Monday, September 15, 2025

BEKA





 SURAYA TATU

                       “AKIPITA ATAJIPITISHA.”
Beka akawa member wa kampuni ya SIGA, akipelekwa hapa na pale kulinda mali za makampuni, mashirika na taasisi mbali mbali, anahamishwa hapa na pale  ili kuywajibikia koazi zake, anafanya kazi zake usiku na mchana, amerikamata bunduki yake mkononi, amevaa magwanda yake  miguuni, ametinga mkanda waqke mmoja mzito  kiunoni , haivui hiyo kofia yake inayompa heshima kichwaqni.
        Beka ni mzuri tena ni mzuri sana, anawavutia hao wanaoiungia na kutoka ndani ya mjengoi nwa benki, lakini hata hivyo wanshindwa kumwambia namna gani wanavyomtamani kwa kuhofia ulinzi wake,  ana uzuri waq sura inayowavutia wanawake wazungu pengine waafrika. Mara ile wanapoingia na kutoka kwenye majengo ya makampuni, mashirika taasisis nakadharika.
        Uchapakazi wake, juhudi zake, uwezo wake wa kufanya kazi ni baadhi ya mambo yaliyomfanya bosi wake wa kampuni ya Siga, amfanyie uhamisho, amtoe Dar es salaam naq kumpeleka Zanzibar, Unguja ndani ya mji wa Kiwenga kufika hguko Beka akawa mlinzi wa mahoteli ya watalii, makampuni, mashirika pamoja na taasisis mbali mbali, alilipwa vizuri, japokuwa maliponaliyolipwa hayakuwa makubwa sana, kiasi cha mboga, na kipindi hicho Beka hakuwa na mahali pa kuishi  ‘Getto’ alilala kwenye moja ya nyumba za Bosi wake Yule mwenye kampuni ya SIGA angali bado hajaanza kujitegemea.
        Hatari ya kupendwa, alipendwa na wengi, hatari ya kulia aliliwa na wengi, Haki! Macho uangaza na macho utambaza, moyo utamani na kutamania, mwili ukumbata na kukumbatia mapenzi nni hisia naq hisia hutoka moyoni, wanawake hawakukoma kumtafuta Beka, wazungu na watalii mbali mbali walipomwona Beka hawakusita kumfuata ili awapatie furaha yao ya moyo.
        Uzuri wa Zanzibar ni kwamba mji huo unawavutia sana watalii wengi wanaokuja Holiday, kujipumzisha  mZanzibar inakuwa ni kijiji cha watalii uhuru wa watalii ndani ya Zanzibar ni mkubwa sana, furaha yao inayoambatana na anasa ni kubwa sana, watalii hao uja na vitu vya bei gharama, watalii ununua vitu ndani ya Tanzania, kwa bei gharama, hawalalami hujuma zinazofanywa na wenyeji wao bnali wanaongeza furaha ya kuwepo Zanzibar. Zanzibar ni kisiwa cha amani kama mchanga wa bahari, Zanzibar imejaa utulivu mapenzi mahaba na upendo wa hali ya juu.
        Mandhari ya Tanzania Zanzibar yana mvuto wa hali ya juu upepo mwanana unaovuma na kukifunika kisiwa cha Unguja, ndege uimba na kukisifu kisiwa kizuri kama mbingu iliyojengwa Macka. Watanzania wanaoishi Zanzibar ni wapole ajabu wema ajabu, nwakarimu na wenye  huruma nyingi, sifa hizi zinaifanya Tanzania Zanzibar iwe kimbilio la wageni wengi kutoka mataifa mbali mbali.
UZURI WA Tanzania Zanzibar  ni nchi iliyo na siasa safi, ulinzi na usalama wa kutosha, kuna miundo mbinu bora, kuna majengo na mahoteli yenye hadhi na heshima, huduma mbali mbali za kijamii inaifanya Tanzania Zanzibar iwe kivuto cha mataifa ya wareno,waarabu, wachina, wafilipino, wamarikani, whindi na mataifa mengine mengi.
        ###########################################
                         ***************************
Huyu msichana aitwaye Bella ameuteka moyo wa Beka, unajua Beka ana historia ya kupendwa,yeye binafsi hana mazoea ya kupenda bali anapendwa na kila jicho tamu la mwanamke, analiliwana na kugombaniwa, hana mazoea ya kulilia au kugombania, anajikuta anashangaa jinsi anavyofuatwa na watoto wa kike.haki! ana nyota ya bahati lakini leo anamwona huyu msichana aitwaye Bella Beka anavutiwa na huyu msichana anajaribu kuvuta picha amwambie jinsi gani anavyompenda huyu binti. Sura ya Beka ni mtaji wake,anajua hilo anajua kuwa sura alyonayo ni mvuto kw watoto wa kike Beka anajisemea moyoni “ Silazi damu, ushindi daima, akipita aatajipitisha.”
        “Akipita atajipitisha.” Hii ni kauri ya Beka ameiweka moyoni anajiaminisha kuwa Bella akijipitisha ATAMTTIZAMA KWA MUDA MREFU UVUMILIVU UKIMSHINDA ATAMWELEZA Beka Jinsi anavyojisikia.
        Duh! Kumbe ni kweli akipitaatajipitisha, mawazo ya Beka yalikuwa Postive, sura yake ndio mtaji wake, japo ni masikini lakini hajali sababu umasikini na utajiri ni mali ya Mungu, Mungu akikupa , asipokupa wajibu wako ni kumshukuru yawezekana kesho au kesho kutwa (leo pia)  atakuongeza (kilicho bora zaidi ya ulicho nacho sasa. Riziki hutoka mikononi mwa mungu haki ya binadamu kupokea, upewe ,usipewe wewe shukuru. Akiokota mwenzio leo wewe usilale lango wazi jitume, jibidishe, fanya kutafuta utapata tu tena utapata zaidi ya kupata.
Kumbe, kumbe Bella ni miongoni mwa walemabinti warembo waliomtamani Beka, tusiende mbali wacha tumchambue chambue huyu Bella jinsi alivyo kiumbe majaliwa. Ni mweusi     tena mweusi sana, mfupi hivi, mwembamba kiasi ana hips don’t lie’ kama vijana wanavbyopenda kuita , wimbo maarufu wa  wa Shakira mwanadada wa kiamerika. Miguu na mikono yake Bella imekonda na kudhoofika.
        Alizaliwa Mbeya, Mbeya mjini. Ujio wake Zanzibar ni wa Bahati, alifika  Dar es salaam akiokea Mbeya mara ile amepewataarifa kuwa kuna kazi ndani ya kiwanda kimoja kikubwa ndani ya jiji la Dar es salaam. Ile anafika ndani ya Jiji la dare s alaam binti akaambia ‘Work is over now’ ‘NO JOB, HAKUNA KAZI’ ‘TAADHARI MBWA MKALI HAPA’ ‘KAZI ZIMEJAA’.oooshit! akapumua kwa hasira, si aliambiwa kuwa kuna nafsi tele za kazi ndani ya kwanda hicho.amepoteza muda amepoteza pesa amepoteza kila kitu.
        Any way, uppo ukabadirishwa na Yule mmiliki wa kiwanda akamwita pembeni Bella akamnong’oneza akamwambia kama sio mbaya mapatie kazi za ndani, kulea motto anayenyonya na kunywa uji,, ashinde na motto, amdekez dekeze,, ampendelee pendelee. Bella hakukubali, hakuwa tayari aliona bora kufa maiskini kuliko hujuma, ulaghai na kujidharilisha. Awali ya yote mwenye kiwanda alifanya kutangaza kuwa kazi ndani ya kiwnda zimejaa tele inakuwaje Bella aingie mjini na kuambiwa ‘NO JOB! KAZI ZIMEJAA.” Duh! Bella alihisi anahujumiwa.
        ”Akha, mie sipo trayari kufanya kazi za kulea makinda yako mama, mie nilijua kuwa nimeletwa ndani ya jiji la Dar es salaam kufanya kazi niipendayo kumbe nahujumiwa, naambiwa niwe House Girl nioshe  visepe vya watoto, niwakoroge uji nitumwe hapa na pale, kwa kweli mama utanisamehe hiyo kazi mie siiwezi.”
        siku iliyofuata Bella akampigia Simu mamaye mdogo anayeishi ZENJI, ndani ya kijiji cha Kiwenga. Simu ilipokelewa na kujibiwa vizuri, Karibu mwana karibu Zenji, karibu kwetu , karibu uje ule samaki wa kila aina karibu uje uyaone maajabu ya Munguy aliyowajalia wazenji kabla ya ukoloni, baada ya ukoloni hata uhuru.” Bi. Mdogo aliongea kwenye simu Bella akapanda meli ikatua Zenji mamaye mdogo akampokea kwa furaha.
        Bi. Mdogo alikuwa anajishughurisha na shughuri ndogo ndogo za kushonaa itambaa alivyouza na kununuliwa na wataliikwake pesa haikuwa tatizo, pesa ilikuwa nje nje, walikula walikunywa akiba ilisaza na uzuri wa Bella sio mvivu  alijitolea kumsaidia mamaye mdogo kazi za kuingiz kipato.
        Bella ndiye mpishi, mpishi wa nyumba ya Bi. Mdogo, Bella ndiye mmwenda sokoni kununua mahitaji mbali mbali  ya  kifamilia. Akipita pale Sultan Hotel mach yake  yanaagaza huku na kule yapate kutua kwenye sura nzuri ya huyu Chotara aitwaye Beka, Chotara anayemtamanisha moyo, Chotara anayemfanya binti akose usingizi Chotara anayempa mawazo huyu binti, mmh! Chotara mashallah! Mzuri ajabu, kumbe Bella akijaliwa watoto Chotara atafurahi sana, kumbe watoto Chotara ni wazuri sana, duh! Wanamvuto, ndio maana Beka anavutia.


Saturday, September 13, 2025

BEKA

 



SURA YA PILI

CHOTARA WA KIAFRIKA NA KIARABU

Sikio la kufa halisikii dawa,  za mwizi harobaini,  Baba alimwambia, Beka Kiburi sio maungwana, mkataa pema pabaya panamwita, Beka alikamatwa na wananchi wenye hasira akapigwa vibaya, akachanwa chanwa kwa visu na nyembe, alimanusura achomwe moto wapetrol, alikamatwa na wizi wa piki piki aliyopora usiku wa kuamkia jana, kipigo alichopewa amsalie mtume, Kama sio Polisi waliofanya juu chini leo hii Beka angelikuwa ni marehemu.

        Kesi yake ilipita mahakamani, akatupea jera miaka miwili sababu aligundulika ametenda kosa . maisha ya jera yakampa changamoto, akatamani qaridhi ipasuke aingie humo. Maisha ya jera yakawa magumu kwake, kula yake ikawa ni ya shida, kunywa shida, uhuru hauopo tena, kutumikishwa kjazi kama mtumwa, kupigwa pigwa na kutakanwa ovyo hatimaye alipoyazoea maisha ya jera aakajifunza Heshima, adabu na utii.

