Tuesday, December 3, 2024

MlSS EVIL




 NILIMKOMESHA MISS EVIL.


      Semeni ndo' jina langu, jina nililopewa na wazazi wangu. Oysterbay ndo' pahali ninapoishi kwa sasa. Mume wangu alichaguliwa na umoja wa mataifa kwenda Haiti🇭🇹 kutuliza fujo na ghasia za Mahaba mia wa huko Haiti kwahiyo nyumbani nipo mie tu pamoja na wanangu wawili Evla mwenye miaka sita na Pedro mwenye miaka miwili.

       Mbali na uwepo wetu sie watatu nyumbani tunao Nyau 🐈😻wawili kidume mwite Marioo na kijike mwite Selenna. Tumejituliza ndani ya hii nyumba yetu mpya tuliyohamia wiki mbili kabla mume wangu hajaenda Haiti kulinda Amani (Niombeeni 🛐📿wangu wa roho👩‍❤️‍👨💞 arejee salama salimini)

       Sikilizeni kisa changu ninachowaletea lazima kiwafunde ujasiri wacheni woga wenu nyie! Baada ya kuhamia nyumba yetu mpya wiki mbili zilopita nilizoeana na majirani wachache wakiwemo Bibi Pili, Dada Maimuna na Bwana Heri Hamduni. Tunaishi private private ingawaje twashirikiana.

Takataka zangu za Nyumba (Waste disposal) Zilijaa full tank, nikaisubiria Gari ya taka iwasili. Mungu mzuri ilipowasili mie Semeni nilijaza viroba vyangu na kuelekea kuvitupa ndani ya Gari ya taka.🗑️🏎️

    "Evla na Pedro jiandaeni tutoke twende Shopping Dears!"  Niliwaambia wanangu waliofurahia ule mtoko maana walijua huko hawatakosa vipipi 🍭vya bure, tu lce cream 🍦🍨twa bure na tududu dudu twa kucheza 🦥🦜watoto🐰🦄🐉🦖🦕🐊🐍🐇. Tulitoka tukaenda zetu Shopper kujumua jumua Viwalo👒👕👖👗 na viatu 👡👞🥿pamoja na mahitaji mengine ya nyumbani.

     Baada ya manunuzi na kuufurahia Mji wa Kariakoo tulirejea Oysterbay Nyumbani. Ilikua ni mchana mzuri wa Jua la saa sita🌥️ Jua lilitupa hamu ya kunywa vitu soft baridi🧊🍸🍹. Mie na wanangu Evla na Pedro tulipofika nyumbani tulipigwa butwaa😱kukuta mazingira yanatisha, hayatamaniki. Ubaraza wangu wote ulijaa takataka nyingi zilizooza na kuharibika. Kulikua na pedi zenye mikojo na vinyesi vya watoto tena zilinuka. Mikate iliyokooza,mifupa na shombo la Samaki na Dagaa ilinuka baya zaidi mlango wangu wa Sebule niliosahau kuufunga kwa bahati mbaya ulifunguliwa na Sebule ilitisha kwa wingi wa takataka, karatasi, pedi, mifupa ya samaki, makopo ya biadhaa za viwandani na kadhalika. Niliogopa na kushangaa 

      "Mama Nyumba inanuka."Evla  mwanangu mkubwa aliongea.

    "It's ok Daring, nitaisafisha " Nilimjibu mwanangu Evla aliyeiziba Pua kwa kutumia madole ya mkono wake. Pedro wangu alijificha mgongoni asiuone uchafu ule. Niliwakuta Nyau wangu wameketi Sofani wakishangaa.

     "Mpuuzi gani amenifanyia hivi!?" Nilijiuliza haraka mie na wanangu tulitoka nje na kwendraa kujaribu kuhoji majirani ni mtu gani aliyelitengeneza jambo Ovu kama Lile!?

     "Pole sana Dear! "Bibi Pili alinifariji nilipoenda kwake kuuliza

     "Aliyekuchafulia nyumba si mwingine bali ni Miss Evil, yule Dada yupo very wicked, anachukiza." Nilimsikiliza Bibi Pili.
    
    "Yule Dada ni mchawi tena mwogope kila mtu hapa Oysterbay anamwogopa , hasogelewi." Bado nilimsikiliza.

      "Ana kawaida Moja ya kunusa nusa na kupeleleza ajue ni nani aliyehama au aliyehamia nyumba mpya na baada ya ugunduzi wake atafanya uovu wa kumwaga Takataka ndani ya nyumba ya huyo aliyehama au aliyehama." Bibi Pili alinisimulia.

      "Nakusihi usijaribu kumsogeleea sababu huyo ni Mlozi na mrogaji. Ukimkorofisha anakuroga unageuka na kuwa kipofu au kiziwi." Bibi Pili mwenye kadirio la miaka themanini alionesha hofu yake.

     "Bibi jambo hili niachie mimi wewe mwenyewe utakuja kunishukuru mara baada ya kumfanyizia huyo Miss EVIL." Niliongea pasina kupepesa macho.

     "Mjukuu wangu we huogopi!?" Alitia hofu

     "Hadi asame!" Niliongeza Msamiati.

     "Ubaya Ubwela... Kisa mkasa." Nilifanya kuondoka nyumbani kwa Bibi Pili mtimani nimeshiba mahasira yenye hasara.

    "Huyu Miss Evil ndo' nani atakaye kumjua mke wa Mwanajeshimpiganaji?" Niliongea pekee yangu.

      "Lazima nimfunde ili siku nyingine awaheshimu wenyeji na wageni!" Nilijiambia

       "Uchawi ndio Nini? Ina maana mtu anakuja kuchafua mazingira ya wengine ili tu aogopwe kwa sababu ni mchawi?" Nilijiuliza.

     "Sasa ngoja ataniheshimu." Nilitoa kiapo mie Semeni nlikatoka na kwenda kununua magunia mwawili makubwa yaliyoshiba. Baada ya kununua yale magunia nikaanza kupita nyumba moja baada ya nyingine kuhoji jirani zangu:

     "Nipe vinyesi vyote, vinyesi vya Umbwa, Nyau, Ng'ombe, Nguruwe na hata kama ni vya watoto wadogo nipeni" Nilidai. Majirani wakishangaa lakini pasina kuhoji walianza kunipa mioyoni mwao walihisi nimerukwa na akili..... Sio kwa hasira zile nilizotembea nazo.

     "Nipeni tafadhali, nipeni. Baada ya dakika Harobaini na Tano ninaomba mje nyumbani kwangu muone ubaya ninaotaka kumtendea Miss Evil " Walipolisikia jina la Miss Evil, Mchawi wanayemeuogopa pale Oysterbay. Yule mchawi ambaye hajaolewa zaidi ya kuishi Single sister walistaajabu na tena walitamani kujua nini kinaenda kuiva huko?!

      Mie Semeni nikayapakia magunia yangu mawili yaliyojaa vinyesi kunako Toroli Kisha nikayaburuta hadi nyumbani kwangu, huko nilijua mie mwenyewe ninaenda kufanya jambo Gani?
 
       Babaye Evla alinifunda kutengeneza Baruti za kurusha kwa mikono kupitia ujuzi ule nikafanya hima kufungasha vinyesi ndani ya mifuko midogo yenye umbo la duara kisha vile vifungasho vyenye kinyesi na umbo la Baruti nikaviweka ndani ya Magunia na kuvipakia ndani yaToroli muda si mreefu majirani wakaitana na kutimia ishirini na wote wakanifuata nyumbani wakiwa na shauku ya kutaka kujua naelekea kumtendea nini adui wa wageni Miss Evil.

      "Twendeni." Niliwaamuru wakanifuata kama Umbwa na mkia wake wamejaa shauku na kiu ya kutaka kujua nini naekekea kumtendea Miss Evil yaani ni ubaya na ubwella. Nyumba ya Miss Evil ilikua ni ya sita kutoka nyumba yangu, tulifika nyumbani kwake.

    'Knock! Knock! Knock' Nilibisha hodi mara tatu nyumba ya Miss Evil bila woga bila wasiwasi, majirani kundi zima walitazama  lango la Miss Evil. Alifungua mlango hapo ndipo akakutana na macho yangu. Mie nilitegemea kukutana na kipipa furani chenye sura ya Simba dume, kumbe wapi! Kile chifupi chikondefu ndicho kinachoogopwa na watu wote pale mjini.😆😅

       "Eeh! Bibi naomba maelezo unieleze kwanini umefanya uamuzi wa kwenda kumwaga takataka zako barazani na sebuleni kwangu?" Nilimuuliza yule chifupi cha Umbwa.

       "Sasa kama nimemwaga barazani na sebuleni kwako unataka kunifanya Nini? Aliniuliza kijeuri akiibetua midomo yake.

    "Umepata Nini chenye faida baada ya kumwaga takataka zako nyumbani kwangu na kuichafua nyumba yangu?" Nilihoji.

      "Ndio utamaduni wangu lazima Kila mhamiaji aonje taka na Kila mgeni lazima aonje taka." Alijibu kipumbavu watu wakamshsngaa.

     "Wewe pia unahamu ya kuonja taka?" Nilimuuliza moyo ukiniambia mrukie huyo, mponde huyo hadi asagike mifupa. Uzuri roho iliniambia mwambia mwaibishe apate onyo na fundo. Hakunijibu, basi nikamvamia na kumsukumia pembeni akaanguka chini puu! Kama gunia la mama, Nikaingia sebuleni kwake nikayatoa yale mabomu ya baruti kunako ile mifuko miwili mkubwa niliyokua nayo. Nikaanza kurusha yake mabomu ya baruti yaliyowaogipesha watuwote pamoja na Miss Evil.

