Saturday, September 13, 2025

GOOD BIE DARING CASANDRAH





 "GOOD BYE MY BABY💕, 


 GOOD BYE CASANDRAH"


Siku ile, siku nzuri kwangu, nilipata nafasi ya kutembea🚶 maeneo ya Pugu Sekondari👩‍🏫, sehemu hiyo ina vichaka vingi uzuri hakuna hatari kama vile uwepo wa Nyoka 🐍au wanyama 🐅🐕🐒 wasumbufu, siku ile nilitoka kanisani⛪ na kutabiriwa baraka tele zitakazonifuata.💰


      Mkono wangu wa mashoto nilishika simu yangu aina ya iphone 13, 📱simu ya bei gharama, sema nilijichanga sana nipate kununua ile simu, nilikua nachati na marafiki zangu, wafanyakazi wenzangu, ndugu na jamaa. Ghafra ilipita Gari aina ya Prado yenye rangi nyeupe, sikukumbuka nambari ya ile Gari nilishtuka tu kuona napokonywa simu mkononi. Ikanyakuliwa mithiri ya Nyau anayenyakua Panya.🐀🐈


     "Mwizi mkubwa wewe!" Nilimpigia kelele🗣️ jamaa aliyeniibia simu, nikafanya kukimbilia ile Gari ili anirudishie simu yangu lakini nilikwisha chelewa jambazi lile lilikwishatoweka na simu yangu.


     "Mshenziii😤" Nilitukana, hasira ikiwa imenikaba kooni, nilitamani nilikamate na kulimeza lile jambazi. Hivi mtu huyu anajua uchungu wa kuibiwa Mali ya kitanzania niliyonunua kwa gharama ya Millioni saba.... Mxiiiuuuuu😡, akatombw** mbali, Mamae.🫥😡." Nililaani vibaya.


Ndani ya ile Gari waliketi Majambazi wawili, mmoja akiwa nd'o yule mnyakuzi wa simu mnyakuzi huyu alikua na mwili wa chuma, mbavu nene, mwili wa mazoezi makali na urefu wa Goliathi. Mwenziwe kidogo hakuwa na mwili wa mazoezi japokua wote walionekana kuwa makatili.


    'Teh teh teh 😂 😂 ' Mnyakuzi wa simu akicheka kwa kebehi aliinyanyua simu yangu na kuichezea.


     'lmekula kwake," Yule Dereva ambaye hana mwili wa mazoezi💪 alichangia hoja.


    "Kudadeki, hapa Mjini kichaa wangu'😂" Jambazi lilicheka tena Gari yao ikatembea mwendo wa kinyonga.


    "Embu ngoja nitest nione kama Mali Bado ni mpya tena swaafi." Jambazi lilifungua Screen ya simu yangu.


        "Chuma Og mjumba!" Dereva alimuunga mkono Jambazi lilioanza kuiwasha simu yangu.


        "Toba!"😕 Macho yalilitoka lile jambazi mara baada ya kuiwasha ile simu yangu. 


        "What a problem!? Frank." Dereva alimuuliza Jambazi mwenziwe.


     "Picha ya Girlfriend wangu Casandrah inatafuta Nini kwenye dude la hili jitu." Frank alimuonesha picha ile Mudi kwenye simu yangu.


       "Duh! Mwanangu Frank ushaibiwa." Dereva alimwambia Jambazi Frank.


       "Mudi embu isimamishe Gari nasema hii njemba itanikoma SIKU ya Leo, 😠kama hajatembelea magoti atatembelea matako yake." Hasira za ghafla zilimkaba Jambazi Frank. Mudi aliisimamisha Gari ambapo Jambazi Frank alitoka na kufunga mlango kwa  kuubamiza. Frank alianza kutembea kwa kasi kunifuata mie niliyechoka kuikimbiza ile Gari ya Majambazi. 


Nilipotazama mbele nilimuona yule Jambazi akinijia kwa kasi ya kimondo🌠 kilichoanguka kule Mbozi Songwe. Alinikaribia, mbona niliogopa baada ya kuuona mwili nzito kama wa mwana mieleka aitwaye John Cena. Misuri yake ilikua imeshiba kama Commando 💪John Baba Jane. Uso wake ulikua, mkavu na mzito wenye mnuno na 😨hasira zilizoelekezwa kwangu kama mtu aliyetafuna Pilipili mbuzi mbichi. Mbona niliogopa.😧


    Niligeuka njia kuelekea upande mwingine ili kumkimbia yule jamaa aliyeniogopesha mie mwenye mwili kimodo na kichwa kidogo kama Pera,🥑 nimekonda na kudhoofika kama fagio la chelewa, mrefu kama mlingoti wa umeme. Nilimkimbia na yeye hakuacha kuongeza kasi ya kunikimbiza,🏃‍♂️woga ulinijaa. Sijui alifuata nini baada ya kuniibia simu, sijui amefuata pesa ambazo hazikua nyingi mfukoni mwangu zaidi ya shilingi elf hamsini.