Aloitumikia jera kama fundi seremala, akiranda randa mbao, akichonga chonga vitu vya aina mbali mbali, vitu muhimu n yumbani; Meza, viti, vitanda, na vinu,  baada ya kutoka jera alitamani angeliendelea na kazi ya kuchonga lakini moyo wake ulibadiri nia akapenda sana awe mlinzi, mlinzi awalindie watu binafsi, taasisis, mashirika na makampuni.

        Mzee Armour babaye Beka akafanya juu chini mwanaye aende kujiunga na kikosi cha wanamgambo ambao mara baada ya mafunzo kuisha Beka alichukuliwa na kampuni ya SIGA aende akalinde pale alipopangiwa.

Beka akawa sasa ni kijana aliyevalia magwanda ya Askari Mgambo analinda hapa na pale alipopangiwa,Keisha iacha ile tabia yake ya kupora, kunyang’anya na kuvamia watu nyakati za usiku, kwa sasa yeye ni kijana mwenye utu na mwenye heshima hana yale matendo ya kuitia hasira jamii. Zile nywele zake zizo jaa Mba, chawa na viroboto hana tena nywele  hizo ametakata na kuwa ni kijana mwenye mvuto hata hivyo ile tabia yake ya kuvuta sigara bado hajaiacha, anaupenda huo moshi usio shibisha mdomo bali unaburudisha rohoni.

        Beka ana sura Fulani yenye mvuto mashallah, kijana ni mweupe wa uchotara na huo uchotara ameurithi kutoka kwa babaye ambaye ni chotara wa kiarabu na kiafrika, ananywele funi ziazokua  kwa kasi na kujiviringa viringa azikate asizikate bado tu zitakuwa nyingi zimwjiviringa viringa.

        Chotara huyu ni mrefu kiasi,so mnene sana, hana kifua cha mazoezi sababu yeye bnafsi hana tabia ya kufanya mazoezi, ngozi yake laini kama ya motto, sura yake laini kama ya motto, uzuri alionao Beka sio wake pekee, wadogoze Aisha na Tunu hawapunguki kwa ubora wa kusifika.

Baleghe yake ilimfanya abadirike vizuri na kuingia ukubwani na huko ukubwani Beka alikutana na mabadiriko mengine mwngi ya kimwili, kisaikolojia nay ale yatokanayo na mazingira yanayomzunguka.

Baleghe yake ilimfanya asumbuliwe na wanawake watu wazima, vigori na vijori, sura yake peke iliatamanisha wengi wapendao sura, ndevu zake kidevuni zilionesha mvuto wa hali ya juu alipendeza na kuwapendeza hao wanawake wapendao Sura, meno yake meupe, macho yake meupe, midomo yake minene na laini, ngozi yake ni ngozi yenye rangi ya chungwa umbo zuri amerithi kutoka kwa babaye mzee Armour  na uzuri wa mzee Armour Mungu hakumtupa alibarikiwa sana ujanani alibarikiwa kwa uzuri na mvuto
Kwa sasa mzeeArmour amekula chumvi nyingi, ujana umempita, uzee umempokea, hana jinsi, anakubaliana na matokeo ya mungu mengi ya binadamu machache ayapangayo Mungu mwanadamu hapangui, ujana na uzee ni mal ya Mungu ni vitu visivyo epukika.

GOOD BIE DARING CASANDRAH





 "GOOD BYE MY BABY💕, 


 GOOD BYE CASANDRAH"


Siku ile, siku nzuri kwangu, nilipata nafasi ya kutembea🚶 maeneo ya Pugu Sekondari👩‍🏫, sehemu hiyo ina vichaka vingi uzuri hakuna hatari kama vile uwepo wa Nyoka 🐍au wanyama 🐅🐕🐒 wasumbufu, siku ile nilitoka kanisani⛪ na kutabiriwa baraka tele zitakazonifuata.💰


      Mkono wangu wa mashoto nilishika simu yangu aina ya iphone 13, 📱simu ya bei gharama, sema nilijichanga sana nipate kununua ile simu, nilikua nachati na marafiki zangu, wafanyakazi wenzangu, ndugu na jamaa. Ghafra ilipita Gari aina ya Prado yenye rangi nyeupe, sikukumbuka nambari ya ile Gari nilishtuka tu kuona napokonywa simu mkononi. Ikanyakuliwa mithiri ya Nyau anayenyakua Panya.🐀🐈


     "Mwizi mkubwa wewe!" Nilimpigia kelele🗣️ jamaa aliyeniibia simu, nikafanya kukimbilia ile Gari ili anirudishie simu yangu lakini nilikwisha chelewa jambazi lile lilikwishatoweka na simu yangu.


     "Mshenziii😤" Nilitukana, hasira ikiwa imenikaba kooni, nilitamani nilikamate na kulimeza lile jambazi. Hivi mtu huyu anajua uchungu wa kuibiwa Mali ya kitanzania niliyonunua kwa gharama ya Millioni saba.... Mxiiiuuuuu😡, akatombw** mbali, Mamae.🫥😡." Nililaani vibaya.


Ndani ya ile Gari waliketi Majambazi wawili, mmoja akiwa nd'o yule mnyakuzi wa simu mnyakuzi huyu alikua na mwili wa chuma, mbavu nene, mwili wa mazoezi makali na urefu wa Goliathi. Mwenziwe kidogo hakuwa na mwili wa mazoezi japokua wote walionekana kuwa makatili.


    'Teh teh teh 😂 😂 ' Mnyakuzi wa simu akicheka kwa kebehi aliinyanyua simu yangu na kuichezea.


     'lmekula kwake," Yule Dereva ambaye hana mwili wa mazoezi💪 alichangia hoja.


    "Kudadeki, hapa Mjini kichaa wangu'😂" Jambazi lilicheka tena Gari yao ikatembea mwendo wa kinyonga.


    "Embu ngoja nitest nione kama Mali Bado ni mpya tena swaafi." Jambazi lilifungua Screen ya simu yangu.


        "Chuma Og mjumba!" Dereva alimuunga mkono Jambazi lilioanza kuiwasha simu yangu.


        "Toba!"😕 Macho yalilitoka lile jambazi mara baada ya kuiwasha ile simu yangu. 


        "What a problem!? Frank." Dereva alimuuliza Jambazi mwenziwe.


     "Picha ya Girlfriend wangu Casandrah inatafuta Nini kwenye dude la hili jitu." Frank alimuonesha picha ile Mudi kwenye simu yangu.


       "Duh! Mwanangu Frank ushaibiwa." Dereva alimwambia Jambazi Frank.


       "Mudi embu isimamishe Gari nasema hii njemba itanikoma SIKU ya Leo, 😠kama hajatembelea magoti atatembelea matako yake." Hasira za ghafla zilimkaba Jambazi Frank. Mudi aliisimamisha Gari ambapo Jambazi Frank alitoka na kufunga mlango kwa  kuubamiza. Frank alianza kutembea kwa kasi kunifuata mie niliyechoka kuikimbiza ile Gari ya Majambazi. 


Nilipotazama mbele nilimuona yule Jambazi akinijia kwa kasi ya kimondo🌠 kilichoanguka kule Mbozi Songwe. Alinikaribia, mbona niliogopa baada ya kuuona mwili nzito kama wa mwana mieleka aitwaye John Cena. Misuri yake ilikua imeshiba kama Commando 💪John Baba Jane. Uso wake ulikua, mkavu na mzito wenye mnuno na 😨hasira zilizoelekezwa kwangu kama mtu aliyetafuna Pilipili mbuzi mbichi. Mbona niliogopa.😧


    Niligeuka njia kuelekea upande mwingine ili kumkimbia yule jamaa aliyeniogopesha mie mwenye mwili kimodo na kichwa kidogo kama Pera,🥑 nimekonda na kudhoofika kama fagio la chelewa, mrefu kama mlingoti wa umeme. Nilimkimbia na yeye hakuacha kuongeza kasi ya kunikimbiza,🏃‍♂️woga ulinijaa. Sijui alifuata nini baada ya kuniibia simu, sijui amefuata pesa ambazo hazikua nyingi mfukoni mwangu zaidi ya shilingi elf hamsini.


       Alinikimbiza, akanifikia kisha akanisukumia teke moja la nguvu miguuni. Ile ngwara ilinitupa chini ya vumbi 'puuu' kama gunia la mahindi makavu🌽 yaliyovunwa shambani. Duh! Niligeuka vumbi.


      "Niache! Niache tafadhali! Nataka Nini kwangu!?" Kama unataka pesa chukua, chukua niachie uhai wangu." Nilimpigia kelele maana alikwisha nialamia na kunikalia mwilini mwangu.


     Nguuuuuu' alinilisha ngumu moja nzito ya chuma, nilisikia maumivu, Nyota na vimulimuli vilinicheka.


     "Nieleze kwanini ndani ya simu Yako unaweka picha ya Girlfriend wangu" Alinionesha picha niliyopiga na Mke wangu juu ya simu yake na yangu.


     "Huyo ni mke wangu Casandrah." Niliongea kwa kugugumia maumivu.


    "Mke wako!? 😠 Mshenzi wewe yaani Girl friend wangu awe mke wako?" Safari hii aliniacha na kunipa uhuru wa kuamka pale nilipoangushwa.


     "Casandrah ni mke wangu na Pete ya ndoa hii hapa mkononi." Nilimhakikishia lakini Bado alikua njia panda haelewi akiitizama picha iliyojuu ya screen ya simu yake na simu yangu.


     "Nitaaminije, embu ngoja, nimepata wazo." Alianza kutuliza hasira.


     "Nampigia." Akaiwasha simu yake na kuiweka loud speaker.akabinya vitufe vya kuita nayo ikapokelewa.


      "Hallow Baby!"  Sauti ya mke wangu ilisikika kwenye ile loud speaker. 🎙️🔊


     "Daring Casandrah ninakumbuka ulinibembeleza sana tutoke  siku moja usiku twende tukajaribu kuvunja apartment na kuiba Mali za watu. Leo usiku saa tano nitakua na nafasi naomba usikose."


     "Waoo! Asante mpenzi Leo itakua ni siku yangu ya furaha." Casandrah mke wangu alisikika.


     "Ok. Baby jiandae Frank alikata simu. Nikashusha pumzi ndefu😤 nisiamini kama kweli mie wangu Casandrah anatamani kushiriki ujambazi baya zaidi mke wangu wa ndoa anachepuka kisirisiri. Astaghfurilah!! Mazito ya Duniani.


      "Niite Bwana Frank. Jambazi alijitambulisha kwangu.