     Sikukomea hapo Bado tu nikiendelea kuichafua nyumba yake kwa milipuko baruti zenye vinyesi: jiko lake lilichafuka,masofa yake yalichafuka na tena yaliunguavpasina kuteketea, Sebule yake ilitapakaa vinyesi ilitisha na kuogopesha. Nilitamani kufanya umafia ndani ya chumba anacholala sema roho iliniambia Sasa tosha. Nikatoka nje na kuwakuta majirani wote a Moja na Miss Evil wanaogopa na kutetemeka. Mkononi nilishika bomu lenye baruti yenye kinyesi nikamsogelea Miss Evil aliyeanguka pale chini akishangaa kisha nikakwambia.

     "Huu ni mwanzo, lwapo nitakuja kusikia kesi yoyote ile inayohusu nyumba ya mgeni au mhamiaji, imetibuliwa na kuchafuliwa na uchafu wako ninakuapia nitayazoa mapipa ya vinyesi chooni nije nipakaze kuta za Nyumba yako. Mpuuzi mdogo weye" Nilimnyoshea madole na hasira zilinikamata. 

Alitetemekatetemeka, akashindwa kuongea tena jeuri zake.

      "Ita Polisi kama unataka" Nilimwambia Bado alikua akitetemeka. Nikaondoka nyumbani kwa mwovu yule kadamnasi ya watu walinisindikiza, wakipiga makofi, vifijo, nderemo na shangwe.

      "Semeni mjukuu wangu wewe ni Jasiri." Bibi Pili alinipongeza.

       "Kwangu wewe ni Legendary hajapatikana mtu mwenye moyo wa kishujaa kama wewe." Bibi Pili aliongea tena.

      "Umemuangusha Goliath yule lnzi aliyepigwa kwa kinyesi." Bibi Pili aliichekesha hadhira. Tuliondoka eneo la Miss Evil tukiwa ni wenye wingi wa furaha. 

Nakuambieni huu ni mwaka wa pili Miss Evil hajapata kufanya upuuzi aliozoea kuwafanyia wageni. Ametulia kama sio yeye aliyekua akiogopwa kwa Ulozi.

...................

TCHAO  🖐️🦇🦉🐾🎃🎭



THE WORST FRIEND

 


JEALOUS FRIEND 🤢👺


(RAFIKI MBAYA)👿


THE WORST ONE.👹


        "Ma. Nimepata rafiki" 💑Cadabra Jesse mwanangu wa darasa la tatu alirejea nyumbani akiwa ni mwingi wa furaha, cheko na bashasha. 😹Nilishangaa kusema kweli imepita miezi Tisa sasa tangu Baba yake aage Dunia kutokana na Car accident (Ajari ya Gari)♿🚗 mwanangu alikua Hana Raha Wala furaha zaidi ya huzuni, upweke, na kujitenga baada ya kifo Cha DadieJesse.


         "Cadabra mwanangu Leo umefurahi sana kwani huyo rafiki anaitwa nani vile?" Nilimuuliza maana siku ya Leo mwanangu ameujaza moyo furaha,💖 anacheka na kuchangamka. Ukitegemea tuna wiki tatu tu toka tuhamie Gogolamboto tukitokea Chanika. Kwa maana hiyo sisi ni wageni hapa Gogolamboto.


"Jinale Hellena Jully. Tumekula pamoja🍛🍜🎉 na kucheza pamoja tena tumefurahia kununya Pipi na Biscuit."🍬🍫🍭 Siku ile Cadabra wangu aliongea kwa uchangamfu ambao hajapata kuwa nao muda mrefu tangu Babake aage Dunia.⚰️


       "Waooo!😘😚😜 My Baby boy basi nenda kabadili nguo za shule ukuje tupate Lunch kidogo Kisha ukaoge🛀 tucheki katuni ya Lucas yule samaki🐟🐬 anayebadilika kuwa binadamu." Niliufurahia uchangamfu wa mwanangu Cadabra 


Unaweza kuniita Singo mama, sikatai ndio ujane ulivyo. Nina biashara zangu hapo Kariakoo, sina njaa, Sina kiu na mwanangu anapata kila kitu utotoni mwake. Kinachonisumbua ni huzuni inayoleta upweke wa kuondokewa na mume wangu mpenzi Jesse Babaake Cadabra.


      Basi kuanzia siku ile mwanangu Card Kila aliporejea kutoka Shule hakuacha kumtaja taja rafiki yake ampendaye Hellena Jully alinitajia sifa za huyo Hellena kwamba ni mpole, mwenye huruma na upendo pia alimsifia anavyopendeza na kushirikiana naye katika michezo🤸🤽‍♀️⛹️🏌️‍♀️🎾🤾‍♂️👯 skuli 🏫🎒 kwa kifupi aliirudisha furaha aliyoipoteza.


     Basi siku moja tukiwa tunapata pochopocho🍕🍟🌮🍜🧆 na mwanangu mwenyewe akaniambia juu ya jambo lake.


    "Ma. Hellena amenikaribisha nikapaone na kupajua nyumbani kwao."Card alimega mkate na kushushia maziwa fresh kwa furaha 🍞🥪 🥛


     "Wacha we! Lini hiyo? Vipi unayo nambari #️⃣🚪1️⃣ya Nyumba yao." Nilimuuliza mwana aliyeboreka furaha.


    "Jumamosi Mama, nambari ya Nyumba yao amenipa pia."Cadabra aliongea kwa furaha.


    "Nimefurahia Sweetheart 👩‍❤️‍👨 Wacha na mie nikamuone huyo mchumbako unayemtajataja," Nilimtania my Son.


    "Nipatie nambari ya simu🤳 ya Mama Hellena kama unayo." Nilibahatisha jambo la kushangaza, kumbe mwanangu alipewa pia nambari ya simu ya Mama wa rafiki yake. Akakimbilia chumbani kwake akachukua nambari alizozitunza kwenye begi lake. Nikachukua nambari ya mama Hellena nikamtumia Text message.


     "Hallow! Mama Hellena mama Cadabra hapa naongea"📱 Nilijitambulisha.


      "Ooh! Mama Card karibu sana, karibu Mama."Alinikaribisha kwa furaha.


     "Asante mama Hellena. Card ameniambia jumamosi ya wiki hii Hellena amemkaribisha aje apaone nyumbani kwako." Nilimtumia Text message tukachati.


     "Ndio, Mama Card umefanya vizuri kuuliza juu ya jambo la watoto wetu, tuwape watoto wetu furaha."Mama Hellena alichangamka.


    "Vipi mwanamke mwenzangu naomba na mimi kesho iyo nije ili nipajue pahali ambapo mwanangu atafikia."🏘️🛣️ Niliomba lengo langu wazazi tufahamiane na tujuane zaidi ikiwezekana tusaidiane baadae juu ya watoto wetu.


      "Haina shida Mama Card karibu sana tunaweza kushea mambo mazuri juu ya maendeleo ya wanetu na yetu pia." Text message za mama Hellena zilijaa upendo.💖💝


     "Naomba niambie kama Kuna chochote Cha mno nibebe kwenye kutaniko letu la Jumamosi!? Nilihitaji kujua.


    "Hakuna la zaidi itapendeza na kuchangamsha iwapo utabeba Wine ya Mzabibu🥂🍾🍷" Mwenzangu aliongea.


   "Poa Mama lake. Naomba nikutakie usiku mwema🌑 mlale unono👋" Nilimuaga na yeye vivyo hivyo akaniaga.



  🛌🛌🛌🌙🌜🛌🌑😴😴😪💤😫



Siku iliyofuata ilikua ni Jumamosi njema, niliichukua Gari yangu ya matembezi🚗 nikampakia mwanangu Cadabra tayari kwenda Mombasa nyumbani kwa best ake ampaye furaha na kumsahaulisha machungu ya kufiwa na Baba mzazi.


    Tulifika salama Mombasa (ile ya Ukonga sio ya Kenya😆) nyumbani kwao Hellena rafiki wa Card kwa msaada wa nambari ya Nyumba ambayo Card alinipatia. Tulienda Moja kwa Moja kugonga mlango. Hellena akatokea kutufungulia, alipomwona Card mwanangu akamrukia kwa furaha nao wakakimbizana sebuleni kwenda kucheza michezo ya kitoto.🧩♟️🔫🎲🎭🧸 Mie mgeni nilimsubiria mwenyeji wangu Mama Hellena akuje kunilaki muda si mreefu Mwanadada mreefu, mwembamba mwenye rangi ya chocolate iliyokooza alitokea, nilishituka mshituko mkuu nilipomwona.


     Nilimtazama mama yake Hellena na yeye alinitizama, hakuna aliyeamini milima🏔️🗻 haikutani ila binadamu tunakutana. 🧗🚵‍♂️Tisa kumi kwa mimi kukutana na Mama yake Hellena niliingia kichefuchefu, roho mbaya ikanivamia, macho yangu meupe yakaiva wekundu, nilitamani kumrukia na kummeza🦈 mama Hellena lakini acha tu nilivumilia uchungu wangu.


     "Joyce bado upo vile vile mkondefu, mchafu usiyebadilika." Neema mama yake Hellena aliongea kunikebehi.


      "Neema nakushangaa bado unavaa vimini vinavyoonesha nguo yako ya ndani 👙 inayowavutia wadudu wadogo wadogo wanaokunyemvua nyemvua." Nilirudisha madongo yaliyojaa mafumbo.


      "Nyoo! Huna jipya Umbwa 🐕Malaya wewe." Alinikasirisha nilitamani kumrudishia jibu baya lakini nilijizuia sababu watoto walikuja pale mlangoni isingelipendeza kuwaona wanasikiliza kelele zetu.


   "Mama Card karibu ndani." Mtoto Hellena Alinikaribisha. Niliachia tabasamu la unyonge nikimtizama hasimu wangu Mama Hellena, mtimani nilijuta inakuaje ninakutana na adui yangu wa miaka ya Chuo kikuu.