       Alinikimbiza, akanifikia kisha akanisukumia teke moja la nguvu miguuni. Ile ngwara ilinitupa chini ya vumbi 'puuu' kama gunia la mahindi makavu🌽 yaliyovunwa shambani. Duh! Niligeuka vumbi.


      "Niache! Niache tafadhali! Nataka Nini kwangu!?" Kama unataka pesa chukua, chukua niachie uhai wangu." Nilimpigia kelele maana alikwisha nialamia na kunikalia mwilini mwangu.


     Nguuuuuu' alinilisha ngumu moja nzito ya chuma, nilisikia maumivu, Nyota na vimulimuli vilinicheka.


     "Nieleze kwanini ndani ya simu Yako unaweka picha ya Girlfriend wangu" Alinionesha picha niliyopiga na Mke wangu juu ya simu yake na yangu.


     "Huyo ni mke wangu Casandrah." Niliongea kwa kugugumia maumivu.


    "Mke wako!? 😠 Mshenzi wewe yaani Girl friend wangu awe mke wako?" Safari hii aliniacha na kunipa uhuru wa kuamka pale nilipoangushwa.


     "Casandrah ni mke wangu na Pete ya ndoa hii hapa mkononi." Nilimhakikishia lakini Bado alikua njia panda haelewi akiitizama picha iliyojuu ya screen ya simu yake na simu yangu.


     "Nitaaminije, embu ngoja, nimepata wazo." Alianza kutuliza hasira.


     "Nampigia." Akaiwasha simu yake na kuiweka loud speaker.akabinya vitufe vya kuita nayo ikapokelewa.


      "Hallow Baby!"  Sauti ya mke wangu ilisikika kwenye ile loud speaker. 🎙️🔊


     "Daring Casandrah ninakumbuka ulinibembeleza sana tutoke  siku moja usiku twende tukajaribu kuvunja apartment na kuiba Mali za watu. Leo usiku saa tano nitakua na nafasi naomba usikose."


     "Waoo! Asante mpenzi Leo itakua ni siku yangu ya furaha." Casandrah mke wangu alisikika.


     "Ok. Baby jiandae Frank alikata simu. Nikashusha pumzi ndefu😤 nisiamini kama kweli mie wangu Casandrah anatamani kushiriki ujambazi baya zaidi mke wangu wa ndoa anachepuka kisirisiri. Astaghfurilah!! Mazito ya Duniani.


      "Niite Bwana Frank. Jambazi alijitambulisha kwangu.


    "Zingo just Zingo." Nilijitambulisha pia ningali nimeshikilia komwe langu lililopigwa  hadi kuvimba nundu nzito kama ya Ngamia.


      "Usiku wa Leo mimi na Casandrah tutatoka kwenda kuiba kwenye duka kubwa kwahiyo jitahidi uwepo ndani ya duka ukiwa umefichama."


    "Duka gani!?" Nilimuuliza


    "Duka lako la nguo." Alinijibu.


    "Unalifahamu!?" Nilimuuliza.


    "We fata maelekezo, duka lako si lipo Chanika? Saa Tano usiku uwe tayari umefichama ndani" Yule mjumba aliniuliza. Nilimuitikia kwa kutikisa kichwa.


    "Ikigundulika kama ni mkeo kweli unatakiwa kumpa talaka yake."


    "Mmh! Niliguna, au ni mtego, nategewa? Tisa kumi nilihitaji kuhakikisha.


    "Mimi nikose, yeye akose na wewe ukose..... Wote tukose." Jamaa alisisitiza.


     "Nikabidhi Simu yangu." Niliomba, akanirudishia kisha akaondoka zake akiwa ameniachia katikati ya lundo la mawazo juu ya matukio yaliyotendeka siku ya Leo.


*************


Mke wangu Casandrah aliniaga kuwa anaingia Night 🌃 shift, yeye ni Daktari katika Hospitali Moja ya Serikali, inayoitwa Nguvu kazi. Nilimuaga ingawaje mtimani niliyaacha machungu yangu ambayo sikutaka kumweleza. Aliondoka nami nikamsindikiza kwa macho ya wasiwasi ambao hakugundua zaidi ya kuniona zaidi natabasamu na kuionesha furaha ya bandia.

