HERENI ZENYE KITO 💎CHA KIJANI💚 KINACHONG'AA (EMERALD GREEN) ZILISABANISHA NIJUE MUME WANGU ANACHEPUKA NA SHOGANGU WA DAMU.
Mie na Boazi tulijuana tukiwa Chuo kikuu cha Dar es saalam. Campus ya Mlimani, mapenzi yetu yalizaliwa yakakua na kumea hadi kuelekea ndoa👰 na maisha matamu ya kutamani Sha. Kwa hakika mwenzangu maishani mwako ukimpata yule wa kukupendeza moyoni💓, yule anayekuwaza wewe tu, mwenzangu utajihisi umenunua ☁️Mbingu ndogo ya Jerusalem au Makka🏞️🕋
Naitwa Queen👑 Moletta. Mie Queen ninaye shoga yangu anayeitwa Majulla👩❤️💋👩 ni shogangu tangu kinda kindaki hadi maisha yetu ukubwani. Tulipokua chuo Majulla alizoea kunipamba kwa sifa kemkem yote juu ya Boazi Boyfriend wangu.🤾
"Usije kumuacha au kumsaliti Boazi Queen Molleta, Boazi ni miongoni mwa wanaume wachache wanaojua kupenda, kuthamini na kujali."😍 Mie Queen nikajiona sasa n'shakua Queen Elizabeth kutokana na sifa kemkem juu ya Boazi.
"Mtazame alivyo na mambo ya kizungu: 🥇First of all anajali muda, 🥈second yupo smart and 🥉third anatimiza promise mbalimbali anazokuahidi." Majulla alimsifia Boazi wakati huo tunaelekea Lecture hall kusikiliza mihadhara.
"Ukiomba mwende ,🕐Beach 🏖️⛱️🩴atakua wa kwanza kukutembelea akikuuliza 'Baby wangu ushakula?' Wakati huo huo atakuletea zawadi ya pipi 🍭au Biscutt 🧇. Jamani kijana anajali hata vitu vidogo vidogo viso na muhimu anajali." Majulla aliongea pasina kutarajia njiani tulikutana na Baby 💕 wangu Boazi. Wawili Sie tukamshangaa.
"I love you Queen!"💖 Alinikumbatia kwa nguvu Kisha akanipiga kiss kinywani💋 alafu tena a akanipatia maua💐 mekundu. Ah! Jamani nilijiona kupendwa na kijana wa ujana wangu.
*********
Basi wapenzi wasomaji mie Queen Molleta pamoja na wangu wa moyo Boazi tukala💍 kiapo cha ndoa⛪ kanisani pembeni ya mkono wangu wa kulia alisimama shogangu Majulla kama Best woman, Rafiki wa ukweli.🙋 Akilinyanyua nyanyua gauni 🥻langu la harusi lililojiburuta chini. Tukala,🥙🥒 tukanywa 🍹🍷na kufurahia💃🕺👯🎶🩰, maisha yandoa Yakaanza.
Ndoa yetu ilijibu, Zakaria mwanangu wa kwanza alizaliwa baada ya miaka 3 ya furaha, raha na deko kwa Zakaria tukampata Zawadi Binti yetu aliyezidisha furaha ya ndoa na hatimaye mwanetu wa mwisho Timothy alizaliwa👶🧒🤱 Sie wenye ndoa tukazidi kupendana zaidi na zaidi.
Majulla hakueleweka na tena sikumuelewa maana alipobeba mimba🫄 ya mwanaume aliyedai yupo ughaibuni 🏙️tena mwanaume wenyewe alikutana naye kwa bahati mbaya Binti yake Taraji akazaliwa baada ya hapo miaka sita mingine alijaliwa kupata kidume, Moze. Mwenzangu aliniambia Baba wa watoto wake yupo ughaibuni yeye ajapo ni ngono tu na kutundikwa kibedi.
Teh teh teh😂😂. Aheri ya mwenzangu sasa wale wasio na watoto wabebe nini? Mawe au barafu?🪨🧊
Zakaria wangu alianza shule🏫, Zawadi wangu aliaanza Shule, Timothy wangu akafuatia,tukawapeleka shule wakamaliza darasa la saba hadi vyuo🎓 wakaenda. Vivyo hivyo kwa Shogangu Majulla watoto wake walikua katikati ya bidii, heshima na akili za kuzaliwa.