     "Karibu pita ndani kwa furaha ya watoto wetu." Neema Alinikaribisha pasina kinyongo nilikubali nikaingia ndani na kuketi sofani, watoto wakarudia michezo yao. Wine 🍷 ya Mzabibu ilifunguliwa lakini jamani nilishindwa kuinywa zaidi ya kuangalia tu. Wakati watoto wetu wanafurahia sie tulitazamana kwa chuki na mahasira.


Jioni ilipoingia niliwasha Gari yangu na kuondoka pamoja na mwanangu Cadabra kurejea nyumbani. Kichwani nilivurugwa nikikumbuka jinsi Neema alivyonitendea Chuo.


     ''''"""""""""""""""""""""""""""""


Tulipokua Chuo kikuu Cha Makumira Arusha, Neema alikua na wivu sana, alijaa wivu, husda na gere. Hakunipenda sababu nilimzidi urembo na uzuri pale Chuo. Sema yeye alijiona kama Malkia wa University. Mara kwa mara alinipatia kazi nzito ili kunishusha nionekane chombo dhaifu.


       Alikusanya nguo zake chafu na kuniletea ili nimfulie tena hakujali kama ndani ya zile nguo Kuna vyupi vyake vilivyochoka na kukomaa, alinilazimisha nimpigie deki chumba chake au kwenda soko kumnunulia mahitaji yake. Alifanya hivyo maana pale Chuo alijiita Malkia 👸 wa Chuo tena alikua na wafuasi wengi waliomuunga mkono.🤝


   Nilipokosea mambo madogo madogo ambayo hayakua na tija yeye alituma wanaume makundi makundi waje wanipige na kunitesa. Mara nyingi niliponea kubakwa au kulawitiwa, kilichoniokoa ni zile mbio za Farasi 🎠🐎 nilizozitimua kuwakwepa wafuasi wake.



       Nilipomriport kwa viongozi wa Chuo🎓, nilisikilizwa malalamiko yangu?❓❔ Hakuna kitu kama hicho, Viongozi pia Walimheshimu maana ni wafuasi wake: Walimheshimu, walimsikiliza na kumtii Malkia wa Chuo kutokana na kuheshimiwa kule Neema alivimba na kujiona ana nguvu za Simba au tembo jike.🦁🐘


     Tukio Moja ambalo linakataa kufutika moyoni mwangu ni Lile tukio lililonifanya kukonda na kudhoofika hatimaye kulazwa Hospitali ya Mirembe kama kichaa mwendawazimu, na ukichaa niliupata. Neema aliniibia Boyfriend wangu Jully mwanaume ambaye tulikubaliana kufunga ndoa👰💍💒 na kuanzisha familia


Na hili kunikomoa Neema alimteka Jully mazima akanidhoofisha na kunifanya niwe mtu wa kulialia😹 na kujiona Nina mikosi. Baya zaidi katika mitihani yangu ya mwisho ya kumaliza Chuo📃📝 rafiki huyu aliwahonga Malectures mamillioni ya pesa (Rushwa)💵💰 ili wanifelishe nionekane nimeyakosea maisha. Nashukuru Mungu Rushwa aliyoitoa haikufua ndafu, wakufunzi walinionea huruma maana waliyajua mateso ninayopitia, wakanisahihishia vema mie nikapasua na kazi nzuri niliipata tena maisha niliyapatia.


     Nilipata mume mzuri, kazi nzuri inayolipa vema, nikajaliwa mtoto mzuri wa kiume tena tukajenga bonge la Mjumba ili kuishi. Sema Mungu Baba alimchukua mume wangu mapema mno.


  ***************


     Nilipoondoka nyumbani kwa Neema Sikutaka tena kumsikia sembuse kuwasiliana naye ingawaje Bado mwanangu Cadabra aliendelea kuufurahia utoto wake na rafikie Hellena. Siku moja simu☎️📞 kutoka Shule kwa mwanangu Card iliita: 'Mama Cadabra tafadhali ukuje haraka Shule Kuna jambo la kujadili kuhusu mwenendo wa mwanao Card.' Mkuu wa Shule alinisistizia.


     'Ok. Madame naja.' Niliachia kazi zangu za kiofisi nikafunga Safari hadi kufika Shule asomayo mwanangu Card na rafikiye Hellena. Nilipofika nilishangaa kumkuta Neema amejaa tele ndani ya Ofisi ya mwalimu mkuu. Nilistaajabu. Baada ya salamu maongezi yalipamba moto🧨


     "Mwanao Card amebadilika sana siku hizi yaani anafikia hatua ya kumpiga rafikiye Hellena hadi kumuumiza."Mkuu alitoa mashitaka juu ya mwanangu Card.


    "Mwanangu hawezi kufanya hivyo angali ni mdogo kupigiana "Nilimtetea mwanangu.


     "Usiseme ni mdogo kupigana ukiwa wewe haumchungi Wala kumuongoza kwa adhabu." Neema aliyenishitakia mwanangu alinikisoa.


   "Kama mwanangu Card amempiga Hellena mbona wewe kama Mama Hellena haujaniambia zaidi ya kukimbilia kwa Mwalimu mkuu? Je, Sina haki ya kujua? Nilimuulizaswali ambalo mwalimu mkuu aliliafiki.


      "Sema wewe umekosea kumlea vizuri mtoto wako hilo ni tatizo kubwa yamkini Bado anamkumbuka marehemu Baba yake." Neema alinikasirisha nilijua tu anautafuta ugomvi.


    "Tafadhali neema usinikumbushe juu ya kifo Cha marehemu mume wangu, habari za kifo cha Baba Card hazihusiani na kikao hiki." Nilimkaripia.


     "Kikubwa wewe tafuta Mwanasaikolojia amjenge mwanao na pia akujenge wewe maana mnaonekana mnevurugwa." Neema alizidi kunichokoza hapo ndipo mwalimu mkuu akayatamka maneno makali ya kuumiza.


       "Nikiendelea kupokea taarifa mbaya kama hizi ninakuapia Mama Cadabra nitamfukuza mwanao asiendelee kusoma shule hii." Nilijua tu Neema keishatoa Hongo ili nitishike lakini kamwe sikutetereka Wala kuogopa.


########


Basi nilichofanya mimi ni kumkataza mwanangu Card asithubutu kuenda nyumbani kwao Hellena tena asithubutu kucheza na Hellena jambo hilo lilimuumiza sana mwanangu. Upweke ukamvamia tena na unyonge ukamrudia, furaha yake ikatoweka lakini siku moja niliskia mlango wa sebuleni yangu ukigongwa nikatoka kwenda kuufungua kidogo nishituke na kushangaa. Hasimu yangu Mama Hellena alisimama mlangoni, usoni akiwa mnyonge mwenye huzuni.


     "Nisamehe 🙇‍♀️Joyce, nisamehe tafadhali."Alianza kuongea 


     "Usijari karibu ndani tuyajenge." Nilikua mpole, aliingia ndani, tukaketi sofani nami nikaanda wine 🍷 ya Mzabibu tukaanza kunywa🥂


     "Ninajuta Joyce, ninajuta kwa mabaya yote niliyokufanyia Chuo hadi huku nyumbani, nilikua ninakuchukia bila sababu maana ulinizidi uzuri na mwonekano. Kila jambo ulifanikiwa ukiwa Chuo na ulikua na akili nyingi kuniizidi mimi."Aliongea.


    "Haya yashapita ule ulikua ni utoto na ujana." Niliurainisha mtimani wangu.


     "Ninaomba mwanao Card arudi kuongea na mwanangu Hellena sababu Hellena huko nyumbani hataki kula Wala kulala analia tu maskini, anamlilia Card."


    "Nimeanza kuogopa jinsi anavyoipoteza amani, nina hofu nitampoteza mwanangu." Neema alichukua kitambaa cha mafua akaanza kujifuta machozi yaliyoanza kumdondoka.😿


     "Pole Neema lakini ni heri wewe uliye na mume anayeweza kumfariji mwanao" Niliongea kiuchokozi kumkumbushia kuhusu Jully Boyfriend wangu aliyenipokonya Chuo 


      "Mbona tuliishaachana na Jully, baada ya kumzaa Hellena nilimwona kama hafai na tena Hana maana. Nilimtimua kwangu kama Umbwa,🐶 mwanaume yule hajui kulea mtoto, Hana mapenzi ya kweli, yupo yupo tu yeye kula, kunywa, na huduma zote nimpatie mie."Neema alilalama kwa uchungu.


     "Pole, ulichagua fungu la kukosa." Nilimfariji


      "Lile halikua fungu langu." Alinifurahiaha kisha akatamka:


     "Kesho nitaenda kumuona mwalimu mkuu, yule mpendwa Rushwa. Nitaenda kueleza ukweli kwamba nilidanganya Cadabra hakumtendea ubaya Binti yangu. Nitaenda kulisafisha jina la Card, mipango yangu michafu itaniumbua."


     "Kweli kabisa, fanya hima maana sisi binadamu hatujakamilika." Nilimwambia, alinielewa. Kuanzia siku ile audui kati ya mimi na Neema ulikatika, t

ulipendana upya na watoto walituunganisha.



:::::::::::::::::::::::::


TCHAO 


❤️👨‍❤️‍👨👩‍❤️‍💋‍👨💝 Let love lead.


*************





Monday, December 2, 2024

SOME TIME SANE, SOMETIME INSANE.

 



MUME WANGU ALIMTIMUA🏃 NYUMBANI🏠 MAMA YANGU MZAZI MWENYE CHANGAMOTO YA AKILI🤪 MARA BAADA YA MAMA KUMFUMANIA AKIGONOKA NA CHANGUDOA. 💏


      Baada ya sherehe ya Noel na Mwaka mpya kufika ukingoni wanangu wawili Rashford na Josea 👩‍👧‍👦walihitaji kurudi shule,🏫🎒👨‍🏫 shule ya boarding, 🛌shule Binafsi ya kulipia.💰llikua ni kawaida ya my Husband kuwapeleka skuli 🚖Kila ifikapo January mosi. Mie nilibaki na mama yangu mwenye changamoto ya akili🧠 yaani kuna wakati akili zake ukimbia anakua kama sio yeye naye atafanya Kila kituko cha kuudhi 🤯au kuchukiza, utoto mwingi hadi tutamchoka. Atavua nguo zake, atapiga kelele, atavunjavunja vyombo na kuharibu pia baada ya muda akili zake zingerudi na kuwa sawa, hapo angelitulia tuli kama maji mtungini.🚰🏺.