 


Kama milivyoelezwa na jambazi Frank saa tatu kamili tayari nilikua nimefika ndani ya duka langu, duka kubwa la nguo, viatu na mapodozi. Nikajificha nje sehemu ambayo giza nene lilinikumbatia asingeliniona mtu sembuse Popo au bundi. Uzuri mie niliwaona wote wapitao mwangani nikatulia hapo nikiusubiria ujio wao.


     Kama zari saa Tano kamili nilimuona jambazi Frank na mke wangu Casandrah wakinyata na kuelekea pahali mlango wa kuingilia duka langu la nguo, nilitulia kama maji mtungini  ili nizione harobaini za wale wezi kwa kutumia ufunguo wa bandia Jambazi Frank aliweza kufungua mlango wa Duka langu, wawili wale wakaingia, sikua na haraka isiyo na baraka nikasubiria.


     "Mmh! Mpenzi Kwanini umenileta hapa?" Casandrah aliuliza akiwa ameshikwa na wasiwasi.


      "Yes, nimefanya hivyo kwa sababu pahali hapa kuna Mali nyingi sababu pia Leo ni siku yako ya kwanza kuiba mineonelea haa ni pazuri na sio mbaya kukuleta." Frank Aliongea bila wasiwasi. Frank akaanza kujichukulia magaunu, mabrouz na mashati yaliyomo ndani ya Duka langu lakini ghafla Casandrah aliiona picha kubwa juu ya Meza Ofisini, ilikua ni picha yetu tuliyopiga siku ya ndoa. Haraka bila kupoteza sekunde  Aliikimbilia ile picha akaifunika juu ya  Meza. Akiamini labda frank hajaiona.


    "Casandrah tizama hizi sketi nzuri mno ni kama zile nilizokununulia last monthly " Frank alimwambia Casandrah.


    "Yes Daring." Casandrah almwitikia Frank. Ghafla tena aliiona picha yetu ikiwa imetundikwa juu ukutani akafanya faster kukimbilia na kuishusha chini ya Meza. Akiwa ni mwingi wa wasi wasi   Frank alimfuata Casandrah ambaye safari hiii Presha ilianza kumziddi nguvu.

  

Sijui anatunza wapi Pesa huyu boya. Frank alimwambia Casandrah Kisha wakatazamana zaidi ya sekunde stini.


     "Labda anatunza kwenye safe." Casandrah alimwambia Frank.


     "Liko wapi hilo safe!?" Frank alimhoji kimasihara.


      "Lipo pale." Casandrah alinyoshea mkono pasina kujua kila neno atamkalo ni mtego kwake. Sijui ni tamaa! Lakini hapana, yamkini Casandrah alijisahau. Frank na Casandrah wakaelekea pale kwenye safe yangu ninayotunzia hella frank akajaribu kuifungua lakini kwa bahati mbaya hakugundua nambari za Siri akafanya kumtazama Casandrah wawili wale wakatabasamu.


     "Hapa tutakua tumefeli maana hatuijui secrete number ya hii  safe.


    "Hapana, hatujakosea wewe ingiza nambari 09897 Casandrah alitoa maelekezo na Frank akafanya kama alivyoambiwa afanye. Safe yangu ikafunguka.


    "Great! Casandrah kumbe wewe ni genius😆👊 unaakili sana pia unafa kwenye mishe zangu zingine." Frank akifurahia baada ya ile safe kufunguka wakazikuta pesa takribani million Tano. Akazichukua zote na pia kulikua na Pete yangu nzuri yenye kito Cha Almasi, Pete niliyachiwa na Baba yangu mpenzi kabla mauti kumkuta.


     "Lakini Casandrah hivi umeijuaje nambari ya Siri ghafla tu safe linafunguka." Frank aliingia wasiwasi.


      "Nilikisia mpenzi vitu kama hivi havinipi shida." Casandrah alijitetea kwa kujing'ata ng'ata. Wakati huo Frank Alisha chukua pes zangu nyingi.


      "Hii Pete tukiuza nakwambia tutavuna pesa mapesa.😆"


    "Si chini ya millioni sabini my wangu." Casandrah aliunga mkono. Ghafla walikuja kusikia sauti ya mlango wa lile duka, wote wakaingiwa woga mzito.


     "Nasikia mtu akifungua mlango." Frank alitoa tahadhari.