    "Zingo just Zingo." Nilijitambulisha pia ningali nimeshikilia komwe langu lililopigwa  hadi kuvimba nundu nzito kama ya Ngamia.


      "Usiku wa Leo mimi na Casandrah tutatoka kwenda kuiba kwenye duka kubwa kwahiyo jitahidi uwepo ndani ya duka ukiwa umefichama."


    "Duka gani!?" Nilimuuliza


    "Duka lako la nguo." Alinijibu.


    "Unalifahamu!?" Nilimuuliza.


    "We fata maelekezo, duka lako si lipo Chanika? Saa Tano usiku uwe tayari umefichama ndani" Yule mjumba aliniuliza. Nilimuitikia kwa kutikisa kichwa.


    "Ikigundulika kama ni mkeo kweli unatakiwa kumpa talaka yake."


    "Mmh! Niliguna, au ni mtego, nategewa? Tisa kumi nilihitaji kuhakikisha.


    "Mimi nikose, yeye akose na wewe ukose..... Wote tukose." Jamaa alisisitiza.


     "Nikabidhi Simu yangu." Niliomba, akanirudishia kisha akaondoka zake akiwa ameniachia katikati ya lundo la mawazo juu ya matukio yaliyotendeka siku ya Leo.


*************


Mke wangu Casandrah aliniaga kuwa anaingia Night 🌃 shift, yeye ni Daktari katika Hospitali Moja ya Serikali, inayoitwa Nguvu kazi. Nilimuaga ingawaje mtimani niliyaacha machungu yangu ambayo sikutaka kumweleza. Aliondoka nami nikamsindikiza kwa macho ya wasiwasi ambao hakugundua zaidi ya kuniona zaidi natabasamu na kuionesha furaha ya bandia.

 


Kama milivyoelezwa na jambazi Frank saa tatu kamili tayari nilikua nimefika ndani ya duka langu, duka kubwa la nguo, viatu na mapodozi. Nikajificha nje sehemu ambayo giza nene lilinikumbatia asingeliniona mtu sembuse Popo au bundi. Uzuri mie niliwaona wote wapitao mwangani nikatulia hapo nikiusubiria ujio wao.


     Kama zari saa Tano kamili nilimuona jambazi Frank na mke wangu Casandrah wakinyata na kuelekea pahali mlango wa kuingilia duka langu la nguo, nilitulia kama maji mtungini  ili nizione harobaini za wale wezi kwa kutumia ufunguo wa bandia Jambazi Frank aliweza kufungua mlango wa Duka langu, wawili wale wakaingia, sikua na haraka isiyo na baraka nikasubiria.


     "Mmh! Mpenzi Kwanini umenileta hapa?" Casandrah aliuliza akiwa ameshikwa na wasiwasi.


      "Yes, nimefanya hivyo kwa sababu pahali hapa kuna Mali nyingi sababu pia Leo ni siku yako ya kwanza kuiba mineonelea haa ni pazuri na sio mbaya kukuleta." Frank Aliongea bila wasiwasi. Frank akaanza kujichukulia magaunu, mabrouz na mashati yaliyomo ndani ya Duka langu lakini ghafla Casandrah aliiona picha kubwa juu ya Meza Ofisini, ilikua ni picha yetu tuliyopiga siku ya ndoa. Haraka bila kupoteza sekunde  Aliikimbilia ile picha akaifunika juu ya  Meza. Akiamini labda frank hajaiona.


    "Casandrah tizama hizi sketi nzuri mno ni kama zile nilizokununulia last monthly " Frank alimwambia Casandrah.


    "Yes Daring." Casandrah almwitikia Frank. Ghafla tena aliiona picha yetu ikiwa imetundikwa juu ukutani akafanya faster kukimbilia na kuishusha chini ya Meza. Akiwa ni mwingi wa wasi wasi   Frank alimfuata Casandrah ambaye safari hiii Presha ilianza kumziddi nguvu.

  

Sijui anatunza wapi Pesa huyu boya. Frank alimwambia Casandrah Kisha wakatazamana zaidi ya sekunde stini.


     "Labda anatunza kwenye safe." Casandrah alimwambia Frank.


     "Liko wapi hilo safe!?" Frank alimhoji kimasihara.


      "Lipo pale." Casandrah alinyoshea mkono pasina kujua kila neno atamkalo ni mtego kwake. Sijui ni tamaa! Lakini hapana, yamkini Casandrah alijisahau. Frank na Casandrah wakaelekea pale kwenye safe yangu ninayotunzia hella frank akajaribu kuifungua lakini kwa bahati mbaya hakugundua nambari za Siri akafanya kumtazama Casandrah wawili wale wakatabasamu.


     "Hapa tutakua tumefeli maana hatuijui secrete number ya hii  safe.


    "Hapana, hatujakosea wewe ingiza nambari 09897 Casandrah alitoa maelekezo na Frank akafanya kama alivyoambiwa afanye. Safe yangu ikafunguka.


    "Great! Casandrah kumbe wewe ni genius😆👊 unaakili sana pia unafa kwenye mishe zangu zingine." Frank akifurahia baada ya ile safe kufunguka wakazikuta pesa takribani million Tano. Akazichukua zote na pia kulikua na Pete yangu nzuri yenye kito Cha Almasi, Pete niliyachiwa na Baba yangu mpenzi kabla mauti kumkuta.


     "Lakini Casandrah hivi umeijuaje nambari ya Siri ghafla tu safe linafunguka." Frank aliingia wasiwasi.


      "Nilikisia mpenzi vitu kama hivi havinipi shida." Casandrah alijitetea kwa kujing'ata ng'ata. Wakati huo Frank Alisha chukua pes zangu nyingi.


      "Hii Pete tukiuza nakwambia tutavuna pesa mapesa.😆"


    "Si chini ya millioni sabini my wangu." Casandrah aliunga mkono. Ghafla walikuja kusikia sauti ya mlango wa lile duka, wote wakaingiwa woga mzito.


     "Nasikia mtu akifungua mlango." Frank alitoa tahadhari.


      "Ndio nahisi ni mwenye duka, embu tufichame." Casandrah alitoa ushauri, haraka wakalirudisha liles afe langu pahali pake. Kila mmoja Alikimbilia pahali akafichama. Wakati Frank Aliikimbilia kwenye makusheni yaliyotundikwa ukutani. Dayana aliingia chini ya Meza kubwa iliyo mule dukani. Jinsi alivyofichama alikua na uwezo wa kumuona aingiaye au atokaye ndani ya ile nyumba.


Niliingia ndani ya duka langu kwa tahadhari isije ikwa mtego nisije pigwa nodo za kichwa na kupotez uhai wangu. Moja kwa Moja nilinyosha hadi Ofisini kwangu huko niliikuta picha nyingine imelazwa juu ya Meza Nikijifanya kushangaa baada ya kufika pale juu ya Meza.


     Ghafla nilitetemeshwa na sauti iliyotoka nyuma ya mgongo wangu.


    "Mume wangu mpenzi." Ilikua ni sauti ya Casandrah. Nikajifanya kushituka.


     "Casandrah unatafuta nini usiku wote huu dukani." Nilimuuliza kwa kujifanya sijui kinachoendelea.


       "Baby umesahau kesho ni siku ya Valentine!? Nimekuja kuchagua viwalo bila kukupa taarifa ili nikusapraizi kwa chaguo zuri la gauni na kiatu poa." Kabla sijamjubi Casandrah tulisikia anguko la chupa sehemu yaliyopo makusheni


Paaa'! Mimi na Casandrah tuligeuka kule mlio wa chupa iliyoanguka.    


    "Umekuja na mtu!?" Nilimuuliza 


     "Hapana, labda ni jambazi. Baby embu piga simu Polisi waje walikamate." Casandrah alitoa ushauri. Hapo ndipo moyo wangu ukaniambia yatosha wacha nimwage unga wa ugali chini ya udongo


   "Unisapraiz mimi au umsapraiz Bwana Frank." Alishituka aliposikia nalitaja jina la Bwana Frank.


     "Frank popote ulipo jitokeze tuzungumze na kuyamaliza." Lile jitu lenye mwili wa chuma lilitoka mafichoni. Hakika Casandrah aliweweseka, mkojo ulimchuruza na meno yaligongana.


    "Nini kinachoendelea mbona sielewi!!!?" Casandrah alikua kama yupo ndotoni akituangalia sie wawili tuliomwangalia kwa jicho la hasira.


   "Casandrah, sikujua kama ungenifanyia hivi yaani unanisaliti na kupanga mipango michafu juu ya maisha yangu." Niliongea.


    "Nisamehe Mume wangu."Alipogundua kosa lake akaomba msamaha.


     "Kwa hiyo huyu ni mumeo si ndio!? Na mimi ni nani kwako?" Bwana Frank alimshitua Casandrah.


     "Mwanamke una roho mbaya wewe, mimi nilijua kuwa nipo pekee yangu kwako nilijua nimepata girl friend mtulivu kumbe unanichanganya na mwanaume mwingine baya zaidi unataka kuniitia Polisi." Casandrah alihisi Dunia inamwangukia.


  "Tena una roho ya kikatili." Niliongea neno.


     "Umeingia na boyfriend wako ghafra unamgeuka unanishauri tuite Polisi ili wamkamate. Casandrah nakwambia hivi tulikwisha kushitukia mapema.


    "Mshenzi huyu ananiruhusu vipi nimwibie mume wake? Nifungue self la mume na kuchukua kila kitu." Frank aling'aka.


    "Sikiliza Casandrah kuanzia Leo mimi na wewe imeisha hiyo, rejea nyumbani ukabebeshe Kila kitu kilicho chako. Nisikuone." Sikuhtaji kuongea mengi.


    "Nisamehe Mume wangu, nisamehe Frank!"


    "Usilitaje jina langu bure, imeisha hiyo.... Mimi na wewe basi!" Frank alimkataa Casandrah.


    "Wote mnanikataa sijui wapi nitakwenda." Alijitetea.


     "Ondoka tafadhali hatuna muda wa kupoteza kujadiliana na msaliti mkubwa kama wewe." Niliongea  Casandrah aliondoka chozi likimbubujika.


     "Asante Bwana Frank umenionesha upande ambao sikujua kama nitakuja kuuona siku Moja." Nilimshukuru Bwana Frank.


     "Njia mbili zikimshinda Fisi uchana msamba. Yamemkuta msaliti mwenye tamaa." Frank alinipa mkono wa shukrani.


*********


TCHAO 💖 

👋👋


**********

Thursday, September 4, 2025

THE LAST CALL

 



THE LAST CALL




EPISODE 2


The next morning, I woke up with swollen eyes. I had barely slept. My mind kept replaying his voice—the weakness, the pain, the way he said, “Thank you for listening, even for a minute.”


I couldn’t shake the feeling that something terrible had happened.