    Uzuri wa changamoto ya kupoteza ufahamu🤯 pale inapofika ukomo mama yangu urejea katika hali yake ya kawaida. Hali ya kujutia matendo yake ya utoto, 🥹hali ya kujionya kutorudia tena matendo haribifu,😮‍💨 hali ya utulivu, amani na furaha🫡. Ajabu changamoto yake ingelirejea tena.😵‍💫

       Basi mume wangu Dionice aliniambia kwa mwaka huu 2024 January niwapeleke watoto warejee kusoma nje ya Mkoa yaani Tanga mjini sikupinga Wala kukataa nilimuomba anitunzie mama yangu mwenye changamoto ya ufahamu, kwa moyo mkunjufu Dionice alikubali Ombi langu. Safari yangu mie Gigyfriday na wanangu Rashford na Josea ilipamba moto.

"""""""""""""""""""""""

"Hallow! Gigy"☎️ Siku ya tatu baada ya kuingia Tanga mjini mume wangu alinipigia simu.

"Hallow! Daring😘"Nilimwitikia wakati huo nipo ndani ya Moja ya hoteli 🏨🏩za kifahari.

"Kuna tatizo kubwa limetokea nyumbani" 🏡Toba!😶 Dionice alinishitua kidogo.  

"Tatizo!?"🤭 Niliuliza kwa mshangao kidogo Wine yangu niliyokua nikiinywa imwagike.

     "Ndio tatizo my wife, ni tatizo kubwa" Aliongea

     "Tatizo gani? Tafadhali nieleze." Nilikaa mkao wa kula kuisikiliza ile changamoto.

     "Bibi mama mkewe ametoweka nyumbani nisijue ni wapi alipoelekea. Safari hii ile grass 🍷🍾ilinidondoka chini puuuu ikadondoka na kuvunjika. Maana nilipata mshituko.

     "Ametoweka! 🏃‍♀️Ametowekea wapi na lini ametoweka?" Maswali mfululizo yalinitoka, hofu na wasiwasi juu ya Mamangu mwenye changamoto ilinivamia.

      "Ametoweka leo🏃‍♀️,sijui ni wapi alipotowekea!? Ningali ninamtafuta." Dionice alinijibu.

     "Vipi ushaenda Police👮‍♂️🚓 kutoa taarifa?" Nilimuuliza, jibu alilonipa lilinivunja maini.

    "Bado nakusubiri wewe uje tuangaike pamoja kumtafuta." Sikutaka kuendelea kuongea kwenye simu,📱nikakurupuka kuondoka ndani ya ile Hoteli 🛋️nikiwa nimeacha Kila kitu changu chenye thamani💰 na kisicho na thamani. Nikashuka ngazi za ile Horofa haraka haraka nikakimbilia uwanja wa Ndege🛫 ilikuwai Ndege ✈️itakayoondoka siku ya Leo kwenda Dar es saalam🌇.

      Niliingia Tanga nikiwa na Gari yetu lakini baada ya kusikia habari juu ya tatizo lililompata Mama ilibidi niiache Gari yetu pale pale Airport, nikapanda Ndege iliyokua inaelekea Dar es saalam. Moyoni nikijilaumu kwanini niliruhusu Dionice amtunze Mama yangu mwenye changamoto? Ni heri na ni bora kama ningelibaki kumtunza mimi mwenyewe.

   "Labda alimuachia ufunguo wa Getini?⛩️" Nilijiuliza, nikiwa nimepagawa yote kwa sababu nilimpenda sana mama yangu na kuumia moyo ilikua lazima.

    "Mama umekwenda wapi rudi tafadhali." Nilisali kimoyomoyo 🛐📿

    "Ninakupenda Mama yangu, ninakupenda Dear." Nililia pekee yangu ndani ya ile Ndege. Safari yangu haikua ndefu sababu kutoka Tanga kwenda Dar ni masaa ⏰machache baada ya kuingia Dar nikafanya pupa pupa kukodi Uber🚖 ilonikimbiza moja kwa moja hadi nyumbani kwangu nilikomkuta mume wangu amekula pozi sebuleni macho kodo kwenye Tv📺 anafuatilia Tamthilia ya Juakali.🌞

     "Daring badala ya kuangaika mitaani kumtafuta Mama yangu wewe umepiga pozi namba nne kwenye Video unatizama Tamthilia" Nililalamika mara baada ya kuingia pale sebuleni.
      
     "Gigyfriday, unastahiri kupumzika kwanza ndipo nikupe taarifa kamili." Alinipokea Kisha akanitaka nipumzike sofani🛋️ akafanya hima kuniletea maji baridi Jokofuni 🧊lakini wapi! Hayakupita kooni. 

     "Muda huu unaoingia ndo' na mimi ni naingia, mwenzio nimekesha🌗 nikimtafuta Bibi Mama mkwe nisimpate." Aliongea. 

     "Ushaenda 🏃Polisi?👮 Nao anasemaje?" Maswali yalinitoka. 
    
     "Nimeenda, nao wameahidi kutusaidia watampata tu." Alinipooza. 

    "Tatizo nini hadi Mama akimbie nyumbani?" Nilihoji. 

    "Gigyfriday si unajua changamoto inayomsumbua Bibi Mama mkwe?" 

    "Duh! Mola wangu amwepushie mabaya Mama yangu" Niliropokwa. 

    "Amka basi twende tukaendelee kumtafuta." Ninavyompenda Mama yangu nilikua tayari kufanya jambo lolote ilimradi apatikane.

       "Gigy my Daring Nimechoka please." Alidekadeka. 

     "We! Mwanaume wa wapi? Embu Amka hapo tukaangaike." Nilimpigia kelele haraka haraka tulichangamka kumtafuta. Tulimtafuta sana Mama yangu, tulimtafuta ndani ya majalala ya takataka🗑️🚮 tukidhani labda amekwenda huko, tulizunguka mtaa kwa mtaa tukiuliza na kuwapigia simu ndugu, jamaa, marafiki 👥na majirani lakini wapi! Ma. Hakupatikana. Hatukukata tamaa tuliendelea kumtafuta Mama.

       ::::::::::::::::::::::::

Siku ya tatu tulijisikia kuchoka sana maana tulikua tunalala popote pale ili tubahatike kumpata Mama. Tuliamua kuelekea nyumbani kwenda kukoga na kubadili nguo maana kwa zaidi ya siku tatu hizi hatukubadili nguo Wala kugusa maji mwilini.

    "Kwanini tusiende kulitangaza🔊🔉 jambo letu kwenye Mablogu.📃 Televisheni 📺na Radion!📻📡"Nilitoa ushauri.

     "Wazo zuri" alinijibu kwa ufupi.

    "Tutangaze donge nono💰 kwa mtu au watu watakao mpata Mama." Nilitoa wazo.

     "Unamaanisha pesa, 💶💸 , kiasi Gani? "Dionice aliniuliza.

    "Nipo tayari kutoa Million Tano 💳💸kwa mtu atakayebahatika kumpata Mama yangu."Nilimjibu Dionice.

    "Gigy pesa zote hizo? Pesa za kufanyia jambo la maana." Alinijibu kama vile hakupendezwa na wazo langu.

     "Najua Dion, lakini pia Mama yangu ni mtu wa maana." Nilimziba mdomo.🤫 Tukasikia muungurumo wa gari ikiingia  uwanjani kwetu, ilikua ni Gari ya Polisi. Sie tulikodoa macho kodo kwenye Dirisha ili kujua kuna Nini? Nikaingiwa na furaha baada ya kumuona Mama yangu akiteremshwa kutoka kwenye ile Gari ya Polisi. Polisi walifanya kazi nzito ya kumsaka hadi kumpata Mama yangu.

     "Twende tukampokee." Nilimwambia Dionice kwa furaha.

    "We, nenda tu ukampokee!" Mume wangu hakuonesha furaha. Nikatoka kwenda kumlaki Mama yangu kwa furaha na kumkuta akiwa mzima mwenye afya, pasina makovu au ubaya mwilini mwake. Nikampokea na kumkaribisha tena Nyumbani kwetu. Aliingia sebuleni na mimi pia niliingia, Mabwana Polisi nao waliingia. Ile tunaingia tu, Mama aliponwona mume wangu alianza kupiga kelele kama amemwona Pepo mchafu.🦹‍♀️👿

      "Mkamateni huyu fedhuli ☠️na firauni mjaa laana." Alimnyoshea dole mume wangu, aliyeanza kuogopa.

      "Kwani amefanya nini Mama!?" Nilimuuliza kwa mshangao⁉️

     "Huyu fedhuli ndio sababu ya mimi kuondoka hapa nyumbani." Nilimsikiliza, Askari walimsikiliza pia.

    "Tatizo nini!? Embu tueleze."Askari mmoja alimtaka mama yangu afungue kunywa ayatoe yaliyofichama moyoni. Mama akaanza kueleza.

     "Gigyfriday huyu mumeo ni shetani👹 asiye na huruma."Alimnyoshea mkono👉 mume wangu aliyeketi sofani kimya akisikiliza.

      "Ulipoondoka kwenda Tanga kuwapeleka wajukuu zangu Shule usiku mmoja nilikua nimelala chumbani kwangu lakini nikaja kuamshwa na milio ya chaga za kitanda chumbani kwenu. Mbali na sauti za chaga niliskia mili ya sauti za mahaba, mwanzo nilivumilia moyoni nilijisemea sauti hizi na vilio hivi vikuu vya mahaba sijazoea kuvisikia ndani ya nyumba hii." Mama aliongea wote tulimsikiliza.

