuta starehe na Raha za ujana.

      Kesi ikaunguruma mie Sabi nikashinda ile kesi, Patrick Akawa mwanangu tena Toma akanishauri  nimuadopt kabisa Ili awe wangu halali. Jamani mie Sina hasara maana wahenga walisema 'Aso na mwana akumbate jiwe, kizuri kiuze. Ukisema chanini hiki kumbe wenzio tunasema Dhahabu hiyo.😹

Wacha nimfunike shuka Patrick mwanangu, kesho afanye Kuwahi kindergarten. Mwanangu kimomboo kimeanza kufanya kazi mdomoni mwake ati anasema:

"I LOVE YOU MOM💗"🥰😘🤣. Na mie ninamjibu P. Wangu

"I LOVE YOU TOO MY PRECIOUS BOY💕. NINAKUPENDA💖, NINAKUJALI NA PIA NINAKUTHAMINI P. WANGU"

-------------
TCHAO.💕

 

 love is all Given and found,🌹 It's all around,🥰 It's hard to tell about,😍 Easy to show,🤩 One sure thing when you feel it You kn...