I rushed through my routine, barely tasting breakfast. My heart was restless, urging me to do something, anything.


By noon, I found myself at the same bus stop where I had seen him the day before. The sun was high, and people moved about with their usual indifference. But my eyes scanned every corner, every shadow.


He wasn’t there.


I asked a nearby shopkeeper, “Please, did you see a young boy here yesterday? About fourteen, thin, with torn clothes?”


The man frowned, then nodded slowly. “Ah, that boy. He’s always around, begging for food. Poor child. But… this morning, people said they saw him lying under the bridge. They carried him away.”


My stomach dropped. “Carried him? Where?”


The man shrugged. “To the clinic, I think. But I doubt he made it. He looked… gone.”


I ran. My legs carried me faster than my breath. I didn’t stop until I reached the small government clinic down the road.


Inside, the smell of disinfectant and despair filled the air. I went to the nurse at the desk. My words stumbled out. “Please… a boy, about fourteen, they brought him here this morning. Where is he?”


The nurse’s face tightened. She didn’t answer immediately. Then she asked quietly, “Are you family?”


“No,” I admitted, my voice cracking. “But… I spoke to him last night. On the phone. Please, I just need to know.”


She hesitated, then pointed to a small room at the end of the corridor.


I walked slowly, every step heavy, like my body already knew the truth. When I pushed the door open, the world stopped.


There he was.


Lying on a narrow bed, covered with a thin white sheet. His face was pale, peaceful, almost like he was sleeping. But I knew better. His chest no longer rose and fell. His small hands rested by his side, empty.


My legs weakened. I gripped the doorframe to steady myself. Tears blurred my vision.


I whispered, “Why didn’t I stop? Why didn’t I give him food yesterday?”


The nurse came in and spoke softly. “He didn’t leave any name. Nothing on him. Just an empty stomach and a tired body. But before he closed his eyes for the last time, he said one thing.”


I turned sharply. “What did he say?”


She looked at me with sad eyes. “He said… ‘At least, someone told me I mattered.’”


My throat tightened. I couldn’t breathe. That was me. Those were my words from last night.


I broke down beside his bed, guilt crushing me like a mountain. All I could think of was how many times I had walked past hungry faces, convincing myself I had no time, no spare change, no responsibility.


But now, one ignored boy had given me a lesson I would never forget.


I left the clinic that day carrying a weight heavier than any burden—his silence.


From that moment, I made a vow. No more excuses. No more blindness. If I saw hunger, I would feed it. If I saw pain, I would ease it. If I saw a stranger reaching out, I would not look away.


Because sometimes, the last call is not just a phone ringing. It is life itself, asking if we still have humanity left.


That boy may never have had a proper burial, or a name remembered by the world. But in my heart, he would forever live on.


The boy who mattered.

The boy who taught me that kindness delayed is kindness denied.


That was how The Last Call ended—

With a silence that still echoes every night I close my eyes.


The nurse looked at me and said softly,

“He didn’t leave any name. But before he closed his eyes, he whispered— ‘At least, someone told me I mattered.’”


My heart broke. I stood there, staring at his lifeless body, tears running down my face.


That was the last call.


THE END







Tuesday, September 2, 2025

THE LAST CALL

 


THE LAST CALL

EPISODE 1 

That night felt strange. I can’t explain it, but the silence in my room was heavier than usual. The ceiling fan hummed lazily above me, and the only light came from the dull streetlamp outside my window.

I had just dropped my phone beside my pillow, ready to close my eyes, when it suddenly lit up. A call was coming in.

Unknown number.

I frowned. Who calls around midnight with no name showing? My first thought was to ignore it. But the phone kept ringing. The sound cut through the quiet like it was meant for me.

Something inside whispered, pick it up.

I swiped the screen and said softly, “Hello?”

At first, nothing. Just silence. I almost cut the call, thinking it was a prank. Then I heard it—
A voice. Weak. Tired. Shaky.

“Please… don’t cut the call. This might be my last.”

I sat up straight. My heart skipped. “What do you mean? Who is this?”

The voice coughed before answering. “Don’t worry about my name. I just needed someone to talk to tonight. You’re the only one who picked.”

Goosebumps ran over my skin. I swallowed hard. Something in his tone felt final, like a goodbye.

“Are you okay? Are you in danger?” I asked quickly.

He chuckled bitterly. Not the kind of laugh that carries joy, but the kind that hides pain. “You don’t remember me, do you? I’m the boy you ignored today… the one who begged you for food.”

My stomach tightened.

Images from earlier flashed in my mind. I had seen him sitting near the bus stop. His clothes were dirty, his lips cracked from dryness. He looked about fourteen, maybe fifteen. His hand stretched out, and he whispered, ‘Please, uncle, I haven’t eaten.’

And me? I walked past. Told myself I was in a hurry. Told myself I had no change. I didn’t even look back.

Now his voice was in my ear, trembling.

“I don’t blame you,” he said. “Nobody ever cares. I just wanted to hear one kind word before I close my eyes… forever.”

I pressed the phone tighter against my ear, my own voice shaking. “Please don’t say that. Don’t talk like that. You’re too young. Life can still change for you.”

He sighed, long and heavy. “What’s the point? Do you know how it feels to beg and still go to bed hungry? Do you know how it feels to be invisible in a world full of people? Tonight… I just want peace.”

Tears filled my eyes. My throat was dry. “Listen,” I said, almost whispering, “I’m sorry. I should have helped you today. I was wrong. But it’s not too late. Tell me where you are, I’ll come now.”

The phone went silent. I thought he had ended the call. My heart pounded hard against my chest.

Then he spoke again, his voice softer. “Why now? Why do people only remember kindness when it’s too late?”

I had no answer. My tears were running freely now. “Because sometimes we’re blind. But I swear, I see you now. Please don’t give up. Stay with me on this call. You matter, do you hear me? You matter.”

There was another pause. His breathing was rough, uneven. I heard a cough.

Then he whispered, “Thank you. Nobody ever told me I mattered.”

I begged, “Don’t thank me, just tell me where you are. I’ll bring food, water, anything. Just hold on.”

But his reply broke me. “It doesn’t matter anymore. I’m tired… but thank you for listening, even for a minute. That’s more than anyone ever did.”

And then—

The line went dead.

I stared at my phone, hands trembling. I dialed back, but the number refused to connect. It was as if he had disappeared into the night.

I sat there in the dark, my phone pressed against my chest, and cried. Not for myself, but for a boy I ignored… a boy I might never see again.

That was how The Last Call began.

MTOTO ALIYETUPWA NDANI YA NDEGE

 





MTOTO ALIYETUPWA NDANI YA NDEGE.

  
SUBIRA



 (PART ONE)

    "No no no. Subira hiyo mimba sio yangu maana Mimi na wewe hatukupanga kuwa na mtoto au familia." Dickson Boyfriend wangu alipinga nilipompa taarifa juu ya mimba yangu.

    "Dick kitanda hakizai haramu, usiikatae hii Mimba ni Mimba yako namtoto atakayezaliwa ni mtoto wetu." Nilijaribu kumshawishi Dick Boyfriend wangu.


     "Narudia tena kusema Mimi sikua na tarajio la kuitwa Baba mapema namna hii, kama umefanya makusudi Subira naomba unieleze, sipo tayari kumpokea huyo kiumbe aliye tumboni kwako." Dick aliongea Kwa msistizo.


     "Tena kuanzia Leo naomba tuachane, siwezi kuishi na mwanamke anayefanya makusudi kuleta mtoto Duniani wakati mie sina tumaini hilo."Dick aliongea tayari kuondoka.

     "Dick mpenzi please usiniache na kumifanyia ubaya huu. Mbona tendo la ndoa tililishiriki pamoja na wakati tunashiriki mbona hsukuzikataa Raha ambazo zimeleta tokeo hili la kubeba mimba." Subira mie nililishika tumbo langu Kwa huzuni, machozi na kilio.


    "Usinijue na Wala nisikujue, shika njia yako mjaa tamaa wewe." Dick alikaza mwendo kuondoka aliniacha pale kwenye kijimvua nikiwa ninalia na tumbo langu. Nililia sana siku ile mvua ingali bado inanyesha Kwa hasira, nikatembea kutoka Kariakoo Hadi Nyumbani Malapa, mtaa wa Sharifu shamba pahali ambapo ninaishi na Baba yangu baada ya Mama kuaga Dunia.

      "Subira." Baba aliyekua akikota moto na kunywa kikombe cha kahawa aliniita.

      "Abee baba!" Nilijaribu kutafuta machozi ingawaje macho yangu yaliiva kama pilipili kichaa.

      "Keti karibu na moto." Kwa upole alinikabidhi kiti pamoja na kombe la kahawa. Nilipoketi na kunywa kombe la kahawa akaniuliza.

      "Naomba nieleze umepatwa na kadhia gani hata macho yako yaive kama damu ya mwanakondoo aliyechinjwa" Nilifuta chozi na kamasi👃🤧 zilizonitoka kama gundi nikaanza kusimulia Dady wangu mkasa wa mie kutemwa na Boyfriend wangu Dick kisa kikiwa ni kukamata ujauzito usiotarajiwa.


Baba hakuonesha furaha, alifura kwa hasira hasara, ile sura yake ya upole ikageuka na kuwa sura ya Mbogo 🐂🐃 aliyejeruhiwa. Akaniambia:


         "Nisikilize👂, umenitia aibu kubwa sana Subira,😱😳 nitaificha wapi sura yangu?🙈 Matarajio yangu yalikua ni wewe kuolewa na mwanaume safi ambaye angelikukuta bikra, huna tumbo hilo👉🤰" Aliendelea kunena.

       "Sasa ninakuambia jambo moja nenda kautoe huo ujauzito wako ili heshima yangu irejee."

      "No, Dady no🙅🔇, siwezi kuutoa huu ujauzito" Niliongea Kwa uchungu hata kahawa ile ya kiafrika aliyonipa niinywe iliniongezea uchungu moyoni." Dady akasimama na kubwata.🔊

     "Huna adabu siku hizi Subira! Sasa nakwambia neno moja usipoutoa huo ujauzito wako Leo naomba nisikukute hapa nyumbani, uondoke, usinijue wala nisikujue." Dingi alitoa kiapo.

     "Please Dady naomba usinifukize naomba unifikirie. Nimeumizwa na boyfriend aliyenikataa alafu na wewe Baba yangu unanishauri nikautoe ujauzito, unaniweka katika hatari' ya kupoteza maisha au kuvurugwa kisaikolojia." Nilitegemea Dady angelielewa na kuonesha huruma.

       " I don't care, nikisema nimesema. Usipoitoa hiyo mimba Leo hii usilale nyumbani kwangu. Aliongea na kutoweka na kuniacha nikilia na kumchukia Dickson umbwa 🐶🦴yule aliyeniharibia maisha.