     "Nikajiwa na wazo kwamba labda Binti yangu Gigyfriday amerejea kutoka Safarini, lakini kwanini arejee pasina kuniambia sembuse kuja chumbani kwangu kunitakia hali? Basi mie nikateremka ngazi za Horofa na kuelekea chini kule sauti za chaga na mahaba zikiendelea kulindima. Bahati nzuri au mbaya mlango wa chumba chenu ulikua umeachwa wazi." Mama alipumzika kidogo kuongea🙇

   "Nikausukuma ule mlango, taa zilikua zinawaka💡. Salale! Macho yangu yalitua kitandani nikamuona Mkwe wangu Dionice akifanya zinaa na mwanamke mwingine."Mama alitoboa Siri.

     "Bibi Mama mkewe ni mwongo👺" Dionice alimpinga Mama yangu.

      "Kama mimi ni mwongo yule mwanamke ni nani haswa pale kitandani unapopaswa kulala na mkeo Gigy?" Mama alimuuliza Dionice.

     "Mwanamke aliyelala kitandani alikua ni Ombaomba niliyemuokota mitaani nikampa maji, 💦chakula🥪 na pahali pa kulala🛌 kama hifadhi. Dionice alijitetea sie twalimsikiliza.

    "Na ile sketi ya kimini👗ya kimini, kitopu,👙 wigi🦰 la bei gharama, mkoba mwekundu👜, viatu virefu vya mchuchumio 👠 baya zaidi amepakaza mdomo wake lips nyekundu💋💄 wote mlikuwa mmelewa bwiiiii 🍻🍺msitamanike." Maneno yaliyomtoka Mama yalitushangaza 😂😶‍🌫️

    "Dionice ni kweli ayaongeayo Mama!?"Nilimuuliza. 

    "La! Hasha,  Bibi Mama mkewe anadanganya. Lakini Gigy si unajua kwamba Mama ana changamoto ya kuvurugwa akili? Yamkini akili zake zilihama ndio maana anaongea wendawazimu." Dionice aliongea mikono yake na miguu ikipata kitetemeshi.

     "Mume wangu lakini si ni wewe ndiye unayedai kuwa ulimleta Ombaomba ndani ya chumba chetu Sasa yawezekana vipi Ombaomba akalala chumbani kwetu wakati vyumba vya wageni vimejaa tele na baya zaidi wote wawili mlilewa?" 🍺🥂Nilimuuliza kwa hasira.👿

       "Alafu tangu Mama ametoweka mbona hukuniambia kama ulimleta Ombaomba chumbani kwetu?" Nilimuuliza.❓

    "Kumbe mimi ninawapeleka watoto shule wewe unafanya ngono na Malaya unaowaita Ombaomba? Hakunijibu zaidi ya kuangalia chini kwa aibu. Mama yangu akaendelea kunena:

    "Nilipomuuliza mkwe wangu kwanini unafanya ngono na Malaya chumba ulalacho na Binti yangu mkwe akanijibu jeuri na kuniambia 'hii ni nyumba yake, ana haki ya kufanya kitu chochote kile.' " Toba! Nilishituka yaani nyumba niijenge mie alafu mwanaume amjibu kunya 💩 Mama yangu.

      "Mkwe wangu akaniambia niondoke haraka ndani ya hii nyumba sababu hii nyumba ni yake, mimi na mwanangu Gigy hatuna chetu hapa." Mama alianza kulia.🥹 Mimi pia chozi lilinitoka 

     "Hii ni nyumba yako 🏡Dion? Ulijenga wewe?" Nilimuuliza, hakunijibu.

      "llibidi niondoke Gigyfriday, niliondoka akinitazama wakati huohuo amemkumbatia Malaya." Mama aliongea kwa uchungu.

     "Nisamehe Gigy, nisamehe Daring....💞 Pombe zilinidanganya " Aliongea.

     "Siwezi kukusamehe, umemvunjia heshima Mama yangu." Nilianza kulia chozi.😭😢

      "Mama kwa sababu sisi hatulioni kosa alilolitenda huyu Bwana Dionice pia hili jambo ni la kifamilia tungependa tuwaachie hii kesi muimalize nyie wenyewe." Bwana Askari aliongea Kisha wakaondoka na kutuacha sie twalumbana na kupigiana kelele ndani ya nyumba.

     "Beba Kila kilicho chako 🧳na uondoke ndani ya Nyumba yangu, muuaji mkubwa wewe."Nilimpigia kelele.

    "Nisamehe Gigyfriday, nisame sweetie. Ibilisi😈👹 alinipitia." Alijitetea

     "Na wewe kampitie huyo lbilisi. Mkeo sikutoshi hadi ufikie hatua ya kutembea na Malaya!? Eeh!? Baya zaidi unalala nae kitanda ninacholala na wewe." Nilimfokea.

       "Nisamehe Daringi 🙇‍♂️please." Sikujali Wala sikumsikiliza.

       "Nasema beba vigagula vyako uondoke. Nilitilia mkazo, akaingia chumbani na kusomba vilago vyake safari ya kuondoka ilifuata.

     "Barua ya Taraka utaipata kwa Mwanasheria ⚖️ infidelity mkubwa wewe." Nilimkemea kwa hasira😡😤

    "I'm Sorry Gigy lm sorry please."Alibembeleza sana

     "I don't care please leave my house now."Aliondoka akiwa mnyonge na mwenye huzuni


***************
(Embu nishaurini wenyewe, nimsamehe au nimbwage kwa Mwanasheria !? Ningali katika machozi na kuvurugwa  🥲) to CT

***************

TCHAO 😢🥹😭🤯

""""""""""""""""'""'''''''''''



     

    



   
      

NJAMA CHAFU (A CONSPIRANCY)

 


BAADA YA KUMFUKUZA 🏃‍♀️🏃‍♂️MKE WANGU WA NDOA MAMA NA DADA YANGU WAKAKIHARIBIU💀 KIZAZI🩸 CHANGU.

"Hamza!" Mama aliniita kwenye Rununu yake📲" Nilisikia sauti ya kwikwi😿 Ma. Alikua akimwaga chozi.

"Naam, Ma. Mbona kama nasikia unalia" 🥲Nilimuuliza moyoni nimejaa maswali kibao.⁉️

"Acha nilie my son. Mkeo huyu ni shetani mkubwa, shetani Ibilisi 🦹‍♀️👿kwa haya anitendeayo nimevumilia miaka yote lakini nimeona mvumilivu ninakula mbovu, Bora nikuambie" Safari hii alitoa kilio kikuu, moyo wangu ulinidunda uchungu ulinivaa kusikia kilio cha Mama mpenzi.

"Tatizo Nini Ma, acha kulia."😤😠 Niliongea simuni.📱

"Sijalia miaka mingi tangu baba yako achukuliwe na Mungu🪦⚰️, Leo acha nilie tu sababu Mkeo ananinyanyasa, ananitesa, ananishusha kwa matukano baya zaidi ananidunda mwili wangu umejaa makovu sema nashindwa kukwambia mwanangu. iiiiiiii😿iiiiiiii uwiii 🥲." Alipaza sauti ya kilio.

"Nini👺? Jasimini anakutesa, anakupiga, anakunyanyasa" Nilipaza sauti 🗣️safari hii hasira zilianza kuninyanyasa.

"Nitafanya nini mwanangu zaidi ya kuvumilia, Leo tu ameniambia niondoke nyumbani hapa, ananifukuza na kunitimua ndani ya nyumba uliyojenga mwanangu,🏘️ ananifukuza kama vile ni yeye aliyejenga nyumba hii" Ma. Alinisimulia.

"Nasema haiwezekani Ma, haiwezekani..... Ngoja nije nimuoneshe kwamba anapaswa kukuheshimu, mpumbavu mkubwa huyo." Nilibwata nikiwa Ofisini✍️ kwangu hima hima nikachukua funguo ya Prado 🚗yangu nikaikoki na kutimua vumbi moja kwa moja hadi Oysterbay nyumbani moyoni nikimlaani mke wangu.👩‍❤️‍👨

"Mpumbavu huyu hajui jinsi nilivyoishi na mama yangu Kwa tabu, shida na mahangaiko."

"Mama alikua akiuza mbogamboga, nyanya na vitunguu ili Mimi nisome na nimesoma kwa tabu hadi kupata Diploma yangu ya Sheria ⚖️👨‍⚖️alafu mjinga yule anampiga na kumnyanyasa Mama yangu."Nilivurugwa.

"Leo atanikoma, ama zangu ama zake ni mwendo wa kutimuliwa tu."Nilibwata ndani ya Gari nikaikimbiza ovyo Hadi masikani huko mlinzi wa geti alinifungulia haraka nikaenda moja kwa moja hadi sebuleni.

"Yu wapi huyo mpuuzi anayekunyanyasa Mamangu."Nilifoka.👺

"Amelala chumbani kwake😴, Ma. Alikua Analia Hadi kamasi zilimchuruza.😪 Nikaenda chumbani alipolala mke wangu nikaubamiza mlango mbaaaaa  Mama Jasimini mke niliyezaa naye watoto wawili:Jasimini na Ali alishituka baada ya kusikia sauti kuu ya mlango ule.

"Twende sebuleni,"Nilimvamia pale kitandani nikamvuta mkono wake kinguvu karibia niutengue ukavunjika Nikamburuta na kumtoa nje kuelekea barazani nilipomuacha Mama.

"Kuna Nini Baba Jasimini? Kuna Nini?" Sikuisikiliza sauti yake. Nikamsukumia sebuleni pale Mama alipokua Analia Kwa uchungu.

"Bibi Mama mkwe mbona unalia umepatwa na Nini? Mke wangu alimuuliza Mama yangu maana alionekana kushituliwa na kilio cha Mama.