Jambo moja lilinitatiza moyo, watoto wa Shogangu Majulla walikua na mfanano na Mume wangu Boazi yaani kuanzia sura, 😊sauti 🔉na matendo lakini kwa jinsi nilivyompenda na kumuamini Boa nisingelimvunjia heshima kumuuliza juu ya watoto wa Shogangu au kumuuliza Shogangu. Juu ya watoto wake, wacha maisha yaendelee.
Basi ndoa yetu ikatimiza miaka ishirini ya🎊🎉 furaha, mapenzi afya na Mahaba. Mie Queen Molleta pamoja na my Husband tukapatana tufanye karamu ya kuadhimisha miaka ishirini ya ndoa yetu 🎂isiyo na chembe ya matukio ya kuvunja moyo au kuumiza. Maandalizi yakanoga tukafanya kuwaalika wageni wapatao Mia, 💯ndugu jamaa a marafiki na miongoni mwa jamaa waliharikwa Shyrose wifi yangu alijitolea kuupamba kumbi wa Sherehe.
"wifi nina imani siku ya leo utapendeza sana zile hereni za Emerald haswa ukivalia gauni jeusi au jeupe utametisha zaidi"💫 Wifi aliniambia tukiwa tunaendelea kuupamba ukumbi.
"Hereni za Emerald?" Nilishangaa kauri ya Wifi yangu.🤔
"Wifi naye! Tuseme kaka Boazi hajakuonesha?" Aliniuluza.
"Wiki jana alikuja Dukani kwangu Buguruni, Duka la maodozi. Akaniungisha Hereni nzuri za kijani. Ina maana bado hajakuonesha?" Maneno ya Wifi Shyrose yakanifanya nipate mwana na taa💡🕯️ ya tahadhari iliwaka ubongoni.🧠
"Wifi yangu unajua kaka yako ana mambo mengi yamkini hizo Hereni amezificha chumbani anatarajia kunipa kama Sapraiziment." llibidi niufiche mshangao wangu kwa kusema maneno niliyobuni kichwani.
"Labda Wifi lakini ninakwambia ukivaa tu utapendeza Nawe utakuja kunishukuru maana niliagiza kutoka Arabuni."
"Jamani Arabuni!!? Kule kwenye mali safi Orginal✨" Nilitania lakini moyoni niliumia inakuwaje Boazi ndani ya wiki yote hii hajanionesha hizo Hereni za Emerald ukitegemea nijuavyo Boazi hajawai kuwa na Siri inayofichika kwangu. Siri zake, Siri zangu, kilicho hake changu, changu chake. Aahgh! Nilighafirika😡.
Ghafra jicho langu likamuona Majulla shogangu akiingia ndani ya kumbi. Wakati huo viti vya kumbi vishaandaliwa, meza ishadaliliwa na keki traaam,🍰 ya kukata na shoka Muziki 📻🎺wa blues ukitambaa masikioni mwetu kwa traaaatiibu. Yote hayo kuna jambo moja lilinifanya nihisi vibaya zile hereni za Vito vya kijani alikua amevaa Majulla wangu. Zile hereni alizoniambia wifi yangu Shyrose. Nyie! Nilipigwa 🥺 butwaa.
"Wifi," Nilimwita wifi kwa sauti ya mnong'ono
"Abee ." Shy aliniitikia.
"Hereni ulizoniambia ni zile alizovaa Majulla?" Nilinong'ona Majulla asije akasikia° Shy aliacha kudarizi kumbi akageukia kule mlangoni kule Majulla alikotokea.
"Jesu!" 🤭Shy alishituka kwa sauti. Nikamuuliza.
"Nini Wifi!?"🙂
"Ndio zile zile kaka alipokuja Dukani kununua nilimkabidhi Japokuwa sikumuuliza kama ananunua ajili yako." Shy alinitobolea Siri.
"Shy wifi yangu, kaka yako Boazi anachepuka ." Nilijikuta naropoka.