      "Ndio nahisi ni mwenye duka, embu tufichame." Casandrah alitoa ushauri, haraka wakalirudisha liles afe langu pahali pake. Kila mmoja Alikimbilia pahali akafichama. Wakati Frank Aliikimbilia kwenye makusheni yaliyotundikwa ukutani. Dayana aliingia chini ya Meza kubwa iliyo mule dukani. Jinsi alivyofichama alikua na uwezo wa kumuona aingiaye au atokaye ndani ya ile nyumba.


Niliingia ndani ya duka langu kwa tahadhari isije ikwa mtego nisije pigwa nodo za kichwa na kupotez uhai wangu. Moja kwa Moja nilinyosha hadi Ofisini kwangu huko niliikuta picha nyingine imelazwa juu ya Meza Nikijifanya kushangaa baada ya kufika pale juu ya Meza.


     Ghafla nilitetemeshwa na sauti iliyotoka nyuma ya mgongo wangu.


    "Mume wangu mpenzi." Ilikua ni sauti ya Casandrah. Nikajifanya kushituka.


     "Casandrah unatafuta nini usiku wote huu dukani." Nilimuuliza kwa kujifanya sijui kinachoendelea.


       "Baby umesahau kesho ni siku ya Valentine!? Nimekuja kuchagua viwalo bila kukupa taarifa ili nikusapraizi kwa chaguo zuri la gauni na kiatu poa." Kabla sijamjubi Casandrah tulisikia anguko la chupa sehemu yaliyopo makusheni


Paaa'! Mimi na Casandrah tuligeuka kule mlio wa chupa iliyoanguka.    


    "Umekuja na mtu!?" Nilimuuliza 


     "Hapana, labda ni jambazi. Baby embu piga simu Polisi waje walikamate." Casandrah alitoa ushauri. Hapo ndipo moyo wangu ukaniambia yatosha wacha nimwage unga wa ugali chini ya udongo


   "Unisapraiz mimi au umsapraiz Bwana Frank." Alishituka aliposikia nalitaja jina la Bwana Frank.


     "Frank popote ulipo jitokeze tuzungumze na kuyamaliza." Lile jitu lenye mwili wa chuma lilitoka mafichoni. Hakika Casandrah aliweweseka, mkojo ulimchuruza na meno yaligongana.


    "Nini kinachoendelea mbona sielewi!!!?" Casandrah alikua kama yupo ndotoni akituangalia sie wawili tuliomwangalia kwa jicho la hasira.


   "Casandrah, sikujua kama ungenifanyia hivi yaani unanisaliti na kupanga mipango michafu juu ya maisha yangu." Niliongea.


    "Nisamehe Mume wangu."Alipogundua kosa lake akaomba msamaha.


     "Kwa hiyo huyu ni mumeo si ndio!? Na mimi ni nani kwako?" Bwana Frank alimshitua Casandrah.


     "Mwanamke una roho mbaya wewe, mimi nilijua kuwa nipo pekee yangu kwako nilijua nimepata girl friend mtulivu kumbe unanichanganya na mwanaume mwingine baya zaidi unataka kuniitia Polisi." Casandrah alihisi Dunia inamwangukia.


  "Tena una roho ya kikatili." Niliongea neno.


     "Umeingia na boyfriend wako ghafra unamgeuka unanishauri tuite Polisi ili wamkamate. Casandrah nakwambia hivi tulikwisha kushitukia mapema.


    "Mshenzi huyu ananiruhusu vipi nimwibie mume wake? Nifungue self la mume na kuchukua kila kitu." Frank aling'aka.


    "Sikiliza Casandrah kuanzia Leo mimi na wewe imeisha hiyo, rejea nyumbani ukabebeshe Kila kitu kilicho chako. Nisikuone." Sikuhtaji kuongea mengi.


    "Nisamehe Mume wangu, nisamehe Frank!"


    "Usilitaje jina langu bure, imeisha hiyo.... Mimi na wewe basi!" Frank alimkataa Casandrah.


    "Wote mnanikataa sijui wapi nitakwenda." Alijitetea.


     "Ondoka tafadhali hatuna muda wa kupoteza kujadiliana na msaliti mkubwa kama wewe." Niliongea  Casandrah aliondoka chozi likimbubujika.


     "Asante Bwana Frank umenionesha upande ambao sikujua kama nitakuja kuuona siku Moja." Nilimshukuru Bwana Frank.


     "Njia mbili zikimshinda Fisi uchana msamba. Yamemkuta msaliti mwenye tamaa." Frank alinipa mkono wa shukrani.


*********


TCHAO 💖 

👋👋


**********

No comments:

Post a Comment

BEKA

 SURAYA TATU                        “AKIPITA ATAJIPITISHA.” Beka akawa member wa kampuni ya SIGA, akipelekwa hapa na pale kulinda mali za ma...