"Unajifanya haujui Mama Jasimini yaani kila siku unanitukana, unanipiga na kuniambia niondoke kwenye nyumba aliyojenga mwanangu Hamza."Ma. Aliongea akilia.

"Mimi!!? Mimi ni wa kukupiga 💪wewe, kukutukana na kukufukuza." Mama Jasimini aliongea kwa mshangao na mshituko. Nilisikiliza tu wakibishana.

"Sasa kumbe! unataka kuniua ndani ya nyumba ya mwanangu wa kumzaa." Mama aliongea Kwa uchungu mzito.

"Bibi Mama mkwe!!" 🤯Mama Jasimini bado alipigwa na butwaa.

"Naomba uingie chumbani na ubebe kila kilicho chako Kisha uondoke."🛅🧳🛍️ Nilimwambia Mama Jasimini kwa hasira.

"Baba Jasimini Bibi Mama mkwe haongei ukweli, hakuna jambo kama hilo mimi kumtenda." Mama Jasimini alijitetea.

"Mama yangu hawezi kudanganya, Mama amenilea katika tabu, shida, na maumivu makuu leo hii kimburukutu wewe unampiga na kutaka kumuua." Nilimfokea Mama Jasimini.

"Siwezi kufanya jambo kama hilo Mume wangu, wallah!! Bilali! Ninakuapia."Alijitetea machozi yakitaka kumdondoka lakini mie sikusikiliza, kwanza yeye sio damu yangu na sio ndugu yangu kuna baya gani nikimtimua?❓

"Kabebe nguo zako zote utoweke." Nilimsukumia chumbani.

"Nisikilize Baba Jasimini nisikilize Dear!"Machozi yalimdondoka.

"Namsikiliza Mama yangu sikusikilizi wewe mpumbavu." Nilipoona anachelewa kuingia chumbani kubeba vigagula vyake nikaingia Mimi na kutoa kila kila chake na kumfukuzia nje kama Jibwa🐕 lisilotakiwa nyumbani

"Nisikilize Baba Jasimini naomba nipe nafasi nijieleze."Lakini wapi sikumtetea niliegemea upande wa Mama tu.

"Ondoka na Tena ondoka nyumbani kwangu,"Niligeuka mnyama mwenye hasira.🐉🦍🦁

"Basi nipe nafasi ya kuondoka na wanangu."z👨‍👦 Alilia.

"Neva eva, hauna watoto hapa. Watoto Hawa ni wa kwangu ulikuja mikono mitupu na uondoke mikonoz🙌 mitupu." Nilikua namsukuma aende nje ya Geti, baada ya kumtoa nje nikamuacha pale Analialia na kugonga geti ahurumiwe.⛩️ Sikujali. (I didn't care)

--------*****--------*****

Mama Jasmin hakukata tamaa kila siku akawa ni mtu ni wa kuja Ofisini ✍️akilia kwa uchungu akidai hajawai kumtendea Mamangu ubaya, aliomba aonane na wanangu. Lakini bado sikumpa nafasi hiyo. Basi akafanya kwenda ustawi wa jamii kudai haki ya kuwaona watoto tuliozaa pamoja, Hilo nalo sikulitaka kabisa na kwa vile mie ni Hakimu 👨‍⚖️na pia nina pesa nyingi 🤑🪙💲💰nikatoa rushwa kubwa kubwa wamnyime haki hiyo, kwa asilimia kubwa wale watu wa ustawi walipokea rushwa na kumnyima ile haki ya kuwaona watoto.

       Mwanamke hakuchoka bado tu aliendelea kunisumbua Ofisini na nyumbani. Nikacheka kwa ule usumbufu wake nikaanza kumtisha kwa kumwambia iwapo ataendelea kunisumbua nitamfanyia 🥷kitu kibaya ambacho hatokuja kukisahau maishani mwake. Akanywea na kuogopa..... Nilidhamiria kumwaribia maisha yake sababu pesa ninazo na cheo ninacho.

Baada ya miezi sita kupita baada ya kuachana na mke wangu Dada yangu Aisha alihamia nyumbani kwangu maana alikua amegombana na Mume wake na Taraka juu aliachiwa. 📝📜Aisha hakuwa na pahali pa kukimbilia zaidi ya nyumbani kwangu akaambatana na Jumanne mwanaye mwenye umri wa miaka kumi na Mitano. Wakati huo wanangu hawakukoma kuniuliza kuhusu pahali alipokwenda mama yao, niliwajibu uongo nikawaambia Mama yenu hawapendi, amewakimbia, hawataki na pia hataki kabisa kuwasikia. Wanangu waliamini hivyo hivyo nilivyowadanganya.

     Kwa vile Mimi ni mtu mwenye pesa zangu basi nikafanya kuwaajiri vijana wawili wawe wanamfuatilia mke wangu na kumchunguza:anafanya Nini?Anapanga mpango gani? Anatembea na nani? Miaka ilivyozidi kwenda nilikuja kuambiwa tayari ameolewa hapo ndipo nilipopata mwanya wa kumwandalia Taraka. Akala Taraka yake na tena sikujali nilipokuja kuambiwa amejifungua mtoto wa kiume. kwani anafaida gani kwangu, ⁉️❓sikuona umuhimu wake.

     -------------------------------

Nilikua ni mtu wa bize bize kazini, mtu wa kazi kazi.kama ningeliondoka saa kumi na moja Alfajiri basi ningerejea saa sita au saba usiku, muda huo ningeliwakuta watoto wangu wamelala, Mama na Dada yangu wamelala pia moyoni Nilifurahia nikijua kuwa familia yangu inaishi kwa furaha. Nilitembea na Ufunguo wangu wa nyumba, nirejeapo kutoka kazi ningelifungua mlango kwa Ufunguo wangu na niondokapo kurejea kazini ningelifunga kwa Ufunguo wangu. Mama na Dada pia walikua na funguo zao za akiba
   
        Ilipita miaka Saba pasina mke niliyempa Taraka kunifuatilia. Siku moja nilijisikia kuumwa mwili💉🥵 wangu wote nikaaga Ofisini mapema yapata saa tatu usiku,🌆 nikaeleka nyumbani kwangu Tabata nipate kupumzika. Kama kawaida niliutumia Ufunguo wangu kuingia nyumbani kwangu nikalilaza Gari langu na kuelekea chumbani kwangu.

      Ile napita karibu na mlango wa chumba cha Dadangu nikayasikia maongezi ya majibizano kati ya Mama na Dadangu, nikatega sikio nisikilize nini wanachobishaniana.

        "Sophia nilikuambia lile tendo la kumfukuza Jasmin mke wa kaka yako lingelileta matatizo ni Bora tungelimwacha alee watoto wake."

      "Lakini Mama hata wewe ulishiriki kusababisha Jasimini mke wa kaka Hamza afukuzwe nyumbani hapa."Dada alimjibu Mama.

       "Kumbuka ni wewe ndiye uliyenishawishi nitunge uongo na kujifanya naigiza mbele ya kaka yako Ili kumpumbaza aamini kuwa Jasimini alikua ananipiga, ananitukana na kunidharau." Mama aliongea Mimi niliyekua nimetega sikio pale mlangoni nilishangaa maongezi yao.

       "Sasa Mama ningelienda wapi ikiwa Mume wangu alinifukuza na pahali pa kukimbilia sikua napo zaidi ya nyumba ya kaka Hamza."Sophia Dadangu alimjibu Mama.

        "Haya Sasa tuachane na hayo maji yashamwagika hayazoleki, ⛲embu niambiwe Sasa tunafanyaje kuhusu Ali mwana wa kaka yako? Je ataendelea kujinyea hivi hivi hadi lini? Tena la zaidi nimekuomba sana mchunge mwanao Riziki tendo la kufanya mapenzi na Aisha mwana wa kaka yako litasababisha majanga mazito ikiwemo kuharibu kizazi cha Aisha au kubeba mimba katika umri madogo."Uwii! Maongezi yao yalinipa Presha.😤🥶🥵

      "Mama punguza lawama, Riziki alianza michezo ya ngono tangu akiwa Shule ya Boarding🏫 walimu walipomgundua wakapelekea afukuzwe Shule na Mimi kupewa Taraka na Mume wangu. Sasa Mama ningefanya Nini ikiwa sikuwa na pa kukimbilia zaidi ya hapa nyumbani kwa Kaka."Dada alijitetea.

      "Nimesema tuachane na hiyo Topic yakuachwa na Mumeo, tujadiliane kuhusu hali mbaya ya Ali mwana wa kakayo kutokwa na choo kikubwa bila speed, 🚽mkanye Riziki kuendeleza mchezo huo pia muamishe Riziki ndani ya chumba alalacho na Ali, kumbuka Ali ni mtoto madogo mwenye umri wa miaka nane tu."Maneno ya Mama yalinifanya nianze kuona kizunguzungu na kuanguka.

     "Nimemkanya Riziki mara ngapi wala asinisikie!?"

    "Na Kaka yako akifahamu itakuaje??"
   
    "Tutatunga uongo mama....." Sikutaka kuendelea kusikiliza maongezi yao nilikwishajua kuna kitu hakipo sawa pale nyumbani. Nikausukuma mlango wa chumba cha Dadangu nikaingia kwa fujo ile wananiona tu walishituka na Ili kutoonesha darili ya kwamba wameyasikia maongezi yao wakajifanya kuibadilisha Topic, wakaanza kujadiliana mambo mengine.

    "Nielezeni vizuri kuhusu Mtoto wangu Ali na Dada yake Aisha." Nilipaza sauti, hawakuamini kama nilikwisha yasikia maongezi yao wakajitetea kwamba hawajui jambo lolote linaloendelea. Nikawabana sana Ili waongee ukweli wa mambo hatimaye mwisho wakajieleza. Mama akaeleza ukweli kwamba yeye na Dada walipanga njama mke wangu atimuliwe pale nyumbani kwangu Ili Dada aje aishi pale nyumbani maana Dada alipewa Taraka na mumewe kwahiyo hakuwa na pahali pa kukimbilia.