"Nashangaa wifi."Shy aliuziba mdomo wake kwa mshangao 🤭
"Tuendelee kuupamba ukumbi." Nikamwambia. Sie tukaendelea kuupamba ukumbi. Majulla alitembea kwa madaha naye akanifikia pale alipokua naupamba ukumbi. Akili ziliniambia nimchokoze ili nione reaction yake itakuaje.
"Hongera mwaya mume wetu Boazi anajua kukupamba hereni za kijani." Majulla alishituka kauri yangu. Akajing'atang'ata na kupepesa macho huku na kule kama ameona Mzimu.
"Ooh! Ooh! Ooh! Mwaya Naomba unipe ruhusa nikaitumie resting room😲🚺" Aliniomba aende kutumia choo.
"Nenda Mke mwenzangu, nenda ukakojoe." Nilimwambia pasina kunena neno aliondoka aibu ikimfuata. Moyoni nilianza kuujua mchezo uliopo Kati ya Boazi my Baby na Best wangu Majulla. Niliumia masikini mie jambo nisilolijua kama usiku wa kiza.
Hazikupita dakika kumi na tano ⌚Boaz mume wangu Aliingia ukumbini aliingia akiwa amejaa tele, mwingi wa furaha na raha za maisha. Akanifuata pale nalipokua namalizia kuupamba pamba ukumbi. Akanishushia busu zitroo shavuni 😍💋😘. Kwani nalisikia rahaa... Nyoo! Nikamgea vidonge vyake
"Eeh! Mume hizo Hereni za Emerald (kito cha kijani king'aacho sana) mbona hadi sasa haujanipa nivae mkeo nipendeze?" Macho Pima yakamtoka👀
"Aah! Aah! Queen my daring nilitaka nikupe kama Sapraiziment🎁 baada ya kuisha kwa hii Anivesary." Alijitetea.
"Nahitaji sasa hivi Babu! Tena nataka ziwe bora zaidi ya zile alizovaa Mke mwenzangu Majulla."Nikamuona anazidi kutetereka na kuingia kigugumizi.
"Usijali Queen, ninakupenda Daring." Naomba uniruhusu nikaitumie Toilent.🚹" Aliongea hivyo wakati huo simu yake ilikua ikiita ovyo. Nilifurahia moyoni maana nilijua Majulla atakua amempigia. Alipoenda Toi 🚻nilimfuata __nyuma nyuma kwa tahadhari pasina yeye kujua.
"Hallow! Uko wapi?"📱Nikiwa nimejibanza kwenye kigiza cha ule ukumbi nilisikia mume wangu akiongea na simu.
"Njoo Restroom, choo cha kike."Sauti ya Shogangu ilisikika.Boazi kama mkia wa Umbwa 🐩akaielekea Restroom, nilimfuata Kisha nikajibanza ndani, pembeni ya mango nisikie nini wanachojadiliana.
"Una nini wewe mwanaume? Yaani unamweleza mkeo juu ya hereni hizi ulizoninunulia." Majulla aliongea kwa hasira.
"Mpenziwangu amini usiamini kamwe singeliweza kumwambia Queen Habari hizi."Nilishangaa kumbe Majulla na Mume wangu ni mtu na mpenziwe. Mmh! Tangu lini?
"Sasa inakuaje Queen mkeo mbele ya Dadako amenitamkia kuwa hizi Hereni umeninunulia?"
"Unasemaje!?" Boazi alishangaa.😒🤨😶
"Hivyo hivyo kama wewe ulivyosikia." Majulla alipandwa kisirani.😠
"Majulla mpenzi wangu kamwe siwezi kufanya ujinga huo. Ninakupenda na kamwe siwezi kusababisha penzi letu liingie dosari."Boazi Alijitetea.
"Nakwambia Boazi sintakusamehe kama utamwambia habari kuhusu watoto niliozaa na wewe." Jesu! 🤭Mapigo ya moyo yalinienda kasi, nilihisi kizunguzungu kunipanda, nikataka kuanguka ndani ya kile choo. Ile nasikia Bestangu Majulla amezaa na mume wangu Boazi, Jamani watu wanasiri, we acha tu! Ina maana Taraji na Moze wana wa Majulla ni wana wa mume wangu pia. Eh! Mola nipe uziwi nisisikie kauri hizi. 🤲
"Mpenzi kamwe siwezi kufanya ujinga kama huo, wewe binafsi umenijua kwa zaidi ya miaka ishirini na tatu tangu ukiwa Chuo, nawezaje kukuharibia siku yako?" Hapana, Jamani sikutaka kuendelea kusikiliza yale maongezi yao, nilihisi nitapata stroke na presha ya kusababishwa na wale wapuuzi. Nikafanya hima kuondoka Resting room, machozi na hisia za kuonewa huruma zilinifunika
....................