       'Sintakuwa tayari kuitoa au kuharibu hii Mimba, bora tu niondoke nyumbani.' Nilijisemea. Nikaingia chumbani kwangu na kuanza kuvipakia vikorokoro vyangu pamoja na pesa  kiasi nilizozitunza kwenye kibubu kisha nikaondoka nyumbani na kuelekea kigogo ya Mburahati nilikopanga chumba na sasa kuanzisha maisha.
      
       Maisha yangu hayakuwa rahisi, nilipaswa kudamka Alfajiri sana kuelekea Posta soko la ferry ⛴️  nikanunue dagaa na mafungu ya Samaki 🎣🎏🦈Kisha ningeliwakaanga na kuwauza Kwa wakina mama wenye familia na vijana wakaao Singo wakajipikia dagaa na ugali wakawale na kushiba. Ilipofika mida ya jioni nilikimbilia kituo cha Manzese huko niliweka kijimeza changu nikauza supu ya Pweza na kachori,🐙🦑 hapo kidogo niliweza kumudu gharama za maisha.

      Basi mimba yangu ikawa kubwa kama mzigo, sikuzile sikutaka kuwasiliana na Baba yangu aliyenitaka niondoke nyumbani kwake, kisa tu nina ujauzito uliokataliwa na boyfriend wangu Dickson ambaye nilimtoa moyoni wala siku sikumtamani tena.

Ninakumbuka miezi Tisa kutimua mvua kubwa ilianza kunyesha mida ya jioni kila mtu alikimbilia nyumbani kwake kujilinda na kadhia ya mvua za Dar. Mie bila hofu nilijibanza ubandani kwangu nikisubiria wateja wangu wamalize kujinywea supu ya Pweza 🥣🍜waondoe ubaridi wa ile mvua.

        Ghafra tumbo lilianza kunikata, uchungu mkali ukanishika, kelele za kuomba msaada zilianza kunitoka. Nilikua pekee yangu wakati huo wateja walikwisha kukimbilia majumbani kwao. Nikaanza kupiga 🔊🔉kelele za kuomba msaada, kilio kikuu, lakini wapi! Sikuziona darili za kupata msaada. Mvua ilipamba moto. Niliona hapa naweza kupoteza maisha Bora niondoke pale ubandani, nijisogeze karibu na nyumba za watu huko niombe msaada.

Taratibu na kwa maumivu ya uchungu nilijitembeza na kujikokota kuelekea kule nyumba za watu zilipo, sikuweza kuendelea. Uchungu mkali ulinizidi nikaanguka chini na kuendelea kulia Kwa uchungu ajabu mvua nayo ilizidi kelele za kilio changu. ⛈️🌧️

       Ashukuriwe Mungu anayejibu maombi haraka, 🛐nikiwa nimejibwaga pale chini ya tope lilipita Gari 🚘zuri aina ya Prado likatua pembeni ya miguu yangu mie niliyekua nikijigaragaza kwa maumivu. 

Aliteremeka mwanamke mtu mzima akiwa ameushikiria mwamvuli☔ wake, aliponiona tu moyo wake ukaingia huruma akaninyanyua pale aliponilaza kwa kuukosa msaada. Akanifariji Kwa maneno ya huruma na upole, ❤️ taratibu akafanya kuniongoza nyuma ya Gari yake akanipakia na kunikimbiza Hospitali.

Nilijifungia salama mwanangu wa kiume niliyembatiza jina Clinton Dickson, yule Mama aliyenichukua na kunipekeka Amana Hospital 🏥 aliichukua na kunirudisha nyumbani kwangu. Hapo tayari siku tatu zishapita tangu tukio la mvua kubwa kunyesha na mie kukimbizwa Leba.

Ah! Mambo niliyoyakuta pale nilipokua naishi kabla sijamzaa Clinton yalinifanya ninwage chozi la kukata tamaa. 

Ilisemekana ile mvua kubwa ilikua ni mvua ya mafuriko, mvua iliyobomoa vijumba na nyumba, ukitegemea mie nilikua naishi kwenye lijumba Cha ubavu wa Umbwa kila kitu niliconunua nakuweka nyumbani kwangu kilisombwa na mafuriko kikatupwa mbali na mto msimbazi. Kwahiyo miesikuwa na hata Safuria au kijiko kunyweshea uji Clinton wangu.

     Tamari, yule Mama aliyenionea huruma, mama mwenye huruma kwangu, akaniomba niende nikaishi nyumbani kwake lakini mie niliyejaa stress na uchungu wa kupoteza kila kitu kutokana na majanga ya mvua za Dar nikikataa nikimuomba naurianisaidie niondoke Jiji la Dar nielekee Arusha popote pale nikaanze upya. Tamari aliendelea kunisihi na kunibembeleza lakini mie nilikata tamaa ya kuendelea kuishi Bongo.

      Basi Tamari mama mwema akanipatia shilingi million Moja ya kuanzia maisha niwapo ndani ya Jiji la watalii Arusha. Uzuri wa kukutana na Tamari ni mwanamke anayejiweza pia anapesa zake. Akafanya kunikatia Tiketi 📜 ya ndege🛩️ mie niliyedanganyankuwa nenda kuishi Kwa BIbi yangu feki aliyepo Arusha.

Nikakatiwa ticketi ya Ndege daraja la kwanza, safari  ya kwenda Arusha ilinoga, ingawaje bado sikufahamu ni wapi nitafikia. Nikiwa ndani ya Ndege nikaingia mawazo yaliyoutesa sana moyo wangu, niliwaza:  

'Nitamlea vipi mtoto huyu ikiwa sina maisha bora'

'MToto Clinton Dickson anahitaji maisha Bora na Mimi mama yake nisingeliweza kumpatia.  Oh! Njia panda nifanye Nini mie Subira?! Nikapata wazo la KIJINGA ambalo hadi Leo hii nikilikumbuka ninajuta kwa upumbavu nilioufanya, Niliichukua kalamu na karatasi Kisha nikaandika ujumbe.



TAFADHALI MCHUKUE MTOTO HUYU UMTUNZE AWE WAKO ANAITWA CLINTON DICKSON. NISINGELIWEZA KUMLEA SABABU NINA MAISHA MAGUMU, NAKUOMBA UMTUNZE, MILIMA HAIKUTANI LAKINI BINADAMU TUNAKUTANA. NI IMANI YANGU KWAMBA IPO SIKU TUTAKUTANA TENA AJAPOKUA MTU MZIMA MWAMBIE NINAMPENDA NA PIA ANISAMEHE KWA UAMUZI HUU MGUMU.


    Niliandika machozi yakinibubujika kama maji ya chemichemi, niliumia kwa ule uamuzi wangu mbaya, Nmekataa uamuzi wa kumtoa tumboni, amekaa tumboni mwangu zaidi ya miezi tisa alafu bila huruma ninamtelekeza? Mama gani mimi, nililia kilio cha kwikwi.🥲


     Ndege ilipotua Arusha lnternational Airport, nilihakikisha kuwa abiria wote wametoka nikabaki mie na mwanangu pamoja na mhudumu mmoja ambaye hakuniona Bali mie ndie nilimuona vizuri, akipanga na kupangilia vitu vilivyo ndani ya ile ndege.


     Nikambusu 😘😚mwanangu shavuni na juu ya komwe lake, nikamkumbatia sana machozi yakinibubujika, nikalia na kumwambia mwanangu 'KWAHERI CLINTON, KWAHERI BABA UISHI SALAMA KWENYE MIKONO ILIYOJAA UPENDO NA AMANI. BABA MOLA AKIPENDA TUTAONANA MAJALIWA.'😭

 Nikabeba kijibegi changu na kumuacha mwanangu Clinton pale juu ya kiti cha Ndege nikafanya kumpita yule mhudumu ambaye beji yake ilisomeka 'ESELINA BOAZI' Mie nikatabasamu😊

               🛬😊


PART TWO


ESELINA BOAZI


Ninakumbuka siku ya jumapili tarehe kumi nane mwezi October tulirusha Ndege ya Air Tanzania.  Iliyofanya Safari zake kutoka Dar es saalam kwenda Arusha. Mimi ni Fry attendant yaani mhudumu wa Ndege kazi yangu ni kutoa huduma kwa abiria.

 Basi Ndege ilipotua Arusha lnternational Airport mie Eselina Boazi nilikua bize nikijishuhulisha na usafi ndani ya ndege, si mnajua tena usafi kitu muhimu na cha lazima,usafi ndio afya ya wasafiri.


     Moyoni nilitingwa tingwa mawazo yaliyokitibua kichwa changu, maana nyumbani Arusha mawifi wenye gubu haweshi kulalamika ati si bora niachie ngazi kuliko kujiketisha nyumbani nikibugia ugali na kujaza choo pale kwa mume wangu wakati nashindwa hata kumletea mtoto wa kusingizia.



     Kusema kweli ndoa yangu yenye miaka sita sasa inachangamoto na jinamizi linaloitwa GUBU, mawifi hawanipendi yaani ni Bora ya mume wangu anayenipenda na kunithamini.


 Kwa wataalamu tumeenda sana mahospitalini nako wanadai hatuna ubaya, kizazi kipo saaafi salama, mbegu za mwenzangu zimeshiba afya tele, sijui tatizo nini jamani sie tukose mtoto 🥲😭 lakini ya Mungu mengi ya binadamu machache.


     Siku hiyo stress ziliusumbua mtima wangu, mawazo yalininyanyasa sana lakini ghafla nilikuja kushituliwa na sauti ya kilio cha mtoto mchanga 'ng'aaa ng'aaa ng'aa' 😿Mola we! Mapigo ya moyo yalinienda kasi. Mtoto!? Nilijiuliza⁉️ Nikamsogelea na kumkuta mtoto mchanga akiwa amelala juu ya kiti cha Ndege.


Nikaangaza macho yangu huku na huko yamkini ninaweza kumuona Mama au Baba wa mtoto lakini wapi! Sikuona mtu. Nikamnyanyua yule mtoto ili nimbebe hapo ndipo nilipokutana na kikaratasi chenye ujumbe kilichodondoka miguuni kwangu. Nikakiokota na kukisoma, kilisomeka hivi:



TAFADHALI MCHUKUE MTOTO HUYU UMTUNZE AWE WAKO ANAITWA CLINTON DICKSON. NISINGELIWEZA KUMLEA SABABU NINA MAISHA MAGUMU, NAKUOMBA UMTUNZE, MILIMA HAIKUTANI LAKINI BINADAMU TUNAKUTANA. NI IMANI YANGU KWAMBA IPO SIKU TUTAKUTANA TENA AJAPOKUA MTU MZIMA MWAMBIE NINAMPENDA NA PIA ANISAMEHE KWA UAMUZI HUU MGUMU.