Wakaeleza Riziki  mtoto wa Dada mwenye umri wa miaka kumi na Tisa umwingilia Aisha Binti mwenye miaka kumi na moja umbaka mwanangu Hadi aridhike na tena hatosheki umwingilia kinyume na maumbile mwanangu Ali ambaye tayari ameharibika anajinyea.     We! Nilicharuka nikawa Mbogo mnyama wa porini nilitamani niwapige Dada na Mama yangu nilichofanya ni kuwafukuza pale nyumbani kwangu wote waondoke warudi kijijini. Hasira zilinipanda baada ya kujua kumbe mama na Dadangu walipanga njama chafu Ili nimfukuze mke wangu mpenzi wao waishi kama Malaika pale nyumbani kwangu. Moyo uliumia na kusikitika.

      Nikafanya mpango wa kuwatafutia Madaktari wanangu. Mishipa ya haja kubwa ya Ali mwanangu iliregea na kusababisha kinyesi kiwe kinamtoka ovyo. Aisha mwanangu alikua kama teja la ngono kila alipokua ameketi peke yake alilia anataka mtu amwingilie wafanye ngono. Hali ile iliniumiza sana maana ukikaa nae tu angelilia mwanaume wa kusex nae inaonekana Riziki alimzoesha ule mchezo mchafu

Niliwaomba Madaktari 🥼🩺👨‍⚕️wanisaidie, nikatafuta wataalamna Wanasaikolojia. Loh! Masikini majuto yaliniandama.

      Ikawa sasa ninautumia muda mwingi wa kukaa na wanangu, 🕐nilitamani kutafuta wasichana wa kazi lakini sikuwaamini kabisa, nilitamani kuacha kazi Ili niwe karibu na wanangu nikaona haitoshi wacha nimtafute Mama yao nimuombe turudiane. Mama yao niliyempa Taraka alikwisha olewa na mtu mwingine. Nilipompa taarifa juu ya kile kisa cha Mama na Dada Wala hakuumia au kusikitika alichosema yeye alisema: "Sasa Mimi nifanye nini kama watoto wameharibika basi pambana warejee kama zamani. Ulikataa katakata nije niwaone na kuwasabahi na sasa imepita miaka Saba ndo' unadai turudiane? Haiwezekani mie nina maisha yangu."

      Kilio kilinitoka nilimpoteza mke mwema kwa ujinga wa kumsikiliza Mama yangu, Mama yangu na Dada wamekula njama na kushiriki kuniharibia kizazi changu. Masikini mimi ni Bora kama ningelimpa mke wangu Jasimini nafasi ya kujieleza kuhusu lile sakata lakini ubaya wake nilimsikiliza Mama yangu.

""""""""""""""""""""""""'""


TCHAO

🥲😥😢🤧😭


""""""""""'"""""""""""""""""
 


Sunday, December 1, 2024

KIKULACHO KIMO NGUONI MWAKO

 



HERENI ZENYE KITO 💎CHA KIJANI💚 KINACHONG'AA (EMERALD GREEN)  ZILISABANISHA NIJUE MUME WANGU ANACHEPUKA NA SHOGANGU WA DAMU.


Mie na Boazi tulijuana tukiwa Chuo kikuu cha Dar es saalam. Campus ya Mlimani, mapenzi yetu yalizaliwa yakakua na kumea hadi kuelekea ndoa👰 na maisha matamu ya kutamani Sha. Kwa hakika mwenzangu maishani mwako ukimpata yule wa kukupendeza moyoni💓, yule anayekuwaza wewe tu, mwenzangu utajihisi umenunua ☁️Mbingu ndogo ya Jerusalem au Makka🏞️🕋

      Naitwa Queen👑 Moletta. Mie Queen ninaye shoga yangu anayeitwa Majulla👩‍❤️‍💋‍👩 ni shogangu tangu kinda kindaki hadi maisha yetu ukubwani. Tulipokua chuo Majulla alizoea kunipamba kwa sifa kemkem yote juu ya Boazi Boyfriend wangu.🤾

      "Usije kumuacha au kumsaliti Boazi Queen Molleta, Boazi ni miongoni mwa wanaume wachache wanaojua kupenda, kuthamini na kujali."😍 Mie Queen nikajiona sasa n'shakua Queen Elizabeth kutokana na sifa kemkem juu ya Boazi.

      "Mtazame alivyo na mambo ya kizungu: 🥇First of all anajali muda, 🥈second yupo smart and 🥉third anatimiza promise mbalimbali anazokuahidi." Majulla alimsifia Boazi wakati huo tunaelekea Lecture hall kusikiliza mihadhara.

     "Ukiomba mwende ,🕐Beach 🏖️⛱️🩴atakua wa kwanza kukutembelea akikuuliza 'Baby wangu ushakula?' Wakati huo huo atakuletea zawadi ya pipi 🍭au Biscutt 🧇. Jamani kijana anajali hata vitu vidogo vidogo viso na muhimu anajali." Majulla aliongea pasina kutarajia njiani tulikutana na Baby 💕 wangu  Boazi. Wawili Sie tukamshangaa.

    "I love you Queen!"💖 Alinikumbatia kwa nguvu Kisha akanipiga kiss kinywani💋 alafu tena a akanipatia maua💐 mekundu. Ah! Jamani nilijiona kupendwa na kijana wa ujana wangu.

*********

Basi wapenzi wasomaji mie Queen Molleta pamoja na wangu wa moyo Boazi tukala💍 kiapo cha ndoa⛪ kanisani pembeni ya mkono wangu wa kulia alisimama shogangu Majulla kama Best woman, Rafiki wa ukweli.🙋 Akilinyanyua nyanyua gauni 🥻langu la harusi  lililojiburuta chini. Tukala,🥙🥒 tukanywa 🍹🍷na kufurahia💃🕺👯🎶🩰, maisha yandoa Yakaanza. 

    Ndoa yetu ilijibu, Zakaria mwanangu wa kwanza alizaliwa baada ya miaka 3 ya furaha, raha na deko kwa Zakaria tukampata Zawadi Binti yetu aliyezidisha furaha ya ndoa na hatimaye mwanetu wa mwisho Timothy alizaliwa👶🧒🤱 Sie wenye ndoa tukazidi kupendana zaidi na zaidi. 

     Majulla hakueleweka na tena sikumuelewa maana alipobeba mimba🫄 ya mwanaume aliyedai yupo ughaibuni 🏙️tena mwanaume wenyewe alikutana naye kwa bahati mbaya Binti yake Taraji akazaliwa baada ya hapo miaka sita mingine alijaliwa kupata kidume, Moze. Mwenzangu aliniambia Baba wa watoto wake yupo ughaibuni yeye ajapo ni ngono tu na kutundikwa kibedi. 

Teh teh teh😂😂.  Aheri ya mwenzangu sasa wale wasio na watoto wabebe nini? Mawe au barafu?🪨🧊

       Zakaria wangu alianza shule🏫, Zawadi wangu aliaanza Shule, Timothy wangu akafuatia,tukawapeleka shule wakamaliza darasa la saba hadi vyuo🎓 wakaenda. Vivyo hivyo kwa Shogangu Majulla watoto wake walikua katikati ya bidii, heshima na akili za kuzaliwa. 

       Jambo moja lilinitatiza moyo, watoto wa Shogangu Majulla walikua na mfanano na Mume wangu Boazi yaani kuanzia sura, 😊sauti 🔉na matendo lakini kwa jinsi nilivyompenda na kumuamini Boa nisingelimvunjia heshima kumuuliza juu ya watoto wa Shogangu au kumuuliza Shogangu. Juu ya watoto  wake, wacha maisha yaendelee. 

       Basi ndoa yetu ikatimiza miaka ishirini ya🎊🎉 furaha, mapenzi afya na Mahaba. Mie Queen Molleta pamoja na my Husband tukapatana tufanye karamu ya kuadhimisha miaka ishirini ya ndoa yetu 🎂isiyo na chembe ya matukio ya kuvunja moyo au kuumiza. Maandalizi yakanoga tukafanya kuwaalika wageni wapatao Mia, 💯ndugu jamaa a marafiki na miongoni mwa jamaa waliharikwa Shyrose wifi yangu alijitolea kuupamba kumbi wa Sherehe.

      "wifi nina imani siku ya leo  utapendeza sana zile hereni za Emerald haswa ukivalia gauni jeusi au jeupe utametisha zaidi"💫 Wifi aliniambia tukiwa tunaendelea kuupamba ukumbi.

    "Hereni za Emerald?" Nilishangaa kauri ya Wifi yangu.🤔

      "Wifi naye! Tuseme kaka Boazi hajakuonesha?" Aliniuluza.

    "Wiki jana alikuja Dukani kwangu Buguruni, Duka la maodozi. Akaniungisha Hereni nzuri za kijani. Ina maana bado hajakuonesha?" Maneno ya Wifi Shyrose yakanifanya nipate mwana na taa💡🕯️ ya tahadhari iliwaka ubongoni.🧠

     "Wifi yangu unajua kaka yako ana mambo mengi yamkini hizo Hereni amezificha chumbani anatarajia kunipa kama Sapraiziment." llibidi niufiche mshangao wangu kwa kusema maneno niliyobuni kichwani.

      "Labda Wifi lakini ninakwambia ukivaa tu utapendeza Nawe utakuja kunishukuru maana niliagiza kutoka Arabuni."

     "Jamani Arabuni!!? Kule kwenye mali safi Orginal✨" Nilitania lakini moyoni niliumia inakuwaje Boazi ndani ya wiki yote hii hajanionesha hizo Hereni za Emerald ukitegemea nijuavyo Boazi hajawai kuwa na Siri inayofichika kwangu. Siri zake, Siri zangu, kilicho hake changu, changu chake. Aahgh! Nilighafirika😡.