Sherehe ile iliendelea taratibu wenyewe wakila na kufurahia, baada ya muda kupita MC wa Sherehe aliniita angarau nikatoe neno la shukrani. Nikiwa nimejaa tele nikampoka MC🎤🎙️ ile microphone nikwatazama wale mahanisi wawili na wapuuzi tena wasaliti: Boazi na Majulla Kisha nikatamka mbele ya watu Mia moja waliohudhuria ile Anivesary.
"Wanawake mwenzangu, Mliojifunga uchungu viunoni mwenu nyie mlioolewa na nyie mnaoishi na waume zenu naomba mniambie inawezekana kweli mume unayelala 😴🛌 naye kitanda kimoja akampatia shogako hereni za Emerald, kito cha kijani.? Niliuliza. Wanawake na wanaume wakageuza shingo zao kumtazama Best wangu Majulla, hata kabla hawajanijibu walianza kumzodoa Majulla.
'Una pepo🪬 wewe sio haba, unawezaje kupokea Hereni alizonunua mume wa mwenzio wakati huo mwenzio hapewi hizo hereni za kito cha Kijani?" Walimtazama kwa macho makali kama Duma mwindaji🐆.
"Aheri ungelipokea Hereni za mwanaume mwingine lakini sio za mume wa mwenzio." Majulla alianza kutetereka maana aliona yashamwagika hayazoleki.
"Yamkini Unalala na Boazi Majulla!?" Wachangiao Umbea walimkosoa Majulla Shogangu. Boazi mume wangu aliona aibu kuongea na wanaume wenzie. Basi mie nikalinogesha lile soga Umbea.👌
"Tena mtajisikiaje wanawake wasomi wenzangu iwapo mtasikia kuwa mwanaume uliyemjua miaka mitatu chuoni, lshirini ndoani leo hii ugundue kuwa mwanaume huyo amezaa na Shogako watoto wawili ambao ni siri nzito kama usiku wa kiza🌑" Uwii! Kama niliamsha Popo, kila mtu alimtazama Majulla na Boazi. Ghafra Majulla akavua viatu vyake vya mchuchumio👠 na kuvitupa kule, akatoka ndani ya kumbi machozi yakimbubujika.
Boazi ambaye hakujua kama nimeshaigundua ile siri yake, ile siri nzito. Alikuja mbele ya ukumbi akapiga goti mbele yangu, watu zaidi ya Mia walimshangaa, wakinong'onezana na kupiga kelele kuulaani ule Ufisadi alioutenda Majulla na Mume wangu Boazi.
"Nisamehe Queen! 🙏🙇Naomba unisamehe Mke wangu, nimekukisea sana." alilia pale chini alipopiga magoti.
"Siwezi kukusamehe Boazi, Dunia aina siri. Umejaribu kunificha siri hiyo kwa zaidi ya miaka 23, umenivunjia heshima ya ndoa yangu kwa kuzini na kuzaa na rafiki yangu. Umenikosea sana Boazi sasa naomba Taraka yangu. Nikuache na huyo umpendaye."Niliongea kwa sauti na tena kwa kipaza sauti.
"Queen Molleta, please nimekukosea sana Daring Nisamehe." Alilia hadi kamasi zilimtoka.
"Tutaonana mahakani mbele ya Mwanasheria wa ndoa, huko ndiko utakako zijua zipi mbivu na zipi mbovu." Nilimjibu jeuri Boazi aliyegaragara pale ukumbini akilia kwa chungu.😭😿🥹
"" "" "" "" "" "" "" ""
TCHAO👋
Atanikuta Mahakamani kwa Mwanasheria wangu. ⚖️🐾,
No comments:
Post a Comment