Nilipomaliza kuusoma ule ujumbe mikono yangu ilitetemeka, macho yalikosa amani moyoni nililaani tendo la mwanamke mwenzangu kumtelekeza mtoto mchanga ndani ya ndege. Wakati sie wenzie tunahangaika kwa waganga na wataalam kutafuta watoto Bado tu magubu ya mawifi yakituandama.


     Any way silaumu wakunga kizazi kingalipo. Nikamchukua mtoto Clinton  Dickson, nikaelekea nyumbani kwangu Buza huko nilikutana na mume wangu niliyemueleza Kila kitu kuhusu mtoto niliyemuokota ndani ya ndege pamoja na kukisoma kipande cha barua kilichoachwa karibu na yule mtoto.


Mume wangu ni mtu mwelewa, alikubali tumtunze  Clinton Dickson. Basi mtoto Clinton akawa wetu, tukamlea kwa furaha na baraka tele.


    Niwaambie ndugu zangu kulea yatima ni baraka tosha sababu tulikua tumepanga kijumba pale Buza mwaka moja baadae tulikuja kushangaa shirika la Ndege likituzawadia nyumba Moja nzuri yenye Kila kitu NDANI, bahati nzuri NDANI ya mwaka ule ule mume wangu' alipandishwa cheo akawa ni mtu wa maana kazini, mwenye mshahara mnono wenye marupurupu. Sio jambo la kushangaza leo tukiwaambia tuna Gari mbili za kutembelea wakati zamani tulikua tukinyunda chini ya Jua lililotubananga.

         ######

Miaka kumi na tano baadae mwanangu Clintoni alikua akiingia kidato Cha kwanza ndani ya miaka hii kumi na mitano bahati nyingine ilitutembelea Mola alijibu maombi yetu nyumba ikajaliwa furaha ya kuwakaribisha wanetu wawili Lea na Andrea. Basi siku moja nikajawa tafakari kwa sasa kijana amekua na anaelekea utu uzima sio vizuri kumkalia kibubu lazima aijue historia yake, ni wapii ametoka? Wapi anaelekea? Nikamwita na kumketisha chini tukanywa kikombe cha kahawa kisha nikamweleza.


       "Nilikuokota mwanangu, nilikuokota ukiwa ndani ya ndege unalia kwa uchungu wa kutelekezwa. Uzuri Mama yako hakukutupa wala kukubwaga makusudi sema changamoto za kimaisha ndizo zilimpelekea afanye maamuzi ya kumuumiza moyo. nina imani Mama yako anajutia kitendo alichokifanya"



      "Mwanangu Mama Yako anakupenda kama kijikaratasi hiki chenye ujumbe kinavyoeleza, anakupenda na alitoa ahadi ipo siku isiyo na jina atajitokeza mfurahi pamoja, tafadhali ajapojitokeza. msamehe na muishi kwa amani" nikaendelea kusimulia.


      "Ishi ukijua mimi kwako ni Godmother, Mama mlezi ninakupenda sana mwanangu na pia ninahitaji UISHI pasina kukumbatia majuto au wasiwasi juu ya historia ya maisha Yako" Nilihitimisha na chozi lilimtoka, akasimama pale alipoketi akanifuata pale nilipoketi kisha akanikumbatia chozi na kilio cha uchungu vilimbubujika.😭


*********
 
Basi baada ya mwanangu kuijua historia ya maisha yake kwa ufupi akawa ni mtu ambaye hajatulia kila siku akiperuzi mitandaoni au kuuliza watu kuhusu pahali alipo Mamaye mzazi. Sikuchukia wala kumkataa sababu ile ilikua ni haki yake, haki ya kuwajua wazazi wake, haki ya kuijua historia yake.

 Baada ya kupita miaka miwili siku Moja nikiwa sebuleni ninapakaza dawa viatu vya mwanangu (Shoe shine )nilikuja kushituliwa na mlio wa simu, nilipoipokea maongezi yetu sikuyapendelea japo nilitarajia ipo siku maongezi yale yatakuja kuniamsha kutoka usingizi wa mawazo ya miaka mingi.

       "Hallow! Nani mwenzangu?" Nilimuuliza mara baada ya kupokea simu.

        "Mrs BOAZI mimi ni Subira Mama mzazi wa Clinton samahani ninaomba tuonane tuongee mengi juu ya suala la Clinton, binafsi ninaumia na kujuta."


        "Ebo! 🥴Miaka yote hii kumi na misaba mwanamke Leo ndio umemkumbuka mwanao, nadhani UNAMATATIZO wewe? Nilikasrika nikakata simu na kuitupia juu ya sofa.


PART THREE.


SUBIRA
 
SUBIRA mie baada ya kumtelekeza mwanangu Clinton Dickson ndani ya Air Tanzania kule Arusha Airport moyo wangu uliniuma sana nikawa ni mtu wa kulia na kujutia uamuzi wangu lakini moyo huo huo ukanipooza kwa kuniambia niondoe wasiwasi kwani mwanangu yupo katika mikono salama. 

     Nikaingia ndani ya Jiji la Arusha na kutafuta ubanda wangu ambao niliulipia kodi ya miezi sita baada ya hapo nkaadhimu kusaka kazi ambayo ingeniweka Mjini kidogo nisake ugali na tembele. Nilipata kazi ya kuosha vyombo na kupuguta deki ndani ya Hoteli Arusha Moja ya Hoteli zenye hadhi ya nyota tano,✨✨ kazi yangu ilinilipa vizuri na kula nilkula vizuri lakini Bado nilijiona nimepungukiwa mtu muhimu maishani mwangu ambaye ni mwanangu Clinton.


          Miaka kumi na misaba kupita bila aibu nikafanya kumtafuta yule mhudumu niliyeamini atanitunzia mwanangu niliyemtelekeza ndani ya ndege. Eselina BOAZI. Niliitafuta nambari yake ya simu ndani ya shirika la Ndege Nikampigia japokua mwanzo alikua ni mkali wa moto binafsi nilitakiwa kujishusha na kunyenyekea maana nilijua kosa na udhaifu wangu.


        "Ninaomba unipe ruhusa ya kuongea na mwanangu Clinton, Sina Raha, Sina furaha nazidi kukonda na kudhoofika kila siku kwa ajili yake. Historia yangu iliniumiza hata nifikirie kumtelekeza ndani ya ndege. Tafadhali nihurumie Nina Mpenda sana mwanangu, Niliongea kwenye simu pamoja na Eselina Boazi.


       "Kwendraaa👌, mwanamke mchafu wewe hufai kuitwa Mama sababu Mama mwema hawezi kumtelekeza mwanaye Kisha aende Duniani kufanya starehe." Eselina Boazi alinijibu kwa hasira.


    "Please Mrs BOAZI.... Please" Sikumaliza kuongea alinikatia simu. Bado tu sikukata tamaa hata zilipopita wiki tatu nilimbembeleza Mama mlezi wa Mwanangu kama wazungu wanavyosema Never give up. Siku Moja Eselina alinipgia simu akanitaka tukutane Royal Arusha Hoteli nilifurahia maana mwanamke huyu ana roho ya huruma na upole.

*******


PART FOUR

CLINTON.

"Wewe ni shetani tena shetani asiye na huruma."Clinton alinipigia kelele tukiwa ndani ya Royal Arusha Hoteli.


     "Huna maana ya kuitwa Mama, Mama gani amtelekezaye mwanaye? Je, ulipenda niwe mtoto chokoraa au nikalelewe kwenye vituo vya watoto yatima?" Aliniuliza wakati huo mie chozi la uchungu lilinitoka.


    "Naomba unisamehe mwanangu, nisamehe damu ni nzito kuliko maji, changamoto za Dunia zilinikatisha tamaa."Nilijitetea.


        "Kukusamehe nimekusamehe lakini usidhani nitakuita Mama, Mama yangu ni mmoja tu ambaye ni Eselina Boazi sio wewe Subira." Mwanangu aliongea ukweli kutoka moyoni.


        "Ninakubali Clinton, ninakubali fanya utakavyo lakini unisamehe tena usinitenge kama nilivyokosea mimi ." Nililia sana siku ile nililia nisiamini kama kweli mie na Mwana tuliyepotezana miaka kumi na misaba Leo angelionesha huruma na upendo kwake nisiyefaa kuitwa Mama.


      "Ninaomba wikiendi niwatembelee nyumbani kwenu mwanangu." Niliomba tu nianzishe undugu mwema.


      "Utakavyo." Nilimwambia Mwana yule mpole mwenye macho yangu na sauti inayofanana na yangu

**********

      Nilipofikisha miaka ishirini na tatu nilielekea Chuo kusoma mambo ya ustawi wa jamii na maendeleo. Umri wangu ulienda sana nikawa ni mtu mzima Sasa ninaye jielewa.


SUBIRA mama aliyenitelekeza hakuacha kumshukuru Mama yangu Eselina Boazi kwa wema na uvumilivu wake kunitunza mie ambaye alinikatia tamaa ya kunilea. Kila siku alikua akimtaja Tamari kama Mama ambaye alimsaidia sana nauri ya ndege ambayo mimi nilitelekezewa humo, Subira Kila siku ananiambia popote alipo Tamari Mungu ambariki sababu Hana cha kumlipa zaidi ya maombi na baraka tele.
________________________

Ngriiiiii ngriiiiii Kengere ya mlango wa nyumba ya  Bi. Eselina Boazi iliita. Dakika tatu badaye nilijitokeza mie Clinton nikamkaribisha na kumpokea Mama yangu mzazi alikua amebeba zawadi alizoniletea. Viatu vya michezo, boksa nzuri, kofia ya kapero na socks ndefu kwa ajiri ya michezo.



       "Asante Clinton, Asante niumekaribia."SUBIRA alinishukuru kwa kumkaribisha akaingia ndani alikomkuta Mama yangu Bi. Boazi na Babaangu Bwana Boazi wameketi wakinywa Wine ya mzabibu kwa furaha. Mama AKATABASAM.


__________________

TCHAO 💖 
________________


Let love 💞 lead.





Saturday, August 23, 2025

CASH MADAME



CASH MADAME.


 SEHEMU YA KWANZA


STEVEN BIKO

            Suzanna ndio jinale halisi, lakini wacha tumpatie jina la  Cash Madame, mama mwenye pesa zake, kama yeye binafsi anavyopenda kuitwa. Yeye ni mama la mapesa, hapa mjini mama kama yeye  vijana wengi utawasikia wakimwita ‘pendeshee’ yaani mama la mapesa kama nilivyo kueleza mpenzi msomaji, Suzann ana pesa mapesa, pesa nyingi kama mchanga wa bahari Suzanna hana shida kama unavyodhani weye mwenye kijicho cha ukapera yeye ni Cash madame mama mwenye pesa zake.