      Ghafra jicho langu likamuona Majulla shogangu akiingia ndani ya kumbi. Wakati huo viti vya kumbi vishaandaliwa, meza ishadaliliwa na keki traaam,🍰 ya kukata na shoka  Muziki 📻🎺wa blues ukitambaa masikioni mwetu kwa traaaatiibu. Yote hayo kuna jambo moja lilinifanya nihisi vibaya zile hereni za Vito vya kijani alikua amevaa Majulla wangu. Zile hereni alizoniambia wifi yangu Shyrose. Nyie! Nilipigwa 🥺 butwaa.

      "Wifi," Nilimwita wifi kwa sauti ya mnong'ono

      "Abee ." Shy aliniitikia.

     "Hereni ulizoniambia ni zile alizovaa Majulla?" Nilinong'ona Majulla asije akasikia° Shy aliacha kudarizi kumbi akageukia kule mlangoni kule Majulla alikotokea.

    "Jesu!" 🤭Shy alishituka kwa sauti. Nikamuuliza.

      "Nini Wifi!?"🙂

      "Ndio zile zile kaka alipokuja Dukani kununua nilimkabidhi Japokuwa sikumuuliza kama ananunua ajili yako." Shy alinitobolea Siri.

    "Shy wifi yangu, kaka yako Boazi anachepuka ." Nilijikuta naropoka.

    "Nashangaa wifi."Shy aliuziba mdomo wake kwa mshangao 🤭

   "Tuendelee kuupamba ukumbi." Nikamwambia. Sie tukaendelea kuupamba ukumbi. Majulla alitembea kwa madaha naye akanifikia pale alipokua naupamba ukumbi. Akili ziliniambia nimchokoze ili nione reaction yake itakuaje.

     "Hongera mwaya mume wetu Boazi anajua kukupamba hereni za kijani." Majulla alishituka kauri yangu. Akajing'atang'ata na kupepesa macho huku na kule kama ameona Mzimu.

   "Ooh! Ooh! Ooh! Mwaya Naomba unipe ruhusa nikaitumie resting room😲🚺" Aliniomba aende kutumia choo.

    "Nenda Mke mwenzangu, nenda ukakojoe." Nilimwambia pasina kunena neno aliondoka aibu ikimfuata. Moyoni nilianza kuujua mchezo uliopo Kati ya Boazi my Baby na Best wangu Majulla. Niliumia masikini mie jambo nisilolijua kama usiku wa kiza.

      Hazikupita dakika kumi na tano ⌚Boaz mume wangu Aliingia ukumbini aliingia akiwa amejaa tele, mwingi wa furaha na raha za maisha. Akanifuata pale nalipokua namalizia kuupamba pamba ukumbi. Akanishushia busu zitroo shavuni 😍💋😘. Kwani nalisikia rahaa... Nyoo! Nikamgea vidonge vyake

     "Eeh! Mume hizo Hereni za Emerald (kito cha kijani king'aacho sana) mbona hadi sasa haujanipa nivae mkeo nipendeze?" Macho Pima yakamtoka👀

    "Aah! Aah! Queen my daring nilitaka nikupe kama Sapraiziment🎁 baada ya kuisha kwa hii Anivesary." Alijitetea.

     "Nahitaji sasa hivi Babu! Tena nataka ziwe bora zaidi ya zile alizovaa Mke mwenzangu Majulla."Nikamuona anazidi kutetereka na kuingia kigugumizi.

   "Usijali Queen, ninakupenda Daring." Naomba uniruhusu nikaitumie Toilent.🚹"  Aliongea hivyo wakati huo simu yake ilikua ikiita ovyo. Nilifurahia moyoni maana nilijua Majulla atakua amempigia. Alipoenda Toi 🚻nilimfuata __nyuma nyuma kwa tahadhari pasina yeye kujua.

     "Hallow! Uko wapi?"📱Nikiwa nimejibanza kwenye kigiza cha ule ukumbi nilisikia mume wangu akiongea na simu.

   "Njoo Restroom, choo cha kike."Sauti ya Shogangu ilisikika.Boazi kama mkia wa Umbwa 🐩akaielekea Restroom, nilimfuata Kisha nikajibanza ndani, pembeni ya mango nisikie nini wanachojadiliana.

     "Una nini wewe mwanaume? Yaani unamweleza mkeo juu ya hereni hizi ulizoninunulia." Majulla aliongea kwa hasira.

     "Mpenziwangu amini usiamini kamwe singeliweza kumwambia Queen Habari hizi."Nilishangaa kumbe Majulla na Mume wangu ni mtu na mpenziwe. Mmh! Tangu lini? 

    "Sasa inakuaje Queen mkeo mbele ya Dadako amenitamkia kuwa hizi Hereni umeninunulia?"

    "Unasemaje!?" Boazi alishangaa.😒🤨😶

    "Hivyo hivyo kama wewe ulivyosikia." Majulla alipandwa kisirani.😠

    "Majulla mpenzi wangu kamwe siwezi kufanya ujinga huo. Ninakupenda na kamwe siwezi kusababisha penzi letu liingie dosari."Boazi Alijitetea.

    "Nakwambia Boazi sintakusamehe kama utamwambia habari kuhusu watoto niliozaa na wewe." Jesu! 🤭Mapigo ya moyo yalinienda kasi, nilihisi kizunguzungu kunipanda, nikataka kuanguka ndani ya kile choo. Ile nasikia Bestangu Majulla amezaa na mume wangu Boazi, Jamani watu wanasiri, we acha tu! Ina maana Taraji na Moze wana wa Majulla ni wana wa mume wangu pia. Eh! Mola nipe uziwi nisisikie kauri hizi. 🤲

    "Mpenzi kamwe siwezi kufanya ujinga kama huo, wewe binafsi umenijua kwa zaidi ya miaka ishirini na tatu tangu ukiwa Chuo, nawezaje kukuharibia siku yako?" Hapana, Jamani sikutaka kuendelea kusikiliza yale maongezi yao, nilihisi nitapata stroke na presha ya kusababishwa na wale wapuuzi. Nikafanya hima kuondoka Resting room, machozi na hisia za kuonewa huruma zilinifunika

....................

Sherehe ile iliendelea taratibu wenyewe wakila na kufurahia, baada ya muda kupita MC wa Sherehe aliniita angarau nikatoe neno la shukrani. Nikiwa nimejaa tele nikampoka MC🎤🎙️ ile microphone nikwatazama wale mahanisi wawili na wapuuzi tena wasaliti: Boazi na Majulla Kisha nikatamka mbele ya watu Mia moja waliohudhuria ile Anivesary.

     "Wanawake mwenzangu, Mliojifunga uchungu viunoni mwenu nyie mlioolewa na nyie mnaoishi na waume zenu naomba mniambie inawezekana kweli mume unayelala 😴🛌 naye kitanda kimoja akampatia shogako hereni za Emerald, kito cha kijani.? Niliuliza. Wanawake na wanaume wakageuza shingo zao kumtazama Best wangu Majulla, hata kabla hawajanijibu walianza kumzodoa Majulla.

     'Una pepo🪬 wewe sio haba, unawezaje kupokea Hereni alizonunua mume wa mwenzio wakati huo mwenzio hapewi hizo hereni za kito cha Kijani?" Walimtazama kwa macho makali kama Duma mwindaji🐆.

    "Aheri ungelipokea Hereni za mwanaume mwingine lakini sio za mume wa mwenzio." Majulla alianza kutetereka maana aliona yashamwagika hayazoleki.

    "Yamkini Unalala na Boazi Majulla!?"  Wachangiao Umbea walimkosoa Majulla Shogangu. Boazi mume wangu aliona aibu kuongea na wanaume wenzie. Basi mie nikalinogesha lile soga Umbea.👌

     "Tena mtajisikiaje wanawake wasomi wenzangu iwapo mtasikia kuwa mwanaume uliyemjua miaka mitatu chuoni, lshirini ndoani leo hii ugundue kuwa mwanaume huyo amezaa na Shogako watoto wawili ambao ni siri nzito kama usiku wa kiza🌑" Uwii! Kama niliamsha Popo, kila mtu alimtazama Majulla na Boazi. Ghafra Majulla akavua viatu vyake vya mchuchumio👠 na kuvitupa kule, akatoka ndani ya kumbi machozi yakimbubujika.

Boazi ambaye hakujua kama nimeshaigundua ile siri yake, ile siri nzito. Alikuja mbele ya ukumbi akapiga goti mbele yangu, watu zaidi ya Mia walimshangaa, wakinong'onezana na kupiga kelele kuulaani ule Ufisadi alioutenda Majulla na Mume wangu Boazi.

    "Nisamehe Queen! 🙏🙇Naomba unisamehe Mke wangu, nimekukisea sana." alilia pale chini alipopiga magoti.

    "Siwezi kukusamehe Boazi, Dunia aina siri. Umejaribu kunificha siri hiyo kwa zaidi ya miaka 23, umenivunjia heshima ya ndoa yangu kwa kuzini na kuzaa na rafiki yangu. Umenikosea sana Boazi sasa naomba Taraka  yangu. Nikuache na huyo umpendaye."Niliongea kwa sauti na tena kwa kipaza sauti.

     "Queen Molleta, please nimekukosea sana Daring Nisamehe." Alilia hadi kamasi zilimtoka.

     "Tutaonana mahakani mbele ya Mwanasheria wa ndoa, huko ndiko utakako zijua zipi mbivu na zipi mbovu." Nilimjibu jeuri Boazi aliyegaragara pale ukumbini akilia kwa chungu.😭😿🥹

"" "" "" "" "" "" "" "" 
TCHAO👋


Atanikuta Mahakamani kwa Mwanasheria wangu. ⚖️🐾,



I promise you

   I PROMISE YOU. (NINAKUAHIDI.) SURA  YA KWANZA. UBAYA WA POMBE. “Umenizingua job, umenizingua kwa muda mrefu sana mpenzi wangu…….kwanini l...