 Jumamosi ya leo ni wikiend moja tulivu, Suzi au tumwite kwa jina alipendalo Cash madame (Mama mwenye pesa zake) anateremka ngazi mbili tatu za hiyo Benk ya NMB tawi la Mwalimu house Ilala boma, ametoka kazini na sasa anaelekea nyumbani kwake, Magomeni mapipa huko ana mjengo wake, bonge la mjengo aliojengewa na mumewe marehemu Mheshimiwa Abdul Kadiri.

                  Suzanna aliteremka chini kwenye ngazi ya Benk ya NMB Mwalimu house, amevalia moja ya sketi fupi yenye rangi ya bluu ikionesha asilimia kubwa ya maungo yake, mapaja manono malaini ya kunenepa, yeye mwenyewe ni mweupe wa rangi ya chungwa la kitanga nakwambieni mwanamama ni mwenye mg’ao wa  dhahabu mnene wa kuridhika, wigi lake jeusi kichwani, kajipaka wanja kwenye kope zake, lipstick midomoni mwake, basi mwanamama anatembea kwa maringo na kwa madaha anaelekea kunako gari yake, gari moja zuri aina ya  Prado. Nadhani gari hiyo mwanamama kaigharamia si chini ya milioni hamsini au milioni themanini na ushee, hiyo ni kazi ya mumewe Bwana Abdul Kadiri kumfanya mkewe mrembo anapata furaha sio mdomoni pekee kunako tabasamu pia moyoni kunako hifadhi hisia za mapenzi ya dhaati

                 Suzi aliifikia gari yake, mara baaada ya kuteremka ngazi mbili tatu za ile Bank ya NMB Mwalimu house, akaingiza mkono wake wa kuume kunako moja ya pochi  zake nene zilizo jaa maburungutu ya pesa, noti mpya mpya zenye rangi nyekundu (Elfu kumi kumi) kama sikosei zilikua yapata milioni saba. Ndio tabia yake,  yeye na pesa pesa na yeye anatembea siku zote na maburungutu ya pesa mikononi mwake, hana shida yeye si ni mtumishi wa Benki na baya zaidi mumewe Marehemu Abdul kadiri hakua mtu mdogo hapa Tanzania mtu  maarufu mwenye cheo chake mwenye mshahara wake, tena mumemewe ni fisi la mafisadi, ashindwe nini? Kama ni pesa na utajiri vitu hivi havikumpa shida.

                Suzi akaitoa Remote ndani ya pochi yake ya mkononi na baada ya kuichomoa hiyo Rimoti akabinya binya vitufe fulani akiwa amesimama pembezoni mwa gari yake na hata baada ya kubinya binya vitufe hivyo gari yake ikatoa mlio wa ‘piiiiiii piiiiiii piiiiiii’ mlio wenye sauti ya chini,  mlango wa gari yake mlango wa mbele, mbele kwa dereva ukafunguka akajitoma ndani, akaingia kwa madaha akisindikizwa na macho pamoja na vimacho vya wanaume vijana wanaouza mitumba hapo soko la Ilala boma yangali yanamtizama kwa matamanio makubwa miongoni mwa macho ya hao vijana  mengine yakijisemea “nitampataje mwanamama mzuri huyu.” Suzi yupo very simple hana magumashi yaani hazingui wala hapotezei akikupenda kakaangu basi ujue kuwa amekupenda balaa, amekupenda penzi la dhaati hakuachi, au labda umuache wewe na roho yako, roho ya wivu na tamaa, roho ya……. Mmmh!  sijui utayaweza? Ushindwe mwenyewe! Teeh teeh teeh (Nacheka mie).

                  Basi ndo hivyo tena, mara baada ya Suzi kuingia ndani ya ile prado yake nyeupe, harufu nzuri ya marashi aliyoyanunua kule Pemba na Unguja yakalipamba gari lake, gari ikanukia na kupendeza zaidi Suzi akaiwasha gari yake naye akaondoka pale Ilala Boma.

                  “Dah! Sijui niende wapi siku ya leo nikajirushe?” Suzi aliwaza yeye na moyo wake yungali yupo round about, kati kati ya makutano ya  barabara ya Uhuru na  Kawawa, gari yake imesimama taa zimeruhusu gari zinazoenda Kawe, Kigogo ya Mburahati, Mabibo, Manzese na Makumbusho.

               “Aaah! Wacha niende beach, nikaangaze angaze macho yangu leo.” Suzi alihitimisha matamanio yake, sasa amebadiri nia badala ya kwenda nyumbani kwake Magomeni ameona wacha aende beach kupunguza mawazo pamoja na kupepewa na upepo mzuri wa baharini.

                      “Beach!” Suzi aliwaza tena, taa za kuruhusu magari, zilimruhusu apite.

                      “Magogoni beach, Kawe beach, Mahaba beach, Kunduchi beach, Kigamboni beach……. Ooooh beach…beach…beach….!!!’ Suzi aliongea kama mwendawazimu, gari yake iliendelea kutembea, mara jicho lake likatua juu ya uso na mwili wa kijana mmoja aliyekua akitembea pembeni ya bara bara, mtaa wa Congo, moyo wa Suzanna ulishituka na kudunda kwa kasi ya ajabu, ndu ndu ndu ndu moyo wake ukaendelea kwenda kasi, hakutaka kwendelea mbele.

 Akaisimamisha gari yake pembeni ya bara bara ya ule mtaa wa Congo, macho yake yalitua kwa yule mwanaume kijana mweusi hivi, mrefu kiasi, sio mrefu sana, ana mwili wa mazoezi,(body bulder) mwili wake umejengeka vizuri, amevalia singled inayo onesha wazi misuri ya mikono yake, misuri mizito minene ana kifua kipana kinachovutia, ana sura nyamvuto yaani sura inayovutia mwanamke, ukimwona mwenyewe utampenda, labda utakubaliana na mie kuwa asilimia kubwa ya wanawake wanaona aibu ndio maana wanashindwa kumtongoza japo wanamtamani sana.

                  Baada ya Suzanna kuisimamisha gari yake hakutaka macho yake yazibwe kwa pazia, kama wasemavyo wahenga bahati haiji mara mbili mbili, chelewa chelewa mwana sio wako, hakutaka apitwe na wakati ndio maana alikuwa macho kodo ili kujua wapi na wapi yule kijana hand some ana elekea.

                 “Ooooh!” Cash madame alivuta pumzi ndefu iliyotaka kumtoa kijasho, kiyoyozi kilicho ndani ya gari yake kilimpooza naye akalainika na kuregea kijike jike, yule kijana alivuka bara bara, kutoka kushoto kuelekea kulia sehemu ambayo gari ya madame imeegeshwa. Kijana yule mwenye body builder alitembea kwa nguvu zake zote wakati huo huo Cash madame alikua akitizama ujio wa yule kijana kupitia kioo cha gari yake, moyoni asitake kuona yule kijana anampita kama gari bovu.

                “Holla! Hallow brother!” Suzanna alimwita yule mwanaume kijana mwenye macho makubwa kama mayai ya bata, makubwa kama mfano wa mwanamke aliyetafuna kungu manga, ana nywele nyingi za kichotara wa kipemba, ni mzuri sio wa sura pekee, jinsi anavyotembea, anavyosimama na anavyomtizama Cash madame. je akifungua kinywa chake apate kuongea? Mmmh! Hiyo sauti yake tamu nakwambieni madame atachanganyikiwa, hiyo sauti yake tamu itampooza madame, italipooza joto alilo nalo, haki ya Mungu! Madame atazimia kwa furaha, presha, presha, presha ya kupanda na kushuka itampalia madame, mama mwenye pesa mapesa.

                  “Yeah madame.” Yule kijana aliitikia, macho ya hawa wawili yakatazamana.

                  “Unaelekea wapi nikupe lift?” Suzi aliongea kwa kujiamini, Keisha toka ndani ya gari yake yupo ‘out’ kisiketi chake kidogo, kilaini, kimepanda juu kinayaacha mapaja yake yakiwa wazi yanaonekana, meupeee pee, si mkorogo wala si mchina ( sio yale ya kutengeneza kwa madawa na makemikali) ni yale ya asili.

                   “Naelekea Posta ya zamani, asante kwa lift.” Yule kijana akaelekea lango la mbele kushoto, akajifungulia na kuingia, sijui kwanini hakusita sita? Yeye mwenyewe alijishanga shangaa na kujikuta tayari amejitoma ndani ya ile gari ya yule mwanamama mrembo aitwaye Suzanna. Wawili wale hawakukumbuka hata salamu zaidi ya kutizamana tizamana kama vile misukule isiyojua nini kinachoendelea.

                  “Namie naelekea Posta,” Suzi alijishaua shaua, akimtizama yule kijana aliyeketi, mbele ya gari yake.

                  “Niite Suzanna, watu wengi upendelea kufupisha Suzi.” Suzi alijitambulisha.

                  “Oooh jina zuri kulitamka lapendeza machoni, lavutia moyoni.” Yule kijana mwenye kifua kipana na mikono ya mazoezi pamoja na mwili ulio jengeka kisawa sawa aliongea, madame alifurahi kusifiwa na yule mwanaume kijana hand some.

                 “Mie ninaitwa Steven Biko lakini watu wengi wanapenda kuniita Steven power, body builder, kwa sababu ya mwili nilionao, mwili wa mazoezi.” Steven alijitambulisha wakati huo huo bado Cash madame angali ni mwingi wa tabasamu, tabasamu pana kama mlango wa pango la kale.

              “Vip umeoa Steven power?” Madame aliuliza.

              “La! Asha, sijaoa.” Steven hakushangazwa na lile swali aliloulizwa na yule mwana mama mtu mzima.

             “Na wewe je umeolewa, una mtu pembeni?” Steven power alimuuliza Madame.

           “Sijaolewa bado.” Madame alimjawabia yule kijana mwenye mwili wa mazoezi.

           “Mmmh!” Steven aliguna mguno ambao Cash madame aliusikia.

                     “Mbona waguna?” Suzi alimtwanga swali Steven Biko.

                   “Siamini kama kweli haujaolewa, kwa uzuri ulio nao utakosaje mwanaume hapa Dar es saalam.” Steven alionesha wasi wasi wake.

                   Teeh teeh teeh teeh! Madame alicheka kicheko cha maringo na madaha.

                  “Kuolewa ni bahati Steven au unataka kunioa wewe?” Madame aliropoka, Steven aliishia kutabasamu, hakutaka kulijibu lile swali la Madame haraka namna ile. Gari ya Madame iliendelea kukata mitaa.

                 “Vipi je tunaweza kupitia Hoteli tukapate Lunch?” Suzi aliongea wakiwa karibu karibu na Serena Hoteli, moja ya Hoteli za kifahari ndani ya jiji la Dar es salaam.

                  “No problems, hakuna matata, binafsi nina njaa kali.” Steven aliongea, gari ilisogea mbele na kwa bahati nzuri wawili wale walifika Serena Hoteli wakaingia wakaketi mbele ya moja ya meza za Hoteli ile, wakimsubiria mhudumu afike awahudumie mahitaji yao. Ala za muziki zilisikika masikioni mwao, magitaa pamoja na vinanda viliwaburudisha wageni waingiao na wale watokao ndani ya ile Hoteli wasijisikie wapweke wajisikie wapo nyumbani wankaribishwa tena na tena

                  Mhudumu aliitwa na kujongea pale walipoketi wale wawili, mhudumu huyu alikua ni msichana mmoja mzuri, mzuri wa kumtosha Steven Biko, waliendana kiujana ujana, yule msichana hakuling’oa jicho lake mbele ya yule mtanashati aitwaye Biko hali ile ilimpa kero na kumtia gere Cash madame, lakini hata hivyo hakujari alihitaji kupotezea, hana shida, kama ni pesa anazo, na kama ni kumpata Steven power sidhani kama atashindwa.

                  “Karibuni wapendwa hapa ndio Serena Hoteli, kuna kila aina ya vyakula na manywaji mtakayo.” Mhudumu aliongea wakati huo huo akaitoa Menyu yenye lundo la vyakula vya bei gharama akawapatia wale wageni Hotelini.

                  “Mie nipe samaki wa kukaanga wakubwa wawili, nyama iliyopigwa rosti, kuku mzima wa kunitosha pamoja na supu ya mbuzi, mtori wake uwe mwingi bakurini.” Steven Biko aliagiza mara baada ya kuisoma Menyu.

                  “Mie niletewe kuku rost wa kunitosha, maziwa mtindi pamoja na wali maini tena unijazie maini bakurini nile nishibe.” Madame alitoa oda yake. Mhudumu aliondoka na kwenda kuwachukulia, hakukawia alirejea na vile vyote alivyo agizwa, mapocho pocho kamili, manywaji ya bei ghari kutoka Ulaya na South Africa.

Basi Madame na yule Kibeni teni wake (dogo dogo) aitwaye Steven Biko, mwanaume mwenye mwili wa mazoezi, aliyejazia, aliye shiba, mzuri wa sura chotara wa kipemba na kiarabu. Waliendelea kula taaratibu taaratibu wakinyofoa nyofoa na kutafuna vipande vya nyama walizoagiza. Malaji pamoja na manywaji ya Bei gharama.

                 “Je, unakunywa Pombe?” Suzi alianza kumchokoza chokoza handsome wake aliyemuokota mtaa wa Congo.

                 “Yeah, niko safi katika unywaji wa pombe kari za kisasa.” Biko alideka.

                 “Good, nitakununulia siku ya leo, unywe utosheke, hata ukipenda agiza kreti mia, nipo tayari kukununulia.” Suzi aliongea.

                  “Waooo! Napenda sana bia pamoja na mizinga ya konyagi.” Biko aliona sasa ni fursa ya kuagiza kila atakacho. Wakati wote ule wangali bado wananyofoa nyofoa minofu ya kuku na samaki.

                   “Biko.” Suzi alimwita Biko.

                   “Naam Madame,” Biko aliitikia, Suzi akiwa ni mwingi wa tabasamu akanena.

                   “I love you so much Biko, nimetokea kukupenda sana, naomba uniamini tena unielewe mie moyo mpweke.” Suzi aliongea akimaanisha.

                   “I love you too Suzi, nimekupenda my.” Biko pasina kupepesa macho, aliongea na kujishaua.

                   “It’s true, ni kweli love?” Suzi alihitaji uhakika kutoka kwa Biko.

                    “Yes my,I mean it…..nina maanisha.” Biko hakuchelewesha jawabu.

“Waitress! Leta bia hapa.” Steven Biko alimpigia kelele mhudumu yule aliye wapokea, yule mhudumu mrembo ambaye mara kwa mara hachoki kumtazama Steven Biko kwa matamanio makuu, japo anashindwa kuelewa atampataje pataje, maana anajua fika kuwa mwanaume yule ana mtu wake, na mtu huyo ni mwanamama mwenye pesa zake.

                  Bia zililetwa, kreti zima, pamoja na konyagi mizinga, meza yao ikasheheni chupa kibao za pombe. Biko hakulaza damu aliendeleza makamuzi, alizishambulia zile bia kwa pupa ni kama vile hajapata kunywa pombe miaka na miaka mingi iliyopita.

                   “Duh! Kumbe yupo konki, konki liquid, konki master. Mnywaji mzuri wa pombe.” Suzi aliongea yeye na moyo wake mara alipomwona Steven Biko akigugumia bia mbili tatu kwa pupa.

                   “Mbona wewe haujinafsi kwa bia mbili tatu?” Biko alimuuliza Madame ambaye wakati wote huo alikua kinywa mvinyo,

                   “Aaah! Love mie tena sio mtumiaji wa kileo chochote kile, mie ni wa vinywaji baridi, soft drink,” Suzi alimjibu Biko.

                    “Jaribu kidogo sweet heart.” Biko alianza kmshawishi Suzi.

                    “Asante, nitajaribu siku nyingine, si unajua fika kuwa mwenzio ninaendesha gari.” Suzi alijitetea. Biko hakuwa na neno zaidi ya kuendelea kunywa kwa mapozi yake yote, vilevi vilipopungua hakusita kuongeza, aliagiza, aliagiza, aliagiza, aliagizaaaa, hadi alipotosheka, akawa bwii’ amelewa chakari.

                     “Mhudumu.” Suzi alimwita yule mhudumu wa ile Hoteli ya kimataifa.

                     “Abee Madame.” Mhudumu alikuja haraka haraka pale alipo Suzi.

                      “Je tunaweza kupata chumba cha kulala?” Suzi alimuuliza yule mhudumu.

                      “Ndio Madame, chumba kizuri kipo horofa ya tano, mlango nambari 25.” Mhudumu alimjibu Suzi

                      “Ok. Kamata hii shilingi laki tatu ni zawadi yako, asante kwa kutuhudumia.” Suzi alimpatia fedha yule mhudumu, mhudumu alizipokea hakukosa shukrani, tabasamu pana lilimpanuka alikenua na kuchekelea moyoni kwa furaha, ile shilingi laki tatu ni pesa nyingi kwake, ni nani mwingine aliye wahi kumpa hiyo zawadi? Mmmh! Hakuna, leo kapokea bahati, bahati kubwa kweli kweli.

                      Steven Biko alikua bwiii amelewa hajielewi, yupo juu ya meza anapepesuka pepesuka macho yake yameregea regea, mwili umeregea hawezi wala hajiwezi, Cash madame akamzoa zoa pale alipoketi na kumpeleka kwenye lift iliyowatua horofa ya tano, wakajitoma ndani ya chumba nambari 25, kufika huko, Suzi akambwaga Steven Biko juu ya kitanda kimoja nadhifu, bora kiloichoboreshwa, na baada ya Suzi kumbwaga Biko juu ya kitanda Madame alianza kumchojoa chojoa viwalo vyote ndani ya mwili wa steven Biko alimchojoa kama vile kuku anaye nyonyolewa manyoya, na baada ya kumaliza kumnyonyoa nyonyoa nguo zake, sijui nini kilicho endelea, sie hatujui, wanajua wao wenyewe kile kilichoendelea.

                              #####################

                     Mapenzi ni ua chanua, mapenzi kikohozi, hayana siri mapenzi wala hayafichiki, ndio hivyo tena ikawa hivyo lile penzi la Cash madame pamoja na Steven Biko yule kijana mwenye mwili wa mazoezi, penzi lao likachanua na kupendeza, tizama leo Cash madame anamtoa Out steven Biko anampeleka Mlimani City anaenda kumfanyia Shopping moja ya nguvu, nguo si nguo bali ni nguo za bei gharama, mashati mawili ya bei gharama, suruali tatu za bei gharama, viatu vya bei ya juu hata ile saa anayoivaa Steven Biko ni saa ya bei gharama, haki! Steven Biko kwa sasa ameanza kujiona tayari amefika pale anapotarajia kufika.

                     Ule umasikini wake wote tayari umekwisha kuyeyuka, tena sasa body builder anaishi kwenye raha na starehe, awali alikua akifanya kazi ya kubeba ‘ndwika’ (mizigo) magunia na mizigo mingine ya wachuuzi soko kuu la Ilala boma, leo kama zari ameangukiwa na bahati nasibu, yeye binafsi anajiuliza aiwache au? Mmmmh! Never, impossible, acheni ajilie vyake vimekuja kama Mana ndani ya jangwa lenye njaa na kiu.

                     Miezi miwili mbele, penzi kunoga, penzi kunogela, mama mwenye pesa zake akamfanyia suprizement yule kijana mzuri mwenye mwili wa mazoezi, akamnunulia bonge la gari Land cruser pajero gari moja jeusi la kupendeza, haki! Steven Biko aliruka ruka kama mwendawazimu kwa yeye kupewa ile gari haijatokea maishani mwake, ni kama ndoto japo ni kweli. Msela akajiona sasa hapo amefika, patamu hapo, hameguki wala hadondoki, hapo panamtosha sana, hapo amefika pengine hapaoni.

                   Basi Steven Biko akaanza kudeka na yeye akadekezwa, Steven Biko akaringa na kujiona yeye ni bora zaidi ya rafiki zake wale wabeba ndwika, wale aliotoka nao mbali kimaisha, wale wasakatonge, wale alioumia pamoja nao alio hangaika nao, haki! Mbona alijiona na tena alijigamba.

                   Miezi miwili mbele, akanunuliwa kiwanja apate kujenga nyumba yake binafsi, maeneo ya kigamboni, ramani ya nyumba yake ikachorwa, haraka haraka nyumba yake ikasimama, nzuri ajabu, nzuri mfano wa zile nyumba zilizojengwa Mbagara kama unaelekea Chamanzi, uzuri wa nyumba hizo zipo ndani ndani, zinapendeza, zimejengwa kisasa, ni za wenye pesa zao matajiri wafanyao biashara zao.

                 Mpenzi yao yakanoga na kunogela, kila alichokitaka Biko alikipata, alikipata haraka pasina kuchelewa, pesa mingi alipewa, zawadi mingi aliletewa, maeneo mengi yenye fahari alipelekwa, Steven Biko alijiona kweli kweli, alijiona tayari amefika, tena amefika pale alipotarajia kufika na ule umasikini uliomkumbata hapo awali ulianza kujimegua megua wenyewe ulijimegua kama gamba la nyoka linavyojivua. Umasikini ule ulikiri kumuacha na kumtema kabisa.

ITAENDELEA 

BEKA

 SURAYA TATU                        “AKIPITA ATAJIPITISHA.” Beka akawa member wa kampuni ya SIGA, akipelekwa hapa na pale kulinda mali za ma...